Upeo wa Uwezo wetu kufikiri? - Kwanini suluhisho la tatizo la maji vijijini ni kuchimba visima?

Kupanga ni kuchagua! Kupanga kunategemea nguvu yako kiuchumi; utapanga kikubwa kama uchumi wako mkubwa na utapanga kidogo kama uchumi wako mdogo.

Duniani kote maji kwa matumizi mbalimbali yanatokana na vyanzo vifuatavyo:
  1. Surface water kwa maana ya mito na maziwa;
  2. Rainwater harvesting kwa maana ya mabwawa yaliyoko katika maeneo makame; na
  3. Groundwater kwa maana ya visima virefu na vifupi pia chemchem.

Maji kutoka katika vyanzo vyote hapo juu unaweza kuyapata kwa kuyafuata huko huko yaliko au kwa kutumia technolojia mbalimbali ukayapampu hadi unakotaka kuyafikisha. Technolojia zinazotumia ni pamoja na:
  • Ku-pump kwa kutumia mafuta au umeme
  • Ku-pump kwa kutumia upepo
  • Kutumia nguvu ya mserereko (Gravity)

Ili uweze kutumia technolojia hizo kwa ufanisi huna budi na nguvu kubwa ya kiuchumi ili uweze kuukamilisha mradi na pia kuuendesha ili uwe endelevu.

Kwa kuwa wananchi wetu wengi ni maskini ambao kipato chao kwa siku ni chini ya dola moja technolojia nyepesi na rahisi kwa wao kuiendesha ni kuwa na kisima cha maji kilichofungwa pampu ya mkono au kutumia ndoo kwa visima vifupi.

Kwa maeneo ya mijini kwa kuwa watu wengi wana uchumi mkubwa pampu za umeme au dizeli hutumika na maji kusambazwa kwa mabomba hadi yanapohitajika (Nyumbani). Nchini kwetu kuna miji kama Arusha, Dodoma na Mtwara ambayo inategemea maji kwa 100% kutoka visimani na kusambazwa kwa mabomba.

Faida mojawapo ya maji ya visima kama vimechimbwa mbali ya makazi ya watu huwa ni safi na salama na kwa kiwango kikubwa hayahitaji tiba (Treatment) hivyo kuwa rahisi kwa miradi ya namna hii kuiendesha. Tofauti na maji ya mabwawa, mito na maziwa ambayo bila ya kufanyiwa tiba ni hatari kwa afya ya binadamu kwa kuwa huwa na tope jingi na vimelea vya magonjwa na hivyo uendeshaji wa miradi hii huwa ghali kwa kuwa na gharama za ziada za madawa ya kutibia maji.

Kwa kifupi serikali inapohamasisha watu kuchimba visima ni kwa sababu ya kuona kuwa wananchi wake wana uwezo mdogo wa kuiendesha. Hata hivyo lengo ni kuwa endapo hali ya uchumi wa wananchi itaimarika basi technolojia inaweza kubadilishwa na kusambaza maji kwa njia ya mabomba. Visima vilivyochmbwa kwa utaalam sahihi vinaweza kudumu kwa miaka mingi na mfano ni Dodoma ambako kuna visima vilichimbwa miaka ya 1930 mpaka leo vinatoa maji!

Safi sana mkuu Ileje kwa kutoa maelezo ya ufasaha katika mada hii.

Nakubaliana kabisa kuwa provision ya maji ni suala la uchumi na uhandisi, na fani hizo ndio zinaweza kutoa majibu sahihi juu ya utatuzi wa wananchi kupata au kutopata maji,of course mipango ikikaa sawa.
 
Idea ya kusambaza maji inawezekana lakini kuna some pre-conditions ambazo zinatakiwa kuwa met.
1. Hali ya uchumi wa wasambaziwa maji kwamba waweze kulipa bills zao
2. Mipango Miji/Vijiji ili kuwa na ramani kwamba bomba kubwa la maji litapita, halafu mabomba madogo yatatandazwa wapi.
3. Huduma ya maji itolewe kwa misingi ya biashara, kwamba ama serikali ainzishe shirika la kutoa huduma hiyo au kampuni binafsi zifanye kazi hiyo. Kampuni binafsi wanaogopa kuingia kwenye hiyo biashara kwa sababu wanakwepa gharama za kujenga infrastructure ya kusambaza maji. Inachukua muda mrefu ku-recover gharama za kutandaza mabomba kwa watumiaji.


Keil, nitakuuliza swali moja (au mawili); hawa wananchi wa vijijini wanatumia fedha kufanyia jambo lolote? Je, gharama ya maji ni kubwa mno kulinganisha na gharama ya vitu kama pombe, vyakula n.k?

Jambo jingine ambalo linaweza kuangaliwa ni jinsi gani vijiji vinaweza kuwa na Community Water Fund badala ya kila mmoja kulipia maji anayotumia...
 
Kupanga ni kuchagua! Kupanga kunategemea nguvu yako kiuchumi; utapanga kikubwa kama uchumi wako mkubwa na utapanga kidogo kama uchumi wako mdogo.

Duniani kote maji kwa matumizi mbalimbali yanatokana na vyanzo vifuatavyo:
  1. Surface water kwa maana ya mito na maziwa;
  2. Rainwater harvesting kwa maana ya mabwawa yaliyoko katika maeneo makame; na
  3. Groundwater kwa maana ya visima virefu na vifupi pia chemchem.

Maji kutoka katika vyanzo vyote hapo juu unaweza kuyapata kwa kuyafuata huko huko yaliko au kwa kutumia technolojia mbalimbali ukayapampu hadi unakotaka kuyafikisha. Technolojia zinazotumia ni pamoja na:
  • Ku-pump kwa kutumia mafuta au umeme
  • Ku-pump kwa kutumia upepo
  • Kutumia nguvu ya mserereko (Gravity)

Ili uweze kutumia technolojia hizo kwa ufanisi huna budi na nguvu kubwa ya kiuchumi ili uweze kuukamilisha mradi na pia kuuendesha ili uwe endelevu.

Kwa kuwa wananchi wetu wengi ni maskini ambao kipato chao kwa siku ni chini ya dola moja technolojia nyepesi na rahisi kwa wao kuiendesha ni kuwa na kisima cha maji kilichofungwa pampu ya mkono au kutumia ndoo kwa visima vifupi.

Kwa maeneo ya mijini kwa kuwa watu wengi wana uchumi mkubwa pampu za umeme au dizeli hutumika na maji kusambazwa kwa mabomba hadi yanapohitajika (Nyumbani). Nchini kwetu kuna miji kama Arusha, Dodoma na Mtwara ambayo inategemea maji kwa 100% kutoka visimani na kusambazwa kwa mabomba.

Faida mojawapo ya maji ya visima kama vimechimbwa mbali ya makazi ya watu huwa ni safi na salama na kwa kiwango kikubwa hayahitaji tiba (Treatment) hivyo kuwa rahisi kwa miradi ya namna hii kuiendesha. Tofauti na maji ya mabwawa, mito na maziwa ambayo bila ya kufanyiwa tiba ni hatari kwa afya ya binadamu kwa kuwa huwa na tope jingi na vimelea vya magonjwa na hivyo uendeshaji wa miradi hii huwa ghali kwa kuwa na gharama za ziada za madawa ya kutibia maji.

Kwa kifupi serikali inapohamasisha watu kuchimba visima ni kwa sababu ya kuona kuwa wananchi wake wana uwezo mdogo wa kuiendesha. Hata hivyo lengo ni kuwa endapo hali ya uchumi wa wananchi itaimarika basi technolojia inaweza kubadilishwa na kusambaza maji kwa njia ya mabomba. Visima vilivyochmbwa kwa utaalam sahihi vinaweza kudumu kwa miaka mingi na mfano ni Dodoma ambako kuna visima vilichimbwa miaka ya 1930 mpaka leo vinatoa maji!

Nimeyapenda sana maelezo yako kwani yanadokeza utaalamu katika masuala haya; hata hivyo ninachohofia ni kuwa mara nyingi tunaanza na mawazo ya "sisi ni maskini" na kutoka hapo tunajiona hatuwezi kufanya mambo mbalimbali au hata kuyafikiria kuyafanya. La pili nadhani linahusiana na innovation. Unapokosa innovation ni rahisi kuona watu hawana kitu chochote na hawajui kuwa with innovation kunakuja ujasiriamali n.k Hivi kwa mfano, ukitatua tatizo la maji kijijini unafungua kwa kiasi gani maisha ya wananchi hao kufanya mambo mengine zaidi ya kuhangaika na maji? Vitu vingi ambavyo ni vigumu kuanzishwa na kuendelezwa mahali ambapo pana shida ya maji ni rahisi kuvianzisha ukishapata maji.

Binafsi - na nina uhakika watu wengine vile vile - naamaini kuwa kuna miundo mbinu ya msingi ya kujenga taifa la kisasa; la kwanza ni maji, nishati, elimu na utawala. Unatakiwa kuvitatua hivi kwa gharama yoyote ili kufanya mambo mengine yawezekane.
 
Keil, nitakuuliza swali moja (au mawili); hawa wananchi wa vijijini wanatumia fedha kufanyia jambo lolote?

Mwanakijiji,

Jibu la swali lako la kwanza ni gumu kiasi. Lakini kwa observation yangu ya sehemu ambazo nimetembelea naweza kusema kwamba pombe huchukua fungu kubwa la fedha zao ni pombe, hasa baada ya kuuza mavuno au kupata malipo ya mauzo yao ya mazao ya biashara. Hapa ninaongelea households ambazo ziko headed na wanaume.

Je, gharama ya maji ni kubwa mno kulinganisha na gharama ya vitu kama pombe, vyakula n.k?

Gharama ya maji ni ndogo ukilinganisha na gharama ya pombe. Vyakula ni almost bure kwa kuwa kila familia inakula kile ilicholima with exception of few items.

Jambo jingine ambalo linaweza kuangaliwa ni jinsi gani vijiji vinaweza kuwa na Community Water Fund badala ya kila mmoja kulipia maji anayotumia...

Idea yako ni nzuri sana kwa kuwa maamuzi yakishafanywa na kijiji, wananchi wengi huwa wanaona aibu kwenda against. Kwa hiyo kama Kijiji kikianzisha Community Water Fund ambayo itatumika kuwasambazia wananchi maji kijijini, ni rahisi sana kufanikisha zoezi. Pia wanakijiji wanajua namna ya kubanana ili kila mtu achangie/alipe kile anachotakiwa kulipa na wanajua ni kipindi gani kizuri cha kuwadai. Kwa vijiji ambavyo vinahusika na uzalishaji wa mazao ya biashara kama pamba na tumbaku, ni rahisi kuwabana wananchi kulipia contributions zao wakati wa malipo ya mauzo yao.

Idea hii inaweza kushusha zaidi gharama ya kusambaza maji kwa kuwa kijiji kizima kila mtu atakuwa na bomba nyumbani kwake, so hata bill nayo inakuwa ni ndogo. Idea ya kusambaza kwa kila mtu kuomba individually, sometimes wengine wanaweza kuona maji si muhimu sana na wakawa wanakwenda kuchota kwa majirani. Huwezi kutandaza bombo KM 30 halafu wateja wako 20 tu, lazima hao wateja wataishia kulipa bills kubwa sana.

Challenge pekee ambayo nimeishakumbana nayo ni namna ya kuwachangisha wanakijiji wote kwa uwiano ulio sawa na hasa linapokuja swala la ukubwa wa household ambayo pia hutumia maji mengi kuliko household ambazo zina watu wachache.
 
Tatizo mnataka kuruka hatua. Maendeleo ni hatua kwa hatua. Na hizi ndizo hatua:

1. Kusota
2. Kutambaa
3. Kutembea
4. Kukimbia
5. Kupaa

Kwa sasa bado tunatambaa, tuimalize kwanza hiyo hatua kisha tutaweza kupiga hatua.
 
