... Inakaribia Kupasuka!.
Preamble: Mimi ni supporter wa ZZK kwenye urais 2015, ila kwa jinsi hii ngoma inavyovurumishwa na kuzidi kutoa mlio mkubwa humu jf, hii ni ishara mbaya kuwa hii ngoma inakaribia kupasuka!.
ZZK: Namkubali sana tuu ila natatizwa na determination yake ya kuwa a "dare devil!" bila kutoa sababu and once defeated anajinyamazia kimya bila kutoa sababu!. "Anayekuja pasi na hodi, huondoka pasi kuaga!".
ZZK alipofanya atempt ya kumvaa Mbowe kwenye Uenyekiti wa Chadema, alikurupuka bila kutoa sababu, na alipojitoa hakutoa sababu za kujitoa!. Ndivyo vivyo hivyo 2010 alipotishia kutogombea Kigoma!, akatishia kutafuta jimbo lolote, na sasa anatishia tena 2015 kutogombea tena ubunge bali kugombea urais kupitia Chadema!.
The proper way ilikuwa sio yeye kutangaza nia bali kuwaonyesha Chadema kwa vitendo kuwa anaweza na ni kwa kupitia vitendo hivyo vya kuonyesha uwezo, ndipo Chadema waonyeshe kuwa wanamhitaji ZZK kupeperusha bendera yake 2015, not the other way round!.
Kwa vile mpiga ngoma hii mkubwa ni ZZK mwenyewe na ikitokea ngoma hii kupasuka kiukweli, then itakuwa ni haki tukisema aliyeipasua ngoma ya ZZK kwenye urais wa 2015 ni ZZK mwenyewe hivyo wapenzi wa ZZK ngoma ikishapusuka, nawaombeni sana msitafute mchawi!.
Pasco.
Udhaifu wa ZZK
- Anatishia kuwataja walioficha pesa Uswiss, Kama anawajua why not mention them like LIST oF SHAME!!!!
-Tume ya Bomani alikuwa Member na bado tunaibiwa madini
-Hashiriki M4C ... So wananchi hawamwoniiii
- Anajiproud zaidi yeye na sio Chama
-Utajiri alio nao ni hatari kwa kiongozi
-Anazunguka zunguka na Vasco Da Gama, why..... Anafurahia adui kuwapiga CDM mabomuuuuuu... Kwa nini hakulaani mauaji ya Morogoro na Iringa????