Uraia wa nchi mbili: Maendelo na Matokeo yake!

Waungwana,

Kwanza nipige hodi kuingia kwenye ukumbi maana nilipotea kwa miezi kibao. Ni busara kuwasalimia wenye kijiwe kila urudipo toka safarini. Nimefurahi kusoma
hoja zenu na hii ni dalili nzuri kwamba wote mu wazima.

Nikija kwenye hii hoja hasa kuhusiana na Mwanakijiji. Anasema uraia wa nchi
mbili unafaidi kwa watu husika lakini hauna faida kwa taifa. Hapo ndipo tunapotofautiana sana.

Katika maendeleo yoyote hapa duniani yanakuja kutokana na juhudi ya mwanadamu kujiendeleza yeye mwenyewe na matokeo yake analeta maendeleo kwa yeye, familia yake na jamii yake nzima.

Kama uraia wa nchi mbili una faidi kwa kundi kubwa la Watanzania wanaoishi nji za nchi na hakuna madhara makubwa kwa taifa naona ni jambo zuri kulikubali hata kama halitabadilisha maishi ya watanzania milioni 30 wengine.

Ni sawa na shule, nchi inasomesha watu wachache kwa mamilioni na mara nyingi faida kubwa inaenda kwa wahusika ingawaje hata wengine wanafaidika indirectly.

Watanzania walioko nje kwasasa wanasaidia familia na jamii zao kwa njia mbalimbali kuanzia kusomesha, matibabu, maendeleo kwenye jamii nk. Kama hawa Watanzania wanaona neema yao hiyo itaongezeka kwa kuwa na uraia wa nchi mbili, naona ni jambo zuri kulitazama suala zima na kama hakutakuwa na matatizo mengine makubwa basi tuwakubalia.

Kitu cha msingi ni kwamba mpaka sasa Tanzania inaruhusu uraia wa nchi mbili kwenye baadhi ya makundi. Inaelekea hili wachangiaji wengi hawalijui. Kama wewe ni Mtanzania na umemuoa mgeni kwa mfano Mcanada na mkaamua kuishi Tanzania, baada ya muda mkeo anaweza kupata uraia wa TZ bila kuambiwa apoteze uraia wa nchi yake ya mwanzo. Naamini kuna mawaziri pia
wana wake zao ambao wana uraia wa nchi mbili. Sina uhakika lakini nadhani hata profesa Mwandosya ambaye alitaka kuwa rais ana mke kutoka Uganda. Huenda huyo mama bado ana magamba yake mawili na sheria inaruhusu hivyo. Lakini kama mwanamke kaolewa na mgeni na wamerudi kuishi TZ, basi huyo bwana hawezi kupata uraia wa TZ mpaka aukane uraia wa nchi alikotoka. Hapo kuna kaubauguzi ka aina fulani.

Pia kuna kundi la watoto, watoto mpaka miaka 18 wanaruhusiwa kuwa na uraia wa nchi mbili. Mfano mtoto akizaliwa UK kwa wazazi ambao wana permanent residence hapa basi moja kwa moja anakuwa na uraia wa UK hata kama wazazi wake wanakuwa sio raia. Wakati huo huo pia anakuwa raia wa TZ kutokana na wazazi wake kuwa Watanzania. Akifikisha miaka 18 inatakiwa aukane uraia wa UK ama sivyo anapoteza uraia wa TZ. Hapa pia ndio kwenye
kasheshe, baadhi ya hawa watoto wameishi miaka yote huku nje lakini pia wanataka kuendelea kuwa na uhusiano na nchi walikotoka wazazi wao. Ukiwaambia sio raia kwasababu una uraia wa nchi nyingine, tayari unawatupa
wananchi kwenye maelfu ambao huenda wangesaidia kuiendeleza nchi yetu huko mbele.

Hapa Europe kuna mifano mingi sana, kuna raia wengi wa nchi kama Italy na Poland waliondoka baada ya vita kuu ya pili kutokana na mambo ya kisiasa. Wengi walikuja UK na USA. Baada ya mabadiliko ya siasa ni watoto zao ndio
wanaongoza kupeleka vitega uchumi kwenye nchi walizotka wazazi wao.