Tatizo mnataka kuruka hatua. Maendeleo ni hatua kwa hatua. Na hizi ndizo hatua:

1. Kusota
2. Kutambaa
3. Kutembea
4. Kukimbia
5. Kupaa

Kwa sasa bado tunatambaa, tuimalize kwanza hiyo hatua kisha tutaweza kupiga hatua.

Sasa lini tutamaliza huko kutambaa?
 
Mwanakijiji,

Jibu la swali lako la kwanza ni gumu kiasi. Lakini kwa observation yangu ya sehemu ambazo nimetembelea naweza kusema kwamba pombe huchukua fungu kubwa la fedha zao ni pombe, hasa baada ya kuuza mavuno au kupata malipo ya mauzo yao ya mazao ya biashara. Hapa ninaongelea households ambazo ziko headed na wanaume.

Naam, nilitarajia hivyo. Hii ina maana hakuna tatizo hasa la "pesa" huko vijijini kwani karibu sisi sote tunajua mojawapo ya matumizi ya kawaida sana kijijini ni haya ya ulabu...




Gharama ya maji ni ndogo ukilinganisha na gharama ya pombe. Vyakula ni almost bure kwa kuwa kila familia inakula kile ilicholima with exception of few items.

Naam, nilichukulia hilo pia. Nashukuru nawe umeliona. Mtu akitaka kuku haendi Tandale anaenda kwenye banda lake.



Idea yako ni nzuri sana kwa kuwa maamuzi yakishafanywa na kijiji, wananchi wengi huwa wanaona aibu kwenda against. Kwa hiyo kama Kijiji kikianzisha Community Water Fund ambayo itatumika kuwasambazia wananchi maji kijijini, ni rahisi sana kufanikisha zoezi. Pia wanakijiji wanajua namna ya kubanana ili kila mtu achangie/alipe kile anachotakiwa kulipa na wanajua ni kipindi gani kizuri cha kuwadai. Kwa vijiji ambavyo vinahusika na uzalishaji wa mazao ya biashara kama pamba na tumbaku, ni rahisi kuwabana wananchi kulipia contributions zao wakati wa malipo ya mauzo yao.

Yes, nimeoana wameanzisha "Community Health Funds" lakini ukiniuliza mimi hakuna kitu cha afya cha msingi kabisa kama maji!

Idea hii inaweza kushusha zaidi gharama ya kusambaza maji kwa kuwa kijiji kizima kila mtu atakuwa na bomba nyumbani kwake, so hata bill nayo inakuwa ni ndogo. Idea ya kusambaza kwa kila mtu kuomba individually, sometimes wengine wanaweza kuona maji si muhimu sana na wakawa wanakwenda kuchota kwa majirani. Huwezi kutandaza bombo KM 30 halafu wateja wako 20 tu, lazima hao wateja wataishia kulipa bills kubwa sana.

Mkiamua kufanya ni "community water" basi kila mdau wa hiyo community ni lazima kwa namna moja au nyingine awajibike iwe katika kulipa, kufanyia matengenezo, kulinda n.k Kila mtu anayekunywa maji hayo (hata kwa jirani) ni lazima awajibike kwayo in one way or another.


Challenge pekee ambayo nimeishakumbana nayo ni namna ya kuwachangisha wanakijiji wote kwa uwiano ulio sawa na hasa linapokuja swala la ukubwa wa household ambayo pia hutumia maji mengi kuliko household ambazo zina watu wachache.

Sidhani kama ni kwa uwiano ulio sasa kwa maana ya mtu na mtu; nafikiri inaweza kufanywa kwa "nyumba kwa nyumba" kutegemeana na idadi ya wakazi ya kudumu. Kwa mfano, nyumba yenye wazee wawili haiwezi kulipishwa sawa na nyumba yenye vijana watano! So, inakuwa ni nyumba kwa nyumba kutegemeana na wakazi lakinivile vile majengo kutokana na matumizi yake. Kwa mfano, mtu mwenye hoteli halipi sawa na mwenye klabu ya pombe tu au shule au zahanati. Ndio hapa naamini vichwa vya Watanzania vitahitaji kugongana kutafuta formula nzuri.
 
