Updates: Kesi ya Mpendazoe v/s Mahanga

[TR]
[TD="class: Headline, align: left"]Mpendazoe ashindwa kueleza idadi ya kura
Imeandikwa na Regina Kumba; Tarehe: 5th March 2012

[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="class: kaziBody, align: left"]



ALIYEKUWA mgombea ubunge wa Jimbo la Segerea mkoani Dar es Salaam, Fred Mpendazoe (Chadema), ameieleza Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kuwa yeye ndiye mshindi wa jimbo hilo ingawa alishindwa kujibu maswali ya mawakili wa wadaiwa yaliyomtaka kueleza ni kura ngapi alipata katika vituo.

Akiendelea kutoa ushahidi wake jana, Mpendazoe katika kesi aliyoifungua ya kupinga matokeo ya uchaguzi katika jimbo hilo, alidai maswali ya mawakili Jerome Msemwa na David Kakwaya yaliyohusu idadi ya kura katika vituo anavyodai alivitembelea siku ya uchaguzi, alisema kuwa
hakumbuki idadi yake.

Alipoulizwa kama ana nyaraka zozote zinazothibitisha ushindi huo anaodai aioneshe Mahakama ili kuunga mkono kauli zake, Mpendazoe alidai kuwa hakuja nazo na kwamba sio kazi yake kujua kwa sababu wapo watu ambao watakuja mahakamani hapo kutoa ushahidi huo wa idadi ya kura alizozipata.

“Inakuwaje unafungua kesi ya makini kama hii ya uchaguzi wakati hujui ni kura ngapi ulipata katika kila kituo unachokilalamikia huoni kuwa unapoteza muda wa Mahakama?” Alihoji
Wakili Msemwa.

Mpendazoe alidai kuwa hawezi kuwa na kumbukumbu ya hesabu zote hizo, lakini kwenye hati yake ya madai mahakamani, ameainisha idadi ya kura alizopata ingawa jumla anadai kuwa ni 56,962 kwa jimbo zima.

Anadai Kiwalani katika vituo 120, masanduku yaliyofika katika kituo cha kuhesabia kura cha Anatoglou bila mawakala kuwepo kwenye gari hiyo, jambo ambalo lilimtia hofu, na alipomuuliza mwakilishi wake kama majumuisho yalifanyika, alimjibu kuwa yalifanyika ya udiwani tu na siyo ya ubunge.

Aidha, alidai kuwa fomu nane za kujaza matokeo ya ubunge zilikosekana Vingunguti hata hivyo alikiri kuwa asingeweza kutembelea vituo vyote vya kupiga kura katika jimbo hilo ila alitembelea vituo tisa tu na vituo vingine alipata taarifa kutoka kwa mawakala wake.

Alipoulizwa na Wakili Msemwa ni wapi alipopata matokeo hayo ya kwamba yeye ndiye mshindi wa ubunge katika jimbo hilo, alidai ni mfumo waliokuwa wakiutumia kupata hesabu hiyo ambao ni mawakala wake kuchukua matokeo mara tu yanapobandikwa katika kila kituo cha kupigia kura.[/TD]
[/TR]
 


DAR ES SALAAM

MANISPAA YA ILALA
SEGEREA
Candidate

Political Party

Number of Votes

Percentage Votes
KIKWETE JAKAYA MRISHO

CCM
50,560
48.09
SLAA WILLIBROD PETER

CHADEMA
37,694
35.85
LIPUMBA IBRAHIM HARUNA

CUF
14,752
14.03
KUGA PETER MZIRAY

APPT - MAENDELEO
209
0.2
RUNGWE HASHIM SPUNDA

NCCR-MAGEUZI
116
0.11
MGAYWA MUTTAMWEGA BHATT

TLP
76
0.07
DOVUTWA YAHMI NASSORO DOVUTWA

UPDP
17
0.02
SPOILT VOTES
1,720
1.64
TOTALS
105,144
100

Ukilinganisha haya matokeo ya kura za Urais na yale ya Ubunge kwa Jimbo hili la Segerea utagundua kuwa kuna tatizo katika IDADI ya wapiga kura za Urais na Ubunge. Hapa ndipo penye matatizo makubwa. Kwamba jimbo hilo hilo moja kura za Ubunge zinakuwa nyingi au ndogo kuliko za Urais kwa chama kilekile,kwa mfano kwanini CCM hao hao wampigie Rais wao watu 50,560 lakini kwenye Mbunge wampigie kura 43,554???Haiwezekani mtu amkatae Rais wa Chama kilekile lakini ampe kura Mbunge wa chama kile kile au kinyume chake!!!Haingii akilini. Kama wewe umechagua Rais wa CCM kwanini hutaki mbunge wake? Rais atafanyaje kazi bila Wabunge?Au kwanini mtu amchague Rais kutoka CHADEMA halafu amkatae Mbunge wa CHADEMA????

Hapa NEC wanadanganya na hii inadhihirisha UCHAKACHUAJI wa KURA!!!
 


DAR ES SALAAM
MANISPAA YA ILALA
SEGEREA
Candidate
Political Party
Number of Votes
Percentage Votes
KIKWETE JAKAYA MRISHO
CCM
50,56048.09
SLAA WILLIBROD PETER
CHADEMA
37,69435.85
LIPUMBA IBRAHIM HARUNA
CUF
14,75214.03
KUGA PETER MZIRAY
APPT - MAENDELEO
2090.2
RUNGWE HASHIM SPUNDA
NCCR-MAGEUZI
1160.11
MGAYWA MUTTAMWEGA BHATT
TLP
760.07
DOVUTWA YAHMI NASSORO DOVUTWA
UPDP
170.02
SPOILT VOTES1,7201.64
TOTALS105,144100

Ukilinganisha haya matokeo ya kura za Urais na yale ya Ubunge kwa Jimbo hili la Segerea utagundua kuwa kuna tatizo katika IDADI ya wapiga kura za Urais na Ubunge. Hapa ndipo penye matatizo makubwa. Kwamba jimbo hilo hilo moja kura za Ubunge zinakuwa nyingi au ndogo kuliko za Urais kwa chama kilekile,kwa mfano kwanini CCM hao hao wampigie Rais wao watu 50,560 lakini kwenye Mbunge wampigie kura 43,554???Haiwezekani mtu amkatae Rais wa Chama kilekile lakini ampe kura Mbunge wa chama kile kile au kinyume chake!!!Haingii akilini. Kama wewe umechagua Rais wa CCM kwanini hutaki mbunge wake? Rais atafanyaje kazi bila Wabunge?Au kwanini mtu amchague Rais kutoka CHADEMA halafu amkatae Mbunge wa CHADEMA????

Hapa NEC wanadanganya na hii inadhihirisha UCHAKACHUAJI wa KURA!!!
Moja ya udhaifu mkubwa wa CHADEMA katika uchaguzi mkuu uliopita ni kuwa na mtandao mdogo na ubahili wa viongozi wa CHADEMA wakiongozwa na Dr Slaa alifanya ubahili hata wa kuchapisha posters zake mwenyewe na vitu vidogo kama skafu kwa ajili ya kampeni.
Nafahamu fika kwa kura halali Fred Mpendazoe ndio mshindi wa jimbo la Segerea, ila nikirudi kwenye point yako ya utofauti wa kura za Rais na za mbunge ni kwamba Udhaifu wa Chadema ulikuwa ni kumwachia mgombea ubunge na udiwani ndio wagharamie wenyewe mawakala wao na hakukuwa na timu ya Kitaifa kuratibu matokeo ya urais, na kinyume chake CCM ilituma maofisa Usalama wa Taifa kwa kila kata hasa Jijini Dar es salaam kuhakikisha kura za JK zinatosha, na ilikuwa ni kazi rahisi sana kuchakachuwa kura za urais kwa sababu Chadema wagombea walikuwa wako bize na matokeo yao ya ubunge na udiwani na watu hawakuwa makini na kuzichunga kura za urais.
 
Biashara yake imeisha huyo . Nafikiri anajuta maisha yake yote , aliwaamini wakina 6 na mwakyembe sasa wamemwachia manyoya .kweli nimeamini LIFE IS NOT A LUMP OF SUGAR.

