Usaliti katika ndoa; Nafanyeje kusaidia familia hii

ngure mtongora

New Member
Sep 13, 2012
1
0
Hallo,JF,

Wadau naomben mawazo yen juu ya tatizo hili,
Nina mjomba wangu ambaye ana mke na watoto watatu wameishi kwenye ndoa huu sasa ni mwaka wa 4. Watoto hawa watatu waliowazaa ndan ya hii miaka wawil ni mapacha,

Hawa watoto mapacha wamekuw wakiugua mara kwa mara hali inayopelekea kulazwa sana hosptal hali hii imesababisha mjomba kukosa raha kabisa katika kutafuta tiba kamili juu ya hawa watoto ndipo mtu mmoja akamwambia kuwa mapacha hao wanaugua kwasababu yeye sio baba yao hivyo ni bora awachukue na kuwapeleka mbali ili wakue na watakapotimiza miaka miwil au mitatu awarejeshe ndo hawataugua,

Kama mjuavyo wanaume tukiambiwa usaliti juu ya mke/mpenzi tunachanganyikiwa kupita kias, ndivyo ilivyokuwa kwa mjomba alijawa na hasira na kuzamilia kwenda kumuua mke wake. Alipofika nyumbani hakumsalimia mke wake na badala yake alihoji swali moja tu ni nani baba wa hawa watoto

Mke alipomweleza kuwa ni yeye alichukua panga kutaka kumkata mlemle chumbani walimokuwa mke kuona vile ndipo alipomweleza ukweli kuwa hao watoto ni wa kaka yangu mim ambaye kamaliza chuo mwaka huu na alikuwa akiishi hapo nyumbani kwa mjomba kwa kipindi chote cha miaka mitatu alipokuwa akisoma chuo,

Kaka yangu aliposikia maneno haya alitoweka nyumbani na mpaka sasa hatujui aliko, jambo hili limezua tafrani kwenye familia na ukoo kwa ujumla,

Wadau naomba mawazo yenu nami niweze kuishauri familia nini tufanye juu ya jambo hili.
 
mmmh, hakuna la kufanya maana watoto hawawezi kumezwa useme watapotea.

Kama vipi watengane tu.

Duh, mtoto anakula mke wa mjomba?
 
Shukrani ya Punda ni mateke.

Kama kweli kitu hiki kipo, napenda kwanza kabisa kumpa pole mjomba yako, wewe mwenyewe na familia yenu yote. Kusema ukweli hii ni aibu kubwa sana iliyotokea na haitoweza kusahalika.

Kama aliyempa mimba mke (ambaye ni shangazi yenu) wa mjombaako ni kakaako, nakushauri ukaawachia wazee walio ndani ya familia wakalishughulikia tatizo hili na kulimaliza. Kama wewe ulikuwa huishi hapo nyumbani kwa mjombaako pamoja kama kakaako utasalimika. Vinginevyo umekwisha.

Kama ulikuwa unakaa hapo ni lazima utakuwa ulikuwa unajua japo hata kidogo kilichokuwa kinaendelea kati ya kakaako na shangazi. Kwa hiyo jiandae kwa maswali na majibu, kisha kufunga virago na kurudi bush. Mjomba ameaibika sana na imani imemtoka kwa wajomba zake.
 
hizi mi huwa naziita NGUMU KUMEZA TAMU KUTEMA!i see hapo huna utakachoweza kufanya,waachie wazee ndo wanaweza kuhandle hilo saga!by the way hivi kumbe hayaa mambo ya wanaume wengine hawadanganywi watoto huwa ni kweli enh?dah!moyo wa mtu ni kiza kinene kweli kweli anasemaga pacha wangu Snowball!
 
watu wengine wambea sasa kimwambia mjomba wako kuwa watoto sio wake amepata faida gani kusambaratisha familia?

Na huyo mjomba akapime si ajabu hazai...... Na kama ana uwezo wa kutungisha mimba watoto wakachekiwe DNA kujua baba halisi ni nani....

