Ushauri kwa wana udsm

special agent

JF-Expert Member
Jun 2, 2012
325
74
Kama kuna kitu cha kushauri kwa sasa kwa wanafunzi walipo UDSM ni kwamba wahakikishe utaratibu wa kupewa vyeti vya taaluma mbali mbali wanazo hitimu unabadilishwa.Kwani utaratibu ulipo sasa wa kusubili mwaka mmoja upite ndiyo mhitimu apate cheti kwa mtazamo wangu ni kwamba umepitwa na wakati.Ni kweli kila mtu anakubali matunda ya pale UDSM lakini kwa hili wajaribu kuiga kutoka vyuo vingine.Kwani wengi imewagharimu kwa kutopata stahili zao ikiwemo mishahara kwani TRANSCRIPT hazikubaliki hazina.Pia hata waajiri wengi ikiwemo selikari wanataka cheti na siyo transcript hivyo basi mimi binafsi nashauri wahusika kwa maana ya wanafunzi na watawala wafanyie kazi ushauri huu kwani wahitimu pamoja kuwa na elimu nzuri wanateseka bila sababu za msingi moja wapo ikiwa ni hii ya kutokua na cheti.Kwani mwanafunzi akisha hitimu masomo yake kuna sababu zipi za kusubiri cheti mwaka mzima .....ni ushauri tuu.
 
Back
Top Bottom