Urais, Halima, Nassari na Kigoma

Status
Not open for further replies.
Nilikuwepo uwanjani pale lake Tanganyika Kigoma, kilichoandikwa ndicho nilichosikia pia. Videos zitawekwa hapa na zitathibitisha.

Siwezi kuwaandikia mwananchi kwani mimi silalamiki kuhusu habari hiyo. Wenye kuilalamikia habari wameandika.

Mimi ninaamini gazeti la Mwananchi ndio gazeti pekee huru la kiswahili hapa nchini. Ndio gazeti pekee ambalo umiliki wake hauna maslahi na waandishi na wahariri wake ni mahiri, hawana njaa na hawapindishwi. Ndio maana huandika ukweli muda wote na wanapokosea hawasiti kurekebisha. Ndio maana ni gazeti linasomwa kwa wingi kuliko magazeti yote nchini. Hakuna gazeti linalofikia hata nusu ya mwananchi kwa kusomwa. Hivyo Mwananchi linaaminika na umma.

Najua kuna watu wana chuki binafsi na mwananchi kama gazeti na wahariri wa mwananchi kama binaadamu. Hayo wayamalize wenyewe huko walikochukiana.

Subirini video ndio tutajua habari ile imepikwa au ni ya kweli. Kwa tuliokuwepo uwanjani tunajua nani alisema nini.
Mh.Zitto wakati wa kampeni za 2010 watu wengi wapenda mabadiliko yenye maslahi kwa taifa tukiwa busy kumnadi Dr.slaa kuwa Rais,nilikuona kupitia taarifa ya habari ukisema 2015 utagombea urais kwangu hiyo ilikuwa ishara ya kutokuwa pamoja na wengine kwenye chama,wakati wa kampeni za arumeru watu wako busy kumnadi Joshua wewe unaongea habhari za urais....kwa kifupi haya yananisababisha nisikuelewe kabisa kama kiongozi wa CDM LABDA KAMA UTAFAFANUA LABDA NAWEZA KUKUELEWA ila kinyume na hapo kama CDM wakikupitisha kama mgombea wao 2015 ntamchagua mgombea yeyote wa CCM NA KADI YANGU YA CDM NITAIRUDISHA HADHARANI.Sina chuki yeyote na wewe lakini mambo unayoyaibua katika wakati ambao kwangu unaonekana sio muafaka yananisababisha niondoke kwenye hiyo list ya wanaokuunga mkono.
 
hiyo ''fideo'' bado tu
Mwanzoni kuna video iliwekwa huko kunakodaiwa lakini baada ya sakata hili kuchukua sura mpya, video yenyewe pamoja na jitihada zangu ilikataa kucheza hata kwenye mtambo wangu ninaouamini. Wasi wasi wangu ni moja tu, je kuna mtu aliistukia na sasa marekebisho madogo madogo inabidi yafanyike kwanza? Hata hivyo tuwe na subira....
 
kwa maoni yangu,chadema ili kipate heshima na ili kisionekane kama taasisi binafsi isiyòfuata demokrasia ya kweli,tunataka sura mpya ktk nafasi ya urais,namheshimu sana mbowe aligombea akakosa amekaa pembeni kampisha slaa.nitampuuza yoyote ambae atataka kuendelea kugombea hata baada ya kukosa.cuf inazorota kutokana na mfumo huu,hatupendi chama wala mtu,tunapenda sera zenye mwelekeo wa kidemokrasia.si dhambi kwa zitto au mwanachadema yoyote kuonyesha nia ya kugombea mwisho wa siku watanzania ndo wataamua nyie ambao munae mgombea wenu mfukoni mutajifia na presha kabla hata ya wakati kufika,kama kweli sisi ni wanamageuzi tusimame katikati.
 
Nyie pigeni kelele lakini 2015 Rais ni Dr Slaa, kama hutaki tafuta kamba ukajinyonge
 
Mkuu Mkandara,
Labda kama nitakuwa nimeyaelewa maelezo ya Zitto vibaya, nimesoma na hajakanusha lolote lile lililoandikwa na Mwananchi, zaidi amesema kilichoandikwa ndicho kilishosemwa.
Kwahiyo nadhani hali ni kama ilivyokuwa jana hadi hapo tutakapo pata mkanda.

