Updates: VodaCom Premier League 2009/2010

TIMU GANI ITAKUWA BINGWA WA LIGI KUU TANZANIA BARA(Vodacom Premier League)


  • Total voters
    72
  • Poll closed .
Angalau leo nimefarijika, maana wekundu wa UK jana walifulia lakini wekundu wa Tz wametupa raha!
 
HATIMAYE mbio za miezi saba ya kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Bara, zinaanza leo kwa miamba 12 kushuka dimbani huku bingwa mtetezi, Yanga akianza na wageni, African Lyon kwenye Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam.
Yanga, mabingwa mara 22 tangu kuanza kwa Ligi hiyo mwaka 1965, leo wanakuwa wa kwanza kuikaribisha Lyon kwenye ligi hiyo ambao ni msimu wa kwanza kwao.
Hata hivyo, ni mechi inayotarajiwa kuwa ya ushindani mkubwa kutokana na ubora wa vikosi vyao, ingawa Lyon wanazidiwa kwa uzoefu.
Katibu Mkuu wa Lyon, Jeshi Zacharia, amesema pamoja na ugeni wao katika Ligi Kuu, lakini ubora wa kikosi chao, unawapa kiburi cha kujiamini dhidi ya Yanga.
“Ni kweli Yanga ni wazoefu zaidi yetu, lakini kwa ubora wa kikosi au kiuchezaji, hilo ni suala jingine…nasi tunajivunia kwa hilo, tutajitahidi kuwajengea vijana hali ya kujiamini,” alisema Zacharia.
Naye Mwenyekiti wa Yanga, Imani Mahugila Madega, kwa upande wake ameifananisha Yanga kama ‘kinara wa mchezo’, ambaye kadiri itakavyokuwa, hauawi.
Alichomaanisha Madega ni kuwa, kadiri itakavyokuwa, Yanga leo itaibuka na ushindi dhidi ya Lyon, hivyo kutwaa pointi zote tatu na kuanza vizuri ligi hiyo itakayofikia tamati Machi 27, mwakani.
Vita nyingine ya ligi hiyo, itakuwa kwenye Uwanja wa Majimaji, mjini Songea, Ruvuma kwa wenyeji Majimaji kuwakaribisha Simba.
Ni mechi ngumu kwani wakati Simba wakitaka kushinda ili kuanza vema ligi hiyo, wenyeji Majimaji watakuwa wakipigana vilivyo kushinda katika uwanja wao wa nyumbani.
Majimaji, timu yenye historia katika soka ya Tanzania, leo watakuwa na kazi moja ya kudhihirisha kuwa hawakupanda Ligi Kuu kwa kubahatisha baada ya kuikosa kwa misimu kadhaa.
Hata hivyo, Simba walio chini ya Kocha Mzambia, Patrick Phiri, safari hii wamejipanga kutwaa ubingwa baada ya kuukosa kwa misimu miwili, ukitwaliwa na watani wao Yanga.
Hata hivyo, vita ya ligi hiyo safari hii inaonekana itakuwa na radha ya aina yake, kwani wakati Yanga wakiwania kutwaa ubingwa wa 23, Simba wamekamia kufanya hivyo kwa mara ya 16.
Aidha, Mtibwa Sugar wenye rekodi ya kutwaa ubingwa huo mara mbili, leo watakuwa katika Uwanja wao wa Manungu, Turiani kuwakaribisha Manyema Rangers.
Mtibwa Sugar, wanaingia katika kampeni ya kuwania ubingwa wa mara ya tatu wakiwa na kiburi cha ubingwa wa Kombe la Tusker na Ngao ya Jamii.
Kivumbi kingine cha ligi hiyo, kitakuwa kwenye Uwanja wa CCM-Kirumba, jijini Mwanza kwa wenyeji Toto Africa kuwakaribisha Moro United ya Dar es Salaam.
Aidha, katika Uwanja wa Kaitaba, Bukoba, wenyeji Kagera Sugar wanaonolewa na Kocha Mganda, George Ssemogerere, watakuwa wenyeji wa Azam FC.
Mechi nyingine, itakuwa katika Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya kwa maafande wa Prisons kuwakaribisha ndugu zao JKT Ruvu ya Pwani.


Source: Gazeti la Tanzania Daima
Hivi kwa nini akina VODACOM na wenzao hawatoi misaada kwenye Mahospitali ambapo pana upungufu wa madawa, vifaa vya kazi? Sponsorship zao mkwenye michezo mimi hazinigusi sana kwani mwannchi wakawaida hafaidiki na misaada hiyo. Waache cheap popularity!
 
