Usafiri dar es salaam wapata uvumbuzi

Mkombozi

JF-Expert Member
Feb 19, 2008
806
426
Nampa ushauri wa bure Waziri wa Ujenzi za kuondoa kero ya foleni Dar es Salaam. Kujenga barabara kila kona sio suluhisho la kudumu, kila siku watu wanaongezeka na kuingia Dar es Salaam. Kifuatacho kifanyike

•Kujenga bandari kubwa ya nchi kavu maeneo ya kibaha au mkoa wa Pwani, then kujenga reli itakayotoka bandarini Dar moja kwa moja hadi kibaha kwaajili ya Treni ya Mizigo ya kuchukoa macontainer kutoka Dar hadi kibaha. Malori yote yaanzie Kibaha kwenda mikoani, Dar kubaki malori yanayobeba mizigo ya Dar tu. Pia Reli hii itatumika kupitia treni la abiria pia.
•Pia wafufue usafiri wa treni Dar, Moja ianzie Posta, kupitia Kariakoo, Manzese, Ubungo, Kimara, Mbezi hadi kibamba. Nyingine Kariakoo hadi uwanja ndege, Tabata.Nyingine Posta, Mwenge, Mbezi beach, Tegeta, book bunju.
•Kuanzisha usafiri wa Makampuni ili kuimarisha usafiri wa uma, vigari vidogo vyote kuondolewa.
•Magari binafsi yapungue hasa sehemu zenye treni.

Hizi mbinu ni za kudumu, ujenzi wa barabara sio suluhisho sana. Pia usafiri imara na wa uhakika itapunguza kasi ya watu kuagiza magari au kutumia magari yao kwenda mjini.
 
Naunga mkono, hoja Dawa ni kuimarisha public transport iwe bora na ya uhakika, jenga underground metro train, na mabasi makubwa ya abiria yawe kwa style ya kampuni , hakuna nchi yenye watu wengi kama china lakini wameweza ku control foleni kwa kuwa na reliable public transport, watu wengi wata opt kutumia public transport kwa sababu ni reliable and cheap kuliko kutumia private transport. huo mradi wao wa BRT umefia wapi?

Dar es laam ni mji wa Bahari wanatakiwa kujenga a lot of piers ili watu wa kawe, mikocheni, mbweni, tegeta, mbezi, temeke waweze kutumia speed boat au ferries kuja mjini posta, tena hiyo ni rahisi kabisa ku implement, serikari ijenge hizo piers iwe inakusanya ushuru lakini uendeshaji wa hizo ferries wapatiwe makampuni binafsi kama mawili hivi au matatu na yawe regurated to keep the fare reasonable
 
Nampa ushauri wa bure Waziri wa Ujenzi za kuondoa kero ya foleni Dar es Salaam. Kujenga barabara kila kona sio suluhisho la kudumu, kila siku watu wanaongezeka na kuingia Dar es Salaam. Kifuatacho kifanyike

•Kujenga bandari kubwa ya nchi kavu maeneo ya kibaha au mkoa wa Pwani, then kujenga reli itakayotoka bandarini Dar moja kwa moja hadi kibaha kwaajili ya Treni ya Mizigo ya kuchukoa macontainer kutoka Dar hadi kibaha. Malori yote yaanzie Kibaha kwenda mikoani, Dar kubaki malori yanayobeba mizigo ya Dar tu. Pia Reli hii itatumika kupitia treni la abiria pia.
•Pia wafufue usafiri wa treni Dar, Moja ianzie Posta, kupitia Kariakoo, Manzese, Ubungo, Kimara, Mbezi hadi kibamba. Nyingine Kariakoo hadi uwanja ndege, Tabata.Nyingine Posta, Mwenge, Mbezi beach, Tegeta, book bunju.
•Kuanzisha usafiri wa Makampuni ili kuimarisha usafiri wa uma, vigari vidogo vyote kuondolewa.
•Magari binafsi yapungue hasa sehemu zenye treni.

Hizi mbinu ni za kudumu, ujenzi wa barabara sio suluhisho sana. Pia usafiri imara na wa uhakika itapunguza kasi ya watu kuagiza magari au kutumia magari yao kwenda mjini.

Seconded.
Wasiwasi wangu hawa jamaa huwa hawafanyii kazi vitu vya msingi kama hivi ulowapa. Hili lingekuwa ni suluhisho la kudumu na si kwa usafiri tu hata makazi, watu wangeenda kujenga makazi bora huko nje ya mji na kuacha kuishi kwenye chumba kimoja Sinza, Tandale, Manzese
 
hihii sio Suluisho la sasa , kama ungeusisha Kuhama kwa Wizara kwenda Dodoma ua Taasisis za fedha kuamia Bagamoyo , barabara za ndani kama Mwananyamala kwenda kijitonyama kuunganisha na sinza, barabara zote za kijitonyama kupigwa lami ili ziweze kupitika kwa urahisi , surender Bridge kupanuliwa kuwa njia nne au kuweka bara bara ya juu kama ikiwezekana , sio kuwa dar kuna magari mengi bali mpangilio tu
 
Back
Top Bottom