Sina wasi wasi kuwa mkanda utachakachuliwa kwasababu walioongea wapo nao watathibitisha ukweli wa kauli zao kama kuna uwalakini. Hii itaondoa wingu nene na zito linalonyemelea sehemu muhimu sana ya siasa za nchi yetu.

Ni mapema sana kutoa hukumu hadi video iwekwe.
Ninarudia kusema hili tatizo ni kubwa sana kuliko mnalivyoliona.
Labda niwe muwazi kidogo, hizi ni dalili za mvutano ndani kwa ndani. Mvutano huo si wa kisiasa ni mvutano wa makundi ya kimasilahi. Mvutano huu ni kama ule Juliana (makamu mwenyekiti BAVICHA) aliouleta na kuzua tafrani ambao CDM wameufunika chini ya kapeti kwa staili ya CCM.

Niliwaonya CDM kuwa lazima chama kisimame kama taasisi inayoongozwa na sheria, kanuni na maadili. Hapa ndipo CDM ilipo leo!

Bila kutoka nje ya mada, Mheshimiwa Zitto weka video ili ukweli uonekane.
Tujue Mwananchi Ltd wamesema nini, Nassar na Halima wamesema nini na Zitto anasema nini.
Ni kwa njia hiyo tu hali na mtafaruku uliopo unaoweza kutumiwa vizuri sana na 'wapinzani' wa CDM kuizamisha utakuwa na ufumbuzi.

Baada ya hapo nasi tutaweka maoni yetu, maswali na majibu. Ukiliangalia hili suala kuanzia tamasha hadi mtafaruku unaofukuta kuna mengi ya kujadili. Kwanza tutoe natural justice ya kusikiliza kila mmoja. Tumemsikia Nassar, Halima, sasa Zitto ana video tumsikilize.

Lakini pia Mwananchi Ltd, nina uhakika wanasoma JF, suala hili ni muhimu sana mkalitolea maelezo. The credibility and integrity of your organization is on the line and seriously compromized. The damage is big, probably it will cost you down the road.
 
chademu waparuana makucha..lolz
i always said kweli we need m'badala, lakini but chademu is definitely NOT m'badala.
m'badala makini na wa kweli utatokea hukohuko CCM..sote tuiunge mkono CCM ijisafishe ili wanetu na wajukuu wetu wafaidike..
makofi tafadhali kwa chama cha mapinduzi..
 
Mimi binafsi kati ya vitu vinavyonipa shida sana kufahamu ni msimamo wa Zitto Kabwe kuhusu mwelekeo wa nchi yetu hasa kuhusiana na jinsi anavyokinzana na mambo mengi sana ndani ya chama chake.

Zitto wewe ni economist, hivyo unapaswa kukaa chini na kuanalyse mwenendo wako na misimamo yako na kufanya maamuzi. Mimi nashawishika kuamini kwamba wewe uko sehemu siyo stahili yako kulingana na tabia ambayo umekuwa nayo siku zote. Zitto nashawishika kuamini kwamba CHADEMA siyo mahali panapokufaa, kwasababu unatofautiana nao kwa mambo mengi sana. Hivyo mimi nakushauri fanya maamuzi na ujiunge CCM labda huko utatimiza ndoto zako. Nasema hivyo kwasababu naamini hata Viongozi wenzako ndani ya CDM huna imani nao, ndiyo maana historia yako imejaa mambo mengi sana kinyume na mwelekeo wa chama chenu.

Zitto, kati ya vitu ambavyo siamini kama hata wewe unaamini ni wewe kuwa na uwezo wa kuongoza nchi kama TZ kwasasa na changamoto nyingi tulizonazo. Kwa nafasi yako na uwezo wako, bado huna uwezo wa kuwa Amiri Jeshi Mkuu mwaka 2015 lkn unaweza kuwa sehemu ya timu itakayowaletea watanzania mabadiliko ya kiuchumi na kijamii kutokana na uwezo wako. Lkn ukishakuwa ndani ya timu ya utendaji, hapo 2020 na kuendelea sasa unaweza ukawa na akili na uwezo wa kutimiza ndoto yako.

