Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,424
- 911,172
Wakati akisulubiwa na Kamati ya Bunge ya Maliasili na Mazingira, aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Maige alikimbilia kwenye vyombo vya khabari na akawasagia Kamati husika akidai imehongwa na yeye ni mtu mwadilifu sana. Akiwa Bungeni aliishutumu Kamati tajwa chini ya uenyekiti wa Mhe. James Lembeli imwogope Mungu na ya kuwa inamwandama kwa kumwonea gere, chuki na fitina.
Mhe. Lembeli alimkumbusha Maige ya kuwa asilitaje jina la Mungu bure kwa kuwa Mungu siyo wa Maige tu bali ni wa wote viumbe vyake..........................La ajabu na kushangaza sana, jana wakati akimkabidhi wizara tajwa mrithi wake Balozi Kagasheki, Mhe. Maige alisahau kauli zake za awali za ya kuwa yeye ni mwadilifu na akakiri ya kuwa alishindwa kuwasimamia watendaji ndani ya wizara yake na hata akatolewa kafara........Hivi kafara hutolewa kwa mtu aliyeshindwa majukumu yake au kwa yule aliyeonewa?.....Maige kwa kukiri huku kunafanya kauli zake bungeni na kwenye vyombo vya khabari kuwa hakuwa mkweli hata kidogo na ya kuwa utetezi wake ulikuwa kwa masilahi yake binafsi na wala siyo ya taifa............na ubinafsi wake ulichanuka pale alipomshukuru JK badala ya Mwenyezi Mungu kwa kumpa ugali na kumnufaisha yeye binafsi............Hili kweli linatisha sana!.......Maige safari hii baada ya kutenguliwa hakumkumbuka Mungu kama alivyokuwa Bungeni na hata kumshukuru angalau kwa kumwachia kuwa hai hadi jana hiyo huku akiwa kinara wa ufisadi au hata kuishukuru familia yake kwa kumruhusu na kumvumilia kuwepo kwake kwenye ulingo wa siasa..................au basi hata kuwashukuru wapigakura wajimbo lake ambao ndiyo waliomweka kwenye chati za siasa hata huyo JK akamwona angeliweza kumfaa kwenye cabinet yake...................Ingawaje hata JK mwenyewe anaonekana ni bomu kwa kuteua watu ambao uwezo wao wa kufikiri ni finyu kama huyu............
Mhe. Maige hakujilaumu yeye binafsi kwa kuelezea umma yawaje baada ya kuwa waziri ndiyo aligundua kumbe yeye ni mjasiria mali nguli na hata angeliweza kujirundikia mabilioni ya mapesa na kuwa na mali nyingi zisizohamishika ambazo kama bila ya kufanya biashara ya siasa hayo yasingeliwezekana.................
Kwa kifupi kauli tatanishi za Maige na kukwepa kujilaumu mwenyewe huku akilaumu washirika wake wa karibu ndani ya wizara aliyokuwa akiiongoza ni dalili ya upeo wake ni finyu............................sioni utetezi mwingine.....................na kwa khali hii baada ya Takukuru kumweka kibindoni usishangae kuona anapatwa na kiharusi au jirani ya balaa za namna hiyo.......................sioni kama ana uwezo wa kuhimili mikikimikiki ya namna hizo hata chembe maana mwenyewe hajui anasimamia nini..........
Mhe. Lembeli alimkumbusha Maige ya kuwa asilitaje jina la Mungu bure kwa kuwa Mungu siyo wa Maige tu bali ni wa wote viumbe vyake..........................La ajabu na kushangaza sana, jana wakati akimkabidhi wizara tajwa mrithi wake Balozi Kagasheki, Mhe. Maige alisahau kauli zake za awali za ya kuwa yeye ni mwadilifu na akakiri ya kuwa alishindwa kuwasimamia watendaji ndani ya wizara yake na hata akatolewa kafara........Hivi kafara hutolewa kwa mtu aliyeshindwa majukumu yake au kwa yule aliyeonewa?.....Maige kwa kukiri huku kunafanya kauli zake bungeni na kwenye vyombo vya khabari kuwa hakuwa mkweli hata kidogo na ya kuwa utetezi wake ulikuwa kwa masilahi yake binafsi na wala siyo ya taifa............na ubinafsi wake ulichanuka pale alipomshukuru JK badala ya Mwenyezi Mungu kwa kumpa ugali na kumnufaisha yeye binafsi............Hili kweli linatisha sana!.......Maige safari hii baada ya kutenguliwa hakumkumbuka Mungu kama alivyokuwa Bungeni na hata kumshukuru angalau kwa kumwachia kuwa hai hadi jana hiyo huku akiwa kinara wa ufisadi au hata kuishukuru familia yake kwa kumruhusu na kumvumilia kuwepo kwake kwenye ulingo wa siasa..................au basi hata kuwashukuru wapigakura wajimbo lake ambao ndiyo waliomweka kwenye chati za siasa hata huyo JK akamwona angeliweza kumfaa kwenye cabinet yake...................Ingawaje hata JK mwenyewe anaonekana ni bomu kwa kuteua watu ambao uwezo wao wa kufikiri ni finyu kama huyu............
Mhe. Maige hakujilaumu yeye binafsi kwa kuelezea umma yawaje baada ya kuwa waziri ndiyo aligundua kumbe yeye ni mjasiria mali nguli na hata angeliweza kujirundikia mabilioni ya mapesa na kuwa na mali nyingi zisizohamishika ambazo kama bila ya kufanya biashara ya siasa hayo yasingeliwezekana.................
Kwa kifupi kauli tatanishi za Maige na kukwepa kujilaumu mwenyewe huku akilaumu washirika wake wa karibu ndani ya wizara aliyokuwa akiiongoza ni dalili ya upeo wake ni finyu............................sioni utetezi mwingine.....................na kwa khali hii baada ya Takukuru kumweka kibindoni usishangae kuona anapatwa na kiharusi au jirani ya balaa za namna hiyo.......................sioni kama ana uwezo wa kuhimili mikikimikiki ya namna hizo hata chembe maana mwenyewe hajui anasimamia nini..........