Upotoshaji Wikipedia Juu ya Nyerere?

Umesema ukweli katika namna ya ukweli sana! Kila siku nazidi kuelewa conviction iliyo ndani ya watu kama mzee Kitine, Ulimwengu, Prof Shivji, Butiku, Warioba na wafananao na hao katika kupigana huku wakiwa ndani ya CCM. Wameelewa kuwa chama chao kimetekwa na genge la maharamia. Dr. Lwaitama wakati fulani aliliweka vizuri hili, "Natamani wananchi waiweke CCM pembeni ili iweze kujipanga upya (kama chama cha upinzani) na hatimaye irudi kama CCM ile ya awali,chama cha wakulima na wafanyakazi".
Nawashauri die-hards wa CCM. Piganieni chama chenu na Historia yenu. Wanyang'anyi mliowaachia chama kwa kujua au kutokujua kwenu, wamedhamiria kabisa kukibadili "jina"! Wameanza na hili la kumfuta kabisa mwasisi wenu kwenye historia na jitihada hizi ni kubwa sana nyakati hizi!

Mkuu Jasusi, sijui kama umeligundua kuwa hawa wapenzi na watetezi wa CCM ya sasa ndio wenye chuki kubwa na Mwalimu Nyerere wakati hicho chama wakiteteacho yeye ndio mwanzilishi wake.
Ila ukiangalia kwa darubini kali, CCM hii ya Kikwete sio ile ya Nyerere ila inatumia usajili wa CCM ya Nyerere ambayo ilishakufa pamoja na mwanzilishi wake.
 
Hii ni kweli kabisa wala haina marekebisho kuna kina Chipaka,Zuberi Mtemvu kina Chifu Mareale kina Fundikira,Abdulrahman Babu,wengine wengi walikimbia nchi kama kina Kambona wengine walifukuzwa jeshini na kuzuiwa nyumbani kama kina Bob Nasser(Nasari).Mahfudhi wengine wakapewa kazi nyingine uraiani lakini kwa masharti kama kina Capt.Mushi huyu mwenye malori mengi mfadhili wa Simba jina simkumbuki alikuwa meneja kampuni ya KAMATA na wengine wengi sana siwakumbuki majina yao,wako waliofia gerezani kwa mateso,lakini hayo hayazungumzwi,hiyo ndiyo taswira ya Mwl.Nyerere kwa upande wa pili,tusipende kuongelea mazuri tu,hata mabaya yapo mengi tena ya kutisha.

Kwamba Nyerere alikuwa havumilii upinzani hilo tunalikubali. Hao uliowataja wengine walimpinga akawaweka detention, wengine kama akina Chipaka walihukumiwa na mahakama kuwa ni wahaini wakafungwa, na wengine walikuwa wamefanya makosa sehmu zao za kazi akwahamishia kwingine.

Lakini Nyerere hakumuua mtu hata moja. Taja jina la mtu moja tu aliyefia gerezani kwa mateso.
 
Akutukanae hakuchagulii tusi

Ni kweli kuna exaggeration katika maandiko hayo lakini ni kweli pia kulikuwa na repression ya hali ya juu wakati wa nyerere; ndio wakati huo watu wa usalama walikuwa kazi yao kubwa kuhesabu vizibo vya bia watu wanazokunywa bar na kwenda kutoa ripoti halafu makachelo wanaanza kufuatilia nyendo za muhusika; kulikuwa hakuna uhuru wa habari ukilinganisha na leo!! Cartoon anazochorwa MKWEREE sidhani kama zingeweza kuruhusiwa enzi za MCHONGA. Alikuwa ni mzalendo wa kweli lakini pia alikuwa na mapungufu ya kibinadamu, all in all he was a BENEVOLENT DESPOT.
 
Mhh! afadhali hawa mafisadi wetu wa sasa hivi wengi wao pesa nyingine wanazibakisha na kuwekeza vitega uchumi hapahapa hivyo pesa inazunguka hapahapa nchini na wananchi wengine wanaambulia kazi katika miradi ya mafisadi, lakini FISADI Nyerere yeye kazi yake alikuwa akichota tu na kuwapelekea Wakristo wenzake nje ya nchi mfano Biafra.

