Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Kuna mtoto wa miaka 6 anasumbuliwa sana na kifua tangu alipokuwa mdogo. Hasa usiku ndio anakohoa zaidi. Chanzo: siku moja alipokuwa na umri wa miezi 9 mama yake alikuwa anamuogesha. Kwa bahati mbaya sabuni ikamwingia puani na kumpalia. Tangu hapo amekuwa akikohoa hadi leo hii. Huwa kinatulia baada ya kupata dawa halafu baada ya muda kinaanza tena. JF doctors msaada tafadhari.