Ndugu wanajamvi, nikiangalia miaka kadhaa inayokuja ni dhahiri kuwa CCM kitaangushwa kwenye uchaguzi wa nchi. Sababu za kuangushwa ni nyingi ila hiyo sio mada yangu kwa sasa. Kwa sasa naangalia nini kitatokea baada ya kuangushwa.
Ninachoona ni kuwa kutakuwa na ulazima wa kukifuta chama hiki kwani kuna uwezekano baada ya tathmini ikagundulika kuwa hakikuwa na vigezo vya kuwa chama cha siasa. Baadhi ya mambo ambayo nadhani yanaweza kupelekea chama hiki kufutwa ni haya yafuatayo:
1. Inaweza kugundulika kuwa kulikuwa na support kubwa ya dola ya kukiwezesha kushinda chaguzi za kisiasa
2. Kwamba Viongozi wake wengi wa chama walihusika katika wizi mkubwa wa rasilimali za nchi hii na kuingia katika mikataba mibovu na isiyo na maslahi kwa nchi ya Tanzania.
3. Kwamba ni chama ambacho pamoja na kukaa madarakani kwa zaidi ya miaka 50 kimeshindwa kabisa kujenga taifa lenye uchumi mkubwa unaoweza kukaribiana na South Africa au Botswana kwa sababu rasilimali tulizonazo ni nyingi pengine kuliko za SA na Botswana.
4. Ni chama ambacho kimeshindwa kujitofautisha kama ni dola au chama, kwa sababu viongozi wake hata kama kutakuwa na ushahidi kuwa wamehusika na uhujumu uchumi, vyombo vya dola haviwaulizi wala kuwachukulia hatua za kisheria; mfano ni sakata la Meremeta, Kagoda, Richmond, n.k.
5. Ni chama ambacho japokuwa viongozi wake wanasafiri nchi za nje kila siku lakini wameshindwa kujifunza wenzetu wanawezaje kupiga hatua za kimaendeleo wakati sisi tunaendelea kudidimia il hali tuna rasilimali nyingi sana nchini.
6. Ni chama ambacho kimekuwa kikiwalaghai wananchi wake kuwa kitafanya hivi na vile wakati wa chaguzi lakini mara wanaposhinda wanawasahau kabisa ingawa huu nao ni ujinga wa wale wanaoahidiwa year in year out na hakuna kinachofanyika lakini bado wanakipigia kura, hilo laweza kuwa si kosa la CCM ni kosa la wananchi wenyewe. Hata hivyo CCM itabanwa kuwa ilifanya ulaghai huku ikijua kuwa inafanya ulaghai.
Ni mengi sana ambayo yanaweza kukifanya CCM kifutwe kwenye uso wa dunia ya Tanzania ila nimeona nisiwachoshe.
Nawasilisha.
Ninachoona ni kuwa kutakuwa na ulazima wa kukifuta chama hiki kwani kuna uwezekano baada ya tathmini ikagundulika kuwa hakikuwa na vigezo vya kuwa chama cha siasa. Baadhi ya mambo ambayo nadhani yanaweza kupelekea chama hiki kufutwa ni haya yafuatayo:
1. Inaweza kugundulika kuwa kulikuwa na support kubwa ya dola ya kukiwezesha kushinda chaguzi za kisiasa
2. Kwamba Viongozi wake wengi wa chama walihusika katika wizi mkubwa wa rasilimali za nchi hii na kuingia katika mikataba mibovu na isiyo na maslahi kwa nchi ya Tanzania.
3. Kwamba ni chama ambacho pamoja na kukaa madarakani kwa zaidi ya miaka 50 kimeshindwa kabisa kujenga taifa lenye uchumi mkubwa unaoweza kukaribiana na South Africa au Botswana kwa sababu rasilimali tulizonazo ni nyingi pengine kuliko za SA na Botswana.
4. Ni chama ambacho kimeshindwa kujitofautisha kama ni dola au chama, kwa sababu viongozi wake hata kama kutakuwa na ushahidi kuwa wamehusika na uhujumu uchumi, vyombo vya dola haviwaulizi wala kuwachukulia hatua za kisheria; mfano ni sakata la Meremeta, Kagoda, Richmond, n.k.
5. Ni chama ambacho japokuwa viongozi wake wanasafiri nchi za nje kila siku lakini wameshindwa kujifunza wenzetu wanawezaje kupiga hatua za kimaendeleo wakati sisi tunaendelea kudidimia il hali tuna rasilimali nyingi sana nchini.
6. Ni chama ambacho kimekuwa kikiwalaghai wananchi wake kuwa kitafanya hivi na vile wakati wa chaguzi lakini mara wanaposhinda wanawasahau kabisa ingawa huu nao ni ujinga wa wale wanaoahidiwa year in year out na hakuna kinachofanyika lakini bado wanakipigia kura, hilo laweza kuwa si kosa la CCM ni kosa la wananchi wenyewe. Hata hivyo CCM itabanwa kuwa ilifanya ulaghai huku ikijua kuwa inafanya ulaghai.
Ni mengi sana ambayo yanaweza kukifanya CCM kifutwe kwenye uso wa dunia ya Tanzania ila nimeona nisiwachoshe.
Nawasilisha.