Naomba ushauri na tiba ya kikohozi na mafua kwa watoto

Kuna mtoto wa miaka 6 anasumbuliwa sana na kifua tangu alipokuwa mdogo. Hasa usiku ndio anakohoa zaidi. Chanzo: siku moja alipokuwa na umri wa miezi 9 mama yake alikuwa anamuogesha. Kwa bahati mbaya sabuni ikamwingia puani na kumpalia. Tangu hapo amekuwa akikohoa hadi leo hii. Huwa kinatulia baada ya kupata dawa halafu baada ya muda kinaanza tena. JF doctors msaada tafadhari.
 
Dawa ya kifua Chukuwa Asali Weka Kitunguu Maji Kikatekate Kichanganye Kwenye Asali Kiweke Masaa 12 Halafu Tumia Kiasi Kama Kipimo cha Hospitali

au jaribu moja kati ya hizi dawa Zabibu: Glassi moja ya zabibu changanya na kijiko kimoja cha asali tumia kwa muda wa wiki, inasemakana zabibu ni burudisho la mapafu.


Atumie kisha unipe feedback Source: Herbalist Dr. MziziMkavu
 
Hakuwezi kuwa na uhusiano kati ya kikohozi cha sasa akiwa na miaka 6 na kupaliwa maji ya sabuni miaka mi5 iliyopita. Huwa mnampeleka hospitali? Ameshaonwa na Paediatrician (daktari bingwa wa watoto)?

Nadhani kuna umuhimu wa mtoto huyo kuonwa na Paediatrician akamsikiliza vizuri kifua kwa kutumia stethoscope na pia kumfanyia X-ray ya kifua. Kuna magonjwa mawili ambayo huwa mara nyingi dalili yake ni kikohozi cha mara kwa mara kwa watoto, nayo ni Pumu (Asthma) na magonjwa ya moyo ya kuzaliwa (Congenital Heart Diseases).

Haya magonjwa daktari anaweza akayahisi kirahisi tu kwa kusikiliza kifua kwa umakini na/au kufanya X-ray.
 
Hakuwezi kuwa na uhusiano kati ya kikohozi cha sasa akiwa na miaka 6 na kupaliwa maji ya sabuni miaka mi5 iliyopita. Huwa mnampeleka hospitali? Ameshaonwa na Paediatrician (daktari bingwa wa watoto)? Nadhani kuna umuhimu wa mtoto huyo kuonwa na Paediatrician akamsikiliza vizuri kifua kwa kutumia stethoscope na pia kumfanyia X-ray ya kifua. Kuna magonjwa mawili ambayo huwa mara nyingi dalili yake ni kikohozi cha mara kwa mara kwa watoto, nayo ni Pumu (Asthma) na magonjwa ya moyo ya kuzaliwa (Congenital Heart Diseases). Haya magonjwa daktari anaweza akayahisi kirahisi tu kwa kusikiliza kifua kwa umakini na/au kufanya X-ray.

Ahaa, nashukuru sana mtaalamu. Nilipata shaka na sabuni hiyo kwani kuanzia siku hiyo ndipu mchaka mchaka huo wa kifua ulipoanza mpaka leo.
 
Nina mtoto wa miezi tisa ila ana mafua nimpe dawa gani ili apone? Msaada please!
 
mpatie mafuta ya samaki.kama ananyonya mnyonyeshe kwa wingi.mkamulie maji ya machungwa mpe.usipende kumpa dawa kwa umri huo.
 
Nina mtoto wa miezi tisa ila ana mafua nimpe dawa gani ili apone? Msaada please!

Pole sana mgaga ila kama hayamletei homa usipende kumpa mtoto dawa bila sababu we ni kiasi cha kummonitor tuu ila chemsha maji yawe ya uvuguvugu weka chumvi kidogo tafuta kitambaa laini mkande na yale maji kuanzia usoni shingoni na kichwani kwa ujumla yatapungua vilevile kama una vitunguu swaumi vitwange umpake kwenye nyayo inasaidia sana hata kwa mtoto mwenye homa kali. Asante
 
Hi
Naomba umpeleke mtoto hospitali akamwone daktari ambaye atampima ampe dawa inayostahili. Watoto huwa wanatofautiana kwenye dalili wanazoonyesha. hata kama hana homa, anaweza kubadilika ghafla. usifuate ushauri ulitolewa hapo juu.
 
