Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
....."Hatua ya Rais Kikwete kumpongeza Kilango ni pigo kubwa kwa kundi la wana CCM wanaodaiwa kujihusisha na vitendo vya ufisadi na imekuja wakati chama hicho kimegawanyika katika makundi mawili, lile linalotuhumiwa kwa ufisadi na lile la wanaoongoza mapambano dhidi yao, akiwamo mbunge huyo wa Same Mashariki.
Rais Kikwete aliielezea tuzo hiyo kama ni tunda linalotokana na Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005 kuhusu vita dhidi ya rushwa......."
*******************
Ina maana anakubaliana na yote AK aliyokuwa akiyasema Bungeni? Kama vile, kwa mfano, fedha za EPA "zinazorejeshwa" lazima zionekane halisi (physically) na ikiwezekana ndani ya viroba ili wote wazione?
Sasa JK mbona hajawahakikishia wananchi hilo limetendeka -- yaani nani karejesha ngapi na lini? Au anampaka mafuta mama wa watu?
Ilipasa JK mwenyewe ndiyo angekuwa shujaa katika vita ya ufisadi kwa kunasa tuzo kama hiyo (iwapo Wamarekani wanayo kwa ajili ya wanaume pia), na siyo kungojea mtu mwingine apate ndiyo ampongeze! Anampongeza nini kwa mambo ambayo JK mwenyewe angeweza kuyasemea na kuwa na uwezo wa kuyatimiza?