Ushauri kwa kijana mwenzetu

The Finest

JF-Expert Member
Jul 14, 2010
21,605
6,071
Nina rafiki yangu mwenye umri wa miaka 29 katika kuhangahika kwenye maisha ya mapenzi amefanikiwa kupata mwanamke ila huyo mwanamke aliishawahi kuolewa na akabahatika kuzaa mtoto mmoja bahati mbaya mume wa huyo mwanamke alifariki kwa ajali ya gari mwaka juzi huyu mwanamke alimueleza huyu kijana situation yote kwamba ana mtoto na aliishawahi kuolewa na mume wake akafariki ili afahamu mapema kabla hawajafika mbali huyu rafiki yangu hakuwa na tatizo na suala hilo.

Na kutokana kwamba amempenda akaona ni busara akimtambulisha kwenye familia yao bahati mbaya baba wa huyu kijana ameishafariki,mama yake yuko Mwanza mtu wa karibu ni kaka yake na shemeji yake,then walipanga siku akaenda akamtambulisha huyu mwanamke kwa kaka yake wala hakukuwa na tatizo lolote walimpokea vizuri yule mwanamke


Vile vile akaona itakuwa vizuri akimfahamisha na mama yake swala zima na hakutaka kumficha mama yake kitu chochote ingawa mama yake ameshtuka kusikia anamdate mtu ambaye tayari aliishawahi kuolewa "Akamuuliza kwani haujaona wanawake ambao wako single"? Inaonekana ni kitu amabacho mama yake akuexpect kutoka kwake ila baada ya mazungumzo marefu mama yake akamwambia kwa vile wewe ndiye unayeoa siwezi kukuingilia sababu that is your happiness ila cha muhimu ni kuhakikisha unafanya maombi na kumwomba mungu.


Sasa huyu kijana amekuwa na mawazo na amekuwa akijiuliza je ni kosa kumdate mtu ambaye tayari aliishaolewa na amekuwa akijiuliza imekuwaje ameangukia kwenye mapenzi ya mwanamke ambaye tayari aliishaolewa and not otherwise?


ANY VIEWS ON THIS...
 
mmmh Sioni pingamizi! ...................................... mpaka kifo kitakapotutenganisha
 
hapo hakuna tatizo mama kushtuka ni kawaida maana hata wewe baadae huko mtoto wako akija na habari kama hii lazima ustuke kwani huyo mwanamke alishaolewa na mtu mwingine bahati mbaya tu alikufa huyo mme. Alichoongea mama ni muhimu kwamba "kwa vile wewe ndiye unayeoa siwezi kukuingilia sababu that is your happiness ila cha muhimu ni kuhakikisha unafanya maombi na kumwomba mungu" hiyo sentensi ya mama imeonyesha ukomavu mkubwa sana wa kifikra
 
Miaka 29 unahangaika na jimama ambalo lilikwishaolewa na kuwa-widowed WHY?

Kama ni tamaa ya mali za marehemu mwambie aendelee; kama ni kutaka mke wa kuoa mwambie tamaa itampeleka pabaya!
 
Suala la kwamba aliolewa au la halina tija, kinachojalisha ni upendo uliopo baina yao. Madhali katika hiyo safari ya mapenzi unafika unapotaka, shida yote ya nini? Haijalishi gari unayopanda ni mpya au la, cha msingi ni kufika safari yako. Pia kama ni 'kutumika kwa mashine' mi sioni tatizo, manake mizigo mingi tunayochukua street huwa ishatumika balaaa (tunashukuru kwa vile haziongei!).
 
Miaka 29 unahangaika na jimama ambalo lilikwishaolewa na kuwa-widowed WHY?

Kama ni tamaa ya mali za marehemu mwambie aendelee; kama ni kutaka mke wa kuoa mwambie tamaa itampeleka pabaya!

Baba Enock Kumbuka mapenzi hayachagui huyo mama hakupenda mmewe afariki...na kama yeye na kijana wameona ni vema kuwa pamoja sioni tatizo hata kidogo...
Mwenyezi mungu awatangulie katika hili jema
Kijana hajakosea hata kidogo..
 
Suala la kwamba aliolewa au la halina tija, kinachojalisha ni upendo uliopo baina yao. Madhali katika hiyo safari ya mapenzi unafika unapotaka, shida yote ya nini? Haijalishi gari unayopanda ni mpya au la, cha msingi ni kufika safari yako. Pia kama ni 'kutumika kwa mashine' mi sioni tatizo, manake mizigo mingi tunayochukua street huwa ishatumika balaaa (tunashukuru kwa vile haziongei!).

Teheteheteh ....... zingekuwa zinaongea pangekuwa hapatoshi hahaha:frusty:
 
Suala la kwamba aliolewa au la halina tija, kinachojalisha ni upendo uliopo baina yao. Madhali katika hiyo safari ya mapenzi unafika unapotaka, shida yote ya nini? Haijalishi gari unayopanda ni mpya au la, cha msingi ni kufika safari yako. Pia kama ni 'kutumika kwa mashine' mi sioni tatizo, manake mizigo mingi tunayochukua street huwa ishatumika balaaa (tunashukuru kwa vile haziongei!).

Mkuu nakuunga mkono asilimia 100%.

No comment other than that......
 
Miaka 29 unahangaika na jimama ambalo lilikwishaolewa na kuwa-widowed WHY?

Kama ni tamaa ya mali za marehemu mwambie aendelee; kama ni kutaka mke wa kuoa mwambie tamaa itampeleka pabaya!

Mkuu this is way too rude! Japo complecations zinakua nyingi ukioa/olewa na widow.
 
Baba Enock Kumbuka mapenzi hayachagui huyo mama hakupenda mmewe afariki...na kama yeye na kijana wameona ni vema kuwa pamoja sioni tatizo hata kidogo...
Mwenyezi mungu awatangulie katika hili jema
Kijana hajakosea hata kidogo..

Tatizo langu ni Umri:

Mandela alimuoa Graca! Ni vyema wajane wakaolewa/oa na watu walokuwa katika "rika" linalowiana"!

29 years of age wengine tulikuwa bado hatujafikiria hata kuoa - na hata mahusiano yetu hayakuwa "so skewed in terms of age"!

Huyu kijana bado mdogo kuwa na mahusiano na mwana-Mama!
 
Wanawake wako wengi kwanini uangukie kwa mwanamke alikwishaolewa tena mwenye mtoto ????????????.Hapana mwambie amwache huyu mwanamke atafute kipusa mwingine wako kibao,kubwa zaidi tajibandika shughuli ya kulea mtoto mbae si wake,tena wanawake waliofiwa na waume zao wakati mwingine wana nuksi unaweza kujikuta unapoteza maisha bure.Nimewahi kuona mwanamke kila akiolewa lazima mwanaume afe mpaka walipofika wanaume watatu watu wakastukia mama ana mapepo ya kuua wanaume,wengine utakuta mume kafa na ukimwi ukiingiza tu umekwisha jaribu kuuliza mwanaume kafa na ugonwa gani.
 
Mkuu this is way too rude! Japo complecations zinakua nyingi ukioa/olewa na widow.


I'm saying it again: Kijana wa kiume kuoa mwanamke ambaye tayari alishazaa na mwanamume mwingine ni kuingia kwenye matatizo yasiyo ya lazima! Mwanaume lazima ufurahie uzao wako wa KWANZA! Kama una miaka 29 bado una nafasi kubwa ya kuingia "labor ward" kumuangalia "mwanamke wako" ambaye hajawahi kuingia mahala hapo.

Acheni kumpotosha kijana - Wasichana warembo wapo wengi tu.
 
Tatizo langu ni Umri:

Mandela alimuoa Graca! Ni vyema wajane wakaolewa/oa na watu walokuwa katika "rika" linalowiana"!

29 years of age wengine tulikuwa bado hatujafikiria hata kuoa - na hata mahusiano yetu hayakuwa "so skewed in terms of age"!

Huyu kijana bado mdogo kuwa na mahusiano na mwana-Mama!


kama mwanamama umri unaruhusu bado hana haki?...may b 25-29....mtoa thread hebu tuambie mwanamama ana age gani...au shida hapa ni kwamba kashaitwa mama?
 
Tatizo langu ni Umri:

Mandela alimuoa Graca! Ni vyema wajane wakaolewa/oa na watu walokuwa katika "rika" linalowiana"!

29 years of age wengine tulikuwa bado hatujafikiria hata kuoa - na hata mahusiano yetu hayakuwa "so skewed in terms of age"!

