Urais: Ni kazi ngumu au rahisi?

Lukolo

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
5,143
3,196
Wadau,

Kwa uzoefu wangu wa uongozi katika idara mbalimbali zikiwemo za serikali na za binafsi, nimekuwa najikuta ninakabiliwa na changamoto nyingi ambazo zinanikosesha usingizi na wakati mwingine zinanifanya nifanye kazi hadi weekend au nifanye kazi hadi usiku bila malipo. Mara nyingi nimekuwa nikikwazwa sana na utitiri wa matatizo yanayokuwepo kwenye idara yangu ambayo kila nikiyaandikia proposal kwa ajili ya utatuzi hayapatiwi ufumbuzi. Ni kutokana na changamoto hizo nimejikuta kila nikipewa nafasi naishikilia kwa muda halafu naanza kutafuta mahali pa kutokea haraka sana ili niachane na cheo hicho nilichopewa.

Lakini kinachonishangaza ni nafasi ya Urais, ambayo mtu akishaingia tu basi hatamani tena kutoka, wengine wanabadili hadi katiba ili aongoze milele. Sasa najiuliza kitu, hivi huko hakuna majukumu kama yale yaliyopo kwenye ngazi za chini? Hivi ukiwa Rais huoni matatizo ya unaowangoza kama ambavyo tunaona tukiwa kwenye hizi nafasi za chini? Au hukumbani na changamoto zenye kukatisha tamaa kama hawa waliopo huku chini.

Kwa mfano Kikwete kasakamwa na watu wa kila aina si magazeti si watu gani, huko mbeya wakamrushia na mawe, ikulu wakamdanganya na kumdhalilisha, mara akaingizwa kwenye kufungua hotel ambayo in two days ilivunjwa na lawama kibao juu ya kushuka kwa uchumi na hali ngumu ya maisha. Kutokana na haya yote hakupaswa aone kwamba hii ni kazi iliyomuelemea na hivyo aamue kuachana nayo? Lakini nashangaa anarudi kwa kasi ya ajabu ... huku akina Yahya wakiwatishia kifo kwa watakaompinga!

Ndiposa najiuliza hivi Urais ni kazi ngumu au ni rahisi tu ambayo hata mimi naiweza?
 
Kwa haraka haraka, mm nadhani urais ni moja kazi rahisi sana duniani more especially ukiwa rais wa Tanzania. Ingekuwa kazi ngumu I'm sure Kikwete asingechukua form tena. Ninasema hivyo kwa sababu Kikwete amewasahau kabisa maskini wa tanzania kwa kuishi kama mfalme lakini still maskini hao hao ambao mlo mmoja kuupata ni ngumu wamejibana na kuuza maandazi kumchangia mfalme kikwete achukue fomu kugombea tena urais. Kwanini nasema kawasahau?

1. Ameendekeza maisha ya anasa kwa kusafiri kila siku (flying president), kununua maBMW lukuki ya ikulu, likizo zake zote ni kwenye mahoteli ya kitalii mbugani.Serikali yake inaendeshwa kwa gharama kubwa(kuna watz wanalipwa mishahara ya UN) Yote haya ni kwa kodi za wananchi ambao hospitalini wanalala chini kwa kukosa vitanda, 13m kati yao wako below poverty line. Infact style ya maisha na uongozi wa Kikwete ni kama vile anaongoza moja ya nchi tajiri zaidi duniani wakati sisi tunaongoza kwa umasikini.

2. Hana nia ya dhati kupambana na ufisadi kwani case zote zilizopo mahakamani kwa sasa ni usanii uliokithiri machoni kwa wananchi. Kila report ya CAG ikitoka zinaonyesha ni ubadhilifu wa ajabu unafanyika lakini hakuna chochote kinachofanyika kukabiliana na hilo. Imefika mahali sioni tofauti ya report ya CAG na mashairi ya mzee Yusuf kwani wakati mashairi ya mzee Yusuf huishia pale Traventine Magomeni, yale ya CAG huishia pale bungeni Dodoma kwa makofi then wanasubiri the next report. Tunao mawaziri lukuki waliosababishia nchi hii/walipa kodi sisi hasara ya mabilioni lakini still hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi yao. Rejea mkataba wa Rites na mingineyo.

3. Amekosa priorities huyu baba. Sorry naomba nitumie mfano wa juzi Taifa. Serikali yake haijuwi kipi muhimu, madawati na vitabu shuleni, dawa na vitanda mahospitalini, barabara, umeme na maji au kuwaona Brazil? Wote tunajuwa kwamba ile deficit ya 2 billion na ushee ya TFF italipwa na guarantor ambao ni sisi kwa kodi zetu kupitia so called serikali.

Hii list ni ndefu sana siwezi kuimaliza, lakini pamoja na madudu yote hayo wale ambao walipaswa kukuadhibu kwa kutotenda yale uliyoahidi ndio wanakuwa wa kwanza kukuchangia form eti ukauchukue form wakati mchana hawajala, then kwanini urais isiwe kazi rahisi?
 
Zamani nilikuwa nauogopa na kudhani kuwa wapo wateule miongoni mwetu wanaofaa kubeba jukumu la kuongoza nchi. Lakini kwa kuangalia mwenendo wa kiuongozi hapa bongo, nazidi kupata picha tofauti. Sijui kwa nchi zigine lakini kwa hapa bongo urais ni rahisi tu. Huhitaji kuwa msomi mwenye busara wala hekima ili uwaongoze wananchi na siku zikasonga mbele bila wasiwasi.
 
Oh well,usemayo ni sahihi,lakini ndiyo maana tuko hapa tulipo.Tuanajaribu kuya solve matatizo yetu kwa kutumia watu na akili zilezile zilizoyasababisha ama ku create matatizo hayo.It won't work.
 
Chezea magamba party system wewe? Mwenyekiti wao wa sasa kapata Urahisi kupitia vijiwe vya kahawa!
 
Zamani nilikuwa nauogopa na kudhani kuwa wapo wateule miongoni mwetu wanaofaa kubeba jukumu la kuongoza nchi. Lakini kwa kuangalia mwenendo wa kiuongozi hapa bongo, nazidi kupata picha tofauti. Sijui kwa nchi zigine lakini kwa hapa bongo urais ni rahisi tu. Huhitaji kuwa msomi mwenye busara wala hekima ili uwaongoze wananchi na siku zikasonga mbele bila wasiwasi.
Lakini kumbuka maneno ya mwalimu Nyerere mwaka 1995, aliposema mtu ambaye anajua majukumu ya Urais yalivyo mazito, hawezi kukimbilia Ikulu, kwa kuwa Ikulu ni mzigo mzito sana. Sasa hawa watu drsign ya JK ambao wameenda Ikulu kwa mission moja tu, kukomba rasilimali za nchi yetu, na anapotokea mtu anahoji uovu huo, ananyamazishwa kwa 'kitu kizito' kwa hiyo kwa Rais wa namna hiyo, ndiye anayedhani urais ni mwepesi, lakini anachosahau, the day will come, lazima tutawaburuza The Hague, ili wakajibie makosa yao huko. Maana huko hawapo kina Zoka, Nchimbi, Mwema, Chagonja, Kamuhanda na Shilogile, ambao wao wanaamini vyombo vya dola, kazi yao ya kwanza ni wa kuwalinda watawala. Ambayo hiyo ni wrong concept. Vyombo vya ulinzi na usalama duniani kote, wajibu wao nambari moja ni kuwalinda raia na mali zao na kulinda maslahi ya Taifa kwa ujumla wake!!
 
