Uranium Mining Projects In Tanzania: Progress...

Kwa Tanzania sidhani kama tunaihitaji teknolojia ya nyuklia kwa sasa, na niliwashangaa sana wabunge wetu walipopitisha sheria hii miaka kadhaa iliyopita. Sijajua walikuwa wanafikiria nini hasa. Nasema hivyo nikiwa na misimamo ifuatayo:

1. Usalama
Kwa jinsi hali ya usalama ilivyo tete kwa nchi masikini kama Tanzania, utunzaji wa masalia ya nyuklia kutoka katika vinu vyake hatutauweza kwa sasa, kwa sababu bado hatujaonyesha uwezo huo kwa teknolojia nyingine tulizo nazo. Mfano tumeshindwa kutunza treni zetu, ambazo teknolojia zake ni rahisi, itakuwaje kwa teknolojia tata ama hii ya vinu vya nyuklia? Tumeshindwa kutunza viwanda vinavyotumia teknolojia rahisi alivyotuachia Mwalimu Nyerere, itakuwaje kwa teknolojia tata kama hii? Tumeshindwa kutunza jenereta za dizeli tulizo nazo, nyuklia tutaiweza? Naogopa yasije yakatukuta kama yale yaliyotokea katika mji wa Chernobil nchini Urusi mwaka 1986, ambapo kutokana na uzembe wa baadhi ya watu, kinu kilivuja na kusababisha hasara na maafa ambayo bado yanadumu mpaka leo.

2. Mahitaji ya Nishati
Kwa Tanzania, bado hatujavuna nishati za maji, jua na upepo kwa matumizi ya nishati kiasi cha kulazimika kutumia nyuklia kwa kuzalisha nishati. Nasema hivi kwa sababu bado sirikali inasuasua mpaka sasa kuendeleza miradi ya nishati za nguzu ya maji kama vile mradi wa Rumakali uliopo wilayani Makete (222 Megawatt), mradi wa Stiegler's Gorge (358 Megawatt) na mwingine ulipo wilayani Njombe (100 Mgawatt). Sasa basi, iwapo tungekuwa tumeendeleza miradi yote hii mikubwa ya umeme na bado kukawa na mahitaji, basi tungekuwa na sababu mwafaka ya kufikiria teknolojia nyingine kama nyuklia, lakini kwa sasa mie naona bado sana.

3. Nguvu ya Kiuchumi Uchumi
Kwa Tanzania masikini kama hii ninayoifahamu mimi, ambayo asilimia arobaini ya bajeti yake inategemea hisani ya wafadhili kutoka nje, itakuwa ni kicheksho na mzaha kufikiria teknolojia ya nyuklia, kitu ambacho huwa kinagharimu pesa nyingi sana kukiendesha. Kama hatuwezi kujenga mitambo ya nguvu za maji ambayo ni bei rahisi, kama nilivyodokeza hapo juu, itakuwaje kwa teknolojia ya nyuklia ambayo huhitaji pesa nyingi? Huu ni mzaha, tena wawazi kabisa.

4. Nishati Mbadala
Kama nilivyodokeza hapo juu, tuna vyanzo mbadala vingi sana vya nishati kama vile nishati ya jua, upepo na mkondo wa bahari, kwa hiyo basi hakuna ulazima wowote wa kuikimbilia teknolojia ya nyuklia kwa ajili ya uzalishaji wa nishati. Itakuwa ni matumizi mabaya ya kile tulichonacho.

5. Kipaumbele
Kwa wakati huu, kuwa na mitambo ya nyuklia isiwe kipaumbele, nadhani hii pesa ambayo tunapanga kuendelezea teknolojia hii ingepelekwa katika upatikanaji wa huduma za afya, miundombinu na elimu ambavyo ndio tunavihitaji sana kwa sasa kuliko hio nyuklia.

Hitimisho
Siungi mkono kabisa Tanzania kuwa na teknolojia ya nyuklia kwa sasa. Najua huenda wanasiasa wasiyasome maoni haya na kuyapa umuhimu, lakini nashukuru kwamba nimetumia haki yangu kama Mtanzania kufikisha kwa jamii kile ninachoona kinafaa kwa taifa kwa sasa, kuliko kung'ang'ania sifa na ujiko.

Nawasilisha.
 
Viongozi wetu wakifika huku dunia ya 1 wanafikia kwenye Hotel kubwa na kula ulabu na vimwana wa kizungu halafu kesho yake wakiwa na macho ya ulevi wanatembezwa kuona technolojia. Kwa macho na akili za kilevi wanadhani kila walicho kiona ni rahisi.

