Baada ya kurejea toka Afrika kusini alikokuwa anatibiwa baada ya kufanyiwa unyama na watu wa TISS,Ulimboka anataka kufanya kile waingereza wanachoamini kuwa ni sawa na Grave mistake. Niliwahi kushauri siku chache kabla hajarejea kuwa mara atakapotua tu uwanja wa ndege wa JKNIA atuambie kwa ufasaha wale waliomteka na kumtesa. Kitendo cha kuendelea kukaa kimya hakiwezi kumuacha salama. Iwe ametishwa,amehongwa ama ameogopa yeye mwenyewe. Jambo moja litakalomtokea kwa yeye kuendelea kukaa kimya ni kuuawa. Ajue kila kukicha majitu ya TISS yanapanga namna ya kummaliza. Kama anafikiri natania akaulize kilichomtokea mkosoaji mashuhuri wa Kenya wakati wa utawala wa Moi ambapo baada ya mitego mingi ya kumuua kugonga mwamba alitekwa na watu wa usalama, akauawa na hatimaye kumwagiwa acid mwili mzima na kutupwa msituni. Aliokotwa na wawindaji ambao walitoa taarifa polisi na mwili wake kupelekwa mochwari. Wakati mhudumu wa mochwari akiuandaa mwili wa marehemu alikuta kitambulisho na ndipo alipogundua kuwa alikuwa ni Muruiki ambaye siku chache alikuwa amepotea. Mhudumu yule alituma sms kwa mmoja wa wabunge wa upinzani wakati bunge likiendelea. Moto uliwaka katika bunge la Kenya. Mpaka leo Muruiki ni marehemu na hakuna aliyekamatwa.
Ulimboka, Don'nt do what the British call as Grave Mistake. Usiposema sasa utakufa hakika. Tafakari.
Ulimboka, Don'nt do what the British call as Grave Mistake. Usiposema sasa utakufa hakika. Tafakari.