Upimaji Ardhi nchi nzima Lukuvi tafuta Ushauri zaidi

Mparee2

JF-Expert Member
Sep 2, 2012
2,572
4,241
Binafsi napenda sana jitihada za Waziri wetu Lukuvi ambaye amekuwa kati ya mawaziri wachapa kazi. Hata hivyo sikubaliani kabisa na hii kauli yake ya kupima ardhi nchi nzima.

Kimsingi hii nchi ina population ya kawaida, hapo inaongezeka kila siku. Kwa kauli yako watu wanajaa na hasa wenye uwezo watajichukulia mapori na kuyapatia hati. Mimi naona unatengeza tatizo lingine litakaloleta mgogoro mkubwa wa ardhi miaka ijayo, pale watoto watakokua wakute kila eneo lina mtu.

Natamani kujua hili umelipata wapi, nchi gani inayoendana na sisi na kama limewasaidia? Mimi sina Elimu ya mambo ya Ardhi ila naona hatari kubwa itakayotukumba baadae, kama hutabadilisha huu muelekeo.

Naomba uelekeze watu wapimiwe Ardhi kwenye yale maeneo wanavyoyamiliki na kuyaendeleza, na Mapori yetu ambayo hayajaendelezwa yaendelee kubaki wazi.

Kwa mtazamo wangu, hili ni la kupima nchi nzima, litatuletea ukabila kwa kila kabila kumiliki maeneo yanayowazunguka, na vijana wengi wajao hawatakuwa na maeneo.

Binafsi naona unaandaa bomu litakalolipuka kwenye miaka ishirini na kuendelea ijayo.

Nakushauri uombe Ushauri kwa wataalam, ila sio wapima Ardhi kwani wengi hatuwaamini hadi wajisafishe.
 
Binafsi napenda sana jitihada za waziri wetu Lukuvi ambaye amekuwa kati ya mawaziri wachapa kazi
Hata hivyo sikubaliani kabisa na hii kauli yake ya kupima Ardhi nchi nzima
Kimsingi hii nchi ina population ya kawaida hapo inaongezeka kila siku.....kwa kauli yako watu wana ja na hasa wenye uwezo watajichukulia mapori na kuyapatia hati ..Mimi naona unatengeza tatizo lingine litakalo leta mgogoro mkubwa wa Ardhi miaka ijayo pale watoto watakokua wafute kila eneo Lina mtu.
Natamani kujua hili wapo umelipata wapi ...nchi gani inayoendana na sisi na Kama limewasaidia?
Mimi sina Elimu ya mambo ya Ardhi ila naona hatari kubwa itakayotukumba baadae ...Kama hutabadilisha huu muelekeo

Naomba uelekeze watu wapimiwe Ardhi kwenye Yale maeneo wanavyo yamiliki na kuyaendeleza ....nayo Mapori yetu ambayo hayajaendelezwa yaendelee kubaki wazi.
Kwa mtazamo wangu ... hili la kupima nchi nzima ...litatuletea ukabila ...kwa kila Kabila kumiliki maeneo yanayowazunguka..
Na vijana wengi wajao...hawatakuwa na maeneo...
Binafsi naona una Andaaa Bomu litakalo lipuka kwenye miaka ishirini na kuendelea ijayo
Nakushauri uombe Ushauri kwa wataalam ...ila sio wapima Ardhi kwani wengi hatuwaamini...hadi wajisafishe
huwezi kuwa developed country kama ardhi ya nchi yako haijapimwa......nadhani pia kupima ardhi kutamaliza tatizo la muda mrefu la migogoro ya ardhi na ugomvi kati ya wakulima na wafugaji....pia itaharakisha uwekezaji hasa kwenye commercial farming na industrial area
 
Yamindinda....kama umenielewa sina tatizo kabisa na kupima Ardhi....
Naomba urudie tena kusoma hapo juu
Nimesema Yale maeneo yanayomilikiwa ikiwa ni pamoja na kuendelezwa yapimwe na kumilikishwa wahusika
Ila Yale maeneo mengine ambayo ni mapori ...yawekewe tu utaratibu ila sio kupima nchi nzima
Naomba mfano wa Nchi tano duniani zilizopima Ardhi Nchi nzima?
 
Yamindinda....kama umenielewa sina tatizo kabisa na kupima Ardhi....
Naomba urudie tena kusoma hapo juu
Nimesema Yale maeneo yanayomilikiwa ikiwa ni pamoja na kuendelezwa yapimwe na kumilikishwa wahusika
Ila Yale maeneo mengine ambayo ni mapori ...yawekewe tu utaratibu ila sio kupima nchi nzima
Naomba mfano wa Nchi tano duniani zilizopima Ardhi Nchi nzima?
Nadhani wakati wa kufanya hilo zoezi ...maeneo ambayo yameshaendelezwa yatakuwa na utaratibu wake.....kama ni shamba linalimwa mwenye shamba atapimiwa eneo ambalo analimiliki....kama ranch basi mfugaji atapimiwa eneo lake pia na kama ni kiwanda hivyo hivyo....kuna hati za kimila pia zitakuwa considered
 
Kupima ardhi ni wazo zuri, ili tujue kiasi gani kipo mikononi mwa watu na kiasi gani kipo mikononi mwa serikali
 
huwezi kuwa developed country kama ardhi ya nchi yako haijapimwa......nadhani pia kupima ardhi kutamaliza tatizo la muda mrefu la migogoro ya ardhi na ugomvi kati ya wakulima na wafugaji....pia itaharakisha uwekezaji hasa kwenye commercial farming na industrial area
kweli kabisa mkuu
 
Back
Top Bottom