Nuclear yaweza kuwa rahisi kuunda mtambo wake, lakini kamwe si rahisi ku umaintain.


Liability ya kumaintain Nuclear Power ni kubwa sana na inataka watu committed. Si ujinga ujinga huu kama wa ITPL na Richmond.
Na kurushiana mpira kama Malaya ndani ya Dangulo.

Tunaweza kuwa na Technolojia endapo tu watu wote wa Generation hii watakuwa Futi 6 chini ya Ardhi( Wamekufa).

Nuclear Power is possible but for the next generation.


Inabidi nianzishe thread tujadiliane mambo ya wajibu wa kizazi cha sasa.
 
Kwa Tanzania sidhani kama tunaihitaji teknolojia ya nyuklia kwa sasa, na niliwashangaa sana wabunge wetu walipopitisha sheria hii miaka kadhaa iliyopita. Sijajua walikuwa wanafikiria nini hasa. Nasema hivyo nikiwa na misimamo ifuatayo:

1. Usalama
Kwa jinsi hali ya usalama ilivyo tete kwa nchi masikini kama Tanzania, utunzaji wa masalia ya nyuklia kutoka katika vinu vyake hatutauweza kwa sasa, kwa sababu bado hatujaonyesha uwezo huo kwa teknolojia nyingine tulizo nazo. Mfano tumeshindwa kutunza treni zetu, ambazo teknolojia zake ni rahisi, itakuwaje kwa teknolojia tata ama hii ya vinu vya nyuklia? Tumeshindwa kutunza viwanda vinavyotumia teknolojia rahisi alivyotuachia Mwalimu Nyerere, itakuwaje kwa teknolojia tata kama hii? Tumeshindwa kutunza jenereta za dizeli tulizo nazo, nyuklia tutaiweza? Naogopa yasije yakatukuta kama yale yaliyotokea katika mji wa Chernobil nchini Urusi mwaka 1986, ambapo kutokana na uzembe wa baadhi ya watu, kinu kilivuja na kusababisha hasara na maafa ambayo bado yanadumu mpaka leo.

2. Mahitaji ya Nishati
Kwa Tanzania, bado hatujavuna nishati za maji, jua na upepo kwa matumizi ya nishati kiasi cha kulazimika kutumia nyuklia kwa kuzalisha nishati. Nasema hivi kwa sababu bado sirikali inasuasua mpaka sasa kuendeleza miradi ya nishati za nguzu ya maji kama vile mradi wa Rumakali uliopo wilayani Makete (222 Megawatt), mradi wa Stiegler's Gorge (358 Megawatt) na mwingine ulipo wilayani Njombe (100 Mgawatt). Sasa basi, iwapo tungekuwa tumeendeleza miradi yote hii mikubwa ya umeme na bado kukawa na mahitaji, basi tungekuwa na sababu mwafaka ya kufikiria teknolojia nyingine kama nyuklia, lakini kwa sasa mie naona bado sana.

3. Nguvu ya Kiuchumi Uchumi
Kwa Tanzania masikini kama hii ninayoifahamu mimi, ambayo asilimia arobaini ya bajeti yake inategemea hisani ya wafadhili kutoka nje, itakuwa ni kicheksho na mzaha kufikiria teknolojia ya nyuklia, kitu ambacho huwa kinagharimu pesa nyingi sana kukiendesha. Kama hatuwezi kujenga mitambo ya nguvu za maji ambayo ni bei rahisi, kama nilivyodokeza hapo juu, itakuwaje kwa teknolojia ya nyuklia ambayo huhitaji pesa nyingi? Huu ni mzaha, tena wawazi kabisa.

4. Nishati Mbadala
Kama nilivyodokeza hapo juu, tuna vyanzo mbadala vingi sana vya nishati kama vile nishati ya jua, upepo na mkondo wa bahari, kwa hiyo basi hakuna ulazima wowote wa kuikimbilia teknolojia ya nyuklia kwa ajili ya uzalishaji wa nishati. Itakuwa ni matumizi mabaya ya kile tulichonacho.

5. Kipaumbele
Kwa wakati huu, kuwa na mitambo ya nyuklia isiwe kipaumbele, nadhani hii pesa ambayo tunapanga kuendelezea teknolojia hii ingepelekwa katika upatikanaji wa huduma za afya, miundombinu na elimu ambavyo ndio tunavihitaji sana kwa sasa kuliko hio nyuklia.

Hitimisho
Siungi mkono kabisa Tanzania kuwa na teknolojia ya nyuklia kwa sasa. Najua huenda wanasiasa wasiyasome maoni haya na kuyapa umuhimu, lakini nashukuru kwamba nimetumia haki yangu kama Mtanzania kufikisha kwa jamii kile ninachoona kinafaa kwa taifa kwa sasa, kuliko kung'ang'ania sifa na ujiko.

Nawasilisha.

Mitambo ya maji kwa mabadiliko ya hewa ya sasa ina walakini. Pili hata kama Tanzania tunazo nguvu mbadala, je ni hatua gani tunachukua kuzitumia nguvu hizo?

Katika NYUKI hakuna ujiko, ni serious business ambayo watu inabidi wapige vitabu vikali, utafiti uwe unafanyika na hakuna lelemama.

Hakuna nchi iliyo na NYUKI kwa ujiko, wote walio na NYUKI ni watu serious katika usalama wa taifa lao au katika masuala ya enegy.
 
Kwa Tanzania, bado hatujavuna nishati za maji, jua na upepo kwa matumizi ya nishati kiasi cha kulazimika kutumia nyuklia kwa kuzalisha nishati. Nasema hivi kwa sababu bado sirikali inasuasua mpaka sasa kuendeleza miradi ya nishati za nguzu ya maji kama vile mradi wa Rumakali uliopo wilayani Makete (222 Megawatt), mradi wa Stiegler's Gorge (358 Megawatt) na mwingine ulipo wilayani Njombe (100 Mgawatt). Sasa basi, iwapo tungekuwa tumeendeleza miradi yote hii mikubwa ya umeme na bado kukawa na mahitaji, basi tungekuwa na sababu mwafaka ya kufikiria teknolojia nyingine kama nyuklia, lakini kwa sasa mie naona bado sana.

Miradi ya maji nayo ina matatizo yake. Norwegians waliutema mradi wa Stiegler kutokana na madhara yatakayotokea kwenye bonde la mto rufiji. Eco system yote itaharibika, vijiji na sehemu kubwa ya Ruaha ( au Selous?) National Park itafunikwa na tusahau wale prawns wa Rufiji. Ukiongezea tatizo la kujaa udongo ndo basi. Hakuna kitu rahisi, mkuu. Lakini naona wanao'promote' hii miradi hawazungumzii haya na kwa vile yuko mChina, environmental issues ndiyo tusahau!
 
Miradi ya maji nayo ina matatizo yake. Norwegians waliutema mradi wa Stiegler kutokana na madhara yatakayotokea kwenye bonde la mto rufiji. Eco system yote itaharibika, vijiji na sehemu kubwa ya Ruaha ( au Selous?) National Park itafunikwa na tusahau wale prawns wa Rufiji. Ukiongezea tatizo la kujaa udongo ndo basi. Hakuna kitu rahisi, mkuu. Lakini naona wanao'promote' hii miradi hawazungumzii haya na kwa vile yuko mChina, environmental issues ndiyo tusahau!

Fundi:

Nimeweka thread mpya pale ya Waafrika Ndivyo Tulivyo?. Katika thread hii tatizo sio NYUKI per se bali ni matatizo yetu wenyewe ya kitaaluma, uwajibikaji na umasikini. Katika mada hiyo, naomba uchangie mapungufu yetu ya kitaaluma na uwajibikaji.
 
Heri ya Mwaka mpya 2008 wana JF wote, nimepata faraja K-T bado tunae, naombeni samahani wote niliowakwaza katika ubishi wa hoja.

Najiuliza hivi kweli tz hatuna amani kuliko Pakistani na India? mbona wana nuclear energy na wamepata safety certificate kutoka atomic agency. Tukumbuke tulivyo commision hydro powers tulidhani sasa tumewini, je ilikuwa kweli?

Hizo wind farms, soler powers, coal energy, power linking yasiwe mapazia ya kutufanya tusione mbele zaidi.
 
Fundi Mchundo nimeandika kwenye hii thread kukupa happy new year tuu! Mawazo yako yanasomeka vilivyo!
 
Kama tungeweza kutunza mabwawa ya mtera na kidatu, tunaweza kujaribu hata kutunza kinu cha Nyuklia. This is a joke, huenda huyo jamaa alikuwa anaongea akiota
 
Mfumo wetu wa elimu unafanya kutokuwa critical thinkers, tizama bado tunafundishia vitabu vilivyokuwa published 60's, sio ajabu kukuta wanafunzi wa udsm wakitumia vitabu vya penina lihamba na ngugi kama reference books! wasomi wetu waoga kupita kiasi, mawazo yao ni kushindwa tu.

