Usaliti katika mapenzi, hali gani unakuwanayo baada ya hapo!?

Uncle Jei Jei

JF-Expert Member
Jan 7, 2011
1,684
2,157
Siku hizi limekuwa jambo la kawaida watu kuongelea jinsi wanavyo wasaliti wenza wao! Wengine hutoa hata mbinu wanazotumia kutembea na wake/waume au wapenzi wa wenzao! Hivi ukishamaliza kufanya tendo la ndoa na mtu asiye wako hasa kwa wanawake! Hivi, hujisikii aibu?? Unapokutana naye au mnapokuwa nyumbani siku hiyo unamuonaje mwenzako!?, humuonei aibu kweli?? Au ndo unamdharau! Na je ikitokea akataka gemu, unafanyaje??
 
Siku hizi limekuwa jambo la kawaida watu kuongelea jinsi wanavyo wasaliti wenza wao! Wengine hutoa hata mbinu wanazotumia kutembea na wake/waume au wapenzi wa wenzao! Hivi ukishamaliza kufanya tendo la ndoa na mtu asiye wako hasa kwa wanawake! Hivi, hujisikii aibu?? Unapokutana naye au mnapokuwa nyumbani siku hiyo unamuonaje mwenzako!?, humuonei aibu kweli?? Au ndo unamdharau! Na je ikitokea akataka gemu, unafanyaje??

Ni mambo machafu na ya aibu ambayo sehemu ya jamii ya Kitanzania imedumbukia ktk dimbwi la matendo haya! Ukosefu wa maadili, malezi mabaya, utandawazi, kukuso utu na ubinadamu, kutokumuogopa na kumheshimu Mungu na kukosa mapenzi ya dhati baina ya wapenzi wawili ni sehemu ndogo ya sababu ambazo zinawafanya watu kuyatenda mambo haya bila aibu!

Nashauri ifike wakati, watoto wetu wafunzwe yafuatayo kusaidia kupunguza matatizo kama haya ktk vizazi vijavyo.
1. Tuwalee watoto ktk imani ya kufahamu kuwa Mungu yupo, then tuwafunze wamuogope na kumheshimu,
2. Tuwape watoto Malezi bora ya kijamii tukiowaonya juu ya tabia mbaya na madhara yake kwa jamii. Watawezi kubaini na kukataa maovu ukubwani maana tayari watakuwa na msingi mzuri wa malezi
3. Waelimishwe juu ya matumizi sahihi ya teknolojia na madhara yake ktk jamii kujenga na kukuza ufahamu wao

Kwa kizazi cha sasa, kila mwenye uelewa anatakiwa kupinga hali ya namna hii, najua ni kitu kigumu na kitachukua muda ila ipo siku itafika na jamii kubadilika. Tusipochukua hatua na kuendelea kukupambatia stori za namna hii tutakuwa tunaendelea kuwakumbatia watu wenye tabia hizi na kuwatia moyo waendelee na tabia hizi.


Mungu okoa kizazi chetu,

Amin.
 
Ni mambo machafu na ya aibu ambayo sehemu ya jamii ya Kitanzania imedumbukia ktk dimbwi la matendo haya! Ukosefu wa maadili, malezi mabaya, utandawazi, kukuso utu na ubinadamu, kutokumuogopa na kumheshimu Mungu na kukosa mapenzi ya dhati baina ya wapenzi wawili ni sehemu ndogo ya sababu ambazo zinawafanya watu kuyatenda mambo haya bila aibu!

Nashauri ifike wakati, watoto wetu wafunzwe yafuatayo kusaidia kupunguza matatizo kama haya ktk vizazi vijavyo.
1. Tuwalee watoto ktk imani ya kufahamu kuwa Mungu yupo, then tuwafunze wamuogope na kumheshimu,
2. Tuwape watoto Malezi bora ya kijamii tukiowaonya juu ya tabia mbaya na madhara yake kwa jamii. Watawezi kubaini na kukataa maovu ukubwani maana tayari watakuwa na msingi mzuri wa malezi
3. Waelimishwe juu ya matumizi sahihi ya teknolojia na madhara yake ktk jamii kujenga na kukuza ufahamu wao

Kwa kizazi cha sasa, kila mwenye uelewa anatakiwa kupinga hali ya namna hii, najua ni kitu kigumu na kitachukua muda ila ipo siku itafika na jamii kubadilika. Tusipochukua hatua na kuendelea kukupambatia stori za namna hii tutakuwa tunaendelea kuwakumbatia watu wenye tabia hizi na kuwatia moyo waendelee na tabia hizi.


Mungu okoa kizazi chetu,

Amin.

Ubarikiwe sana mtumishi!! Maombi yako ni dhati! Ki ukweli inatia maudhi, ndo maana nikiwauli wahusika hawaonagi aibu mbele ya watu wao?? Afadhali umeongezea, basi waöne aibu hata kwa Mungu aonae sirini!!
 
HorsePower katoa ufumbuzi wote,hakuna cha kuchangia hapa zaidi ya kumuunga mkono na kuhimizana ktk kufuata na kutekeleza ushauri wake
 
mpaka ameweza gonoka na mwengine tayari kashakudharau....so ata akija back home ni kawaida tuu
 
Back
Top Bottom