Ushauri; Masters ya Open University of Tanzania

Kichwa Ngumu

JF-Expert Member
Nov 6, 2010
1,726
312
JF members heshima kwenu.
Mi ni mwajiriwa wa serikali kada ya uasibu na nipo mkoani sehemu ambayo siwezi kusoma jioni na mbaya kutokana na nafasi yangu ya kazi kwa kipindi kirefu nimetaka kwenda shule kama Mzumbe nikanyimwa ruhusa licha ya kutimiza vigezo vya kwenda shule.
sasa nimeona nazidi kuuweka usiku ukizingatia uwezekano wa kupata ruhusa ni mdogo natoka nisome open university kama long distance naomba kushauriwa kwa mambo yafuatayo.
  1. thamani ya chuo serikalini/ubora wa elimu
  2. kutambulika cheti kwenye vyuo vingine
  3. na mambo mengine ambayo unaona yatanifaa
 
Itakusaidia kama utafanya serikalini maisha yote,ila kwenye tahasisi makini za private hawachukui watu wa open..inshort iyo ni masters jina.
 
Ushauri wa huyo bwana ni sahihi na ni mkweli.Nilisoma module kumi kati ya kumi na tano nikaacha.
Kwa sababu hizo alizosema. Tena jamaa alivyoondika ni mstaarabu naombe niendeleze ustarabu wake.
Think about it.
 
Ushauri wa huyo bwana ni sahihi na ni mkweli.Nilisoma module kumi kati ya kumi na tano nikaacha.
Kwa sababu hizo alizosema. Tena jamaa alivyoondika ni mstaarabu naombe niendeleze ustarabu wake.
Think about it.
hahahaha wewe ulishindwa bwana ukakimbia,nenda Mzumbe aka maharage ya Mbeya utasoma muda mfupi utamaliza halafu utaajiliwa na makampuni makini!
 
je elimu ya open university haithaminiwi kwasababu mwanafunzi huwa hakai darasani?
 
kama una kauzembe na haraka unataka ajira za mizengwe na cheti cha masters pekee nenda Mzumbe na kama unahitaji concrete knowledge na unajimudu katika taratibu/discipline ningekushauri Open University na hata waajiri wataona tofauti, ni huluka tu za mazoea, watu waliowengi hawasemi ukweli wanakimbia wanashindwa, for sure angalia hapa..http://www.webometrics.info/rank_by_country.asp?country=tz
 
Shahada za kitanzania hazina soko hata kwenye jumuia ya afrika mashariki kwenyewe. Ukienda ulaya ndiyo usiseme. Lazima wakutupe darasani hasa chuo chenyewe kama ni vile vinavyoheshimika. Wazungu wanajua elimu yetu ilivyochakachuliwa na ufisadi. Kwa Open University ukweli ni kwamba wengi wamejenga dhana kuwa ni chuo ima cha wanasiasa aina ya akina Mrema au watu waliofeli au wenye tamaa ya kuwa na shahada mradi shahada. Leo nimeshangaa kusoma makala ya mtu mmoja aitwaye Hamza KONDO eti mwanafunzi wa PhD na mhadhiri OUT. Jamaa hajui hata kuandika makala kwa kiswahili. Hivi mtu kama huyu kweli anaweza kuandika academic paper au dissertation?
 
Back
Top Bottom