It's very sad unapokuwa na watu wenye kufukiri kama wewe maana kama jambo hulijui kwanini ulete habari za vijiweni tena za watu ambao hawajawahi kuona kuta za madarasa na kutuletea humu. Uzuri wa mtu utabaki kuwa uzuri wake na hauwezi kufutwa na propaganda za watu mnaoyaona mambo kwa umabli wa Manzese. Yamkini, ndio maana Wakenya wanatucheka sana Watanzania kwa sababu ni wazembe kujisomea na hatutaki hata kufanya utafiti ili kwamba kila tutakachokisema kiwe backed na relevant references. Nimetumia neno RELEVANT makusudi maana watu wengi humu wanapenda kutumia biased, prejudiced and unobjective minds, publications na mengine ili kutuaminisha mambo. Wana JF tumieni hazina ya wazee ambao bado wanaishi ili watupatie ukweli wa Mwalimu sio uzushi. Tena tafuta wale ambao hata for some reasons differed with him and will tell us balanced story. Mtei kwa mfano anasema ali differ na Mwalimu to some areas lakini anakiri kwamba the bottomline kuwa aliipenda Tanzania to her dimension and was not corrupt at ALL. Nilimsikia akihojiwa na Hamza Kassongo nikawa interested sana na masimulizi yake maana hayana mizengwe anaelezea walikotoutina katika misimamo yao kiuchumi lakini hatujui hata ushauri wa Mtei wa kuingia mikataba na IMF wakati huo ingetufikisha kokote. Tumeingia miongo kama 3 iliyopita na tunashuhudia hata kile kidogo tulichokuwa nacho tumeuza. Tuache matusi, habari za vijiweni na tujikite kwenye utafiti tukitumia observation, survey, discussion, dialogue, questions and relevant objective documentary review
 
Mkuu! tunazungumzia watu ambao wako tayari kuuwa raia zao ili kufikia malengo yao achalia mbali "kuvunja" mahusiano ya kibalozi.
Halafu na Nyerere naye kwa nini amkubali "personal assistant" ambaye ni mtumishi wa Serikali ambayo ni "hasimu" yake kama alivyokuwa akidai?...Nyerere was a controversial figure throughout most of his life, if not entirely!
Mkuu una ushahidi wowote? au na wewe umekuwa ni muhanga wa propaganda za Nyerere.
Ushahidi upo. Fuatilia ile kesi ya Bibi Titi Mohammed na ndugu zake Kambona, uone Hanga alikuwa na role gani katika njama zile. Tena bahati nzuri kama ulikuwepo nyakati zile kesi nzima iliandikwa magazetini. Yet still, tafuta kitabu cha Godfrey Mwakikagile. Nyerere hakuwa controversial hata kidogo. Kwa sisi tuliomfahamu, he was very predictable.
 
Kwamba Nyerere alikuwa havumilii upinzani hilo tunalikubali. Hao uliowataja wengine walimpinga akawaweka detention, wengine kama akina Chipaka walihukumiwa na mahakama kuwa ni wahaini wakafungwa, na wengine walikuwa wamefanya makosa sehmu zao za kazi akwahamishia kwingine.

Lakini Nyerere hakumuua mtu hata moja. Taja jina la mtu moja tu aliyefia gerezani kwa mateso.

Saini yake ndio iliyomnyonga MWAMWINDI!! Je, hapo hakuua? Nionavyo mimi kama kuua ni kutoa uhai wa binadamu kwa kutumia mamlaka yako then hata wale walioliwa na simba wakati wa "villagization" waliuawa na muasisis wa sera ile !! This does not mean that he did not mean well for his people: these acts were meant to help advance the well being of his people, remember Mwamwindi had to be hanged after murdering Dr. Kleruu the champion of ujamaa policy in Ismani ward Iringa region..
 
Halafu CK Tumbo amekuwepo hadi mfumo wa vyama vingi unaanza. Hawakuhangaika kumuuliza yaliyomsibu wakati ule. Kuiweka pamoja TANZANIA wakati ule wa Mwalimu haikuwa kazi ndogo kama wanavyoibomoa sasa.

Hawana uwezo wa kuongoza. Changamoto zilizopo zimewazidi kimo na zinaweka weaknesses zote wazi wazi. Ndio maana tunaona sasa watu wanajitahidi kuleta mada ambazo wanafikiri zitaweza kuziba mapungufu yao kirahisi kama ukabila na udini. Hoja za sasa hivi ziangalie zilivyokaa kaa. Ni kujaribu kuzima maswali yoyote kwenye weakness za wazi wazi za uongozi tulizonazo. Utaachaje kuhangaika na mafisadi na kuhangaika na watu wadogo wadogo wasio na tija wala impact yoyote kwa uwepo na ustawi wetu? Maana ufisadi ndio ule ulioitwa uhujumu uchumi...siku hizi ukiufanya vizuri unaitwa kigogo.
 
propaganda za Wamalawi hizi,....ulishaingia kwenye blog zao ukaona wanavyomtukana nyerere?.....na wengi wao wapo hapahapa bongo, wanajifanya wabongo...
 
Jasusi nimecheka sana...watu walimdharau Nyerere akiwa hai wakaishia kwenye kona. Sasa hivi wanamdharau amekufa wanafikiri watamuua tena mara ya pili. Wanalijenga jina lake maana kadri wanavyoshindwa kuonyesha wana uwezo kuliko yeye ndio jina lake linavyopaa juu juu.
Nyerere alipaishwa jina lake na Waingereza.
Alisomeshwa na Waingereza akapewa "personal assistant" na Waingereza na ndio Waingereza haohao waliomrudisha madarakani wakati alipopinduliwa, hivyo jina lake haliwezi kupaa tena bila ya ridhaa ya Waingereza! ndio walio na vielelezo vyote kuhusu Nyerere.
 
Saini yake ndio iliyomnyonga MWAMWINDI!! Je, hapo hakuua? Nionavyo mimi kama kuua ni kutoa uhai wa binadamu kwa kutumia mamlaka yako then hata wale walioliwa na simba wakati wa "villagization" waliuawa na muasisis wa sera ile !!


Ndinani, ni kweli kabisa alitia saini yake ili Mwamwindi anyongwe, lakini yeye hakumhukumu Mwamwindi anyongwe. Hili ni swala la kisheria na nisingependa kujadili zaidi kwani sijui sheria ilivyo.

Kuhusu villagization ni vile vile ni swala la kisheria na kutafakari zaidi.
 
Hawana uwezo wa kuongoza. Changamoto zilizopo zimewazidi kimo na zinaweka weaknesses zote wazi wazi. Ndio maana tunaona sasa watu wanajitahidi kuleta mada ambazo wanafikiri zitaweza kuziba mapungufu yao kirahisi kama ukabila na udini. Hoja za sasa hivi ziangalie zilivyokaa kaa. Ni kujaribu kuzima maswali yoyote kwenye weakness za wazi wazi za uongozi tulizonazo. Utaachaje kuhangaika na mafisadi na kuhangaika na watu wadogo wadogo wasio na tija wala impact yoyote kwa uwepo na ustawi wetu? Maana ufisadi ndio ule ulioitwa uhujumu uchumi...siku hizi ukiufanya vizuri unaitwa kigogo.
Ndahani,
Umewasikia mashahidi wa Mramba? Yumo Chenge, John Momose Cheyo, Marehemu Balali( kama angekuwa hai), Mkapa( hajathibitisha kama atapanda kizimbani),... Siku hizi ufisadi ni sifa mama ya kugombea UONGOZI kule CCM na serikalini.
Viongozi wa DINI nao wanajiimarisha kwelikweli. Wana nguvu kuliko serikali. Hata sensa ya mwaka huu itafanyika kwa huruma yao.
 
Ushahidi upo. Fuatilia ile kesi ya Bibi Titi Mohammed na ndugu zake Kambona, uone Hanga alikuwa na role gani katika njama zile. Tena bahati nzuri kama ulikuwepo nyakati zile kesi nzima iliandikwa magazetini. Yet still, tafuta kitabu cha Godfrey Mwakikagile. Nyerere hakuwa controversial hata kidogo. Kwa sisi tuliomfahamu, he was very predictable.
Nilikuwa ninataka kukujibu lakini nimekumbuka maneno ya Bigaraone:
"Nimetumia neno RELEVANT makusudi maana watu wengi humu wanapenda kutumia biased, prejudiced and unobjective minds, publications na mengine ili kutuaminisha mambo. Wana JF tumieni hazina ya wazee ambao bado wanaishi..."
 
Wala Nyerere hakutoa hukumu. Alitia sahihi kama Rais wa NCHI ili watu hawa wanyongwe. Hili ni hitaji la kisheria ambalo hata hivo alilikwepa na kuliepuka kwa watu wengi tu. Kuna watu humu wanasutwa na dhamira zao kwa uongo wanaouandika juu ya Mwalimu. Wasubiri baadhi yetu tutoweke hapa duniani.

Ndio maana nimewataka wanaJF kama kweli mnataka na nigependa iwe hivyo JF iwe chemichemi ya elimu tutumie hazina ya watu bado wanaishi walioona uetndaji kazi wa Nyerere. Tuanche habari za vijiweni. Watu walikuwa wanasutwa na dhamira zao kwa sababu ya umakini wa Nyerere. Alikuwa ni msomi mzuri wa riporti zote zilizokuwa zikipelekwa kwake na wizara pamoja na taasi za chini yake. Na ziliitimishwa na mkutano wa kuelezea reporti hizo-presenstations. Kwa wanapenda kuchakachua walishushuriwa hapo na wakaanzisha chuki kwake. Hivyo WildCard wewe n hazina nzuri na ningeomba uendelee kutusaidia katika kutoa ukweli wa mambo na ikibidi mtuandikie vitabu maana humu kuna wapotoshaji wanafikiri wakim brand Nyerere ndio vioongozi wao wasiojua hata kusoma reports watasafishika na kupata sifa za Mwalimu- a briliant, charismatic, philosopher, leader. Tumedanganywa kuwa wana uwezo wa kusikiliza na kujenga hoja lakini wakaishia kusema hawajui kwanini nchi yao maskini na kupokea misaada mingi, hawajui wawekezaji vioni macho wanaolitia taifa hasara. Mikataba mibovu ni ya serikali zilizopita lakini wakasahau kuwa wakiwa mawaziri wa wizara ya madini ndio walihusika na mikataba ya madini ya asilimia 3 ya mrahaba. Mambo ni mengi ila Mungu atusamehe
 
Ni kweli kuna exaggeration katika maandiko hayo lakini ni kweli pia kulikuwa na repression ya hali ya juu wakati wa nyerere; ndio wakati huo watu wa usalama walikuwa kazi yao kubwa kuhesabu vizibo vya bia watu wanazokunywa bar na kwenda kutoa ripoti halafu makachelo wanaanza kufuatilia nyendo za muhusika; kulikuwa hakuna uhuru wa habari ukilinganisha na leo!! Cartoon anazochorwa MKWEREE sidhani kama zingeweza kuruhusiwa enzi za MCHONGA. Alikuwa ni mzalendo wa kweli lakini pia alikuwa na mapungufu ya kibinadamu, all in all he was a BENEVOLENT DESPOT.

Well said. Nyerere alikuwa na mapungufu yake. Uchumi kwa kweli hakuumudu kabisa na alikuwa hapendi upinzani wowote ule wakati wa utawala wake. Hilo aliwahi kulisema mara kadhaa.

But Nyerere was not a dummy. He was very intelligent and eloquent and well-read. Those who say everything was written fro him dont know Nyerere at all. You could read your "Risala" to Nyerere and he would write nothing however long your "Risala" but when he stood up he would deal with all points raised one by one without reading anywhere. That was Nyerere. He could explain complicated things to novices but he could confront any intelligent person in the world. Reporters who were assigned to interview Nyerere knew very well that they had to do they assignment before confronting him. Some of us remember very well how he dealt with the reporters who came with the US Foreign Minister, Henry Kissinger and how he swayed the world opinion on Cuban involvement in the war in Angola.
 
Ndahani,
Umewasikia mashahidi wa Mramba? Yumo Chenge, John Momose Cheyo, Marehemu Balali( kama angekuwa hai), Mkapa( hajathibitisha kama atapanda kizimbani),... Siku hizi ufisadi ni sifa mama ya kugombea UONGOZI kule CCM na serikalini.
Viongozi wa DINI nao wanajiimarisha kwelikweli. Wana nguvu kuliko serikali. Hata sensa ya mwaka huu itafanyika kwa huruma yao.

Ndio hao vigogo wa CCM wanaomcheka Nyerere. Imekula kwao maana Tanzania itakuwepo hata bila ya mimi na wewe. Wanafikiri yanayoendelea yafafunikwa chini ya kapeti...kumbe ndio itakuwa vigezo vya kuwaweka kwenye mizani siku za baadae.
 
Swali zuri sana.

Tanzania ina mambumbumbu wengi.
Sasa kumrudisha Kassim Hanga kule Zanzibar kuna uhusiano gani na kuwekwa kizuizini wakati hata sheria ya Detention hii Karume au Makamo yoyote wa Rais hakutakiwa kuitumia ndani ya Jamhuri hii hata kama Rais amesafiri na Vice President ana-act.
 
Well said. Nyerere alikuwa na mapungufu yake. Uchumi kwa kweli hakuumudu kabisa na alikuwa hapendi upinzani wowote ule wakati wa utawala wake. Hilo aliwahi kulisema mara kadhaa.

But Nyerere was not a dummy. He was very intelligent and eloquent and well-read. Those who say everything was written fro him dont know Nyerere at all. You could read your "Risala" to Nyerere and he would write nothing however long your "Risala" but when he stood up he would deal with all points raised one by one without reading anywhere. That was Nyerere. He could explain complicated things to novices but he could confront any intelligent person in the world. Reporters who were assigned to interview Nyerere knew very well that they had to do they assignment before confronting him. Some of us remember very well how he dealt with the reporters who came with the US Foreign Minister, Henry Kissinger and how he swayed the world opinion on Cuban involvement in the war in Angola.


As for being INTELLIGENT, you can say that again; these pretenders have always known that they are anthills compared to Mwalimu!!
 
ukweli unauma.....

Nyelele arikuwa mtu mzuli sana, wakati wa Nyelele aliimalisha sana hari ya watu wake kierimu na rishe bola, vyakura kama mahalage

mchere, sukali, virikuwa vikipatikana kira kona ya Jamhuli ya Tanzania

Hebu check kwenye red unafanya makusudi au ndio uelewa wako wa kiswahili?.....

Mkuu Bumela,

Tatizo la internet ndilo hili. Wale watoto wanaoanza kujua kuandika na kusoma nikija nyumbani kwako kukutembelea unawaambia waende wakacheze, maana mazungumzo hawatayaelewa.

Sasa, huku mitandaoni huwezi kuwazuia, maadamu wanajua kutengeneza ID na kuweka password basi matokeo yake ni kama huyo unayemsema, yaani unajikuta unajadili na mtoto wa darasa la pili.

Ukijali sana watu kama hawa, unaweza kukata tamaa kufungua JF.
 
Huyo hakuwa Chief Fundikira?
Chifu Fundikira alikuwa mwakilishi wetu kwenye East African community 1963. Alichukua kazi hiyo baada ya kupoteza uwaziri katika kesi ya kwanza Tanganyika ya kupokea rushwa.
 
Ndio hao vigogo wa CCM wanaomcheka Nyerere. Imekula kwao maana Tanzania itakuwepo hata bila ya mimi na wewe. Wanafikiri yanayoendelea yafafunikwa chini ya kapeti...kumbe ndio itakuwa vigezo vya kuwaweka kwenye mizani siku za baadae.
Hawamcheki ila wanajaribu kuiandika upya historia ya Tanzania. Hawawezi. Sasa hivi ukijaribu kumgusa fisadi yeyote kwa kumpeleka mahakamani, Mkapa lazima atajwe, tena awe shahidi. Kikwete naye atakapostaafu ukimsimamisha waziri yeyote kwenye awamu yake naye ataitwa kuwa shahidi. Ndivyo wanavyoitafuna nchi hii kwa ushirikiano wa hali ya juu.
 
Back
Top Bottom