Kwanini sisi tunataka tujifungie na kuwanyima kizazi chetu kijacho nafasi ya kushiriki kwenye maendeleo ya TZ?

Kama alivyosema Lowassa, wananchi wengi walioko nyumbani hawaelewi hili
jambo ni nini na ni moja kati ya masuala ambayo ukifuata wingi wa watu wanaopinga bila kuangalia matakwa ya kundi husika unaweza kujikuta unatunga sheria mbovu kwa maendeleo ya taifa.

Mtanzania.
 
Swahiba nimekupata,
Kwanza, bado natetea kabisa kuwa DC kwa Tanzania bado, nafikiri kabisa watanzania bado ule mwamko haujatufikia bado, kama alivyosema mmojawetu hapo juu je ni asilimia ngapi ya watanzania watafaidika? Angalia hao wabongo walio nje Versus Wageni watakao faidika. Tumeongelea tu hiyo social/ community impact na DC, je tumeongelea kuhusu political/ economic deeply? Kwa mifano tu:

AGOA - Hivi jiulize, hii ni kama ile "affirmative action" ya marekani kwa waafrika, tumefaidika nini Africa au Tanzania? Sijasikia hata kampuni moja ya Tanzania ambayo imexport huko marekani at least USD 1million per annum. Sunflag wale wahindi wa Arusha wameitumia hiyo, indigeneous hata mmoja hayupo.
EU- Everything but ...- Hii imemsaaidia nani Africa particulary Tanzania? Ile minofu ya samaki, nani ana-export na nani anafaidika, go deep, na sisi tunabakiziwa mapanki.
China Import Tax Treaty for Africa- Ushuru 0 (ZERO) kwa bidhaa zote zitokazo nchi 25 za Africa including Tanzania. Je how did a common man in Tanzania utilize this?
Kuna treaty nyingi sana ambazo zinaweza kutuondoa katika umasikini, lakini hakuna action inayochukuliwa na serikali aut Taasisi kuhamasisha watu kutumia hizi treaty kuuondoa umasikini kwa kutumia hizi opportunities; nani anafaidika? Je tunayo competition advantage?

We have to workout this first!

Kuhusu China na overseas Chinese:
Mchina yoyote mwenye damu ya mtu wa China anaitwa overseas Chinese, haina lolote kuhusu Uraia. Ukiproove tu wewe una Uchina ndani yake basi wewe ni Overseas Chinese. Hii ya passport ya China hamna kabisa uhusiano huo. Overseas Chinese wako kokote duniani na treatment yao kwa serikali ya China ni special tu wakati unaongelea investment, lakini kuhusu uraia, wako treated sawa sawa na foreigners wengine. Ni Taiwanese (ROC= Repulic Of China) na HOng Kong residents (SAR = Special Administration Region) wako treated na card maalum, lakini si suala la DC. Chinese American au Tanzanian Chinese hawana kabisa hiyo treatment. Wanatumia tu passport zao za respective countries.
Note above: PRC = People's Republic of China (China haitambui ROC, inatambua tu Taiwani ni Kisiwa cha PRC na ni province yake).

Sasa turudi huko kwenye suala letu la DC. Je hawa wachina, wahindi au na wowote wale serikali zao ziliruhusu kwanza DC ndiyo zikaendelea , answer is no. So what happened? Kamuulize mshindo mkeyenge, KANIKI ndiyo rangi yake, hata dobi afanyaje rangi ndiyo hiyo hiyo!

Kwanza nikupe mfano: Wahindi, wachina, wapakistani na wengine kwa nini wametapakaa duniani? Wao walienda nchi za wengine wakaangalia na kustudy sheria za hizo nchi na kuweka makazi, wengine waliangalia loopholes how they can use sheria za nchi hizo na kufanya mambo yao. Wengi wa hawa walikana uraia wao, lakini siyo kuwa damu damu walikana, everything they did for the sake of life. Na hii ni fact dunia nzima. You have to weigh where advantages are then you workout your possibilities. Kwa hiyo kwa wale wahindi, wachina, au pakistanis walioenda marekani kwa kuukana uraia wao (wachina) siyo kuwa walikana ndugu zao, walisacrifice for the sake ya ndugu zao walio nyumbani. Leo hii kuna zaidi ya Wachina 57million as overseas Chinese, na hawa wana roots china, je hiyo western union ina ingiza ngapi kwa siku au mwezi? Je kwa nini sisi tufanikiwe tu hadi ije DC?