Hebu tuangalie, Gurmet lodge nikati ya hotel aghali duniani US$ 1500ppn na booking za 2008 zimeshajaa bado tunasema biashara ya utalii hatuwezi! watanzania wanajitosa kumiliki machimbo ya makaa ya mawe makubwa kuliko yote duniani tunasema ufisadi hadi tunashinikiza tume iwachunguze!

Hivi tunajua kuwa bank M ni bank yenye teknolojia ya hali ya juu kabisa duniani sasa iko japan au tz? Jamani tujengeni mawazo kuwa nasisi tunaweza, tusisingizie utumwa na ukoloni ulioisha 200yrs na 46yrs.
 
Mfumo wetu wa elimu unafanya kutokuwa critical thinkers, tizama bado tunafundishia vitabu vilivyokuwa published 60's, sio ajabu kukuta wanafunzi wa udsm wakitumia vitabu vya penina lihamba na ngugi kama reference books! wasomi wetu waoga kupita kiasi, mawazo yao ni kushindwa tu.

Hebu tuangalie, Gurmet lodge nikati ya hotel aghali duniani US$ 1500ppn na booking za 2008 zimeshajaa bado tunasema biashara ya utalii hatuwezi! watanzania wanajitosa kumiliki machimbo ya makaa ya mawe makubwa kuliko yote duniani tunasema ufisadi hadi tunashinikiza tume iwachunguze!

Hivi tunajua kuwa bank M ni bank yenye teknolojia ya hali ya juu kabisa duniani sasa iko japan au tz? Jamani tujengeni mawazo kuwa nasisi tunaweza, tusisingizie utumwa na ukoloni ulioisha 200yrs na 46yrs.

Eddy you made my day:

Ukiangalia posti nyingi hapa ni za kutoa lawama kwa serikali yetu. Je hao waliopo madarakani wametoka wapi kama sio miongoni mwetu?

Na sababu kubwa ya wao kuvurunda, ni kukulia kwenye mawazo ya kuwa kuna vitu sisi hatuviwezi na wanashindwa ku-copy na ku-paste vitu vilishofanyiwa kazi miaka kibao iliyopita.

Tanzania na Malawi zilikuwa za mwisho dunia kuwa na station za TVs. Na sababu zilizotolewa ni kuwa Tanzania haiwezi kuendesha TV kutokana na gharama zake na kwamba matangazo ya TV yatawafikia matajiri tu. Hivyo malengo yaliwekwa kuendelea matangazo ya radio mpaka mwishoni mwa 80 kulikuwa na radio kati ya 300,000 kwa taifa lenye watu zaidi ya millioni 25.
 
Kama tungeweza kutunza mabwawa ya mtera na kidatu, tunaweza kujaribu hata kutunza kinu cha Nyuklia. This is a joke, huenda huyo jamaa alikuwa anaongea akiota

Hiyo sio ndoto. Anayewajibika katika vitu vidogo ataonyesha uwajibikaji katika vitu vikubwa pia.

Muhasibu ambaye ni mwizi kabla ya kutumia computerized-system. Atakuwa mwizi akitumia computerized-system.
 
Bin Maryam you are very optimistic and you think positive and probably it is true iko siku tutaiweza hii Nuclear technology.

Lakini kabla ya kuifikiria hii technology nadhani ingekuwa jambo la busara kwa Tanzania kuonyesha kwamba hii ngoma tutaweza kuicheza. Mfano ingekuwa ni vizuri kuonyesha kuwa tunaweza kujenga barabara imara na kuzi-maintain, itakuwa ni vizuri kuonyesha kwamba tunaweza kujenga a physics lab kwenye shule zetu za sekondari, maana shule zetu karibu zote hizi mpya hazina hata physics Lab sasa hao wafanyakazi watakaokuja kufanya kazi huko kwenye nuclear power plants si lazima hata basic physics waijue kabla hawajaiweza nuclear physics? Yaani physics Lab tena zilizochakaa utazikuta tu kwenye zile shule walizotujengea wakoloni miaka ya 47.

Kazi ndogo ndogo za kujenga hospitali za maana hatuziwezi, Kuhesabu kura tu ni mbinde tunashindwa kusimamia, Je jamani hiyo nuclear tutaiweza?

