Nimeshangazwa na usafiri wa mbezi. Nilikuwa nasafiri kutoka posta mpya kuelekea mbezi kwa msuguli, nilishangaa nilipofika kituo cha posta majira ya saa 11.30 nilikuta watu wamefurika sana; bahati nzuri akatokea abiri mmoja akanishauri nihame nikapandie bus kituo cha akiba then nirudi posta halafu mbezi; nilikubali nikaondoka naye hadi akiba; pale pia kulikuwa na abiria wengi sana; nikaamua kupanda bus ya ubungo inayoingia kwanza posta; nililipa 250/= then posta nikalipa tena 250/= hadi ubungo. nilipofika ubungo nilishangaa zaidi bus nyigi zinazoanzia ubungo zinaishia kimara. ok niliingia kwenye bus ya ubungo-msata nilitoa 1000 nikamweleze konda naelekea mbezi; alifoka na kuniambia gari ya shamba hii ila inaenda kulala inaisha kimara; nikamwambia well kama itaendelea nitaendelea kama itaishia kimara sawa, alichukua 250/= tulipofika kimara pale napo watu walikuwa wengi sana alifika pale akashusha watu wote then akaaza safari upya uzuri na mimi nilifanikiwa kuingia nikalipa tena 250/ kutoka pale ile gari ilienda hadi mbezi tuliposhuka akachukua tena watu pale kuelekea kibamba kwa 200/ SAFARI KUTOKA POSTA HADI KIBAMBA 250AKIBA+250UBUNGO+250KIMARA+250MBEZI+200KIBAMBA=1200/= anayepand bus ni mshahara wa kima cha chini; KWELI ATAFIKA?:confused2: