Uraia wa Sioi utata mtupu,CCM kutangaza mgombea mpya ARUMERU leo!!

Jamaa kazaliwa Kenya na inasemekana hakuwahi kuukana uraia wake mpaka leo.. This was a technical error kwa Sioi..
 
Fitina ni kawaida ya CCM, Huyu yupo karibu na EL wakati huo huo kiukweli Lowassa hatakiwi na fungu fulani ndani ya CCM, kwa kifupi ngoma inayotaka kuchezwa hapa ni ile ile type ya Bashe-Nzega
Hata mimi nimeishtukia, hii ni habari njema kwani hivi ni vita vya panzi!. Kiukweli tukubali tukatae, angesimama Sioi, Chadema ingekuwa na kazi ya ziada!. Akipitishwa mwingine yoyote ni ushindi wa kiulani kama kumsukuma mlevi!.
 
Kwahiyo kama Sioi si raia wa Tanzania ni Mkenya basi hata baba yake Marehemu Sumari alikua ni Mkenya sio? Hili swala la uraia hapa bongo linautata sana! Hata Jenerali Ulimwengu alishaambiwa kua si raia wa Tanzania na wakamtosa.
 
Hii inaonyesha kwamba "CCM"inawenyewe,
Sasa naombeni mawazo yenu,nna mpango wa kugombea ubunge 2020,but kwa kuanzia naanza na udiwani,sasa ili niwe na uhakika nifanye nini?bcoz I'm a tanzania citizen,but nataka kujihami na MIRUFAA yao ya kupinga pinga.
 
Jamaa kazaliwa Kenya na inasemekana hakuwahi kuukana uraia wake mpaka leo.. This was a technical error kwa Sioi..

Kama huo ndiyo ukweli hakuna jinsi lazima apigwe chini.

Mnamkumbuka Mungai yule hybrid wa Mkenya na Mtanzania (baba na mama) alivyoigharimu nchi hii? He wasn't loyal to Tanzania from production of tea and timber against Kenya to improvement of education system in Tz.
 
sumu+uraia+mauaji+rushwa+umri+fitina+majungu+makundi=sera yetu kwa sasa wakati tunasubiria tarehe ya mazishi ya marehemu chama.:lol:
 
Habari za uhakika kutoka kwa wazito wa NEC ya CCM ni kuwa SIOI SUMARI atapigwa chini na mgombea aliyemfuata Bw. Sarakikya atateuliwa kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi wa Arumeru Mashariki.

Hata hivyo mpango huo umeendelea kuwa mgumu kufuatia mashambulizi mapya ya nguvu ambayo mgombea mwingine Elishilia Kaaya ameyaanza. Habari ni kuwa Elishilia amekwaza na jinsi mpango ulivosukwa wa kumzunguka kiasi kwamba watu aliokuwa nao karibu ndio walioshiriki kummaliza ili kumjengea mazingira mazuri SIOI.

Hata hivyo SIOI SUMARI inaelezwa na NEC kuwa hana mvuto wa kisiasa kabisa ila kwa nguvu ya koo na washili ana nafasi kubwa ya kushinda kwenye kunyang'anyiro.

NEC imejiridhisha kuwa Sarakikya ana uwezo na mvuto wa kisiasa kuweza kupeperusha bendera ya ccm dhidi ya mgombea wa CHADEMA.
 
Habari za uhakika kutoka kwa wazito wa NEC ya CCM ni kuwa SIOI SUMARI atapigwa chini na mgombea aliyemfuata Bw. Sarakikya atateuliwa kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi wa Arumeru Mashariki.
Hata hivyo mpango huo umeendelea kuwa mgumu kufuatia mashambulizi mapya ya nguvu ambayo mgombea mwingine Elishilia Kaaya ameyaanza. Habari ni kuwa Elishilia amekwaza na jinsi mpango ulivosukwa wa kumzunguka kiasi kwamba watu aliokuwa nao karibu ndio walioshiriki kummaliza ili kumjengea mazingira mazuri SIOI. Hata hivyo SIOI SUMARI inaelezwa na NEC kuwa hana mvuto wa kisiasa kabisa ila kwa nguvu ya koo na washili ana nafasi kubwa ya kushinda kwenye kunyang'anyiro.

NEC imejiridhisha kuwa Sarakikya ana uwezo na mvuto wa kisiasa kuweza kupeperusha bendera ya ccm dhidi ya mgombea wa CHADEMA.

Utumbo :juggle:
 
Moja ya hotuba za Mwl Nyerere ambaye alikuwa anaongea falsafa aliwai sema,ukianza dhambi ya ubaguzi utaendelea,ni kama kula nyama ya mtu,ukianza hutaacha...Sasa CCM imezoe kuwabagu watanzania kwa kudai vyama vingine ni vya kidini nk...dhambi hii itawala wao mpaka watashangaa..na kwa hili wajiandae kuvuna matunda yake.
 
Ngoja cc imalize kikao tutajua ukweli . Hata mimi nimesikia hivyo.
 
Hata mimi nimeishtukia, hii ni habari njema kwani hivi ni vita vya panzi!. Kiukweli tukubali tukatae, angesimama Sioi, Chadema ingekuwa na kazi ya ziada!. Akipitishwa mwingine yoyote ni ushindi wa kiulani kama kumsukuma mlevi!.

yaani hata awekwe nani CCM hawawezi kushinda ARUMERU....
 
Kuna zengwe ameundiwa mtoto wa Sumari kwamba Uraia wake una walakini, hapo ndio utachoka kabisa, CCM bana!!
 
Back
Top Bottom