Mtumishi Wetu
JF-Expert Member
- Oct 12, 2010
- 5,712
- 1,906
Waheshimiwa wana JF naomba kutoa mawazo na maoni kwa kamati itakayo kutana na Rais wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete. Nina imani sote tutachangia ili kwa wale wakubwa wa CDM watakaokutana na Rais wetu wapate mawazo mapya na kujipanga kwa uzuri zaidi kuyawakilisha kwa mkulu wa boma letu la TZ:-
1. Kwanza inahitajika busara na hekima kuu waliyo jaliwa hawa viongozi wetu ili waweze kuteka mtililiko wa kikao ili kiweze kuwa na matunda mazuri kwa nchi yetu.
2. Kwanza wajue kabisa kama wanavyo elewa kuwa wanawakilisha Watanzania na hapo ndipo ulipo mustakabari wa taifa letu, kupona au kuingia kwenye misukosuko.
3. Nawaomba watumie lugha isiyo na jaziba, yenye wingi wa ushawishi ili mkulu wa boma letu aelewe kuwa yeye anatawala kwa muda mfupi tu uliobaki miaka minne tu. Hivyo ni bora akaona ni busara kuwapa Watanzania katiba iliyo bora ambayo inadumu vizazi hata vizazi. Atoke kwenye box la chama awaze kama raia wa kawaida mwenye nia ya kuleta mabadiliko, nchi ipone!! Na yeye atabaki kwenye vitabu vya kumbu kumbu vya mashujaa wa nchi hii!!!!!!!!
4. Kinyume cha hapo Watanzania hawatakubali kudanganywa na hila za kupewa katiba fake ambayo haina nguvu kama hii iliyopo isiyo na uwezo wa kudhibiti na kulinda rasirimali zetu; Isiyoweza kukemea watu wanaojichukulia madaraka na kuingia mikataba fake ya kufilisi nchi yetu.
5. Mfahamishe kuwa akiwa kichwa ngumu katiba kwa namna yoyote na kwa kipindi chochote kile itapatikana na yeye atahukumiwa na historia kwa kufanya usanii kwenye maswala muhimu ya ukombozi wa taifa letu.
Hadi hapo nawasilisha,naomba mawazo yenu waheshimiwa!
1. Kwanza inahitajika busara na hekima kuu waliyo jaliwa hawa viongozi wetu ili waweze kuteka mtililiko wa kikao ili kiweze kuwa na matunda mazuri kwa nchi yetu.
2. Kwanza wajue kabisa kama wanavyo elewa kuwa wanawakilisha Watanzania na hapo ndipo ulipo mustakabari wa taifa letu, kupona au kuingia kwenye misukosuko.
3. Nawaomba watumie lugha isiyo na jaziba, yenye wingi wa ushawishi ili mkulu wa boma letu aelewe kuwa yeye anatawala kwa muda mfupi tu uliobaki miaka minne tu. Hivyo ni bora akaona ni busara kuwapa Watanzania katiba iliyo bora ambayo inadumu vizazi hata vizazi. Atoke kwenye box la chama awaze kama raia wa kawaida mwenye nia ya kuleta mabadiliko, nchi ipone!! Na yeye atabaki kwenye vitabu vya kumbu kumbu vya mashujaa wa nchi hii!!!!!!!!
4. Kinyume cha hapo Watanzania hawatakubali kudanganywa na hila za kupewa katiba fake ambayo haina nguvu kama hii iliyopo isiyo na uwezo wa kudhibiti na kulinda rasirimali zetu; Isiyoweza kukemea watu wanaojichukulia madaraka na kuingia mikataba fake ya kufilisi nchi yetu.
5. Mfahamishe kuwa akiwa kichwa ngumu katiba kwa namna yoyote na kwa kipindi chochote kile itapatikana na yeye atahukumiwa na historia kwa kufanya usanii kwenye maswala muhimu ya ukombozi wa taifa letu.
Hadi hapo nawasilisha,naomba mawazo yenu waheshimiwa!