Tanzania jamani ni nchi masikini sana ingawa resources za kuwa tajiri tunazo, watu wanaingia nuclear baada ya kuweza kuzi-utilise other energy resources kikamilifu, sasa sisi hiyo gesi, hayo makaa ya mawe bado hatujaweza kuya-utilise wakati technolojia yake ni ndogo kuliko nuclear. Je nuclear technology tutaiweza? kwa mawazo yangu kwa sasa bado uwezo wetu Tanzania mdogo sana.
 
Bin Maryam you are very optimistic and you think positive and probably it is true iko siku tutaiweza hii Nuclear technology.

Lakini kabla ya kuifikiria hii technology nadhani ingekuwa jambo la busara kwa Tanzania kuonyesha kwamba hii ngoma tutaweza kuicheza. Mfano ingekuwa ni vizuri kuonyesha kuwa tunaweza kujenga barabara imara na kuzi-maintain, itakuwa ni vizuri kuonyesha kwamba tunaweza kujenga a physics lab kwenye shule zetu za sekondari, maana shule zetu karibu zote hizi mpya hazina hata physics Lab sasa hao wafanyakazi watakaokuja kufanya kazi huko kwenye nuclear power plants si lazima hata basic physics waijue kabla hawajaiweza nuclear physics? Yaani physics Lab tena zilizochakaa utazikuta tu kwenye zile shule walizotujengea wakoloni miaka ya 47.

Kazi ndogo ndogo za kujenga hospitali za maana hatuziwezi, Kuhesabu kura tu ni mbinde tunashindwa kusimamia, Je jamani hiyo nuclear tutaiweza?

Tanzania jamani ni nchi masikini sana ingawa resources za kuwa tajiri tunazo, watu wanaingia nuclear baada ya kuweza kuzi-utilise other energy resources kikamilifu, sasa sisi hiyo gesi, hayo makaa ya mawe bado hatujaweza kuya-utilise wakati technolojia yake ni ndogo kuliko nuclear. Je nuclear technology tutaiweza? kwa mawazo yangu kwa sasa bado uwezo wetu Tanzania mdogo sana.

Pedro:

Wanafunzi wa India na Pakistani wanazikuta Lab University. Kwanini wewe unataka Lab iwepo mpaka shule za msingi ili uweze kufanya maajabu yako?

Nyerere aliweza kutengeneza Vifaru na magari ya kivita pale Nyumbu kwa kutumia wanafunzi waliosoma miembeni na kuwapeleka Bulgaria. Think about that Bro.

Na point yangu sio kuwa watanzania watumie NYUKI sasa. Lakini kwa miaka 20 inayokuja inawezekana kuanza program ndogo ndogo. Gas tuliyonayo inamuda wake (20 years) na makaa ya mawe vilevile ya muda wake.

Ukiwalambisha sana watanzania Gas na Makaa ya mawe watasahau kuwa hizo ni akiba zinazoweza kwisha kama vile mabwana yanavyoweza kukauka.

Besides, the Stone Age didn't end because people then ran out of stones. The Stone Age ended because people invented alternatives.
 
Astoundingly as it may sound what an extraordinary way of cohesion shown by contributors to this thread.

I shall agree with Pedro
“Bin Maryam you are very optimistic and you think positive and probably it is true iko siku tutaiweza hii nuclear technology”

Bin Maryam I strongly agree with your views(on this thread), their quite coherent with IDIMI and the rest of the posts on this thread.
“Uwezekano wa Tanzania kuwa na NYUKI ni mkubwa kuliko uwezekano wa Tanzania kujenga ujamaa”

Hii mind-set, mind-set, mind-set! (VISION) Inatufaa kwa mambo mengi tu Watanzania.

Mimi nitahitaji strategically thinking people like you for 2025!

Pitiani na hapa basi-Nafikiri itaweza kuondoa woga kidogo.http://www.howstuffworks.com/nuclear-power.htm
 
Astoundingly as it may sound what an extraordinary way of cohesion shown by contributors to this thread.

I shall agree with Pedro


Bin Maryam I strongly agree with your views(on this thread), their quite coherent with IDIMI and the rest of the posts on this thread.

Hii mind-set, mind-set, mind-set! (VISION) Inatufaa kwa mambo mengi tu Watanzania.

Mimi nitahitaji strategically thinking people like you for 2025!