Zitto, tanzania ya sasa ilipofikia inahitaji mtu mwenye msimamo na asiyeyumbayumba kama ulivyo na rangi nyingi katika utendaji (rejea yanayoendea PPF na wewe kama mwenyekiti wa kamati husika lkn umewekwa mfukoni na Urio kwasababu tu anakupa support ya pesa wkt pale kuna uozo mkubwa sana).

Zitto, kuna watu wanakupoteza na kukudanganya kwa mwamvuli wa UDINI, UKANDA NA UKABILA na wewe unaykumbatia. Hii siyo ajabu kwani propaganda ya CCM siku zote ndiyo hizo lkn wewe pia nikichunguza kwa makini nagundua kwamba unakubaliana na hizi hoja hafifu hata kama kuna kitu kikitokea, basi watu wasiseme kisa UDINI na wewe huyu mdudu mbaya wa UDINI haujawahi kuukemea kabisa kwa kuwafafanunulia watu. Na kwa mantiki hiyo tunashawishika kuamini kwamba wewe unatumia hii dhana ya udini kama mtaji kwako kwa mambo ya kipuuzi ili upate sympathy ya wale wasiotaka kushugulisha akili zao.
Pole sana kwa kutotaka kutoka ndani ya Box bila kujua gharama ya kuwa na rangi nyingi katika dunia ya leo.
TELO.

Kwa umri alio nao sasa Zito, siyo mtoto mdogo. Haya yanayoonekana kuyafanya, hasa tabia ya unafiki, ZITO HAFAI KUWA RAIS WA NCHI IWE NI MWAKA 2015, 2020 AU HATA 2050. Mtu mnafiki hafai, hafai kwa namna yeyote ile kuwa kiongozi. Tunataka kiongozi mwenye rangi moja, tukimtazama kulia tumwone ni yule yule, tukimtazama kushoto, mbele, ndani na nje awe ni yule yule. Zito hayupo hivyo. Kuna ule msemo usemao, 'MUNGU HAMFICHI MNAFIKI'. Mnafiki hampendezi mwanadamu wala Mungu. Ni aheri anayekuja kwako akijulikana ni mbaya na akawa mbaya kweli kuliko anayekuja akijifanya mzuri kumbe ni mbaya. Taifa hili tukitaka lisonge mbele ni lazima tuchague viongozi wanaoeleweka walio na sura moja, sasa hivi tuna viongozi wengi wanafiki ndiyo maana mambo yetu hayaendi. Hawa ndiyo wakiwa hapa bara wanasema, 'zanzibar siyo nchi', akikutana na wazanzibari anasema, 'tukiwa ndani zanzibar ni nchi', what a nosense!
 
Zitto AJIULIZE SWALI RAHISI TU, KWANINI WANACHADEMA WALIO WENGI HAWAMPENDI NA HAWAMWAMINI?
KWANINI SIKU ZA KARIBUNI HAKUWAHI KUHUTUBIA MKUTANO WA HADHARA ARUSHA? NA ARUSHA NI MOJAWAPO YA NGOME KUBWA ZA CHADEMA TZ?
 
Kuhusu hayo yaliyosemwa huko Kigoma nadhani mi nasubiri video zituambie ukweli. Hasi zikiwa hazijahaririwa (kwenye hayo maneno) itakuwa vizuri zaidi.
Lakini ni vizuri pia kumkumbusha mkuu Zitto kwamba hope yake ya mafanikio kiuongozi, at least kwa sasa, iko Chadema. Ameshiriki kuijenga na kuifikisha Chadema hapo ilipo. Chadema sasa inaaminiwa na wananchi. Kitu kinachosumbua akili za watu ni kuona anahusishwa na hata kupigiwa debe na Ccm. Chama ambacho sasa siyo kipenzi cha wananchi tena.
Zitto, uwe makini sana na ccm. Wanaweza kukuvurugia ndani ya chama chako. Na ukweli ulivyo sasa hivi ni kwamba wakikuvurugia ndani ya Chadema itakuchukua several decades kujijenga upya.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
yuko twittere huko bize na kusambaza taarifa za kifo cha rais wa ghana.
Ukiangalia blog yake kaweka video za tamasha tar 19/07/2012,kaupload video za wasanii wakiwa jukwaani,kama hi video anayozungumzia ipo kwanini hajaupload mpaka leo
 
...Hotuba za Wabunge wote zilirekodiwa kwenye video neno kwa neno na video hizo zitawekwa ........kama mwandishi kaandika ambayo wabunge hawa hawakuyasema basi itaonekana kwenye videos hizo. Wabunge wenyewe wanajua kwenye nafsi zao nini walisema Kigoma na kipi kiliwasukuma kusema walioyasema Kigoma...

Napata taabu sana kuelewa statement hapo juu. Ninahisi akina Mdee na Nassari waliongea yale maneno. Zitto (na wahariri wa Mwananchi) walizipitia tape kwa umakini mkubwa sana na wana uhakika wapo sahihi. No wonder habari imechukua siku 6 kutoka. Ninahisi mtafaruku mkubwa ndani ya chama utafuata...
 
Niliwaonya CDM kuwa lazima chama kisimame kama taasisi inayoongozwa na sheria, kanuni na maadili. Hapa ndipo CDM ilipo leo!

Mtu yeyote anaye thubutu kujijenga kama mtu na kushindwa kuijenga taasisi ni hatari kwa maisha yake binafsi maisha ya raia wenzake na dunia kwa ujumla kwani taasisi ina maisha marefu kuliko kitu kingine chochote. Sisi sote tutapita lakini taasisi inauwezo wa kuishi milele iwapo tu wanaounda taasisi kwa wakati watakubali kujikana nafsi zao na kuishi ndani ya taasisi kila moja akiwa kiungo katika nafasi fulani kwa wakati.....CDM kama tasisi lazima iilinde tasisi yake kwa nguvu, akili na uwezo wake wote. Yeyote anayejaribu ama anayethubutu kuidhoofisha taasisi hii lazima adhibitiwe kwa nguvu zote!

Hakuna mtu aliyewahi kufanikiwa yeye binafsi na hayo mafanikio yakadumu kwa muda mrefu bila ya kwanza kujenga taasisi imara hii ni akili ya kawaida kabisa kwa wale wenye maono ya muda mrefu na kwa faida pana ya jamii nzima ya taifa hili. Hiki ndicho kinachotutofautisha sisi (wengi wetu wenye mtizamo wa leo na kusahau kesho nayo inahitaji kuwekeza) na dunia ya wale wanaoitwa walioendelea! Maendeleo yoyote yanayolenga urefu wa maisha ya mtu binafsi (muda mfupi) ni matokeo ya umasikini wa kimawazo, ki-rasilimali na kimazingira....The time preference for the poor people is high thats why they give a very high discount rate to the future as they would want to have the benefits now....Hawawezi ku-invest for future!

Hakuna shortcut tujenge taasisi kwanza ikiwa imara na ikatokea tuka occupy space ya kuiongoza huku ikivuta nyuma taasisi kubwa ya jumuiya ya watanzania itaweza kuipeleka kwenye direction inayoeleweka vinginevyo hata tukipata nafasi hizo na huku centre bolt imekatika hilo gari si litatuangamiza sote dereva na abiria iliyowabeba?
 
Ukiangalia blog yake kaweka video za tamasha tar 19/07/2012,kaupload video za wasanii wakiwa jukwaani,kama hi video anayozungumzia ipo kwanini hajaupload mpaka leo

Ndo maana mimi huwa nawaheshimu sana slaa na mbowe, hawana mda kabisa na porojo za huyu jamaa
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom