Malafyale
JF-Expert Member
- Aug 11, 2008
- 13,813
- 11,126
Akijibu hoja hiyo, kamishina wa NEC Profesa Chaligha alisema,"Kuhusu uandikishaji mpya wa wapigakura alisema jambo hilo haliwezekani kwa sasa na kusisitiza kuwa watakaoruhusiwa kupiga kura ni wale tu waliomo kwenye Daftari la mwaka 2010 na kusisitiza kuwa jambo hilo ni la kisheria"(Mwisho wa kunukuru)
Serikali ya CCM iliruhusu uandikishaji wa wapiga wapya Igunga na vijana wengi wakajiandikisha waliokuja kuwaadhibu vibaya kwenye sanduku la kura na toka wakati ule wakawa wamejua jinsi ya kuiminya demokrasia-KUTORUHUSU VIJANA WAPYA WASAJILIWE KWENYE DAFTARI WAKATI WA CHAGUZI NDOGO.Serikali inajua inachokifanya na nashangaa kwa nn uongozi wa kitaifa wa vyama vya upinzani hawatolei msimamo suala hili!
Upinzani sio mpaka mshindwe kwenye uchaguzi ndiyo mchachamae!Kuruhusu uchaguzi huu uendelee ni sawa na janga la kitaifa na eleweni kuwa kama mtakaa kimywa basi mnazikosa kura maelfu kwa maelfu ya vijana waliokuwa na umri wa miaka 16 na 17 mwaka 2010 na ambao sasa wana haki ya kupiga kura!Simamieni demokrasia na ndipo mtaongeza viti bungeni kwa urahisi zaidi!Mkiwakosa vijana hawa likely CCM ikashinda Arumeru-Mashariki kwani base yao ya wapiga kura hasa wanawake na wazee itakuwa ipo haijatingishwa!
kama NEC itazidi ng'ang'ania kuwa daftari la wapiga kura halitaboreshwa Arumeru-Mashariki nawashauri kwa umoja wenu tangazeni kujitoa kwenye uchaguzi halafu mnakwenda Mahakamani kufungua kesi ili Mahakama itamke"kupiga na kupigiwa kura kwa mtu mwenye miaka kuanzia 18 jimboni Arumeru-Mashariki hakuwezi zuiliwa kwa sababu tu ni gharama kubwa kuwaandikisha kwani ni haki yao msingi ndani ya katiba"
Serikali ya CCM iliruhusu uandikishaji wa wapiga wapya Igunga na vijana wengi wakajiandikisha waliokuja kuwaadhibu vibaya kwenye sanduku la kura na toka wakati ule wakawa wamejua jinsi ya kuiminya demokrasia-KUTORUHUSU VIJANA WAPYA WASAJILIWE KWENYE DAFTARI WAKATI WA CHAGUZI NDOGO.Serikali inajua inachokifanya na nashangaa kwa nn uongozi wa kitaifa wa vyama vya upinzani hawatolei msimamo suala hili!
Upinzani sio mpaka mshindwe kwenye uchaguzi ndiyo mchachamae!Kuruhusu uchaguzi huu uendelee ni sawa na janga la kitaifa na eleweni kuwa kama mtakaa kimywa basi mnazikosa kura maelfu kwa maelfu ya vijana waliokuwa na umri wa miaka 16 na 17 mwaka 2010 na ambao sasa wana haki ya kupiga kura!Simamieni demokrasia na ndipo mtaongeza viti bungeni kwa urahisi zaidi!Mkiwakosa vijana hawa likely CCM ikashinda Arumeru-Mashariki kwani base yao ya wapiga kura hasa wanawake na wazee itakuwa ipo haijatingishwa!
kama NEC itazidi ng'ang'ania kuwa daftari la wapiga kura halitaboreshwa Arumeru-Mashariki nawashauri kwa umoja wenu tangazeni kujitoa kwenye uchaguzi halafu mnakwenda Mahakamani kufungua kesi ili Mahakama itamke"kupiga na kupigiwa kura kwa mtu mwenye miaka kuanzia 18 jimboni Arumeru-Mashariki hakuwezi zuiliwa kwa sababu tu ni gharama kubwa kuwaandikisha kwani ni haki yao msingi ndani ya katiba"