Uraia Pacha Tanzania: Siasa ya Bernard Membe na hatma yake

Swala ni Membe kutaka GF wake awe huru Tanzania na California pia. Swala la waaekazaji wazawa ni janja tu wa waziri kupitia hapa kwa masilahi binafsi.

Kwa sisi wengine tungependa kujuwa kuwa mtu akiwa na uraia wa nchi mbili anakuwa analeta hasara gani wala sio suwala la Umembe au nani? Membe ataondoka lakini hali hii ya Watanzania kunyimwa haki yao itaendelea mpaka lini?
 
MwanaFalsafa1

Kaka! Hivyo unafikiri kila kilichopitishwa hapo mwanzo kilikuwa sahihi? Kama ni hivyo basi tusingedai Katiba mpya!
Hivyo unafikiri ni sahihi kumnyanganya uraia wa kuzaliwa mtu eti kwa kuangalia maslahi? Yaani unafikiri ni dhambi mtu kupata sifa ya kuweza kuendesha maisha yake akiwa nje ya nchi yake? Hii ndiyo inayowalazimisha Watanzania wachukuwe uraia wa nchi nyengine ili wapate sifa ya kuwafanya wapate masilahi ndani ya nchi ya ugenini. Sasa iwapo wenyeji wa nchi ile hawajali wewe kubaki na uraia wa nchi yako uliyozaliwa inakuwa kichekesho kuwa wewe uliemzaa unasema huyu si mwanangu.

Hili suwala la mtu kuukana uraia wa Tanzania limewekwa katika Katiba kimakosa kama mambo mengi yaliyowekwa huko nyuma na tuikaamuwa kuyabadilisha kwa maslaha yetu. Huko nyuma ilikuwa sheria mtu asifanye kazi zaidi ya moja kujitafutia riziki, asipangishe nyumba yake na sheria chungu nzima zisizo na tija kwa mwananchi.

Hili la kumkataa raia wa Tanzania eti kwa kuangalia maslahi si sahihi halafu Kaka unasema eti mtu huyu awe na moyo wa kuekeza kwao na huku umemkataa? Nafikiri ipo haja ya kutafakari na kuondokana na ukungu tuliotandaziwa na siasa za Kijamaa.
 
Last edited by a moderator:
Kwani akiwa nao utamfanya asifanye hayo anayotaka kufanya? Pengine ungetwambia hasara za kuwa nao!

Mkuu mimi sija kataa kuwa na uraia wa nchi mbili. Ila napima hasara na faida zake. Ili kuonyesha faida zake ni lazima mtu aorideshe faida za kuwa na uraia wa nchi mbili. Huyo niliyemquote alilist yeye anazo ona ni faida za dual citizenship. Mimi nimemuuliza swali rahisi tu kwamba hivyo alivyo viorodhesha haviwezi kufanyika bila dual citizenship? Sasa mimi swali sija jibiwa tayari naulizwa swali? Tukifanya hivyo we will be going in circles. Mimi sijakataa faida zake nimeomba tu kuambiwa ni vitu gani mtu anaweza akafanya na dual citizenship chenye manufaa kwa taifa ambacho hawezi kufanya bila hiyo dual citizenship.
 
Mkuu Ngekewa,


Kaka! Hivyo unafikiri kila kilichopitishwa hapo mwanzo kilikuwa sahihi? Kama ni hivyo basi tusingedai Katiba mpya!
Hivyo unafikiri ni sahihi kumnyanganya uraia wa kuzaliwa mtu eti kwa kuangalia maslahi? Yaani unafikiri ni dhambi mtu kupata sifa ya kuweza kuendesha maisha yake akiwa nje ya nchi yake? Hii ndiyo inayowalazimisha Watanzania wachukuwe uraia wa nchi nyengine ili wapate sifa ya kuwafanya wapate masilahi ndani ya nchi ya ugenini. Sasa iwapo wenyeji wa nchi ile hawajali wewe kubaki na uraia wa nchi yako uliyozaliwa inakuwa kichekesho kuwa wewe uliemzaa unasema huyu si mwanangu.

Sheria za nchi lazima ziangalia interest za taifa kiujumla. Huwezi sema sheria ianzishwa ilimradi tu kumridisha mtu. Kwa hiyo napingana na wewe la hili la kuanzisha katiba eti bila kuangalia maslahi. Kwa hiyo unataka kusema mkuu kwenye sheria zetu tusiwe tunaangalia tena maslahi ya taifa bali tuweke tu sheria? Hili silielewi kabisa. Unless ufafanue mkuu una maanisha nini ukisema si lazima kuangalia maslahi.

Hili suwala la mtu kuukana uraia wa Tanzania limewekwa katika Katiba kimakosa kama mambo mengi yaliyowekwa huko nyuma na tuikaamuwa kuyabadilisha kwa maslaha yetu. Huko nyuma ilikuwa sheria mtu asifanye kazi zaidi ya moja kujitafutia riziki, asipangishe nyumba yake na sheria chungu nzima zisizo na tija kwa mwananchi.

Mkuu sasa una nichanganya. Hapo juu ulisema tusimnyime mtu kisa maslahi. Sasa hapa unaongelea maslahi. Which is which?

Hili la kumkataa raia wa Tanzania eti kwa kuangalia maslahi si sahihi halafu Kaka unasema eti mtu huyu awe na moyo wa kuekeza kwao na huku umemkataa? Nafikiri ipo haja ya kutafakari na kuondokana na ukungu tuliotandaziwa na siasa za Kijamaa.

Mkuu hapa nani kamtakaa nani inategemea unaangalia kwa upande gani. Kwa upande mwingine unaweza ukasema mtu huyu kaikataa Tanzania kwa kuamua kuchukua uraia wa nchi nyingine. So it depends how you look at it.
 
Mkuu Kiranga,

Nakubaliana na baadhi ya points zako ila mimi nina swali. Samahani lakini nataka tu kujua zaidi faida ya dual cizitzenship. Je mtu kuwa na dual citizenship kuta guarantee wao kuwekeza nyumbani? Je ni majority gani ya Watanzania waliopo nje wana uwezo wa kuja kuwekeza nyumbani? Wataletauwekezaji wa aina gani? Nadhani haya ni maswali muhimu kujiuliza na kujaribu kupata majibu badala ya kuassume tu kwamba kuwa na dual citizenship kuta maanisha kuongezeka kwa uwekezaji.

Sipingani na dual citizenship lakini pia kwa sasa sikubaliana nao moja kwa moja. Ndiyo maana hapa nauliza maswali mengi ili nielewe na nijifunze zaidi. Kwa bahati mbaya so far watu wengi wanajibu kwa kutumia hisia badala ya kuorodhesha ni nini kweli kinaweza kufanyika kwa maslahi ya taifa na hiyo dual citizenship ambacho hakiwezi fanyika sasa. Maana wengi wanaongea kana kwamba ukiruhusu hiyo dual citizenship tu basi uwekezaji utaongezeka maradufu.
 
  • Thanks
Reactions: Nzi
Wahindi kibao wamekuja kufanya kazi/ kusoma US, wameishi, wamechukua uraia, wameona India kuna maendeleo sasa yanayohitaji mchango wao, wamerudi kwao kuendeleza nchi. Wanaipeleka India katika mashindano ya kibiashara kwa benefit zote za raia wa Marekani...
Mjomba, India hairuhusu Dual Citizenship na Wahindi waliochukua Uraia Marekani hawana lao India.

Overseas Citizens of India:

  • You do not get Indian passport.
  • No voting rights.
  • Can not be candidate for Lok Sabha/Rajya Sabha/Legislative Assembly/Council
  • Can not hold constitutional posts such as President, Vice President, Judge of Supreme Court/High Court etc.
  • Cannot normally hold employment in the Government.
Source: KATIBA YA INDIA, na taarifa ya Ubalozi inayowatahadharisha Wahindi wabobezi kwamba mkiondoka imekula kwenu: Dual Nationality | Embassy of the United States New Delhi, India
 
Mkuu Kiranga,

Nakubaliana na baadhi ya points zako ila mimi nina swali. Samahani lakini nataka tu kujua zaidi faida ya dual cizitzenship. Je mtu kuwa na dual citizenship kuta guarantee wao kuwekeza nyumbani? Je ni majority gani ya Watanzania waliopo nje wana uwezo wa kuja kuwekeza nyumbani? Wataletauwekezaji wa aina gani? Nadhani haya ni maswali muhimu kujiuliza na kujaribu kupata majibu badala ya kuassume tu kwamba kuwa na dual citizenship kuta maanisha kuongezeka kwa uwekezaji.

Sipingani na dual citizenship lakini pia kwa sasa sikubaliana nao moja kwa moja. Ndiyo maana hapa nauliza maswali mengi ili nielewe na nijifunze zaidi. Kwa bahati mbaya so far watu wengi wanajibu kwa kutumia hisia badala ya kuorodhesha ni nini kweli kinaweza kufanyika kwa maslahi ya taifa na hiyo dual citizenship ambacho hakiwezi fanyika sasa. Maana wengi wanaongea kana kwamba ukiruhusu hiyo dual citizenship tu basi uwekezaji utaongezeka maradufu.

Kusafiri bila kuhangaika na mambo ya kwenda kuomba visa. Uraia wa nchi mbili utapunguza kero ya msafiri baina ya hizo nchi mbili (mojawapo kati ya hizo ikiwa ni Tanzania) kwa kuepuka hicho kizingiti cha kuomba visa. Hii siyo faida?

Uraia wa nchi mbili utawapa Watanzania fursa ya UHURU wa kuwa raia wa nchi zingine ambazo hazina tatizo na wao kuwa raia wa nchi hizo. Kumbuka, uraia wa kupewa kwa sehemu nyingi unakuja na masharti na vivyo hivyo itakuwa vyema na sisi tukaambatanisha masharti yaendanayo na uamuzi wa namna hiyo.

Kwa mfano, mtu akiamua kuwa raia wa Canada basi atapoteza baadhi ya haki na fadhila zinazoambatana na uraia wa kuzaliwa. Tunaweza tukatunga sheria inayotamka kuwa Mtanzania yeyote anayeamua kuchukua uraia wa kwingine atapoteza haki yake ya kuwa mwanajeshi, jaji, au nafasi kadha wa kadha za kiuongozi za kuchaguliwa n.k.

Sasa bwana Mwanafalsafa huoni kwamba uraia wa nchi mbili utapanua wigo wa uhuru - uhuru wa kuamua kwenda kutafuta maisha kwingineko ambako wanakaribishwa bila hofu ya kupoteza uraia wao wa kuzaliwa?

Vilevile, uraia wa nchi mbili utawasaidia watu kwa kuongeza milango ya fursa huko walikoenda kutafuta maisha. Kuna baadhi ya kazi mtu ukiwa kwenye nchi za watu huwezi kuzipata hadi uwe raia. Sasa wapo watu ambao wanashindwa kuzipata kazi hizi si kwa sababu hawana sifa bali wanaogopa/ wanasita kuchukua uraia wa hizo nchi walizopo kwa sababu wanahofia kupoteza uraia wao wa kuzaliwa. Hii wewe kwako si faida? Au unadhani watu wakipata kazi kama hizi wala hawatakumbuka kwao walikotoka?

Pia, hakuna sababu yoyote ya msingi ya mtu, tena mtu ambaye ni raia mwema na mtiifu, kupoteza uraia wake wa kuzaliwa kwa sababu tu eti kachukua uraia wa nchi nyingine. Hakuna mtu mwenye haki ya kumnyang'anya raia mwema na mtiifu uraia wake wa kuzaliwa.

Watanzania wakati umefika wa sisi kwenda na wakati. Cha muhimu ni kwenda na huo wakati kwa kutumia hekima na busara na kujifunza kutoka kwenye makosa ya wengine. Ugumu uko wapi hapo?
 
Ni kakundi kadogo mno ka wa tz wenye acces na izo faida za uraia wa nchi nyingi,mnaposema kusafiri, ni wa-tz wangapi wanaoshindwa kusafiri hata nje ya mikoa yao walozaliwa?
 
jamani watanzania tusiwe wagumu kukubali maendeleo, yameshatokea na tusipoendana na hali halisi tutapata hasara. Katika enzi hizi uraia wa nchi 2 ni muhimu sana. Watanzania wote walioko nje wako kimasomo au kikazi kwa sababu kuna maslahi zaidi. Pesa wanazopata huko wakiituma nchini hua ni kubwa sana na inawezafanya vitu vikubwa mfano dola ikiwa us ni ndogo lkn ikitumwa tz ni kubwa. Watanzania hufanya kazi nje lkn wanatuma pesa kuendeleza nyumbani. Kuwanyima huu uraia ni kuwanyima haki ya msingi na kunarudisha nyuma maendeleo
 
Mimi binafsi ni raia wa Tanzania na ninaishi Tanzania! Nimekuwa nikijiuliza swali hili mara nyingi sana maana mimi si kama hao wanaotaja USA, Canada, Brazil, India Singapore na Mexico kama mifano michache ya uraia wa nchi mbili na kutuhamasisha na sisi tuige huko. Naamini sisi kama nchi tuna mifumo yetu (ambayo pia huendana na wakati), sasa tunatakiwa tuitazame, tuifanyie utafiti wa kina kweli kweli kisha tuzungumze sio kutaja tu mifano! Tofauti zetu na hao ni nyingi mno sio kuwaiga tu!

Masuala yanayotajwa kama faida ya dual citizenship hayana msingi wowote zaidi ya manufaa binafsi kwa wanaoulilia: kwa mfano mtu anasema anakosa sifa ya kugombea uongozi!!!! Sasa wenzangu jamani mtu amezaliwa ughaibuni, amekulia huko, amesomea huko, ameoa/kuolewa huko na ana uraia wa huko miaka yoote hii, leo tunahitaji Mbunge ndo anakuja Waooh! hii ni kashfa kabisa, tena ni matusi, anaelewa nini huyu kuhusu sisi?? Wengine wanadai wawe na haki ya kupiga kura nchi zote mbili! hii ni commedy kabisa.

