Ushauri kuhusu Kilimo cha Umwagiliaji

josam

JF-Expert Member
Nov 22, 2011
2,241
1,031
Ndg wanajamvi, natumai hamjambo.

Ninahitaji mshauri katika mambo ya kilimo cha umwagiliaji. Contact me via inbox.
Karibu na asante sana,
Josam
 
Ndg wanajamvi, natumai hamjambo.

Ninahitaji mshauri katika mambo ya kilimo cha umwagiliaji. Contact me via inbox.
Karibu na asante sana,
Josam
Sema ni ushauri gani unataka au umekwama wapi ili tuweze kukupa ushauri
 
Ninahitaji ushauri/ taarifa nyingi juu ya aina gani ya umwagiliaji unao stahili, kujua vifaa vya umwagiliaji na gharama zake, mahali vinapo patikana, chanzo sahihi cha umeme (hakuna umeme wa Tanesco), je itumike water pump ya petrol au diesel, au windmill au solar energy? Na ninacho hitaji ni kupump maji kwenda kwenye tank reservoir iliuopo kwenye higher elevated area kisha kumwagilia mashamba kwa kutumia normal gravitation. Mpaka hapo umenisoma mtaalamu?
 
Mazao yanayo hitaji kumwagiliwa ni mashamba ya Kahawa, migomba, maharagwe na mahindi. Kila kimoja kinajitegemea
 
Ninahitaji ushauri/ taarifa nyingi juu ya aina gani ya umwagiliaji unao stahili,
Mazao yanayo hitaji kumwagiliwa ni mashamba ya Kahawa, migomba, maharagwe na mahindi. Kila kimoja kinajitegemea
Kabla sijakujibu swali lako, je unachanzo cha maji cha uhakika?? je ni kipi?

Vipi kuhusu ardhi, je iko kwenye muinuko au tambarare?

je hayo mazao yamelimwa sehemu moja au kila zao na plot/shamba lake?

nijibu tuendelee

Karibu
 
Kabla sijakujibu swali lako, je unachanzo cha maji cha uhakika?? je ni kipi?

Vipi kuhusu ardhi, je iko kwenye muinuko au tambarare?

je hayo mazao yamelimwa sehemu moja au kila zao na plot/shamba lake?

nijibu tuendelee

Karibu

Chanzo cha maji kilichopo ni tingatinga na kitakacho fanyika ni kuchimba Kisima kandokando ya tingatinga hilo. Maji ni ya uhakika.
Ardhi ni tifutifu kuna sehemu nyingine udongo umechanganyikana na changalawe ndogondogo. Shamba lipo kwenye mwinuko.
Kahawa na maharagwe yamelimwa ktk shamba moja. Plot ya shamba la Migomba imelimwa na maharagwe pia. Kuna plot ya maharagwe peke yake. Mikakati ya baadaye; Mahindi kulimwa plot yake pekee, kulima mazao ya vitunguu, nyanya, kabeji, miti ya matunda nk. Hivi vitalimwa ktk plot zinazo jitegemea pekee.
 
Chanzo cha maji kilichopo ni tingatinga na kitakacho fanyika ni kuchimba Kisima kandokando ya tingatinga hilo. Maji ni ya uhakika.
.
Kama maji ni ya uhakika basi ni vyema
Ardhi ni tifutifu kuna sehemu nyingine udongo umechanganyikana na changalawe ndogondogo. Shamba lipo kwenye mwinuko.
hapa unauwezekano wa kutumia drip irrigation.\
Kahawa na maharagwe yamelimwa ktk shamba moja. Plot ya shamba la Migomba imelimwa na maharagwe pia. Kuna plot ya maharagwe peke yake. Mikakati ya baadaye; Mahindi kulimwa plot yake pekee, kulima mazao ya vitunguu, nyanya, kabeji, miti ya matunda nk. Hivi vitalimwa ktk plot zinazo jitegemea pekee.
Je hukomvua zikoje?? sijajua una capital kiasi gani kwa ajili umwagiliaji ila kwa hali ya shamba ilivyo na hali halisi ya huko... ushauri wangu ni kama ifwatavyo:
1. Njia za umwagiliaji.
Kwa sababu hakuna umeme, nakushauri utumie drip irrigation ya tank (by gravity), chakufanya uwe na pump yoyote utayotumia kujaza maji kwenye tank lako ambalo litakua juu kwa urefu flani, then kutoka kwenye tank utayapeleka shambani kwa drip system. Katika maelezo yako umesema una uwezo wa kupata pump ya solar au wind, japo zitakua na gharama kubwa kiasi ya kuanzia, ila ukipata moja wapo itakua msaada mkubwa kwako kwa muda mrefu!! incase ukiwa na pump ya solar au wind yenye uwezo mkubwa unaweza unganisha hata spinkler irrigation system (japo sishauri sana uitumie hii katika shamba lenye mwinuko).

Drip itakufaa sana kwenye mazao kama maharage, mahindi, nyanya, kabeji na mazao yote ya muda mfupi. Lakini simaanishi kwamba huwezi tumia drip kwenye kahawa na migomba la hasha...

Tofauti na drip, kwa sababu umesema huko hamna umeme na kuna chanzo cha uhakika cha maji, unaweza pia tumia furrow irrigation (umwagiliaji wa mifereji) hasa kwa mimea kama kahawa na migomba!

Je pump yako ya maji ina uwezo gani?

Usisite kuuliza kama una swali, karibu!
 
Ndg Upepo wa pesa,
Ninakushukuru sana kwa maelezo yako. Nita rudi kwako baada ya kuamua ni njia gani nitumie kati ya Drip au Sprinkler. Pump sijanunua lakini itakuwa na uwezo wa kupump maji kati ya lita 1000-1200 kwa saa.
 
Wapi naweza kupata vifaa (fittings) kwa ajili ya drip irrigation system au sprinkler system?
 
Nitafute nadhani nitakupa ushauri pamoja na huduma zote unazotaka..
Niko full kuanzia drip system za aina tatu na Solar Water Pump

0757065007/0688105073
 
Ndg wanajamvi, natumai hamjambo.

Ninahitaji mshauri katika mambo ya kilimo cha umwagiliaji. Contact me via inbox.
Karibu na asante sana,
Josam
Nitafute nadhani nitakupa ushauri pamoja na huduma zote unazotaka..<br />Niko full kuanzia drip system za aina tatu na Solar Water Pump pia Diesel/Petrol water pump ntakuagizia supplier mzuri kwa bei nafuu
0757065007/0688105073
 
Nitafute nadhani nitakupa ushauri pamoja na huduma zote unazotaka..<br />Niko full kuanzia drip system za aina tatu na Solar Water Pump pia Diesel/Petrol water pump ntakuagizia supplier mzuri kwa bei nafuu
0757065007/0688105073
Nimekusoma man
 
Back
Top Bottom