Ushahidi: Kikwete anakumbatia watoa/wala rushwa

255Texter

Senior Member
Aug 31, 2007
150
8
Kwa siku nyingi wananchi wa Tanzania tumekuwa tukisikia madai kwamba Rais wa nchi ni mtetezi au ni swahiba au anakumbatia watu wanasadikika kuhusika na vitendo vya rushwa, lakini madai hayo yamekuwa yakikanushwa na watu mbali mbali katika serikali na ndani ya CCM.

Lakini hivi karibuni tumeona kwa uthibitisho, vitendo ambavyo vinaashiria bila kupingwa kwamba kiongozi huyu wa CCM ambaye anataka aongezewe muda mwingine wa miaka mitano ya uraisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni kigeugeu inapokuja swala la kuonesha msimamo dhidi ya vitendo vya rushwa na wahusika wa vitendo hivyo. Uthibitisho wa picha na taarifa za wanahabari zimeonesha jinsi JK alivyowapigia chepuo tena bila aibu, wahusika wa vitendo vya rushwa kama Bw. Basil Mramba na Bw. Edward Lowassa, huku akimsafisha bila wasiwasi Bw. Lowassa toka ile kashfa ya Richmond.

Sasa, cha ajabu kupita vyote, ni pale JK ambaye ni mwenyekiti wa CCM na ndiye aliyeongoza vikao vya NEC-CCM ambayo alitoa 'hukumu' dhidi ya watu mbalimbali akiwamo Bw. Frederick Mwakalebela ambaye alienguliwa toka nafasi ya kugombea ubunge wa Iringa mjini kwa madai kwamba alihusika katika rushwa. Bw. Mwakalebela hivi sasa anakabiliwa na mashtaka ya kuhusika na vitendo vya rushwa, mashtaka ambayo pia yanamkabili na mkewe.

Cha kustaajabisha ni kwamba huyu huyu mtuhumiwa wa rushwa ambaye CCM amemhukumu na kumuondoa kabisa katika nafasi ya kugombea ubunge, leo amekuwa ni mtu wa kukumbatiwa na JK.

Ingawa mimi na wewe ambao tunaamini utawala wa sheria na haki ya kila binadamu, Bw. Mwakalebela tunamchukulia kwamba hana hatia hadi hapo itakapothibitishwa na mahakama kwamba kweli alihusika na vitendo vya rushwa na kuhukumiwa. Hivyo, mimi binafsi simhukumu. Ila NEC-CCM na huyu JK tayari walisha muona huyu bwana hafai, kwamba ni mtoa rushwa na ndiyo maana wakamuengua. Sasa huu unafiki wa JK kumkumbatia mtoa rushwa unaashiria nini? Je, ni mwendelezo wa kile kitabia cha JK cha kujichanganya na watoa rushwa? Au hii ndiyo inaashiria kwamba kesi ya Mwakalebela itapigwa zengwe na jamaa ataachiwa huru, kwa sababu ni "mwenzetu" ?

Waingereza wanasema - picture speaks louder than words.

Rais mkumbatia watoa rushwa(according to NEC-CCM).


mwakale-1.jpg

mwakale-2.jpg
 
Hapa ndipo CCM inatuchanganya na kutuona hatuna akili kabisa.chenge ana tuhuma nzito kuhusu rada na madudu mengine lakini yupo kwenye kamati ya maadili ya chama.Mramba ana case mahakamani,aliyempeleka mahakamani anasimama na kumnadi.Naamini JK anajua makosa yao vizuri ila hana ujasiri wa kuwatema na naamini kuna njia nyingine anayotaka kutumia kuwatelekeza lakini kwa gharama za walipa kodi kwani kuna chaguzi ndogo zitakuja kwa uzembe wake.
Nimesoma humu ndani ya kuwa Bashe nae ameteuliwa kuwa kampeni manager wa chaguo la Bi Mkubwa (WAMA), ni vituko.
 
Mkuu 255 kama ulikuwa kichwani kwangu, I was thinking on the same page!!!!!!!!!!! Yaani huyu JK busara ni sufuri kabisa!!!!!!!
 
Ana uchu mkubwa sana wa madaraka!!!!!!

Halafu eti unategemea mahakama itakuwa huru kwenye kesi hiyo kwa mazingira kama haya. Damn! hapa ndiyo umuhimu wa debate unapokuja haya yalikuwa ni maswali ambayo angeulizwa tuusikie umakini wake. But this guy will be there in the records as the worst presdaa ever!!!!
 
Ni pigo kubwa kwa Hoseah!!! Anangoja nini kujiuzulu? Lakini kwa kuwa naye ni kibaraka, sidhani kama analielewa vyema hili.
 
Ni pigo kubwa kwa Hoseah!!! Anangoja nini kujiuzulu? Lakini kwa kuwa naye ni kibaraka, sidhani kama analielewa vyema hili.
Kiwango cha nchi yetu viongozi kutowajibika kwa wananchi ni cha kutisha, na sijui mwisho wake utakuwa lini.
 
Kwa siku nyingi wananchi wa Tanzania tumekuwa tukisikia madai kwamba Rais wa nchi ni mtetezi au ni swahiba au anakumbatia watu wanasadikika kuhusika na vitendo vya rushwa, lakini madai hayo yamekuwa yakikanushwa na watu mbali mbali katika serikali na ndani ya CCM.

Lakini hivi karibuni tumeona kwa uthibitisho, vitendo ambavyo vinaashiria bila kupingwa kwamba kiongozi huyu wa CCM ambaye anataka aongezewe muda mwingine wa miaka mitano ya uraisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni kigeugeu inapokuja swala la kuonesha msimamo dhidi ya vitendo vya rushwa na wahusika wa vitendo hivyo. Uthibitisho wa picha na taarifa za wanahabari zimeonesha jinsi JK alivyowapigia chepuo tena bila aibu, wahusika wa vitendo vya rushwa kama Bw. Basil Mramba na Bw. Edward Lowassa, huku akimsafisha bila wasiwasi Bw. Lowassa toka ile kashfa ya Richmond.

Sasa, cha ajabu kupita vyote, ni pale JK ambaye ni mwenyekiti wa CCM na ndiye aliyeongoza vikao vya NEC-CCM ambayo alitoa 'hukumu' dhidi ya watu mbalimbali akiwamo Bw. Frederick Mwakalebela ambaye alienguliwa toka nafasi ya kugombea ubunge wa Iringa mjini kwa madai kwamba alihusika katika rushwa. Bw. Mwakalebela hivi sasa anakabiliwa na mashtaka ya kuhusika na vitendo vya rushwa, mashtaka ambayo pia yanamkabili na mkewe.

Cha kustaajabisha ni kwamba huyu huyu mtuhumiwa wa rushwa ambaye CCM amemhukumu na kumuondoa kabisa katika nafasi ya kugombea ubunge, leo amekuwa ni mtu wa kukumbatiwa na JK.

Ingawa mimi na wewe ambao tunaamini utawala wa sheria na haki ya kila binadamu, Bw. Mwakalebela tunamchukulia kwamba hana hatia hadi hapo itakapothibitishwa na mahakama kwamba kweli alihusika na vitendo vya rushwa na kuhukumiwa. Hivyo, mimi binafsi simhukumu. Ila NEC-CCM na huyu JK tayari walisha muona huyu bwana hafai, kwamba ni mtoa rushwa na ndiyo maana wakamuengua. Sasa huu unafiki wa JK kumkumbatia mtoa rushwa unaashiria nini? Je, ni mwendelezo wa kile kitabia cha JK cha kujichanganya na watoa rushwa? Au hii ndiyo inaashiria kwamba kesi ya Mwakalebela itapigwa zengwe na jamaa ataachiwa huru, kwa sababu ni "mwenzetu" ?

Waingereza wanasema - picture speaks louder than words.

Rais mkumbatia watoa rushwa(according to NEC-CCM).


View attachment 14097

View attachment 14098
Mwakalebela hapa amekumabtiwaje sasa? Kwani amerudishiwa tena nafasi ya ugombea? Au kule kukumbatiana wakati wa kusalimiana na kwenyewe hakutakiwi?
 
He is desparate to win the election again.

Kama anaona una umuhimu wowote katika yeye kushinda atakuhitaji hata kama wewe ni mla rushwa, mwizi, jambazi, au muuwaji.

He is so desperate
 
Jamani CCM ina double standards..kama we ni mtu wao kwa maana uko katika mtandao wa JK au mwanae au kuna kigogo wa ndani ya CCM anakulinda basi maamuzi yao juu yako ni tofauti na mwana CCM mwingine raia tuu alietokea kupendwa na wananchi bila kuwa na mtu wa kumlinda ndani ya CCM. Ndo maana kina Mramba,RA na EL wataendelea kupeta na wengine wakiangukia pua na kubaki kusubiri fadhila za u-DC!
 
hata kama ningekuwa mimi ningemkumbatia. This is politics, kuwa na kesi mahakamani si kuwa ndo umekuwa ugomvi, hayo niyakawaida. well done.
 
Binafsi naona bora kidogo ya Mwakalebela, lakini kuwapitisha Lowassa, Chenge na Mramba halafu anaenda kupigia kampeni ni utani wa hali ya juu na kuonyesha kwamba serikali ya JK si makini na anafanya mchezo wa kuigiza na hayuko serious. anawaona watz kama vichanga.
Mtu yeyote mwenye akili timamu wakiwemo wasaidizi wake including kitchen cabinet wanashangaa, mfano Mramba serilkali ya JK inamshitaki kwa rushwa halafu anaenda jukwaa anasema mchagueni huyo ndiye kiongozi safi anayefaa, simweli naona ni kama ametutukana watanzania kupita kiasi ni bora afute hizo kesi tujUe moja kuliko VIINI MACHO VYA NAMNA HII
 
Chama Cha Mafisadi, Chama Cha Majambazi, Chama Cha Mabazazi, Chama Cha Mijitu... orodha iendelee!
 
He is desparate to win the election again.

Kama anaona una umuhimu wowote katika yeye kushinda atakuhitaji hata kama wewe ni mla rushwa, mwizi, jambazi, au muuwaji.

He is so desperate

this is real what happening now to mkwere
 
Nafikiri yeye pia ni mtoa na mpokea rushwa, niyo maana anawakumbatia wenzake. Tofauti hapa ni kwamba yeye ndiye aliyeshika mpini hivyo kwa sasa hakuna wa kumchukulia hatua, labda akimaliza uongozi wake, utasikia mengi tu.
 
Back
Top Bottom