Pitiani na hapa basi-Nafikiri itaweza kuondoa woga kidogo.http://www.howstuffworks.com/nuclear-power.htm

NDIYO MAANA NAIPENDA NA KUIAMINI KAULI MBIU YANGU KAMA ILIVYO HAPO CHINI!!!!
 
Pedro:

Wanafunzi wa India na Pakistani wanazikuta Lab University. Kwanini wewe unataka Lab iwepo mpaka shule za msingi ili uweze kufanya maajabu yako?

Nyerere aliweza kutengeneza Vifaru na magari ya kivita pale Nyumbu kwa kutumia wanafunzi waliosoma miembeni na kuwapeleka Bulgaria. Think about that Bro.

Na point yangu sio kuwa watanzania watumie NYUKI sasa. Lakini kwa miaka 20 inayokuja inawezekana kuanza program ndogo ndogo. Gas tuliyonayo inamuda wake (20 years) na makaa ya mawe vilevile ya muda wake.

Ukiwalambisha sana watanzania Gas na Makaa ya mawe watasahau kuwa hizo ni akiba zinazoweza kwisha kama vile mabwana yanavyoweza kukauka.

Besides, the Stone Age didn't end because people then ran out of stones. The Stone Age ended because people invented alternatives.

Again, Bin Maryam unaongea kama mwanasiasa. Aliyekuambia nani kuwa wanafunzi wa Pakistan na India wanakuta lab vyuo vikuu? India kila siku ilikuwa na matabaka. Imekuwa na world-class scientists kwa muda mrefu tuu.Naamini the same is true for Pakistan. Huu umahiri wao kwenye sayansi haukutokea hewani. Wameujenga kwa muda mrefu. Usisahau kuwa population ya India inazidi population ya watu weusi na kwa hiyo wana pool kubwa tuu ya utalamu. Industry ya technology na sayansi ni kubwa katika nchi hizi. Si maabara tuu, wanatengeneza wenyewe vifaa vya kwenye maabara, wanapublish wenyewe kwa bei nafuu vitabu vya sayansi na wanaandika wenyewe sehemu kubwa ya vitabu hivyo.

Sisi kote huko hatujafikia. Si shule za sekondari tu kukosa walimu wa sayansi, vitabu, maabara ( ndiyo maabara ni muhimu katika kupata uelewa katika nyanja hii), kompyuta hata kwenye vyuo vikuu vyetu hayo matatizo yapo. Hiyo pool ya wataalam wa nuclear science (kuanzia scientists, engineers, fundi wachundo n.k) tutaitoa wapi?
Fundi Mchundo mwenzangu ni lazima unaelewa kuwa the science behind nuclear power sio ngumu kiasi hicho. Ni namna gani unaweza kui'harness' bila kuleta madhara na cha msingi zaidi utakavyoweza kudispose hiyo inayoitwa 'spent fuel'! Huu uwezo hatuna kwa bahati mbaya na kwa hivyo ni foolhardy kuanza kuentertain mawazo kama haya badala ya kuangalia njia mbadala kibao zilizo ndani ya uweza wetu. Wazimbabwe wamepiga hatua katika matumizi ya wind power, Centre for Appropriate Technology wana utaalam wa kutoa umeme kwenye maporomoko yasiyozidi mita moja (ndio, moja), waizraeli wako mbele kwenye matumizi ya sola n.k.

Kwa bahati mbaya hii ni ishara ya the very mind-set unayoipiga vita. Kupenda makubwa badala ya tunavyoviweza. Maprofesa India hawaoni taabu kupanda baiskeli, sisi tunataka SUVs. Uwezo wa kuhudumia hayo mashangingi hatuna lakini bado tumeyang'ang'ania.

Ni vifaru vingapi na magari ya kivita vilivyotengenezwa na Nyumbu? Katika zaidi ya miaka kumi wameweza kutengeneza magari yasiyozidi 26! At what cost? Tumeweza kumuuzia nani? Hizi ndizo sifa zisizo na maana ambazo tunazipenda.

Tuvifanye tunavyoviweza kwanza. Hivyo vingine vitakuja tuu. Tuwekeze kwenye elimu kama walivyofanya wenzetu na haya unayoyataka yatakuja tuu. Tusipende pupa. Tujiulize, kuna nchi kibao zilizotuzidi uwezo lakini hazijajiingiza huko kwa sababu gani? Sio wajinga hao. Alternatives zipo, lakini si hii unayokazania. Itatupa false security ati kwa sababu tuna uranium tusiangalie njia mbadala! Tunajijua.
 
Back
Top Bottom