wewe unaonyesha jinsi gani ulivotanguliza tumbo na maslahi binafsi mbele.,mpendazoe ni mpiganaji anayetaka kuuondoa utawala dhalimu madarakani alijaribu kuanzisha ccj watanguliza tumbo kama wewe wakamsaliti na akajitosa chadema wakachakachua lakini bado anapambana mahakamani, ni wa kuungwa mkono na wapenda mabadiliko lakini wachumia tumbo kama wewe watampuuza kwa kuona alikubali kuachia ubunge kwa ajili ya mageuzi, hongera kamanda mpendazoe songa mbele
 
nimekuwa mfuatiliaji mzuri wa kesi za kupinga matokeo ya uchaguzi. Kesi ya Lema inapata coverage nzuri hapa JF kunakuwa na updates kila baada ya nusu saa kutoka mahakamani Arusha. Lakini hii ya kamanda mpendazoe vipi! wana CDM mlioko Dar kwanini hamtuhabarishi. tunasikia kuwa makongoro kashikwa saburi kwenye kesi hii. Tunaitambua kazi nzuri inayofanywa na Peter Kibatala (wakili wa Mpendazoe) tujulisheni kama anavyofanya nanyaro Arusha
saburi au masaburi?
 


DAR ES SALAAM
MANISPAA YA ILALA
SEGEREA
Candidate
Political Party
Number of Votes
Percentage Votes
KIKWETE JAKAYA MRISHO
CCM
50,56048.09
SLAA WILLIBROD PETER
CHADEMA
37,69435.85
LIPUMBA IBRAHIM HARUNA
CUF
14,75214.03
KUGA PETER MZIRAY
APPT - MAENDELEO
2090.2
RUNGWE HASHIM SPUNDA
NCCR-MAGEUZI
1160.11
MGAYWA MUTTAMWEGA BHATT
TLP
760.07
DOVUTWA YAHMI NASSORO DOVUTWA
UPDP
170.02
SPOILT VOTES1,7201.64
TOTALS105,144100

Ukilinganisha haya matokeo ya kura za Urais na yale ya Ubunge kwa Jimbo hili la Segerea utagundua kuwa kuna tatizo katika IDADI ya wapiga kura za Urais na Ubunge. Hapa ndipo penye matatizo makubwa. Kwamba jimbo hilo hilo moja kura za Ubunge zinakuwa nyingi au ndogo kuliko za Urais kwa chama kilekile,kwa mfano kwanini CCM hao hao wampigie Rais wao watu 50,560 lakini kwenye Mbunge wampigie kura 43,554???Haiwezekani mtu amkatae Rais wa Chama kilekile lakini ampe kura Mbunge wa chama kile kile au kinyume chake!!!Haingii akilini. Kama wewe umechagua Rais wa CCM kwanini hutaki mbunge wake? Rais atafanyaje kazi bila Wabunge?Au kwanini mtu amchague Rais kutoka CHADEMA halafu amkatae Mbunge wa CHADEMA????

Hapa NEC wanadanganya na hii inadhihirisha UCHAKACHUAJI wa KURA!!!
Jimbo hilo hilo moja, waliopiga kura ya Rais ni 105,144 na waliowapigia wabunge ni 104,436. Tofauti ya kura 708! Inamaana kuna watu 708 waliokwenda vituoni na kuwapigia kura wagombea Urais pekee na hawakumpigia kura Mgombea Ubunge hata mmoja! This is NEC bana!
 
Mpendazoe kesi hii atashinda na uchaguzi ukirudiwa Makongoro ndio kwishney hata wakihonga pesa za wizi za Masaburi!!
 
naomba Mungu haki itendeke walau katika hili maana ni ukweli usiofichika kuwa jamaa waliover kuchakachua
 
Biashara yake imeisha huyo . Nafikiri anajuta maisha yake yote , aliwaamini wakina 6 na mwakyembe sasa wamemwachia manyoya .kweli nimeamini LIFE IS NOT A LUMP OF SUGAR.
Vipi yule mgonjwa wenu hajafatu huko ujerumani....
 
Mahanga 1(4).jpg

Mbunge wa Jimbo la Segerea, Makongoro Mahanga (CCM).

Shahidi wa pili Gervas Barandaje (29),
amedaikuwa kura za urais zaidi ya 10,000 za Kata ya Kiwalani, Jimbo la Segerea, hazikujumuishwa katika matokeo yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, 2010. Barandaje ambaye ni shahidi wa upande wa mlalamikaji, alikuwa mratibu wa mawakala wote wa Kata ya Kiwalani wa Chadema alitoa ushahidi huo katika kesi ya kupinga ushindi wa Mbunge wa Jimbo la Segerea, Makongoro Mahanga (CCM).

