Ronal Reagan
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 5,299
- 3,055
Wanabodi,
Wimbi la CCM kuendelea kudhoofika na kukataliwa na jamii limeendelea kuthihirika si tu ktk chaguzi bali hata ktk maeneo mengine ya jamii.
Kwa taarifa za uhakika nilizonazo mbali na fedha za walipa kodi kufujwa ktk, kutisha watu kwa kesi za ajabu ajabu ....CCM na serikali yake wasivyo na aibu wamekwenda mbali hata kuwashinikiza walimu wa shule binafsi (English Medium) 'kuonesha utii na mshikamo' kwa ujio wa Kikwete mjini Arusha, kwa kufunga shule zao kesho Alhamisi 1/11/12 na pia kwenda kwenye maandamano na baadaye Sheikh Amri Abeid.
Ni jambo 'dogo' lenye kielelezo kipana cha jinsi ambavyo JK na CCM hawako serious na mambo ya maana kama elimu, afya, uchumi nk ila wako makini kwenye mambo ya upuuzi. Sasa kwa kukatiza vipindi vya masomo siku ya kesho:-
1) Je serikali itafidia vipi wazazi, wanafunzi na walimu?
2) Kwa vile CCM wamepoteza mvuto, utashi na uhalali wa kutawala je kuna sababu za msingi za kusubiri mpaka 2015?
3) Hivi kuna haja gani ya kufuja mamia ya mamiliioni kuandaa sherehe ambazo hazina tija kwa Mtanzania? Mbona viongozi hao wamekosa huruma, weledi na maono kiasi hiki; badala ya kuwekeza ktk kutatua kero za msingi za maji, afya, barabara ambazo zina umri wa utawala wa CCM, wao ni kutumbua bata mbele ya walala hoi.
Mwisho,
Nawomba wabunge wa upinzani akina Mnyika, Lissu, Zitto na wengine muangalie namna ya Bunge kuiwajibisha serikali sikivu ya CCM kwa kuendelea kuididimiza nchi hii. Asasi za kiraia nazo ziishinikize serikali hii tusirudi enzi zile za chama kushika hatamu.
Wimbi la CCM kuendelea kudhoofika na kukataliwa na jamii limeendelea kuthihirika si tu ktk chaguzi bali hata ktk maeneo mengine ya jamii.
Kwa taarifa za uhakika nilizonazo mbali na fedha za walipa kodi kufujwa ktk, kutisha watu kwa kesi za ajabu ajabu ....CCM na serikali yake wasivyo na aibu wamekwenda mbali hata kuwashinikiza walimu wa shule binafsi (English Medium) 'kuonesha utii na mshikamo' kwa ujio wa Kikwete mjini Arusha, kwa kufunga shule zao kesho Alhamisi 1/11/12 na pia kwenda kwenye maandamano na baadaye Sheikh Amri Abeid.
Ni jambo 'dogo' lenye kielelezo kipana cha jinsi ambavyo JK na CCM hawako serious na mambo ya maana kama elimu, afya, uchumi nk ila wako makini kwenye mambo ya upuuzi. Sasa kwa kukatiza vipindi vya masomo siku ya kesho:-
1) Je serikali itafidia vipi wazazi, wanafunzi na walimu?
2) Kwa vile CCM wamepoteza mvuto, utashi na uhalali wa kutawala je kuna sababu za msingi za kusubiri mpaka 2015?
3) Hivi kuna haja gani ya kufuja mamia ya mamiliioni kuandaa sherehe ambazo hazina tija kwa Mtanzania? Mbona viongozi hao wamekosa huruma, weledi na maono kiasi hiki; badala ya kuwekeza ktk kutatua kero za msingi za maji, afya, barabara ambazo zina umri wa utawala wa CCM, wao ni kutumbua bata mbele ya walala hoi.
Mwisho,
Nawomba wabunge wa upinzani akina Mnyika, Lissu, Zitto na wengine muangalie namna ya Bunge kuiwajibisha serikali sikivu ya CCM kwa kuendelea kuididimiza nchi hii. Asasi za kiraia nazo ziishinikize serikali hii tusirudi enzi zile za chama kushika hatamu.