Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,551
- 19,418
Mojawapo ya matatizo ya kisiasa nchini kwetu ni kufanya vyama vya saisa kama sehemeu ya kupatia ajira ya kudumu au mradi wa ukoo fulani. Kwa mfano, tangu nimeisikia CUF katika nyanja za siasa, mgombea wa urais huko Zanzibar amekuwa ni Maalimu Seif Shariff Hamad ambaye pia ndiye amekuwa Katibu Mikuu wa CUF miaka yote, na mgombea wa urais wa Muungano amekuwa ni Profesa Lipumba miaka yote ambaye pia ni mwenyekiti wa CUP muda wote huo. Kwa upande wa TLP tunamjua Mrema na mbwebwe zake wakati kwenye CHADEMA tunamfahamu sana Freeman Mbowe na Helicopter yake: sina uhakika sawasawa, ila nadahani kuwa Mbowe aligombea Urais mara mbili wakati ambapo pia amekuwa ni mwenyekiti wa CHADEMA muda wote huo.
Vyama vya upinzani mnatakiwa muondoke usingizini. Siku zote simamisheni mtu ambaye mna uhakika kuwa ataweza kuwaletea ushindi badala ya kuangaliana wenyewe kwa wenyewe. Kama mnafahamu historia sawasawa, mtakumbuka kuwa McKinnon aliachia ngazi kwenye chama cha Labor hapo Uingereza mara tu baada ya kubwagwa na John Major; hiyo ilisababisha Tony Blair kuingia ulingoni akiwa kijana mdogo na kupata ushindi ambao umeiweka Labor madarakani kwa zaidi ya miaka kumi sasa. Kwa marekani pia mtakumbuka kuwa wakati Al Gore aliposhindwa kwa mbinde mwaka 2000 aliacha mambo ya siasa za uchaguzi ili kuwapisha wengine, na mambo yaliendelea hivyo hadi Obama alipoibuka na kutwaa ushindi kwa tiketi ya Demokrati. Somo kubwa hapo ni kwamba ukisimama kwenye uchaguzi na ukashindwa hata kwa kuonewa kama alivyofanyiwa Al Gore, basi pisha njia waje watu wengine na mawazo yao mapya kwa sababu yale ya kwako yatakuwa yameshapitwa na wakati.
baada ya somo hilo, sasa nasema hivi: Upinzani Tanzania achaneni na utaratibu wa ukiritimba wa kuwabeba watu waliojaribu miaka yote bila kuwaletea mafanikio kisiasa. Kama mtu aligombea akashindwa basi asipewe nafasi ya kugombea tena ati. Radi haipigi mara mbili.
Ninafahamu kuwa Rais Nixon alibwagwa na Kenndey mwaka 1960 na baada ya miaka kama minane hivi akaibuka tena na kushinda kiti hicho; lakini sote tunafahamu fika alikoishia. Watu wasifanye siasa za vyama kama profession yao; hiyo ni huduma kwa jamii tu, na kama jamii ikishakutosa basi usitafute mianya ya kung'ang'ania.
Baada ya Longolongo hizo hapo juu, napneda kusisitiza kuwa mwelekeo wa Tanzania kipindi kijacho kwa sasa hivi unategema zaidi sera na nguvu za upinzani kuliko CCM. Kama Upinzani wakifanya Vizuri, nchi itakwenda pazuri ila kama upinzani utakufa, basi nduipo nchi yetu itakpozidi kudidimia kama mabavyo tumekuwa tunadidimia miaka yote.
Vyama vya upinzani mnatakiwa muondoke usingizini. Siku zote simamisheni mtu ambaye mna uhakika kuwa ataweza kuwaletea ushindi badala ya kuangaliana wenyewe kwa wenyewe. Kama mnafahamu historia sawasawa, mtakumbuka kuwa McKinnon aliachia ngazi kwenye chama cha Labor hapo Uingereza mara tu baada ya kubwagwa na John Major; hiyo ilisababisha Tony Blair kuingia ulingoni akiwa kijana mdogo na kupata ushindi ambao umeiweka Labor madarakani kwa zaidi ya miaka kumi sasa. Kwa marekani pia mtakumbuka kuwa wakati Al Gore aliposhindwa kwa mbinde mwaka 2000 aliacha mambo ya siasa za uchaguzi ili kuwapisha wengine, na mambo yaliendelea hivyo hadi Obama alipoibuka na kutwaa ushindi kwa tiketi ya Demokrati. Somo kubwa hapo ni kwamba ukisimama kwenye uchaguzi na ukashindwa hata kwa kuonewa kama alivyofanyiwa Al Gore, basi pisha njia waje watu wengine na mawazo yao mapya kwa sababu yale ya kwako yatakuwa yameshapitwa na wakati.
baada ya somo hilo, sasa nasema hivi: Upinzani Tanzania achaneni na utaratibu wa ukiritimba wa kuwabeba watu waliojaribu miaka yote bila kuwaletea mafanikio kisiasa. Kama mtu aligombea akashindwa basi asipewe nafasi ya kugombea tena ati. Radi haipigi mara mbili.
Ninafahamu kuwa Rais Nixon alibwagwa na Kenndey mwaka 1960 na baada ya miaka kama minane hivi akaibuka tena na kushinda kiti hicho; lakini sote tunafahamu fika alikoishia. Watu wasifanye siasa za vyama kama profession yao; hiyo ni huduma kwa jamii tu, na kama jamii ikishakutosa basi usitafute mianya ya kung'ang'ania.
Baada ya Longolongo hizo hapo juu, napneda kusisitiza kuwa mwelekeo wa Tanzania kipindi kijacho kwa sasa hivi unategema zaidi sera na nguvu za upinzani kuliko CCM. Kama Upinzani wakifanya Vizuri, nchi itakwenda pazuri ila kama upinzani utakufa, basi nduipo nchi yetu itakpozidi kudidimia kama mabavyo tumekuwa tunadidimia miaka yote.