Lakini kumbuka maneno ya mwalimu Nyerere mwaka 1995, aliposema mtu ambaye anajua majukumu ya Urais yalivyo mazito, hawezi kukimbilia Ikulu, kwa kuwa Ikulu ni mzigo mzito sana. Sasa hawa watu drsign ya JK ambao wameenda Ikulu kwa mission moja tu, kukomba rasilimali za nchi yetu, na anapotokea mtu anahoji uovu huo, ananyamazishwa kwa 'kitu kizito' kwa hiyo kwa Rais wa namna hiyo, ndiye anayedhani urais ni mwepesi, lakini anachosahau, the day will come, lazima tutawaburuza The Hague, ili wakajibie makosa yao huko. Maana huko hawapo kina Zoka, Nchimbi, Mwema, Chagonja, Kamuhanda na Shilogile, ambao wao wanaamini vyombo vya dola, kazi yao ya kwanza ni wa kuwalinda watawala. Ambayo hiyo ni wrong concept. Vyombo vya ulinzi na usalama duniani kote, wajibu wao nambari moja ni kuwalinda raia na mali zao na kulinda maslahi ya Taifa kwa ujumla wake!!

send message KWA WABUNGE!!
 
Salamu nyingi ziwafikie wana JF. Ningependa pia kuanza thread hii kwa kuwapongeza wale wote ambao wameshatambua kuwa tunahitaji mabadiliko na pia wanashiriki katika harakati za kuyasaka mabadiliko hayo.

Kwa muda mrefu nimekuwa ninafuatilia hali ya siasa katika nchi yetu hasa kipindi hiki kuelekea uchaguzi wa mwaka 2015. Katika ufuatiliaji wangu huu nimeelewa kuwa bado wanasiasa wengi wanachukulia uraisi kuwa ni kitu rahisi. Ndio maana nimeona nianzishe mjadala huu nilioupa kichwa “ Uraisi utakuwa urahisi hadi lini?”. Kwa mawazo yangu, hasa kwa kuzingatia hali ya dunia ya sasa, wakati ule wa kuchagua raisi kwa msukumo wa pilau, kofia, khanga, na vitenge, umeshapitwa na wakati. Pia ule wakati wa kuchagua raisi kwa ahadi tupu bila udhibitisho namna hizo ahadi zitatekezwa umepitwa na wakati. Rais ajaye ni lazime awe ameitumikia nchi na mafanikio ya kazi yake yaweze kudhibitishwa kuwa yanagusa watanzania wengi kama sio wote. Hatutaki kiongozi ambaye amepata vyeo kwa sababu za urafiki na anayeteua. Hatutaki raisi ambaye amepata kuwa kiongozi kwa sababu ya umaarufu wa baba, babu, mama au mjomba.

Je, tutapataje raisi mwenye sifa hizo hapo juu? Ni lazima katika uchaguzi wa raisi (na vongozi wengine) kuwepo na mdahalo utakaoshirikisha wagombea wote. Midahalo ni njia pekee inayotoa fursa ya kuwasikiliza na kuwauliza maswali wagombea. Ndio njia pekee ambayo wagombea uraisi wanaweza kutoa mawazo yao kuhusu tunakotoka na tunakoelekea na pia kueleza wana mipango gani ya kuwezesha nchi kufikia tunakoelekea. Ingawaje midahalo hutumika katika nchi nyingi zilizoendelea, lakini pia kwa sababu sasa katika nchi yetu tuna television na radio station nyingi, hii njia pia inawezekana hapa Tanzania na uwezekano wa midahalo hii kuwafikia wananchi wengi ni mkubwa. Binafsi ninaona ni vema hili jambo la midahalo wakati wa kugombea uraisi liwekwe kwenye katiba. Hii itasaidia kulazimisha ushiriki wa vyama vyote na kama mgombea wa chama cho chote hatashiriki basi atakuwa amekosa sifa za kuwa raisi/kiongozi.

