Urithi unaenda kwa nani?

JosephElly

JF-Expert Member
Jun 5, 2012
2,432
1,034
Endapo baba akifariki akaacha watoto wawili wakike (18+) na wakiume (18+), lakini hajaacha wosia uridhi wa ardhi ya marehemu itaridhiwa na mtoto yupi? Au watoto wote?

Je endapo marehemu akiacha wosia wa kumuachia mali yote mtoto mmoja tu wakiume, mahakama inaweza vunja wosia endapo watoto wengine wa marehemu wakifungua kesi ya madai?
 
Endapo baba akifariki akaacha watoto wawili wakike (18+) na wakiume (18+), lakini hajaacha wosia uridhi wa ardhi ya marehemu itaridhiwa na mtoto yupi? Au watoto wote?

Je endapo marehemu akiacha wosia wa kumuachia mali yote mtoto mmoja tu wakiume, mahakama inaweza vunja wosia endapo watoto wengine wa marehemu wakifungua kesi ya madai?
Familia iliyofiwa itagawana mirathi kulingana na aidha itikadi/imani ya dini yao, au watatumia mahakama kuhamua jinsi ya kugawana mali, wakati mwingine sheria za kimila utumika katika kugawana urithi. Kumbuka kwamba urithi ni haki ya kila mtoto aliye hai.

Kwa swali lako unabidi ufafanue, mirathi hiyo inatakiwa kugawanywa kwa utaratibu upi?
 
Ni vizuri hii mada ungeipost JF jukwaa la sheria,nadhani ungepata ushauri,kwani kule ndio mahala pake.
 
inategemeana na aina ya sheria itakayotumika kugawa mirathi hiyo. kuna aina tatu zinazotumika, kwa kifupi, kuna mirathi inayogawanya kwa dini ya kiislam, mirathi kugawanywa kimila na ile kiserikali. yaani either kutumia sheria ya kiislam, kutumia sheria za kimila na kutumia sheria ya kiserikali yaani Indian succession Act ya mwaka 1885. kama watawaganya kwa kutumia sheria ya kiselikali, basi wasichana na wavulana watagawanywa kihalali bila kubaguana kwenye gender.hii ndo sheria isiyo na matatizo. kama ni kiislam itagawanywa kwa quran, kama ni kimilia, kwa kifupi ni kwamba, wanawake huwa hawamiliki ardhi/nyumba ila wanaweza kuruhusiwa kuishi ndani hadi pale watakapoolewa. sheria ya kimila ina matatizo sana. kuchagua sheria huwa kuna kipimo kupima kama marehemu alikuwa anaishi maisha ya aina gani. watu wengi wa vijijini huwa wanadhaniwa kuwa waliishi kwa kimila labda utoe ushahidi mpya kubatilisha hilo, wale walioishi miijini muda mrefu na hawakuwa wanafuata mila na desturi katika maisha yao huchukuliwa kama waliishi maisha ya kisasa hivyo sheria ya kiserikali itatumika, wale waliokuwa wanaishi maisha ya kiislam sheria ya kiislam itatumika. mjane anapata 1/8 na iliyobaki wanagawana warithi wengine kama watoto na ndugu wa karibu. sheria ya kiserikali inaweza isigawe mali kwa ndugu wakati mwignine, mali zikaenda kwa watoto.
 
Opps... Naona nimeipost hapa kwa bahati mbaya .... Msaada mod kunihamishia jukwaa :sorry:
but ninaongelea endapo sheria za mahakama zitatumika
 
Opps... Naona nimeipost hapa kwa bahati mbaya .... Msaada mod kunihamishia jukwaa :sorry:
but ninaongelea endapo sheria za mahakama zitatumika

Mahakama inaamuwa? mahakama haiamui mahakama inahukumu. Mjiamulie nyie mnataka sheria ipi itumike, mkishindwa kujiamulia, mahakama itaamuwa kutokana na sheria ya Dola. Mahakama kama mahakama haina sheria.
 
Endapo baba akifariki akaacha watoto wawili wakike (18+) na wakiume (18+), lakini hajaacha wosia uridhi wa ardhi ya marehemu itaridhiwa na mtoto yupi? Au watoto wote?

Je endapo marehemu akiacha wosia wa kumuachia mali yote mtoto mmoja tu wakiume, mahakama inaweza vunja wosia endapo watoto wengine wa marehemu wakifungua kesi ya madai?
kuna dalili za kuchakachua wosia hapa
 
Hapo nimeongelea kesi mbili tofauti, endapo wosia haupo. Na endapo wosia ukiwepo.. mpalu
but napenda kufahamu endapo mahakama ndo itahusika na utoaji wa maamuzi
 
Last edited by a moderator:
Mahakama inaamuwa? mahakama haiamui mahakama inahukumu. Mjiamulie nyie mnataka sheria ipi itumike, mkishindwa kujiamulia, mahakama itaamuwa kutokana na sheria ya Dola. Mahakama kama mahakama haina sheria.

Wewe acha kupotosha mahakama inafanya maamuzi kwenye makosa ya madai na inahukumu kwenye makosa ya jinai......na kuna maamuzi yanayofanywa na mahakama ni sheria(PRECEDENT) kuna mazingira flani mahakama inatoa mwongozo unaofanana na kutunga sheria...ZOMBA kama hujakaa darasani kusoma sheria usijaribu kupotosha watu umu sheria is a noble proffessional don dare to put your politics.
 
Wewe acha kupotosha mahakama inafanya maamuzi kwenye makosa ya madai na inahukumu kwenye makosa ya jinai......na kuna maamuzi yanayofanywa na mahakama ni sheria(PRECEDENT) kuna mazingira flani mahakama inatoa mwongozo unaofanana na kutunga sheria...ZOMBA kama hujakaa darasani kusoma sheria usijaribu kupotosha watu umu sheria is a noble proffessional don dare to put your politics.

Wewe ndio katika wale waliojazwa Ubaguzi wa Ujinga. Mahakama inahukumu haiundi wala kutunga sheria, maamuzi ya mahakama ni hukumu, mahakama inaweza kuweka kanuni lakini si sheria au sharia. Usitake kupoteza watu.
 
Wewe ndio katika wale waliojazwa Ubaguzi wa Ujinga. Mahakama inahukumu haiundi wala kutunga sheria, maamuzi ya mahakama ni hukumu, mahakama inaweza kuweka kanuni lakini si sheria au sharia. Usitake kupoteza watu.

Wewe ni mbumbumbu wa sheria siwezi bishana na mimi nimekaa darasani wewe ni BUSH LAWYER.
 
hapo nimeongelea kesi mbili tofauti, endapo wosia haupo. Na endapo wosia ukiwepo.. mpalu
but napenda kufahamu endapo mahakama ndo itahusika na utoaji wa maamuzi
ndugu kama kingereza kinapanda na si mvivu wa kjisomea unaweza kupitia hapa chini
 

Attachments

  • FAMILY LAW 15.docx
    36.6 KB · Views: 595
Wewe ni mbumbumbu wa sheria siwezi bishana na mimi nimekaa darasani wewe ni BUSH LAWYER.
Ulikuwa unajazwa Ubaguzi wa Ujinga kwenye kuta nne, mwenyewe unajiona ndio umesoma. Ungekuwa unajuwa maana tu ya neno "mahakama" kuwa ni panapotolewa hukumu, usingeyasema yote hayo. Labda Kenya ndio mnatunga sheria mahakamani, nyang'au wahed wee!
 
inategemeana na aina ya sheria itakayotumika kugawa mirathi hiyo. kuna aina tatu zinazotumika, kwa kifupi, kuna mirathi inayogawanya kwa dini ya kiislam, mirathi kugawanywa kimila na ile kiserikali. yaani either kutumia sheria ya kiislam, kutumia sheria za kimila na kutumia sheria ya kiserikali yaani Indian succession Act ya mwaka 1885. kama watawaganya kwa kutumia sheria ya kiselikali, basi wasichana na wavulana watagawanywa kihalali bila kubaguana kwenye gender.hii ndo sheria isiyo na matatizo. kama ni kiislam itagawanywa kwa quran, kama ni kimilia, kwa kifupi ni kwamba, wanawake huwa hawamiliki ardhi/nyumba ila wanaweza kuruhusiwa kuishi ndani hadi pale watakapoolewa. sheria ya kimila ina matatizo sana. kuchagua sheria huwa kuna kipimo kupima kama marehemu alikuwa anaishi maisha ya aina gani. watu wengi wa vijijini huwa wanadhaniwa kuwa waliishi kwa kimila labda utoe ushahidi mpya kubatilisha hilo, wale walioishi miijini muda mrefu na hawakuwa wanafuata mila na desturi katika maisha yao huchukuliwa kama waliishi maisha ya kisasa hivyo sheria ya kiserikali itatumika, wale waliokuwa wanaishi maisha ya kiislam sheria ya kiislam itatumika. mjane anapata 1/8 na iliyobaki wanagawana warithi wengine kama watoto na ndugu wa karibu. sheria ya kiserikali inaweza isigawe mali kwa ndugu wakati mwignine, mali zikaenda kwa watoto.

Huu ndio ushauri wa kisheria kwa jinsi nnavoifahamu mimi sheria.
Isipokuwa tu hiyo India Succession Act ni ya mwaka 1865.
Ila mengine yote umepatia. Humu ndani naona Zomba na mwenzake wanabishana tu vitu visivo na msingi na kutukanana bila kujibu swali la msingi.
I‘m on mobile otherwise i would‘ve given you a ‘like‘ my fellow learned bro.
 
inategemeana na aina ya sheria itakayotumika kugawa mirathi hiyo. Kuna aina tatu zinazotumika, kwa kifupi, kuna mirathi inayogawanya kwa dini ya kiislam, mirathi kugawanywa kimila na ile kiserikali. Yaani either kutumia sheria ya kiislam, kutumia sheria za kimila na kutumia sheria ya kiserikali yaani indian succession act ya mwaka 1885. Kama watawaganya kwa kutumia sheria ya kiselikali, basi wasichana na wavulana watagawanywa kihalali
dah... Ahsante sana kwa hii info bro
 
Back
Top Bottom