Hivi kwa nini akina VODACOM na wenzao hawatoi misaada kwenye Mahospitali ambapo pana upungufu wa madawa, vifaa vya kazi? Sponsorship zao mkwenye michezo mimi hazinigusi sana kwani mwannchi wakawaida hafaidiki na misaada hiyo. Waache cheap popularity!
mwananchi wakawaida ni yupi..
 
Yanga 1 Azam 1 chupuchupu kwa jangwani.
Leo Simba wamempiga mtu 4-1 JKT ruvu.kweli simba huu mwaka wao???kama Arsernal.
 
Kwa Simba niliyoiona leo kama Yanga watatia mguu tarehe 31 Oktoba, lazima wanywe! Kocha wao mpya kutoka Serbia alikuwepo uwanjani na alikuwa anashangilia mabao ya Simba. Ila aliondoka kabla mchezo haujaisha na kusababisha kuzomewa na wana-Simba.
Yanga ninavyo wajua huenda wasipeleke timu..
 
Hivi kwa nini akina VODACOM na wenzao hawatoi misaada kwenye Mahospitali ambapo pana upungufu wa madawa, vifaa vya kazi? Sponsorship zao mkwenye michezo mimi hazinigusi sana kwani mwannchi wakawaida hafaidiki na misaada hiyo. Waache cheap popularity!


Fungua thread kuhusu sponsorship ya VODA, usituharibie hapa ebo!
 
SSC tupo mbioni kufungua web site ya uhakika. Mwaka flani, zamani enzi za Siang'a nilikuwa na utaratibu wa kununua viatu swafi vipya na kuzawadia player of the month, ambaye alikuwa anateuliwa na kocha kutokana displin, maudhurio ya mazoezi na kufuata maagizo ya kocha. Ilisaidia sana kuongeza motisha na kuwafanya players wawe na mori ya kutisha. Ofcourse zawadi hiyo ni ndogo, lakini kubwa pia kwa kule nyumbani hasa kupata viatu vya kisasa, leather na quality ya juu. Nashauri tuanze tena utaratibu huu, hasa kwa wale wapenzi wa kweli !!

Pia kwa wale ambao hawana forms za uanachama, huu ndo muda muafaka wa kujiunga. Najua mambo yakienda kama yalivyopangwa, December tutakuwa na presida, wa nguvu ambaye ana quality zote, na ambaye hata akienda kuongea na akina Blatter, basi watajua kweli kuna timu kubwa bongo- Simba. Stay tuned...
 
Najua mambo yakienda kama yalivyopangwa, December tutakuwa na presida, wa nguvu ambaye ana quality zote
I like this actually. Simba ni timu kubwa sana na kwa maana hiyo inahitaji viongozi wenye nidhamu ya uongozi na siyo blah blah za Uswahilini na kushikiana bakora kila kuchapo. Simba ubingwa ni wa nyumbani msimu huu
 
I like this actually. Simba ni timu kubwa sana na kwa maana hiyo inahitaji viongozi wenye nidhamu ya uongozi na siyo blah blah za Uswahilini na kushikiana bakora kila kuchapo. Simba ubingwa ni wa nyumbani msimu huu

Agreed........!
 
Hivi kwa nini akina VODACOM na wenzao hawatoi misaada kwenye Mahospitali ambapo pana upungufu wa madawa, vifaa vya kazi? Sponsorship zao mkwenye michezo mimi hazinigusi sana kwani mwannchi wakawaida hafaidiki na misaada hiyo. Waache cheap popularity!

Unasahau kwamba udhamini ni sehemu ya matangazo.....Mambo ya hospitali ni ya serikali, sio ya makampuni. Makampuni yanafanya kazi, yanatengeneza pesa kisha yanalipa kodi. Wafanyakazi wa makampuni hayo pia nao wanalipa kodi. Kwa hiyo ni jukumu la serikali kutumia kodi hiyo vizuri kutoa huduma kwa jamii....Sio kuiba fedha za walipa kodi na kununua magari ya kifahari!
 