Na huyo mke mechi za nje hakikisha hayafungwi magoli, au ndo alikua anamlindia mumewe heshima baada ya kuona mimba haitungwi na miaka inaenda?
 
dah! Kweli hujafa hujaumbika

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
duh!! hii kweli noma yaani wewe unamkaribisha mtu kumbe yeye anakumegea goma lako. basi yeye mjomba akubali kuwa mke kamegwa na sasa mke lazima aondoke na akamtafute huyo kaka yako aliyempa hiyo mitoto....kweli ukiingia kwenye ndoa wee ingia ukijua utamegewa tuu mke wako.
 
duh!! hii kweli noma yaani wewe unamkaribisha mtu kumbe yeye anakumegea goma lako. basi yeye mjomba akubali kuwa mke kamegwa na sasa mke lazima aondoke na akamtafute huyo kaka yako aliyempa hiyo mitoto....kweli ukiingia kwenye ndoa wee ingia ukijua utamegewa tuu mke wako.
.
This is very controversial. Inabidi busara inayoongozwa na Mungu ndo itumike lakini kama ni mwanadamu hilo suala litakuwa gumu. Hivi ule msemo wa kitanda hakizai haramu bado ni valid ktk dunia yetu ya sasa yenye vitu kama DNA.
 
.
This is very controversial. Inabidi busara inayoongozwa na Mungu ndo itumike lakini kama ni mwanadamu hilo suala litakuwa gumu. Hivi ule msemo wa kitanda hakizai haramu bado ni valid ktk dunia yetu ya sasa yenye vitu kama DNA.

it tricky or sure but i guess hapa mke ndio inabidi tumuulize inakuwaje yeye anamegwa mpaka anapata mimba jamani. kumegwa sio kitu kipya bwana tatizo ni hiyo mpaka u actually fall pregnant.
 
Ama ilikuwa ni confession iliyotokana na hofu ya Upanga??? Hapo ndo ujue mwanamke ni nani. Ukijua mwanamke ni kiumbe gani, hutamjaribu!
 
Mtafuteni mjomba arudi home. Mbona kwetu kule migombani tunakorudi wakati wa x-mass watoto wengi sio wetu tunasaidiwa na kaka na wadogo zetu na wakati mwingine naye baba mzazi anatupia lakini hatuna noma. Ukitaka kujua panda Dar Express usishukie Arusha, telemka mkoa mmoja kabla ya Arusha hutastaajabu hili. Kawaida sana, naomba radhi ndugu zangu nimetoa siri ya kwetu.
 
Mjomba ameyataka mwenyewe. Katika Dunia ya leo alianzaje kulichukua na kuishi na dume zima (toto la dadake)?

Ulimwengu wa leo ishi na watoto wanaotokana na viuno vyako tu. Angalia sasa malipo na shukurani aliyopewa!!
 
Hallo,JF,wadau naomben mawazo yen juu ya tatizo hili,nina mjomba wangu ambaye ana mke na watoto watatu wameishi kwenye ndoa huu sasa ni mwaka wa 4 watoto hawa watatu waliowazaa ndan ya hii miaka wawil ni mapacha,hawa watoto mapacha wamekuw wakiugua mara kwa mara hali inayopelekea kulazwa sana hosptal hali hii imesababisha mjomba kukosa rah kabisa katika kutafuta tiba kamili juu ya hawa watoto ndipo mtu mmoja akamwambia kuwa mapacha hao wanaugua kwa sababu yeye sio baba yao hivyo ni bora awachukue na kuwapeleka mbali ili wakue na wtakapotimiza miaka miwil au mitatu awarejeshe ndo hawataugua,kama mjuavyo wanaume tukiambiwa usaliti juu ya mke/mpenzi tunachanganyikiwa kupita kias,ndivyo ilivyokuwa kwa mjomba alijawa na hasira na kuzamilia kwenda kumuua mke wake.alipofika nyumbani hakumsalimia mke wake na badala yake alihoji swali moja tu ninani baba wa hawa watoto mke alipomweleza kuwa ni yeye alichukua panga kutaka kumkata mlemle chumbani walimokuwa mke kuona vile ndipo alipomweleza ukweli kuwa hao watoto ni wa kaka yangu mim ambaye kamaliza chuo mwaka huu na alikuwa akiishi hapo nyumbani kwa mjomba kwa kipindi chote cha miaka mitatu alipokuwa akisoma chuo,kaka yangu aliposikia maneno haya alitoweka nyumbani na mpaka sasa hatujui aliko,jambo hili limezua tafllani kwenye familia na ukoo kwa ujumla,wadau naomba mawazo yenu nami niweze kuishauli familia nini tufanye juu ya jambo hili.
Kama vile unachoongea ni cha kweli vile
 
Back
Top Bottom