Ushauri kuhusu Nissan march k12

rajabkisauti

JF-Expert Member
Aug 16, 2015
566
314
Kama kichwa kinavyo sema hapo juu nataka kununua gari aina ya nissan march ila nataka ushauri vip kuhusu spare,ulaji wa mafuta,high way stability,speed na uimara.
b021a2040d3dbf4304e2e54994e9b76a.jpg
47325fa3ddb89e0e1587e8f86185cc14.jpg
 
Ndugu yangu Nissan March mm ninako, kiukweli gari hizi ni sawa na ndoa ya Kikristo. Ukitaka kuiuza hutopata mteja.na Spea zake ziko juu kidogo na sio nyingi sana.
Nissan March iko poa mbona. Sema wewe utakuwa unakauzia bei ya Almasi au Dhahabu... Uza bei ya kawaida uone kama hakanunuliwi fasta...
 
Sasa mkuu hicho kigari highway unaenda nacho wapi au kliniki? Usitushughulishe ubongo kanunue gari ya maana kama unataka bana matumizi nunua bajaj itafaa sana
 
Viko poa ila vikianza kuchoka huwa vinavujisha oil kwenye cylinder head sijui tatizo ni nini?
 
Kama kichwa kinavyo sema hapo juu nataka kununua gari aina ya nissan march ila nataka ushauri vip kuhusu spare,ulaji wa mafuta,high way stability,speed na uimara.
b021a2040d3dbf4304e2e54994e9b76a.jpg
47325fa3ddb89e0e1587e8f86185cc14.jpg



Kutokana na uzoefu wangu
usinunue gari aina hii NISSAN MARCH, Passo usinunue...hata Extrail usinunue
Nunua gari za aina ya toyota...
VITZ za aina zote nunua, Raum, Ist etc....

Nissan march kama alivyosema mshauri mwingine spare ni ghali ila yategemea na kipato chako, pili haliuziki...
Passo sio imara...
Magari ya toyota ndio mpango mzima.

Wkt unanunua gari angalia sana baadhi ya vitu...kama ulaji wa mafuta, Engine yake ni aina gani, Uimara...rangi..kama ni used ni ya mwaka gani...hivyo ndivyo muhimu...
 
Nimewahi kuwa nayo kwa muda wa miezi 8. Nakiri kabisa ni gari nzuri sana, ulaji wa mafuta ni mzuri, very stable barabarani. Kwa highway nilikuwa na uwezo wa kwenda 140-160kph. Spare zake ni ghali kdg lkn durable for long time. Sikuwahi kuijutia gari hii. Ila angalizo unaponunua kwa mtu hasa hapa nchini kuwa makini sana. Hasa kwenye miguu ya mbele. Ugonjwa wake mkubwa uko hapo. All the best...
 
Kama una mwembe wa kushindia nyumbani kwako basi nunua Nissan March, ikianza ugonjwa wa kugonga kwenye Engine basi utakuwa unashinda kwenye mwembe na kubadilisha mafundi utakavyo, kweli kiwese ni kunusa tu upo Morogoro
Mmmmmh! Yuko morogoro na misukosuko kibao
 
Back
Top Bottom