Za leo wandugu,

Mtoto wangu anasumbuliwa sana na mafua, yanamfanya kushindwa kupumua na kukosa raha kabisa hata ya kula. Nimejaribu dawa za hospitali za kuzibua naona hazimsaidii. Nini nitumie mbadala kinakachoweza kuzibua hizo pua!.

Asanteni.:embarassed2:
 
Za leo wandugu,

Mtoto wangu anasumbuliwa sana na mafua, yanamfanya kushindwa kupumua na kukosa raha kabisa hata ya kula. Nimejaribu dawa za hospitali za kuzibua naona hazimsaidii. Nini nitumie mbadala kinakachoweza kuzibua hizo pua!.

Asanteni.:embarassed2:
Unge weka umri wa mtoto inge saidia sana wataalam binafsi mimi huwa nachemsha maji halafu una weka chumvi kidogo halafu unamdondoshe matone mawiwili kila pua.
 
Unge weka umri wa mtoto inge saidia sana wataalam....binafsi mimi huwa nachemsha maji halafu una weka chumvi kidogo halafu unamdondoshe matone mawiwili kila pua...

Mtoto ana umri wa mwaka mmoja na nusu sasa.
 
Mpeleke kwa ENT surgeon haraka anaweza kuwa na adenohypertrophy au nasal polypsy kama hana allergy.
 
Mpeleke kwa ENT surgeon haraka anaweza kuwa na adenohypertrophy au nasal polypsy kama hana allergy.
Asante ndugu yangu,
Yeye kwa kweli yuko na allergy ya vyakula vingi (maziwa,ngano,samaki na mayai)i, na isitoshe kalizaliwa mapema sana na wiki 26 kakiwa na 650gram. Huku tulipo ni msimu wa winter kuisha, kwa hiyo kuna mlipuko wa mafua makali sana, ambayo naona ndo yamempata pia. Kwa hio ndo yanamtesa hivyo kwa kweli. Na hospitali zetu mafua sio ugonjwa.
 
Pole sana mkuu hasa ukizingatia mwaka mmoja bado mdogo.Mpeleke hosp lakini atapata ufumbuzii
 
kumfukiza pia inasaidia! weka maji ya moto kwenye beseni katia limao likiwa ha maganda yake changanya na chumvi kidogo.kaa nae kisha mjifunike na shuka safi. avute mvuke 2mnts on and 5 mnts off hadi maji yapoe. inakuwa kama steam bath. imemsaidia kweli mwanangu who is two years now!
 
kumfukiza pia inasaidia! weka maji ya moto kwenye beseni katia limao likiwa ha maganda yake changanya na chumvi kidogo.kaa nae kisha mjifunike na shuka safi. avute mvuke 2mnts on and 5 mnts off hadi maji yapoe. inakuwa kama steam bath. imemsaidia kweli mwanangu who is two years now!

Kuwa makini na dawa zinazopendekezwa. Miezi miwili iliyopita niliugua mafua na pua kuziba. Nilipowaona Hospitali nikaandikiwa dawa fulani hivi ya matone. Kweli ukiweka tone moja tu pua mwaa! zinazibuka . Lakini amini toka wakati huo sisikii/ sinusi harufu yeyote. Nimepoteza uwezo wangu wa kunusa. Kabla nilikuwa sensitive sana kwa harufu lakini sasa hata harufu ipi siinusi!
 
Kuwa makini na dawa zinazopendekezwa. Miezi miwili iliyopita niliugua mafua na pua kuziba. Nilipowaona Hospitali nikaandikiwa dawa fulani hivi ya matone. Kweli ukiweka tone moja tu pua mwaaaaa zinazibuka . Lakini amini toka wakati huo sisikii/sinusi harufu yeyote. Nimepoteza uwezo wangu wa kunusa. Kabla nilikuwa sensitive sana kwa harufu lakini sasa hata harufu ipi siinusi!

mkuu hiyo ni side effect ya dawa hiyo uliyotumia pole sana Da! Jf bwana
 
Vuta subira kidogo naona mzizi mkavu anamalizia malizia kupasha misuri moto kaa mkao wa kula..

Ukiwa mvivu wa kusoma kamwe utaishia kumchukia mzizimkavu.
 
Back
Top Bottom