Huyu kijana bado mdogo kuwa na mahusiano na mwana-Mama!

Hatuwezi jua Huyo Widow ana miaka mingapi mpaka sasa labda mmewe alimwacha akiwa bado Binti ...Mtoa mada Mjane ana miaka mingapi?
Lakini me bado kuona Tatizo kama wao wanapenda lazima kuna vitu vimewavutia kuwa pamoja:A S 8:
 
I'm saying it again: Kijana wa kiume kuoa mwanamke ambaye tayari alishazaa na mwanamume mwingine ni kuingia kwenye matatizo yasiyo ya lazima! Mwanaume lazima ufurahie uzao wako wa KWANZA! Kama una miaka 29 bado una nafasi kubwa ya kuingia "labor ward" kumuangalia "mwanamke wako" ambaye hajawahi kuingia mahala hapo.

Acheni kumpotosha kijana - Wasichana warembo wapo wengi tu.

hii jamii yetu bwana inatunyanyapaa sana wanawake, lakini kwa mwanamke kumkuta mwanaume na mtoto ni jambo la kawaida kabisa, mwanamke akikutwa na mtoto ni habari nyingine, kwani hataona uzao wake wa kwanza hata kama huyo mwanamke alishaingia labor?
 
Wanawake wako wengi kwanini uangukie kwa mwanamke alikwishaolewa tena mwenye mtoto ????????????.Hapana mwambie amwache huyu mwanamke atafute kipusa mwingine wako kibao,kubwa zaidi tajibandika shughuli ya kulea mtoto mbae si wake,tena wanawake waliofiwa na waume zao wakati mwingine wana nuksi unaweza kujikuta unapoteza maisha bure.Nimewahi kuona mwanamke kila akiolewa lazima mwanaume afe mpaka walipofika wanaume watatu watu wakastukia mama ana mapepo ya kuua wanaume,wengine utakuta mume kafa na ukimwi ukiingiza tu umekwisha jaribu kuuliza mwanaume kafa na ugonwa gani.


no wonder ndoa za sasa hazidumu, hao vipusa mnaowasemea ndio wanafanya ndoa kila kukicha kula na matatizo kibao, mnaangalia upusa hamuangalii zaidi......mbona cc wanawake tunaweza kuwalea watoto tuliowakuta nao waume zetu?....kashasema mwanaume alifariki kwa ajali.
 
Baba Enock, shukuru Mungu sana ulibahatika kuoa mapema na inawezekana ulioa aliyepitiwa na watu wengi sana ila hukuona wala hukujua kama watu wallipita kilichokudanganya tu ni le kwamba hakuwa amezaa.

Wanawake walioachika na waume zao wako juu wanaolewa kila siku ya Mungu kuliko hao unaofikiria wewe na kuwaita the way you want.

Kija kaza buti oa fasta kabla hawajakuwahi wenzio.
 
Wanawake wako wengi kwanini uangukie kwa mwanamke alikwishaolewa tena mwenye mtoto ????????????.Hapana mwambie amwache huyu mwanamke atafute kipusa mwingine wako kibao,kubwa zaidi tajibandika shughuli ya kulea mtoto mbae si wake,tena wanawake waliofiwa na waume zao wakati mwingine wana nuksi unaweza kujikuta unapoteza maisha bure.Nimewahi kuona mwanamke kila akiolewa lazima mwanaume afe mpaka walipofika wanaume watatu watu wakastukia mama ana mapepo ya kuua wanaume,wengine utakuta mume kafa na ukimwi ukiingiza tu umekwisha jaribu kuuliza mwanaume kafa na ugonwa gani.

no wonder ndoa za sasa hazidumu, hao vipusa mnaowasemea ndio wanafanya ndoa kila kukicha kula na matatizo kibao, mnaangalia upusa hamuangalii zaidi......mbona cc wanawake tunaweza kuwalea watoto tuliowakuta nao waume zetu?....kashasema mwanaume alifariki kwa ajali.
 
kama mwanamama umri unaruhusu bado hana haki?...may b 25-29....mtoa thread hebu tuambie mwanamama ana age gani...au shida hapa ni kwamba kashaitwa mama?
nilitaka kuuliza hivyo hivyo thanks Nyamayao leo tumeamkia kumoja nini?
 
Back
Top Bottom