Mwana Mpotevu
Platinum Member
- Sep 7, 2011
- 3,295
- 2,500
Angalieni namna waandishi wa habari wanavyoanza kusalitiana kuhusu misimamo yao ya kususia habari za kipolisi baada ya kifo cha mwangosi. Nimeikuta hii Tanzania Daima..............................
MWANDISHI wa habari wa Radio Free Afrika mkoani Mara, Maxmilian Ngesi, amefukuzwa uanachama na Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Mara ( MRPC ) baada ya kukiuka makubalino ya chama hicho yaliyoafikiwa juzi ya kutoandika kabisa habari za Jeshi la Polisi.
Akizungumza na Tanzania Daima, Mwenyekiti wa (MRPC ) Emmanuel Bwimbo, alisema kuwa Ngesi amekiuka makubaliano ya waandishi wenzake na chama kwa ujumla baada ya kusikika akitangaza habari za Jeshi la Polisi kwa kumkariri kamanda wa polisi wa mkoa wa Mara.
Bwimbo alisema kuwa kitendo hicho kinaonyesha jinsi gani mwandishi huyo alivyokiuka makubaliano ya pamoja na kuwasaliti wenzake ambao wamekubaliana kwa pamoja kuwa hawataandika habari za jeshi hilo kutokana na kuzuiwa waandishi kutoandamana katika maandamano ambayo yaliitishwa nchini kote kulaani kitendo cha mauaji ya mwandishi wa kituo cha Chanel Ten, mkoani Iringa, Daud Mwangosi.
Alisema Ngesi kama mwanachama alitakiwa kutii maamuzi ya chama na tamko la chama chake kwa vile tamko hilo limewataka wanachama wote na siyo kwa mkoa wa Mara tu lakini pia baadhi ya mikoa imetoa matamko na misimamo hiyo lakini cha kushangaza yeye amekaidi na kwenda kinyume.
Alisema kamwe chama hicho hakiwezi kuvumilia mwandishi atakayekiuka agizo hilo na hatua ambayo imechukuliwa kwa Ngesi ni mfano kwa waandishi wengine hadi hapo tamko hilo litakapotenguliwa.
MY Take: Je watafanikiwa??
MWANDISHI wa habari wa Radio Free Afrika mkoani Mara, Maxmilian Ngesi, amefukuzwa uanachama na Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Mara ( MRPC ) baada ya kukiuka makubalino ya chama hicho yaliyoafikiwa juzi ya kutoandika kabisa habari za Jeshi la Polisi.
Akizungumza na Tanzania Daima, Mwenyekiti wa (MRPC ) Emmanuel Bwimbo, alisema kuwa Ngesi amekiuka makubaliano ya waandishi wenzake na chama kwa ujumla baada ya kusikika akitangaza habari za Jeshi la Polisi kwa kumkariri kamanda wa polisi wa mkoa wa Mara.
Bwimbo alisema kuwa kitendo hicho kinaonyesha jinsi gani mwandishi huyo alivyokiuka makubaliano ya pamoja na kuwasaliti wenzake ambao wamekubaliana kwa pamoja kuwa hawataandika habari za jeshi hilo kutokana na kuzuiwa waandishi kutoandamana katika maandamano ambayo yaliitishwa nchini kote kulaani kitendo cha mauaji ya mwandishi wa kituo cha Chanel Ten, mkoani Iringa, Daud Mwangosi.
Alisema Ngesi kama mwanachama alitakiwa kutii maamuzi ya chama na tamko la chama chake kwa vile tamko hilo limewataka wanachama wote na siyo kwa mkoa wa Mara tu lakini pia baadhi ya mikoa imetoa matamko na misimamo hiyo lakini cha kushangaza yeye amekaidi na kwenda kinyume.
Alisema kamwe chama hicho hakiwezi kuvumilia mwandishi atakayekiuka agizo hilo na hatua ambayo imechukuliwa kwa Ngesi ni mfano kwa waandishi wengine hadi hapo tamko hilo litakapotenguliwa.
MY Take: Je watafanikiwa??