Wawekezaji: Naomba msaada kwa hili sina data, sijawahi kusikia mwekezaji wa MAANA mtanzania anaetamba kweli kweli kiasi cha kuhitaji kuja kuwekeza hapa na akakosa nafasi ukiacha hawa wakwetu hapa tunaowafahamu. Sana sana watakwambia wanatuma pesa nyingi sana huku, wapi Bwana kumtumia pesa za matumizi mzazi wako ndo tukuite mwekezaji na kukupa dual citizenship? HAPANA!

Kwa kumalizia: Kuna mchangiaji mmoja kasema huduma za afya ni bora zaidi huko ughaibuni kuliko hapa kwetu! Sielewi ni nani aliziboresha huko aliko na yeye anazitumia tu (kama kupe) hana wazo wala mpango ni namna gani za nyumbani zitaboreshwa na anafikiria kuwapeleka hata wazazi wake wakatibiwe huko! na sie tusioweza kufika huko ndo tufe tu au ulikuwa una maana gani? Kimsingi hili suala halina MASHIKO ya jumla zaidi ya mtu mmoja mmoja na halina tija kwa taifa mpaka usawa huu.
 
  • Thanks
Reactions: Nzi
Mimi ni Mtanzania ambaye nitachukua passport ya Marekani mwaka huu. Naomba ufahamu yafuatayo ndugu yangu

1. Hakuna kipengele Chochote kwenye application ya passport ya hapa inayosema unatakiwa kukana uraia wa nchi yako. Nimefanya application sijaona sehemu hiyo. Hii ni kwasababu Marekani wanaruhusu watu kuwa na uraia wa nchi mbili.
2. Uenyeji: Huku marekani watu wengi wamekuja kutafuta maisha kwenye kazi masomo na mambo mengineyo mengi. Uraia unasaidia mambo yafuatayo (a) Huna sababu ya kuomba vibali vya kusafiria hasa kwenye kazi- Wamerakani wengi hawahitaji vibali vya kusafiria kwenye kwenye nchi nyingi za nje hivyo inapunguza usumbufu na gharama kubwa za visa hasa kama kampuni yako inahitaji wewe usafiri.(b) Vilevile unaweza ku vote (c) Kuna kazi ambazo zinahitaji raia tu hasa kwenye IT au research kama Nasa, Petagon n.k. Kuna kitu kinaitwa Goverment Clearance ambayo ni ngumu kupata kama huna uraia. (d) Sheria- Kuna sheria nyingi za immigration zinabadilika hivyo watu wengi wanapenda kutoa pressure ya kuishi kwa woga woga hasa kama wana familia mfano ukipata kesi hata kama ndogo lakini huna uraia unaweza kuwa deported/kurudishwa nyumbani bila kujali ukubwa wa kesi au familia yako. (e) Ukiwa na Uraia unaweza kuwaleta wazazi wako huku kwenye vitu kama matibabu n.k bila kuingia gharama za internation. Healthcare ya Tanzania kwa mfano ni ya chini sana hivyo ki afya unaweza kuwaleta wazazi wakapata matibabu au screening za afya kwa bei nafuu sana (f) Biashara- Kuna mikopo inayohitaji uwe raia kama small Business administration loans.
Umuhimu wa uraia wa Tanzania: Tanzania kwasababu ndiyo ulikotokea hakuna mtu anayependa kupoteza uraia kwasababu ya familia mfano watu wengi wangependa kwenda kuzikwa na ndugu zao, mirathi pia iko nyumbani Tanzania. Ndugu wengi pia wako nyumbani Tanzania hivyo watu wakienda kusalimia ndugu hawataki kupewa siku na serikali za kukaa nchini au serikali kukuambia huna haki ya kumiliki ardhi hata kama ni ya baba yako. Nchi nyingi wanaelewa hili na ndiyo maana kuna Dual Citizenship kama isingekuwa muhimu USA, Canada, UK, Nigeria, India, China, Brazil, Mexico, n.k wasingeruhusu!!
Uoga wa Tanzania: Tanzania inasema inaogopa hawa watu wanaweza kukimbia nchi!!?
Je hii inafada gani kwa Mtanzania wa Kawaida? Kama wewe ni Mtanzania na unaishi Tanzania basi Mtanzania mwingine kuchukua uraia wa nchi nyingine hutabadilisha maisha yako hivyo hili siyo swali la msingi. Lakini kama wewe ni Mtanzania mwenye uraia wa nchi unayoishi basi itakusaidia hivyo wanaosema itamsaidia vipi Mtanzania wa kawaida huu si msaada bali ni haki tu ambazo huyu Mtanzania anazipata kwasasa! na hataki kuzipoteza kwasababu hizo hapo juu!

Je hawa watakuja kuchukua ardhi yetu! Hawa watu wanaomba uraia wa nchi mbili ni wa Tanzania kwa sasa na kama wanataka kuchua kitu basi wangeweza kuchukuwa kabla ya kuchukua uraia wa nchi nyingine hivyo hili nalo si la msingi!
Wataiba pesa ka kukimbia nje? Kwanza hili siyo la kweli kwani uraia wa nchi mbili hauzuii mtu kukimbia! au kuiba pesa. Ukweli vilevile Watanzania walioko nje wanapeleka nyumbani pesa nyingi kuliko pesa inayotoka nyumbani kwenda nje hivyo kama ni uizi badi ni kwa nchi wanazoishi na sio Tanzania.

Tatizo lingine Watanzania wanaona kama kunakitu cha kuiba Tanzania je ni nini cha kuiba hapo! Kama kuna vitu vingi vya kuiba je ni kwanini Watanzania wanapigania ubalozini kwenda nje kwenye vyuo na kutafuta maisha? Je kama una ndugu nje kwasasa ni Mfisadi? amawahi kukuomba hata pesa? Tanzania imemsadia nini kumlipia chuo? Tuacheni kuwachukia Watanzania wenzetu walio nje hawa si wafisadi ni vijana wanaotafuta maisha kama wengine.

Nyekundu: Ndugu yangu, kwa taratibu za Tanzania, kama ukishachukua passport ya nchi nyingine, automatically unakua umeukana utanzania, kwa sababu sheria haziruhusu mtu kuwa na passport ya nchi nyingine!! Hivyo si lazima kuwe na kipengele kwenye izo application procedures za nchi nyingine ndio ionekane umeukana utanzania.

Kjanii: I don't see any national interests kwenye hayo maelezo yako. Yote uliyoyaeleza yanalenga katika kufaidika wewe binafsi na familia yako!! So still naamini dual citizanshep has no national benefits.

Bluu: Kama ndio hivyo kwanini hujiangaishe kuchukua uraia wa nchi nyingine wakati bado unatamani kupata privileges za kuwa mtanzania?!?! Hapa inajidhihirisha ulivyo mbinafsi!

Njano: Ndugu yangu ingawa tunaishi katika globalised world, lakini nchi kama nchi haiwezi kua inafanya kila jambo kwavile taifa fulani linafanya. Suala la dual citizenship lazima lijadiliwe kwa kina na watanzania (kupitia a national debate) ili sisi kama watanzania tuweze kujirisha kwamba suala hilo lina faida nyingi kwa taifa kuliko faida nyingi kwa mtu binafsi. Sisi watanzania tunapenda kufananisha nchi yetu na yanatokea katika nchi zingine kwa mambo binafsi, lakini mambo ya faida kwa taifa wala. Mfano, wewe unaishi Marekani, kwanini uishauri serikali ya Tanzania itumie mfumo wa IRS katika ukusanyi wa kodi na kudhibiti money laundering na watu kutajirika bila concrete financial bases?

Nyeusi: Hapa unaendeleza kuelezea juu ya personal benefits.

Zambarua: Ndugu yangu, naona kuishi nje kumekufanya usahau hali ilivyo hapa. Kwa serikali hii ya CCM hayo uliyazungumza ni vigumu kuyaepuka. Hujasikia jinsi raia wa kigeni siku hizi wanavyojichukulia ardhi utafikiri ya kwao? Hivyo uoga wa waTZ katika suala la ardhi ni genuine kutokana na hali ilivyo sasa. Pia kama hao unaowaita watanzania walio nje wangechukua ardhi wakati ni watanzania, mimi sina shida katika hilo. Kuhusu wizi wa pesa, bado suala la mfumo mbovu uliopo sasa hautaweza kudhibiti suala hilo. Kuhusu pesa nyingi kutoka kwa hao watanzania walio nje, sidhani kama una takwimu sawa, kwanza unafahamu idadi yao? Pia pesa wangeweza kuleta nyumbani hata kama wangekua hawana passport za nchi nyingine. Mfano ,takwimu zinaonyesha kua wakenya, wanaigeria na waghana walio nje ni kati ya mataifa ya Afrika yanayoongoza katika remittances; na hao sio wenye uraia wa nchi mbili tu!!

Damu ya mzee: hizo dharau sasa. Umesahau tuna kila aina ya maliasili hapa? Kwanini ujiulizi juu ya ujio wa wazungu na makampuni yao hapa? Wanafuata nini? Hao si umeshasema wanafuata maisha bora!! Hivyo wanakimbilia mambo yao binafsi.