Tatizo mnataka kuruka hatua. Maendeleo ni hatua kwa hatua. Na hizi ndizo hatua:

1. Kusota
2. Kutambaa
3. Kutembea
4. Kukimbia
5. Kupaa

Kwa sasa bado tunatambaa, tuimalize kwanza hiyo hatua kisha tutaweza kupiga hatua.

Nadhani umekosea.. kuna hatua ya Kuota mbawa!!! Kipepeo na ndege wote wanaruka angani lakini safari yao kufika kuruka angani ni tofauti kwelikweli.
 
Nadhani umekosea.. kuna hatua ya Kuota mbawa!!! Kipepeo na ndege wote wanaruka angani lakini safari yao kufika kuruka angani ni tofauti kwelikweli.

la hasha! mwalimu alikosea aliposema tukimbie wakati wengine wanatembea, na waziri mkuu mstaafu naye akakosea aliposema tunapaa. kinachopaswa ni kuwa wanyenyekevu na kukubali hali halisi. hata kipepeo huanza kama bua na chura huanza kama kiluwiluwi. kidogo kidogo hujaza kibaba. hatua kwa hatua tutafika.
 
Hakuna kiongozi hata 1 yuko serious na maendeleo ya taifa hili, wote wanafanyia kazi maendeleo ya familia zao tu!. Dawa ni moja tu, mikoa ijitegemee kimapato na matumizi ili ishindane kimaendeleo! serikari kuu ibaki kuziba mapungufu yanayotokana na tofauti za mali asili. Itakua ni rahisi kujua kodi tunayotoa inakoenda na tutahoji.

Wenye sera ya Majimbo ni Chadema, wasomeni vizuri bila ushabiki
 
la hasha! mwalimu alikosea aliposema tukimbie wakati wengine wanatembea, na waziri mkuu mstaafu naye akakosea aliposema tunapaa. kinachopaswa ni kuwa wanyenyekevu na kukubali hali halisi. hata kipepeo huanza kama bua na chura huanza kama kiluwiluwi. kidogo kidogo hujaza kibaba. hatua kwa hatua tutafika.

Nilipotumia hili neno ''tutafika'' kama jina langu sikumaanisha kwa spidi hii. Lazima mwendo ufanane na nguvu tuliyo nayo. kwa sasa tunatumia 1/8 ya nguvu tuliyo nayo, hatutafika kabisaa!
 
Nilipotumia hili neno ''tutafika'' kama jina langu sikumaanisha kwa spidi hii. Lazima mwendo ufanane na nguvu tuliyo nayo. kwa sasa tunatumia 1/8 ya nguvu tuliyo nayo, hatutafika kabisaa!

haraka haraka haina baraka. mbio za sakafuni huishia ukingoni. kawia ufike. pole pole ndio mwendo.
 
Mara nyingi sana nimesikia wanasiasa wakitoa ahadi za kuchimba visima kama njia ya kutatua tatizo la maji - iwe mjini au vijijini. Hebu angalia vichwa hivi vya habari kisha usome swali langu tena:

Wamarekani kuchimba visima 20 Dakawa

Watumia Sh400 mil kuchimba visima

Dewji achimba visima kwa milioni 500 Singida


Abood aingiza mitambo ya kuchimba visima

Mbunge aanza kuchimba visima 60 jimboni

Ujenzi visima vya maji Morogoro, wakazi pembezoni mwa mji kunufaika.