SSC tupo mbioni kufungua web site ya uhakika. Mwaka flani, zamani enzi za Siang'a nilikuwa na utaratibu wa kununua viatu swafi vipya na kuzawadia player of the month, ambaye alikuwa anateuliwa na kocha kutokana displin, maudhurio ya mazoezi na kufuata maagizo ya kocha. Ilisaidia sana kuongeza motisha na kuwafanya players wawe na mori ya kutisha. Ofcourse zawadi hiyo ni ndogo, lakini kubwa pia kwa kule nyumbani hasa kupata viatu vya kisasa, leather na quality ya juu. Nashauri tuanze tena utaratibu huu, hasa kwa wale wapenzi wa kweli !!

Pia kwa wale ambao hawana forms za uanachama, huu ndo muda muafaka wa kujiunga. Najua mambo yakienda kama yalivyopangwa, December tutakuwa na presida, wa nguvu ambaye ana quality zote, na ambaye hata akienda kuongea na akina Blatter, basi watajua kweli kuna timu kubwa bongo- Simba. Stay tuned...


Mkuu Mafuluto vipi kuhusu SIMBATV, Ni Muhimu kwa Timu kubwa kama Simba kuwa na Television yake binafsi. Naomba mlitazame hilo jamani
 
Mkuu Ndege,

Ni kweli lakini si unajua tena priorities. Ni sawa na kuvaa suti kila siku wakati huna chupi ndani.

Kwa sasa priority namba moja ni kiwanja kikubwa- plot imeshapatikana na kulipiwa advance. Tunataka kujenga a sport complex, wenye kila kikorombwezo- gym, hostel, pools, hostel, n.k.
Baadhi ya source za funds zimeshapatikana, na kuna watu kama addidas, na wengine wameonyesha nia ya partnership. Sasa mambo haya yanataka kuwa na president credible, msomi, na mwenye kuweka kwenda na kuongea na mafogo. We got the guy ready. Mtu mzima mwenye heshima zake. Sio hao wanaotembea wanakula miwa na karanga za kuchemsha kila kukicha, na kuomba omba shs 200 !!

Lakini pia, tufike wakati na sisi tuwe wapenzi wa kweli. Timu lazima tuichangie kwa hali na mali, ili iendelee kutupa furaha. Huwezi amini haya mafanikio yote unayoyaona sasa yametokana na wapenzi wa kweli kukaa, na kupanga mikakati. Hata akina MO sasa anaona aibu, maana hatuombi ombi tena vijipesa vyake. Vijana wanakula balanced diet, wanalipwa, na kuna posho zinazotokana na performance, na mchano wa jumla ktk timu. Hatuna mambo ya kizamani tena eti kuwanyang'anya simu ili wasihongwe n.k. Pia wana psychological sessions, mbali na mafunzo ya kila siku uwanjani. Kama hivi kesho wanakwenda visiwani kupumzika, na j'mosi wanakuja DAR kwa pipa la kukodi, wanacheza na Azam na then wanapaa kurudi.

Kwa taarifa yako tuna timu ya U- 20 na U -17 yenye vijana wazuri sana. Tunawekeza, kwa manufaa yetu later, na hata kwa manufaa ya taifa- tutauza players na kujazia yosso wengine waliopo.
Ndiyo maana unaona hata kocha wetu anakaa msasani, nyumba nzuri na sio hao akina naniii, kocha anakaa guest kariakoo huku akishindia chips dume na tudagaa !
 
Wandugu, najua inaweza isiwe mahala pake lakini nadhani ni vyema kutoa pole kwa familia ya Masanja

Alikuwa na special presence kwenye football yetu na hakika ni mmoja wa wapenzi wa kweli wa soka. Inasikitisha pia namna alivyofariki... sipati picha ni bahati mbaya kiasi gani alikuwa nayo siku ya tukio

Natumaini wanasoka watavaa vitambaa vyeusi na kumpa dakika moja katika mechi zijazo

Kwaheri another fallen star!!!

Now back to Soka la Bongo... NAsubiri mapigo ya Papic kama atasimama kwa mnyama,

MTM
 
kama kawaida Mnyama anaongoza kwa goli moja lilofungwa dakika ya 24 na Hilary Echesa...
 
Mpira umekwisha simba imefanikiwa kuondoka na pointi zote tatu na goli moja lililofungwa dakika ya 24 kwa shuti ilililopigwa na Echesa nakumaliziwa na beki wa Azam kwa bahati mbaya, ilikuwa mechi ngumu sana. sasa tuna msubilia Yebo Yebo... Maji Maji 1 Africa Lyon 1...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom