US honours Kilango


....."Hatua ya Rais Kikwete kumpongeza Kilango ni pigo kubwa kwa kundi la wana CCM wanaodaiwa kujihusisha na vitendo vya ufisadi na imekuja wakati chama hicho kimegawanyika katika makundi mawili, lile linalotuhumiwa kwa ufisadi na lile la wanaoongoza mapambano dhidi yao, akiwamo mbunge huyo wa Same Mashariki.

Rais Kikwete aliielezea tuzo hiyo kama ni tunda linalotokana na Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005 kuhusu vita dhidi ya rushwa......."


*******************

Ina maana anakubaliana na yote AK aliyokuwa akiyasema Bungeni? Kama vile, kwa mfano, fedha za EPA "zinazorejeshwa" lazima zionekane halisi (physically) na ikiwezekana ndani ya viroba ili wote wazione?

Sasa JK mbona hajawahakikishia wananchi hilo limetendeka -- yaani nani karejesha ngapi na lini? Au anampaka mafuta mama wa watu?

Ilipasa JK mwenyewe ndiyo angekuwa shujaa katika vita ya ufisadi kwa kunasa tuzo kama hiyo (iwapo Wamarekani wanayo kwa ajili ya wanaume pia), na siyo kungojea mtu mwingine apate ndiyo ampongeze! Anampongeza nini kwa mambo ambayo JK mwenyewe angeweza kuyasemea na kuwa na uwezo wa kuyatimiza?
 
JK ni hypocrite tu

Aka msanii/nyoka/popo/kinyonga/mnafiki/etc. Hawezi kutambua mchango wa Anna Kilango wakati bado kuna mafisadi wanadunda mtaani na hakuna jitihada za maksudi kuwashughurikia. Hawezi kudanganya umma kuwa ni ilani ya CCM ya 2005 kupambana na rushwa/mafisadi ikizingatiwa JF ndio waanzilishi na wafichuaji wa ufisadi wakifuatiwa na opposition parties kurusha live bungeni. Kama rais appreciation yake kwa Kilango/watanzania kwa ujumla ilikuwa ni kuonyesha jitihada za makusudi kuwashughurikia mafisadi sio mpaka alaazimishwe sana halafu bado anatupiga changa la macho
 
Rais Kikwete ampongeza Anna Kilango kwa ujasiri dhidi ya ufisadi

Na Leon Bahati,

MWANANCHI, March 29, 2009

RAIS Jakaya Kikwete amempongeza Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango kwa kutunukiwa tuzo ya kimataifa ya Mwanamke Jasiri kwa mwaka 2009 na kwamba, ni ishara ya dunia kuutambua mchango wake katika kupambana na ufisadi nchini.


Taarifa iliyotolewa jana na Ikulu kwa vyombo vya habari, ilielezea kuwa Rais Kikwete alipokea kwa furaha kubwa habari za Kilango kutunukiwa tuzo hiyo.


Wiki hii, Kilango ambaye amekuwa mkali kwa kauli mbalimbali dhidi ya ufisadi, alikabidhiwa tuzo hiyo na Kaimu Balozi wa Marekani nchini, Larry André.


Tuzo hiyo ya mwaka ilianzishwa kwa lengo la kutambua na kuthamini mchango wa mwanamke aliyeonyesha ujasiri wa kiwango cha juu na uongozi mzuri.??Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania ulimteua Kilango kuwa mmojawapo kati ya washiriki waliowania Tuzo ya Kimataifa ya Mwanamke Jasiri ya Mwaka 2009, kutokana na ujasiri aliouonyesha katika kukosoa na kuupa changamoto uongozi wa chama chake ili uweze kushughulikia kikamilifu suala la rushwa. ??Kwa kufanya hivyo alivunja utamaduni wa kisiasa uliokuwa umejengeka bila kujali vitisho kwa usalama wake binafsi. Bila kuchoka wala kutetereka, alishikilia azma yake ya kupiga vita rushwa na kuuliza maswali mazito yaliyoibua mijadala iliyochangia sana katika jitihada za kuongeza uwazi na utawala bora ndani ya chama tawala.


Hatua ya Rais Kikwete kumpongeza Kilango ni pigo kubwa kwa kundi la wana CCM wanaodaiwa kujihusisha na vitendo vya ufisadi na imekuja wakati chama hicho kimegawanyika katika makundi mawili, lile linalotuhumiwa kwa ufisadi na lile la wanaoongoza mapambano dhidi yao, akiwamo mbunge huyo wa Same Mashariki.


Rais Kikwete aliielezea tuzo hiyo kama ni tunda linalotokana na Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005 kuhusu vita dhidi ya rushwa.


"…CCM na serikali yake, vimetoa fursa pana zaidi kwa wananchi, wanahabari na viongozi, wakiwemo waheshimiwa wabunge, kushiriki kikamilifu zaidi," alisema Rais Kikwete kupitia taarifa hiyo na kuongeza:


"Kutunukiwa kwa tuzo hiyo ni ishara ya kutambua na kuthaminiwa kwa mchango wako katika mapambano dhidi ya rushwa."


Kilango ambaye ni mke wa mwanasiasa mkongwe, John Malecela, alikuwa miongoni mwa wabunge waliosimama kidete bungeni Februari mwaka jana kuhakikisha kuwa viongozi waliohusika katika mkataba tata wa Kampuni ya Richmond na serikali wanaadhibiwa.


Kashfa ya Richmond ilisababisha Waziri Mkuu, Edward Lowassa kujiuzulu na mawaziri wawili, Nazir Karamagi aliyekuwa akishikilia Wizara ya Nishati na Madini na Dk Ibrahim Msabaha aliyekuwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Ni mwepesi mno kutoa pongezi lakini yeye mwenyewe juhudi zake katika mapambano dhidi ya mafisadi hazionekani kabisa. JK why are missing in action!? :confused:
 
Jamani labda mimi ni kipofu, naomba mtu yeyote aorodheshe mambo angalau matano ya ushujaa aliyofanya huyu tunayeambiwa ni shujaa.

Kama kupiga kelele za kiusanii kujijengea jina ni ushujaa, basi tumekwisha.
 
Jamani labda mimi ni kipofu, naomba mtu yeyote aorodheshe mambo angalau matano ya ushujaa aliyofanya huyu tunayeambiwa ni shujaa.

Kama kupiga kelele za kiusanii kujijengea jina ni ushujaa, basi tumekwisha.

Wewe si kipofu. Kama ungekuwa kipofu usingeona hii posti. Jukwaa la mbunge ni bungeni.
 
Wewe si kipofu. Kama ungekuwa kipofu usingeona hii posti. Jukwaa la mbunge ni bungeni.

- This is what we call kumkoma nyani giladi, bila ya kumuangalia usoni!

- Labda Mkulu naye aonyeshe aliyokwisha yafanya kwa taifa, zaidi tu ya matusi kila kukicha hapa JF!

FMES!
 
anna kilango nyange malecela alifukuzwa kazi kwa kosa la kuiba fedha za mwajiri wake--gulf air. anapiga kelele ili apewe madaraka apate nafasi ya kuiba. same mashariki tumeingia hasara kumchagua kuwa mbunge.
 
anna kilango nyange malecela alifukuzwa kazi kwa kosa la kuiba fedha za mwajiri wake--gulf air. anapiga kelele ili apewe madaraka apate nafasi ya kuiba. same mashariki tumeingia hasara kumchagua kuwa mbunge.

Naomba uanzishe thread nyingine katika celebrities forum na uje na evidence siyo kuweka vitu loosely, maana kama ni kuchafuana kuna ze utamu website wanapofanya kazi hii, lakini JF tunataka analysis.
Gulf Air imefungwa na haipo tena so it is easy kuitaja, pia kugeneralize kwamba anaiba haieleweki kwani hujasema aliiba nini na kitu gani. Acha personal attacks on people.
 
Back
Top Bottom