Ninajua kuna wengine watauliza midahalo ya nini wakati kuna mikutano ya kampeni? Mikutano ya kampeni itaendelea kuwepo lakini tatizo la hii mikutano wananchi hawapewi nafasi ya kuuliza maswali. Pia utakuta wagombea wengi huwa wanatumia shida za watu wanaoishi maeneo ya mikutano kuwadanganya wenyeji na mara wakiwachagua hawarudi. Mifano mizuri ni ile meli kubwa ziwa Victoria na ujenzi wa Dubai kule Kigoma, ahadi ambazo hadi leo hazijatekelezwa na pengine hata aliyeahidi hakumbuki kama aliahidi hivyo, na kama anakumbuka, hakosi usingizi kwa kushindwa kuzitekeleza. Kama mgombea hatoweza kueleza kwa kina atawafanyia nini watanzania na kujibu maswali muhimu kuhusu maendeleo ya nchi yetu, huyo hatufai. Hatutaki tena kuweka mtu ikulu kwa manufaa ya wachache au familia. Tunataka raisi wa watu wote, raisi ambaye atahakikisha kuwa huduma bora za afya ni haki ya watanzania wote, raisi ambaye atahakikisha vijana wanapata elimu bora ili waweze kushindana na vijana wa mataifa mengine kwa utaalamu, raisi ambaye atahakikisha kuwa kodi za watanzania zinatumika kuwaletea wananchi maendeleo, raisi ambaye akisikia tembo wanateketezwa anahakikisha majangili yote wanakamatwa, raisi ambaye hatoruhusu rasilimali za nchi kumilikiwa na wageni, raisi ambaye hatasubiri kuambiwa bali anafuatilia matatizo ya watanzania, na mwisho, raisi ambaye anajua na kuzingatia kuwa “Uraisi sio rahisi”.
 
Naunga mkono hoja suala la midahalo ni muhimu sana kwa wanasiasa wetu wa ngazi hata za ubunge. Kwa sabb kuna waheshimiwa huwa wanasemewa tu.... Wanashindwa kujenga hoja hata kwenye mikutano au vikao mbalimbali. Pia lazima aseme alishawahi kufanya nini huko alikokuwa mwanzo...
 
Kulitakiwa kuwe na sheria ya kumshitaki rais anaetoka madarakani, kama kikwete anatakiwa kunyongwa kabisa kwa kuuza maliasili zetu

Sent from my Nokia Lumia using Tapatalk
 
Uraisi ni kazi ngumu kwa mtu anayeelewa resposibilities za raisi kwani ni kujitoa kwa watu, kuchukua maamuzi sahihi ambayo hayataleta madhara kwa watu nk... hayo yote yanafanywa kwa kichwa kizuri kilichotulia ila kwa mtu asiyeelewa maana ya uraisi na kwenda ikulu kufanya yake... aiseeee ni kazi raisi sana ambayo hata mtoto mdogo anaweza kufanya.
 
Kulitakiwa kuwe na sheria ya kumshitaki rais anaetoka madarakani, kama kikwete anatakiwa kunyongwa kabisa kwa kuuza maliasili zetu

Sent from my Nokia Lumia using Tapatalk

Hahaha...
Kuna kipindi nilikua nafikiria kuwa, raisi anapoingia madarakani kwa ahadi nyingi, ni sawa na kuwa na contract between wananchi na raisi, anapotoka madarakani bila kutimiza ahadi zake ni sawa na kubreach the contract iliyopo... kubreach the valid contract ni kosa na aliyebreach anapaswa afidie either kwa kufanikisha ahadi zake ambazo hakuzifanya kwa mali zake kuuzwa na ahadi kutimizwa...
Ila hadi kunyongwa..... wewe umefika mbali...
 
Hawezi kwenda UDSM, Akienda benki hadi atoroke, Hawezi kwenda mlimani city.

Kila anakokwenda wanatangulia wiki kabla ( vijana wapelelezi) huwezi kumtembelea Rafiki.

Kila unakokwenda unatangazwa lawama kila kona wakati hadi kanisani walindwa kila kitu wewe nchi nzima usiku na mchana unafanya kadri ya uwezo wako.

Hivi kuwa Rais kuna raha gani labda huwa wanaejoy nini kwa mfano!!!!!
 
raha yake unauwezo wa kugonga demu yeyote unayemtaka hapa tanzania bila kujali mke wa rugemalila au la
 
Back
Top Bottom