Bluu mpauko: Mimi binafsi simchukii mtu yeyote alieenda kutafuta maslahi mazuri, ninachochukia na suala la wao kushinikiza uwepo wa dual citizenship ili waendelee kufaidi maslahi mazuri ambayo kama taifa halifaidiki kwa kiasi kikubwa!

Asante.


 
Naomba niongezee lingine hapa

Masilahi binafsi au ya umma

Maslahi binafsi ya mtanzania mara nyingi ndiyo maslahi ya umma Mfano. Mimi nikifanya kazi hapa nitatuma pesa kumsaidia mtoto wa kaka au dada kwenda shule ni maslahi ya binafsi na ni maslahi ya uma. Mimi nikituma pesa za matibabu kwa mzazi wangu Tanzania ni maslahi binafsi na maslahi ya uma. Mimi nikituna pesa ya kujenga nyumba ni maslahi binafsi na maslahi ya uma. Mimi nikija Tanzania kutembea na kutumia pesa ni maslahi binafsi na maslahi ya uma. Mimi nikipata elimu kwa pesa yangu mwenyewe bila ufisadi au kuiba kwenye kampuni ni maslahi ya nchi na maslahi ya uma. Mimi nikipata mwanga kwasababu ya kuishi nje na kukuelimisha hapa ni maslahi ya binafsi na maslahi ya uma. Kuna mengi hivyo hoja ya kusema kwamba kunatofauti ya maslahi ni potofu na isiyoangalia mbali. Maendeleo ya watu binafsi ndiyo yayoleta maendeleo ya nchi.

Hayo yote uliyoyataja huwezi kuyafanya ukiendelea kua na passport ya Tanzania ukiwa nje? Yaani kufanya yote hayo ni mpaka uwe na dual citizenship?! Si kweli!
 
Kwa sababu hauendani na mabadiliko ya dunia. Nikikwambia kuna mtanzania ambaye ni raia wa UK alinyimwa visa ya kuja TZ utaamini? unadhani huyo atawekeza TZ?

Hebu legeza ubongo wako na ufanye tathmini ya kina kwa nini Wachina, Wahindi na Wanageria wametapakaa duniani kote mpaka wamefungua mabenki yao na TV station zao? Usihitimishe kwa majibu mepesi kama vile population yao.

Umepata kujiuliza why mathalani wahindi faida zao hawaziweki TZ?

Ondokana na mawazo ya kipindi cha vita baridi pamoja na psychological effects za ukoloni.

Uraia wa nchi mbili ni muhimu sana kwa taifa lolote linalotaka kuondokana na umaskini.

Hivi unajua Tanzania inapoteza kiasi gani kwa mwaka kwa sababu ya watu wake kubanwa na uraia wa nchi moja?

Nyekundu: ndugu, huyo sidhani kama ataitwa mtanzania tena..ndie maana alihitajika kupata visa kwanza. Angekua mtanzania hasingepaswa kuomba visa.

Bluu: ndugu, unataka kumaanisha kote walipotapakaa hao kuna dual citizenship???!? Mbona wachina wapo kibao hapa Bongo na wamewekeza lakini hakuna dual citizenship?!

Kijani: ndio maana nimeomba msaada wa kupata faida za suala hilo kwa taifa. Basi kama mtu unaeona kua suala hilo lina faida kwa taifa, ebu nifafanulie juu ya faida hizo.

Njano: sijui. Ebu nipatie takwimu hizo.

Asante
 
Membe na viongozi wengine wengi CCM wana maslahi binafsi kwenye hili swala la uraia wa nchi mbili. Watoto wao wengi wako nje na wengine ameshachukuwa uraia wa huko, e.g Membe - Canada. Hiki wanachosema kuhusu kuwawezesha kuwekeza nchini ni kiini macho. Kwani ni kitu gani kinawashinda kufanya hivyo kwa sasa? Ni vizuri hili swala lisiangaliwe kinadharia kwa sababu litachochea kwa kasi ya ajabu kuhamisha 'capital' na rasilimali nyingi. Kwa sasa Rostam yuko wapi? Na yule dalali wa Rada yuko wapi? Watu watahujumu uchumi kwa kiwango cha juu na kutuweka! Dont tell me interpool maana hata sasa wapo lakini dalali wa rada bado anapeta!

Hawa wanasiasa wamekuwa waongo sana, hivi kuna watanzania wangapi nje ya nchi? na kati yao ni wangapi wana uwezo wa kuwekeza kiasi kwamba ni lazima tubadili kanuni za uraia.

Binafsi ningependa hili jambo la uraia liwe-implemented baada ya kuweka misingi imara ndani ya nchi kwa ajili ya kuzuia capital-outflow na pia kudhibiti watuhumiwa wa makosa mbalimbali makubwa kukimbia. Sidhani chini ya uongozi tulionao kwa sasa tuko tayari lakini kama ikatokea (and I hope it will happen -soon) tukawa na uongozi imara wa nchi na wenye uthubutu wa kusimamia sheria basi uraia wa nchi mbili utakuwa wa manufaa. but not now. SORRY.

​That is what I am talking about.
 
Kunyima watu dual citizenship ni kujirudisha nyuma. Hao matajiri wenyewe kina Marekani na Uingereza wanajua umuhimu wa hiki kitu katika biashara ya kimataifa. Mara nyingine tunajifungia milango wenyewe halafu tunalaumu mvua hazinyeshi.

Wahindi kibao wamekuja kufanya kazi/ kusoma US, wameishi, wamechukua uraia, wameona India kuna maendeleo sasa yanayohitaji mchango wao, wamerudi kwao kuendeleza nchi. Wanaipeleka India katika mashindano ya kibiashara kwa benefit zote za raia wa Marekani.

Dual Citizenship ni kama vyama vingi vya siasa, ni trend ambayo utake usitake inakuja, sasa uamuzi ni wetu kama tunaamua kuikubali leo ili tupate a leg up on it's advantages au tuikubali miaka 50 ijayo wakati wenzetu hawaongelei dual citizenship tena, bali washachafua dunia wanataka kuikimbia waende kuhamia sayari nyingine.

Wakati sie tutakuwa tumebanana Kisarawe kwa kuwa hatutaki raia wawe na dual citizenship.

Hii habari ya kuwaminyia watu dual citizenship haina tofauti na ile habari ya kukataza watu kusafiri na kuwa na passport, baadaye tutakuja kuangalia nyuma na kusema "duh, hapa tuliboogie step sana" kama hatutaikubali.

Huwezi kuniambuia mei leo nije kuwekeza Tanzania kwa terms za foreigner eti kwa sababu nimechukua uraia wa Marekani. Na Marekani kuna mi ofshore investment siwezi kui explore kama naishi kwa green card.

Kwa hiyo hiyo dual citizenship ikija poa, isipokuja napo poa vile vile, tutakuja kwa visa tu au kuchukua permanent residency ya huko.

Vyema. Niorodheshee faida na hasara za dual citizenship ili niweze kuchuja pumba na mchele.
 
People with dual citizens enjoy many privileges, example of voting in both countries, owning property in both countries, and having government health care in both countries. These are just few exhibits.

To say the truth, dual citizenship is becoming more common in our increasingly interconnected, global economy. Many countries are now seeing the advantages of dual citizenship and are liberalizing their citizenship laws (India, the Phillippines, and Mexico are recent examples).

Dual citizenship has the advantages of broadening a country’s economic base by promoting trade and investment between the dual citizen’s two respective countries.

So, it is better for Tanzania to adopt and/or allow dual citizenship.

What you have said can be done without dual citizenship!! Still I am asking, what is so special about dual citizenship?!
 
Mwanafastafa Je mimi nikichukua uraia wa USA na bongo nina kunyima au kukuzuia nini wewe kwenye maendeleo yako. Au je Mimi nitakuwa na hasara gani kwa jamii ya Tanzania?. Hivi mnavyosema hivyo je USA wangekuwa na mawazo kama hayo kungekuwa na Watanzania hapa kweli kwamba kila mtu akija huku ni kwasababu ya kutaka kuiba na sisi tunavyotuma pesa nyingi kutoka nchi hii ingekuwa Tanzania ingekuaje? Lakini ndiyo maana hii nchi ni tajiri. Watanzania bado tunafikiria kimasikini na kama msikokuwa makini tutaachwa sana na wenzetu kama wa Rwanda ambao wanawatumia sana ndugu zao walio nje

Hayo yote unayosema bado hayahitaji dual citizenship!!
 
Kwa sisi wengine tungependa kujuwa kuwa mtu akiwa na uraia wa nchi mbili anakuwa analeta hasara gani wala sio suwala la Umembe au nani? Membe ataondoka lakini hali hii ya Watanzania kunyimwa haki yao itaendelea mpaka lini?

Pengine donge limekupofuwa!

Kusafiri bila kuhangaika na mambo ya kwenda kuomba visa. Uraia wa nchi mbili utapunguza kero ya msafiri baina ya hizo nchi mbili (mojawapo kati ya hizo ikiwa ni Tanzania) kwa kuepuka hicho kizingiti cha kuomba visa. Hii siyo faida?

Uraia wa nchi mbili utawapa Watanzania fursa ya UHURU wa kuwa raia wa nchi zingine ambazo hazina tatizo na wao kuwa raia wa nchi hizo. Kumbuka, uraia wa kupewa kwa sehemu nyingi unakuja na masharti na vivyo hivyo itakuwa vyema na sisi tukaambatanisha masharti yaendanayo na uamuzi wa namna hiyo.

Kwa mfano, mtu akiamua kuwa raia wa Canada basi atapoteza baadhi ya haki na fadhila zinazoambatana na uraia wa kuzaliwa. Tunaweza tukatunga sheria inayotamka kuwa Mtanzania yeyote anayeamua kuchukua uraia wa kwingine atapoteza haki yake ya kuwa mwanajeshi, jaji, au nafasi kadha wa kadha za kiuongozi za kuchaguliwa n.k.

Sasa bwana Mwanafalsafa huoni kwamba uraia wa nchi mbili utapanua wigo wa uhuru - uhuru wa kuamua kwenda kutafuta maisha kwingineko ambako wanakaribishwa bila hofu ya kupoteza uraia wao wa kuzaliwa?

Vilevile, uraia wa nchi mbili utawasaidia watu kwa kuongeza milango ya fursa huko walikoenda kutafuta maisha. Kuna baadhi ya kazi mtu ukiwa kwenye nchi za watu huwezi kuzipata hadi uwe raia. Sasa wapo watu ambao wanashindwa kuzipata kazi hizi si kwa sababu hawana sifa bali wanaogopa/ wanasita kuchukua uraia wa hizo nchi walizopo kwa sababu wanahofia kupoteza uraia wao wa kuzaliwa. Hii wewe kwako si faida? Au unadhani watu wakipata kazi kama hizi wala hawatakumbuka kwao walikotoka?

Pia, hakuna sababu yoyote ya msingi ya mtu, tena mtu ambaye ni raia mwema na mtiifu, kupoteza uraia wake wa kuzaliwa kwa sababu tu eti kachukua uraia wa nchi nyingine. Hakuna mtu mwenye haki ya kumnyang'anya raia mwema na mtiifu uraia wake wa kuzaliwa.

Watanzania wakati umefika wa sisi kwenda na wakati. Cha muhimu ni kwenda na huo wakati kwa kutumia hekima na busara na kujifunza kutoka kwenye makosa ya wengine. Ugumu uko wapi hapo?

Faida kwa taifa je?! Maana umeorodhesha faida kwa mtu binafsi tu!!
 
jamani watanzania tusiwe wagumu kukubali maendeleo, yameshatokea na tusipoendana na hali halisi tutapata hasara. Katika enzi hizi uraia wa nchi 2 ni muhimu sana. Watanzania wote walioko nje wako kimasomo au kikazi kwa sababu kuna maslahi zaidi. Pesa wanazopata huko wakiituma nchini hua ni kubwa sana na inawezafanya vitu vikubwa mfano dola ikiwa us ni ndogo lkn ikitumwa tz ni kubwa. Watanzania hufanya kazi nje lkn wanatuma pesa kuendeleza nyumbani. Kuwanyima huu uraia ni kuwanyima haki ya msingi na kunarudisha nyuma maendeleo

Hayo yote yanawezekana bila ya kua na dual citizenship​!!
 
Kuna wapinzani na watetezi wa hoja ya uraia wa nchi mbili. Watetezi wa uraia wa nchi mbili wapo Benard Membe na wengineo wengi ambao viongozi wa serikali. Hoja yao kubwa ni kwamba tukiruhusu uraia wa hoja mbili watz walioko nje watawekeza nyumbani nasi tutainua uchumi wetu. Vile vile kuna suala la kuvutia wawekezaji wengi zaidi hasa wale ambao watawekeza kwa kujiamini kutokana na kupata uraia.

Hawana hoja nyingi sana.Wapinzani wa uraia wa nchi mbili wanadai kwamba, tukiruhusu tutawapa mafisadi mwanya wa kutokamatika maana akifanya ufisadi ktk nchi yetu anakimbia nchi nyingine( Rostam?) ambayo yeye anauraia nao pia. Pia wanadai huu upopo utapunguza uzalendo kwa sababu mtu mmoja hawezi kupenda nchi mbili kwa wakati mmoja.

Vile vile wanadai kuwa kutokana na umaskini wetu wenye hela hasa nchi za magharibi wanaweza kumweka mtu yeyote madarakani kupitia mamluki wao ambao watakuwa wamepewa uraia hapa kwetu Tanzania. Zaidi sana pengo kati ya maskini na tajiri zitaongezeka sana. Kwa kuwa matajiri toka nje ( wakipata uraia) watakuja kufanya biashara wakishirikiana na matajiri watz wachache.

Binafsi niko pagumu kuamua ni jambo gani la kuunga mkono na lipi la kupinga. Nawasilisha.
 
Back
Top Bottom