Hawa watu wana miamko ya utafutaji, wakienda mahali popote basi huweka nanga na kuanza kufanya kazi. huanzisha community zao, na hufanya mambo yao kama vile wako kwao, na sheria wanazifuata.

Swahiba, ona India na China, biashara zao kwenda marekani au EU kuna quota system, MFN (most favoured nation status), au tax. Sisi tunaambiwa tu-export tunavyoweza hata hivyo hatuna cha ku export. Hata kutumia huo unafuu wa AGOA, EU, China, kuwaita wawekezaji, bado tuko pale pale! What we are lacking? We are lacking Either the revolution theory or we do not know if we are poor.
 
Katika mwaka uliopita, immigrants duniani kote walituma dola Billioni 167 katika nchi zao mbali mbali duniani, does this fact adds anything kwenye huu mjadala? Nawauliza mnaofahamu?
 
Intersted Obseever,
Swahiba hapa bado kabisa hujanikuna!
Ebu rudia kusoma hapo juu haswa kipengele hiki kisha fafanua pale nilipohighlight:-
Most of these members elected to the Legislative Yuan hold dual citizenship, but must renounce their foreign citizenship (at the American Institute in Taiwan for American citizens) before being sworn in.
Tukirudi ktk swala la Wachina. mshikaji kuna tofauti kubwa sana kati ya hawa jamaa na sisi.
Kwanza hao Wachina unaowazungumzia sijui millioni 50 ni pamoja na wale waliochukuliwa UTUMWA.. yaani vizazi vitatu hadi vinne wamezaliwa nje... hatuzungumzii watu hawa!
Kama nilivyosema ktk mada mojawapo hawa bado ni Wachina kwa asili sina maana wana dual citizenship na hawa waliikana nchi yao kama Wajamaica, Wamerakani weusi n.k.
Mimi sizungumzii watu hawa ama Waamerika weusi wapewe dual citizenship bali nazungumzia Watanzania ambao tumetoka nje hivi majuzi hata miaka 50 haijafika. So tusubiri hadi hapo tutakapo poteza kabisa asili yetu ndipo muweze kutufikiria. besides, nyie akina nani haswa kuidai Tanzania kuliko sisi hali wakati wa Nyerere tulikuwa hatuna tatizo hili... period. Lilikuwepo lakini halikuwa hoja kabisa unapewa pasi bila maswali ya kipuuzi. WHY NOW... mnaogopa kuwa tutakuja chukua UONGOZI?
Hoja zenu nyingi zina-question uwezo wetu sisi hali hakuna kati yenu anayezungumzia Mapungufu yapi yatatokana na sisi kupewa hiyo dual.
AGOA na mengineyo uliyotaja mzizi wake unatoka ndani Tanzania na sio nje. Kuvurunda kote kunatokana na viongozi ndani ya nchi kuwathamini na kuwapa wahindi haki kuliko mimi kwa sababu tu wanaishi/wamezaliwa TZ. Hawa bado wahindi ndugu zangu na matokeo ya makosa yenu ndio haya mnatakiwa kujifunza. Kwa hiyo kama kuna marekebisho ama swala la kujadili hayo ni kuzungumzia Watanzania wenye asili za nje na sio sisi WAZAWA... narudia tena WAZAWA ambao tunaishi nje.
Mwisho nakupa challenge, Kwa miaka 20 sasa hivi ya Utandawazi mmeshindwa kuitangaza nchi au sio? basi tupeni uwezo huo sisi kisha mtaona...tupeni uwezo wa kuitangaza nchi huku nanyenzo zinazotakiwa kama wanavyofanya wenzetu na hizo deal za biashara nje ziwekeni chini ya Watanzania kupitia balozi zetu kisha mtaona mandundu ambayo tunaweza kuyafanya.
Trust me, Umeme msingepata wa Richmond hilo moja nakuhakikishia!
Interested Obserever, sisi tunaishi huku tunafahamu mbinu zote za hawa jamaa tofauti kabisa na wewe unayeishi TZ, mnaamini kwamba hatuwezi kwenda mbele bila misaada. Maswala ya Dar leo hii mimi nitakuuliza wewe na nina hakika kabisa siwezi kuishi Dar hata kwa mwezi bila kuwa na mwenyeji... Hivyo hivyo Afrika inahitaji wenyeji nje na hakuna mwenyeji wa wewe kufikia isipokuwa ndugu yako wa damu - Mtanzania.
 
Interested Obserever, sisi tunaishi huku tunafahamu mbinu zote za hawa jamaa tofauti kabisa na wewe unayeishi TZ na kuamini kwamba hatuwezi kwenda mbele bila misaada. Maswala ya Dar leo hii mimi nitakuuliza wewe na nina hakika kabisa siwezi kusishi Dar hata kwa mwezi bila kuwa na mwenyeji... Hivyo hivyo Afrika inahitaji wenyeji na hakuna mwenyeji wa wewe kufikia isipokuwa ndugu yako wa damu - Mtanzania.

Sijui niseme nini Mkandara hapo! Mwenyewe nimeshuhudia baadhi ya mawaziri na wajumbe wa kamati za bunge wanavyojishaua na kujibaraguza mbele ya wazungu huku ughaibuni. Inasikitisha na kuwa kichekesho at the same time.
 
Yaliyotokea Lebanon juzi baada ya vita na Israel tumeona faida ya uraia wa nchi mbili

Hatuombei lakini tazama scenario ya vita Tanzania...watakao faidika ni akina nani?

Hilo la investments nalo halina mpango kwa sababu wakati wa globalization hakuna atakaekwambia kuwa hataki investment na kwa hilo huhitaji kuwa na uraia wa nchi mbili kuinvest...after all nchi ambayo inahitaji investment ndio itakuwa inakulamba miguu
 
DRWHO,
Hilo la Lebanon, Israel watakao faidika na vita ambayo hatuombei...n.k
Pia swala la Investment na kulambwa miguu!..
Unajua tena wengine vichwa vigumu....kuweka 1x1... tunaona 2. Kidogo inahitaji ufafanuzi.
 
DRWHO,
Hilo la Lebanon, Israel watakao faidika na vita ambayo hatuombei...n.k
Pia swala la Investment na kulambwa miguu!..
Unajua tena wengine vichwa vigumu....kuweka 1x1... tunaona 2. Kidogo inahitaji ufafanuzi.



Ahaaa

unajua baada ya vita vya kwanza baina ya wakristo na waislam pale Lebanon wengi wao waliondoka na kwenda FRANCE,UK,AUSTRALIA&USA in 1980's baada ya hapo wakajikita huko na kuanza maisha yao na kama unavyoua hawa jamaa wengi wana jua sana mambo ya biashara hivyo nchi yao ilipotulia wakarudi na ARI MPYA ya kuijenga nchi yao lakini walibaki na uraia wa nchi zilizowapa hifadhi


Sasa kwa sababu walikuwa na uraia wa nchi hizo ilikuwa ni rahisi kwao kuwa na access ya mitaji waliopata kule nje hivyo waliporudi walikuta wanasiasa amabo wako tayari ku catch up na nchi zinginezo za Middle East...mkind you LEBANON HAWAJAKALIA MAFUTA KAMA WAARABU WENGINE hivyo walitia akili ni kuadjust kutokana na serikali kuwa nao bega kwa bega

FAST FOWARD 2006
Vita baina ya Lebanon na Israel juzi dunia ilishuhudia walebaon zaidi ya laki moja walio na uraia wa nje wakiwa AIRLIFTED na kuokoa maisha yao kwa sababu serikali yao LEBANON ilishindwa kuwahakikishia usalama wao na hiyo ni kwa sababu ya dual citizenship na wengi waliwachukua na ndugu zao

Lakini pia baada ya mambo kutulia leo hii jamaa wamerudi tena wanarebuilt their homeland kutokana na mitaji waliokuja nayo na serikali yao iko OPEN MINDED katika hili


GLOBALIZATION:

Dunia iko so globalized kiasi cha kwamba haya mambo ya citizenship yanapotea kwa kiwango kikubwa mno..vile vile serikali nyingi hazina ubabe mbele ya multinationa companies kama zamani au kwa maneno mengine ni kuwa National Sovereignity ziko under threat...kwa sababu kampuni kama GENERAL MOTORS na BOEING wanapesa zaidi ya tusema serikali ya serikali ya Tanzania hivyo huhitaji kuwa na uraia wa nchi mbili kuinvest Tanzania na pili wakikuletea zengwe basi Mozambique is just next door & the same applies to RWANDA au BURUNDI sasa wasi wasi walikuwa naoa hawa wanaotaka dual citizenship ni wa bure tu...cha muhimu ni kuwa na mitaji then they will listen to you its that simple na lazima watakusikiliza kama kweli wanataka kuwa competitive katika dunia


mfano mwingine ni kuwa hivi sasa hivi hii EAC itajakuwa kuwa kama EU ambako watakuwa na pasiport moja hivyo huhitaji kuwa na uraia wa Tanzania kuwa na freedom ya kuinvest ndani ya bongo kwa sababu unaweza ukawa na uraia wa lets say USA na KENYA hivyo rights zako zinakuwa protected under the EAC law sasa itakuwa kama waingereza walivyokuwa wakipoteza pesa kulimit migrants from Poland amabo baada ya nchi yao kujiunga na EU walirudi hapa kama raia wa EU & on top of that serikali ya UK iliwalipa pesa pamoja na tiket ya ndege kuwarudisha Warsaw sasa kama si uwenda wazimu nini huo?
 
DRWHO,
Ama kweli wewe daktari! nimekupata na dose yako imenisaidia sana.
tena hapa umezua hoja moja kali sana... Hii EAC ina maana Mkenya na Mrwanda anaweza kabisa kuwa na nafasi ndani TZ na asihoifiwe kuliko mimi?. I mean jamani hizi dialogue kwa mzawa hata nashinda kuzielewa hali mgeni anapeta na uraia wetu kirahisi tena kwa nia mbaya.
Matatizo yote ya nyuma tumeyapata kutokana na Wageni kuwa na pasi zetu lakini nashangaa wageni bado wanasikilizwa kuliko sisi. I think kama kweli serikali inataka kuangalia swala hili la Uraia basi WAGENI ndio ingekuwa issue muhimu zaidi.
 
Dual citizenship report ready
SUKHDEV CHHATBAR in Dodoma
Daily News; Wednesday,August 01, 2007 @00:02

THE dual citizenship report has been finalised and presented to the cabinet for scrutiny. Presenting expenditure estimates for the Ministry of Home Affairs for 2007/8, the Minister, Mr Joseph Mungai, said Zanzibar’s views on the subject would be taken into consideration before arriving at the final decision.

He did not disclose what those views were.

Proponents of dual citizenship lobby to allow Tanzanians abroad to invest back home and boost the economy, not as foreign investors but as nationals. The citizenship law of 1995 does not provide for dual citizenship.

Tanzanians living abroad have been lobbying for sometime now to allow them bring their estimated $2.5 billion wealth and expertise into the country. Most of them had left the country in the early ’70s and ’80s.

Mr Mungai also said that national identity cards (IDs) project has made headway and is expected to be ready by 2009. It is estimated that the project will cost the government about $35 million.

“We have already acquired a building for the project,” he added. In collaboration with the ministry of Civil Service Management and other stakeholders, efforts were underway to form an agency which would supervise the distribution of the IDs, he said.

To improve work of the immigration department, Mr Mungai said that construction of Immigration offices in Dar es Salaam has already started. The immigration college’s rehabilitation was in the final stages in Moshi and planned to be opened next month. The department will also recruit 374 officers and planned to send 140 others for different refresher courses.

The prisons department will employ 812 new officers and train 300 to augment critical shortage of staff and to offer better services. The government will also rehabilitate and improve roads to high-security prisons in Maweni (Tanga), Uyui (Tabora), Ukonga (Dar es Salaam) and special prisons at Isanga (Dodoma), Lilungu (Mtwara) and Keko (Dar es Salaam).

To reduce prison congestion, the home ministry would apply non-custodial sentences (such as fines, canning and compensation) and setting free accused if the prosecution fails to prepare a case within 60 days.

The fire-brigade unit will be equipped and that all brigades will now be pooled under one authority. Mr Mungai also said that the government was committed to close all refugee camps in the country by end of the year.
 
The government of Tanzania has once again said the report on DUAL CITIZENSHIP is ready.


Unfortunately the same has been said since MKAPA's era, on checking my notes this is the fourth year we are hearing the same thing.

First there was a commission, Tanzania Law Review Commission who were tasked with the research, they finished and wrote a 'report'. Then there was chit chat from numerous ministers of Home Affairs and Foreign Affairs promising the same thing.

The presidents weren't spared, First President Mkapa said he did not think that DUAL CITIZENSHIP is a priority for now [that was 2004] and then he said the government would look into it....

When he left ''the government was still looking into it''...

Then came the incumbent President, Jakaya Kikwete said virtually the same thing when responding to our RISALA; he acknowledged that DUAL CITIZENSHIP has been raised everywhere he goes and hence the cabinet 'would look into it''...


Now yesterday Joseph Mungai stated in the parliament that the ''report'' is ready! I am sorry Hon. Mungai we have heard of ''the report'' nearly four years now....and NO please stop looking into it start ''ACTING ON IT''...

The problem with our government is that the system is moving so slow you will forgiven for thinking they don't care...some officials have even accused us of ''causing a storm in a teacup'' when we advocate a speedy process...

Unless it's has changed but the last time I checked our motto was ARI MPYA KASI MPYA NA NGUVU MPYA...it's time we see the slogan on DUAL CITIZENSHIP...
 
Yakub,
Don't be persimistic. I think things are in motion. That's the way I am reading it.
 
Dear Jasusi nothing in motion!!I Read the facts from my brother said Yakub carefully,I understand our people down there(TZ),they are very slow for action,I dont know why is it so?Imagine as my bro Yakub said,this matter started since Former President Ben,and they said it was priority by then(2004)since then till now nothing has been done,they have got a very pleased language,"we are working on it",you are working on it till when?And we are saying ari mpya ,kasi mpya and nguvu mpya,where is ari mpya,nguvu mpya and kasi mpya on this?We need ari mppya ,kasi mpya and nguvu mpya on this!!In some countries they under go revolution,others evolution,we Tanzania,we under go confussion.Time has come sepataret boys from men,boys should go to school men shuld go to fight!!Tumechoka kula makoko na sisi tunataka waliiiiiiii!!!!!
 
Waungawana hivi ni nini haswa kinakwamisha kupitishwa kwa hili jambo!Kwa Ufahamu wangu ni karibu miaka SABA sasa tumekuwa ktk majadiliano ya kukubali au kukataa Dual Citizenship,lakini hatima yake siioni!.Mliopo karibu na Maandiko hayo ya akina Mungai tupeni hints nini kinapendekezwa humo!.Wapo watu wengi hawataki kuukana Uraia wao,wanasubiri hatima ya Debate hiyo!,lakini mbona nyumbani watu hawajali muda?.Ingekuwa Busara walimalize hili ili watu wajue wachague nini!.Naomba kutoa Hoja!
 
Waungawana hivi ni nini haswa kinakwamisha kupitishwa kwa hili jambo!!

Hakuna kingine zaidi yakuwa hili jambo haliwaathiri wao na familia zao. Ingekuwa japo watoto wao wanahitaji dual citizenship bila shaka siku nyiiingi lingekuwa limeshatungiwa sheria.

Wao na watoto wao wanaweza kwenda, kuishi na kuwekeza popote pale kwenye sayari hii ya muumba. Maslahi wajameni. Jambo lolote lenye maslahi kwao na makuwadi wao basi litapitishwa haraka sana kama hilo la EA federation kichaa.

Kitu kingine (may be) ni hofu pengine ya kuwa wakiiruhusu hoja hii vichwa kibao vitarudi na hivi wameishi kwa walipa kodi wanaojali matumizi ya kodi zao bila shaka wanaweza kuleta changamoto kwa walipa kodi wa Tanzania kiasi watawala wanahofu kuwaruhusu hawa jamaa waje ni kutaka kujitilia mchanga kwenye kitumbua.
 
Back
Top Bottom