denoo49
JF-Expert Member
- Mar 29, 2011
- 6,113
- 6,937
Binafsi nimekerwa sana na utoaji huduma wa hizi ofisi za usajili wa vizazi na vifo. Kuna kila dalili ya harufu ya rushwa ili uweze kupata huduma. Kipindi ofisi hizi zinaanzishwa walikuwa watoa huduma na washauri wazuri kwa mteja ila mpaka kufikia sasa kama huna "kitu" ni utazungushwa mpaka.....! Nina mifano ya dhahiri na wazi nilikutana na mwenzangu takribani ni siku ya nane sasa katika hizi ofisi tukiwa na shida ya aina moja ila mwenzangu alihudumiwa ndani ya siku moja akamaliza tatizo lake ila mimi mpaka leo hii ni mwendo wa kupigwa tarehe na kupewa sababu zisiso kuwa na msingi... mara vitabu vya kumbukumbu havionekani, mara ndani kuna joto mpaka umeme urudi tuweze kutafuta vitabu, na nyinginezo kama hizo.