Sasa kuna vitu najiuliza:

a. Kwanini mara nyingi suluhisho la haraka linalochukuliwa kukabiliana na tatizo la maji ni kuchimba visima na hivyo kuwasababisha wananchi kuyafuata maji kutoka majumbani mwao badala ya kufikiria mfumo wa kuwaletea maji hayo (yanayopatikana kwenye visima hivyo) kwa wananchi?

b. Je, kuna uwezekano wa kubuni njia ya kuunganisha visima kadhaa kutengeneza mfumo wa maji wa mahali (local water supply system) badala ya kuwa na visima kimoja kimoja? Kwa mfano, visima 50 (au hata kimoja tu) vinajaza maji kwenye tanki la jumuiya na kutoka kwenye tanki (lililoko uphill) mabomba yanarudishwa wa wananchi? Kinachohitajika ni kutengeneza pump ya upepo kusukuma maji mlimani.

c. Ni kweli kuchimba visima vingi yaweza kuwa ni suluhisho la sasa "hivi" la maji lakini ni visima vingapi ambavyo vimebakia kutumika baada ya miaka na viko katika hali gani na je ndilo suluhisho bora zaidi? Kuna namna nyingine yoyote ya kuweza kutumia maji yaliyoko ardhini kutengeneza mfumo wa maji safi katika jamii mbalimbali?

Ninajua kuna wataalamu wa mambo mbalimbali hapa ambao wanaweza kutusaidia kujibu swali hili: Je inawezekana kutumia maji ya visimani kuweza kuyafikisha kwenye nyumba ya kila mwanakijiji badala ya kila mwanakijiji kulifuata bomba au kisima kilipo?

nadhani upeo wetu kwa pamoja hauna shida....kama wewe umekuja wazo endelevu basi upeo upo.teh teh...shusha mambo wataalamu wetu waende mbali zaidi.Wazo lako zuri kwani visima vya watu binafsi vingi vinafikia hali ya kuwa contaminated na baadaye kuwa havifai kabisa.So kuwa na visima ambavyo vinatoa maji bila kufikiwa na watu ambao wanaweza vichafua au kuvifikishia maambukizi itakuwa ni vyema zaidi.
 
Nimeyapenda sana maelezo yako kwani yanadokeza utaalamu katika masuala haya; hata hivyo ninachohofia ni kuwa mara nyingi tunaanza na mawazo ya "sisi ni maskini" na kutoka hapo tunajiona hatuwezi kufanya mambo mbalimbali au hata kuyafikiria kuyafanya. La pili nadhani linahusiana na innovation. Unapokosa innovation ni rahisi kuona watu hawana kitu chochote na hawajui kuwa with innovation kunakuja ujasiriamali n.k Hivi kwa mfano, ukitatua tatizo la maji kijijini unafungua kwa kiasi gani maisha ya wananchi hao kufanya mambo mengine zaidi ya kuhangaika na maji? Vitu vingi ambavyo ni vigumu kuanzishwa na kuendelezwa mahali ambapo pana shida ya maji ni rahisi kuvianzisha ukishapata maji.

Binafsi - na nina uhakika watu wengine vile vile - naamaini kuwa kuna miundo mbinu ya msingi ya kujenga taifa la kisasa; la kwanza ni maji, nishati, elimu na utawala. Unatakiwa kuvitatua hivi kwa gharama yoyote ili kufanya mambo mengine yawezekane.

Kuna jambo ambalo serikali imekuwa ikilihubiri sana kwa wananchi, nalo ni ushirikishwaji wa wananchi katika kupanga mipango yao ya maendeleo. Lakini ukweli ni kuwa utekelezaji wa sera hii umekuwa mgumu sana na badala yake miradi mingi ya maendeleo vijijini imekuwa ikipanga kutoka juu (TOP - DOWN), kwa maneno mengine inakuwa imposed! Hivyo kuna wakati kijiji kinazidiwa na uwingi wa miradi inayotekelezwa hapo, kwa mfano kunaanzishwa miradi ya maji, barabara, shule ya kata, zahanati ushirika, michango mbalimbali nk kwa wakati mmoja na wananchi wanatakiwa kuchangia ama kwa fedha au kwa nguvu zao. Inapotokea namna hii wananchi wanashindwa kwa kuwa pia wanawajibika katika miradi yao binafsi kama mashamba, kujijengea nyumba nk. Matokeo yake ni miradi mingi kutekelezwa chini ya kiwango nakuharibika katika muda mfupi sana na umaskini kuendelea kuikabili jamii husika!

Ni kweli kuwa wananchi wakipata huduma ya maji wanakuwa wameokoa muda mwingi wa kuyatafuta na kutumia muda huo kwa shughuli zingine. Lakini huduma hii haitolewi bure bali wanatakiwa kugharimia uendeshaji wake kwa kutoa fedha. Uwezo wa kifedha kwa wananchi wengi vijijini ni mdogo sana. Kwa mfano vijiji ambavyo vinategemea zao la mahindi kwa chakula na biashara, chukulia familia imevuna magunia 50 assume watahifadhi nusu kwa ajili ya chakula na nusu iliyobaki watauza ili waweze kupata mahitaji mengine. Hata ikiuza gunia moja kwa Sh.50,000/= itapata Sh.1,250,000/= kwa mwaka. Fedha hii haitatosha kukidhi matumizi ya familia yakiwemo ada za watoto, matibabu, mavazi, pembejeo kwa ajili ya msimu unaofuata nk. Hivyo uwezo wa familia hii kugharimia maji ni mdogo na hata kama maji ya bomba yapo wata-opt kuyafuata katika chanzo cha asili badala ya kutoa fedha. Kwa kuwa familia za namna hii ni nyingi vijijini miradi hiyo itabaki white elephant na matokeo yake miradi hiyo kufa kwa kukosa fedha za uendeshaji au kwa kuhujumiwa na wanavijiji wenyewe! Kuna mifano mingi hapa nchini. Mkoa wa Rukwa ambao ulipata ufadhili wa NORAD miaka ya 1980 ilifikia upatikanaji wa maji kwa zaidi ya 80% lakini leo hii miradi mingi ilishakufa na sidhani kama upatikanaji wa maji hivi sasa unazidi 50%. Hali hiyo pia iko katika mikoa ya Lindi na Mtwara iliyopata ufadhili wa FINIWATER (FINIDA), mikoa ya Mbeya, Iringa na Ruvuma iliyopata ufadhili wa DANIDA nk.

Hivyo kama unavyohitimisha ni kweli kuna miundombinu ya msingi ambayo inatakiwa kujegwa ili maendeleo yapatikane lakini ili miundombinu hii iweze kudumu na kuwa endelevu wananchi wanatakiwa kuwezeshwa kiuchumi! Moja ya mbinu ya kuwawezesha wanavijiji wetu ni kwa serikali kutoa ruzuku kwa pembejeo za kilimo ili wananchi wawe na chakula cha kutosha na pia kupata mazao mengi ya biashara. Utaratibu wa kuwauzia mbolea kwa bei ya soko kama ilivyo sasa mfuko wa kilo 50 kwa Sh. 100,000/= hautawakomboa wakulima!
 
haraka haraka haina baraka. mbio za sakafuni huishia ukingoni. kawia ufike. pole pole ndio mwendo.
Falsafa za wavivu wa pwani wanaoshinda kwenye bao!!, ukizifuata utakwama! Eti mwenda pole hajikwai (badala ya mwenda pole anakawia kufika)
 
Tunaweza kufanya hivyo,ila hatujataka. Na kama hatujataka hatutaweza kufanya lolote hata iweje. Inanihuzunisha sana kuona jinsi tunavyopeleka mambo. Kweli hatuwezi kufika popote

ni kweli hatujatyaka, sisi pamoja na viongozi wetu. Hasa SISI TUNAOJUA kwamba INAWEZEKANA, sijui kwanini tunataka HAO
viongozi wasiojua ndo wafanye, au tunasubiri tupate ubunge ndo tuonyeshe mchango wetu? Au sisi mchango wetu ni kukosoa?
 
Falsafa za wavivu wa pwani wanaoshinda kwenye bao!!, ukizifuata utakwama! Eti mwenda pole hajikwai (badala ya mwenda pole anakawia kufika)

asiyesikia la mkuu huvunjika guu - tulienda kwa kasi tukajikwaa, uchumi ukavunjika
 
Back
Top Bottom