Bado nipo nipo
Member
- Nov 19, 2011
- 69
- 11
Kwa hali ya kawaida kabisa, inajulikana kuwa Muungano baina ya nchi ni maafikiano kati ya nchi na nchi. Na mnapoungana mmeridhia kuwa pamoja kwa mambo yote, sasa mimi nahoji juu ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Zanzibar ina rais wake, na Jamhuri ya Muungano ina Rais wake. Sasa huyu rais wa jamhuri ya Muungano ana nguvu ipi dhidi ya Zanzibar? Na kama hana mamlaka yoyote juu ya Zanzibar uhalali wa Muungano uko wapi? Katiba ijayo ibadilishe hiki kitu maana sikielewi elewi vile!