Alitoa ushahidi huo mbele ya Jaji, Profesa Ibrahimu Juma wakati akiongozwa na wakili wa mlalamikaji, Fred Mpendazoe (Chadema), Peter Kibatara, katika Mahakama Kuu Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam. Alidai kuwa akiwa katika ofisi ya Ofisa Mtendaji kwa ajili kufanya majumuisho kwa Kata ya Kiwalani, wasimamizi wasaidizi walianzisha vurugu za kudai posho kwa ofisa mtendaji wa kata hiyo.

Alidai wasimamizi waligoma kukabidhi fomu za matokeo ya wagombea wa urais, ubunge na udiwani wakidai kulipwa posho zao kwanza kama walivyokubaliana. Alidai baada ya mtendaji kukabidhiwa fomu hizo aliwafahamisha waratibu kwamba hawataweza kufanya majumuisho ya kura za udiwani kwa sababu fomu za matokeo ya vituo 23 hazipo. Shahidi alidai baada ya kumuhoji kupata ufafanuzi zaidi alidai fomu hizo ni za urais, ubunge na udiwani na hajui alipoziweka hivyo apewe muda wa kuzitafuta.

Alidai wapiga kura katika kila kituo idadi yao ilikuwa kati ya 450-500, na kwamba aliendelea kumsumbua ofisa mtendaji kila baada ya saa mbili akitaka kujua kama fomu zimepatikana, lakini siku ya pili yake aliwafahamisha kuwa zilipatikana fomu 16 na zingine hazijulikani zilipo.

Alidai kulikuwa na kundi kubwa la watu waliokuwa wakisubiri matokeo ya udiwani ambayo yalitakiwa kutangazwa katika kata na baadaye
aliingia mtu aliyekuwa kavaa tisheti yenye nembo ya tume akiwa kaongozana na askari polisi zaidi ya nane wenye silaha. Mtu huyo alipofika alitoa amri kwamba ametumwa na Mkurugenzi wa NEC kuondoka na msimamizi wa uchaguzi wa kata pamoja na vifaa vya uchaguzi.

“Tulihoji bila kuogopa polisi, ataondokaje naye wakati kuna fomu hazijaonekana kwa ajili ya kufanya majumuisho, alijibu ameagizwa hivyo kwa sababu saa 72 za kutangaza matokeo zimeshapita hivyo kila kitu kitafanyika Anartoglo,” alidai Barandaje na kuongeza kuwa askari polisi waliwapangua waratibu kutengeneza njia kisha msimamizi wa uchaguzi kata alifuata na kuondoka kuelekea alikohitajika pamoja na vifaa vya uchaguzi.

Alidai kuwa baada ya kuondoka msimamisi wananchi walihamaki wakihoji kwanini waliruhusu aondoke wakati kuna fomu za matokeo hazikupatika na kuwa hasira hizo ziliwafanya wachome ofisi ya Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kiwalani.
 
Mahanga 1(4).jpg

Mbunge wa Jimbo la Segerea, Makongoro Mahanga (CCM).

Shahidi wa pili Gervas Barandaje (29),
amedaikuwa kura za urais zaidi ya 10,000 za Kata ya Kiwalani, Jimbo la Segerea, hazikujumuishwa katika matokeo yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, 2010. Barandaje ambaye ni shahidi wa upande wa mlalamikaji, alikuwa mratibu wa mawakala wote wa Kata ya Kiwalani wa Chadema alitoa ushahidi huo katika kesi ya kupinga ushindi wa Mbunge wa Jimbo la Segerea, Makongoro Mahanga (CCM).

Alitoa ushahidi huo mbele ya Jaji, Profesa Ibrahimu Juma wakati akiongozwa na wakili wa mlalamikaji, Fred Mpendazoe (Chadema), Peter Kibatara, katika Mahakama Kuu Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam. Alidai kuwa akiwa katika ofisi ya Ofisa Mtendaji kwa ajili kufanya majumuisho kwa Kata ya Kiwalani, wasimamizi wasaidizi walianzisha vurugu za kudai posho kwa ofisa mtendaji wa kata hiyo.

Alidai wasimamizi waligoma kukabidhi fomu za matokeo ya wagombea wa urais, ubunge na udiwani wakidai kulipwa posho zao kwanza kama walivyokubaliana. Alidai baada ya mtendaji kukabidhiwa fomu hizo aliwafahamisha waratibu kwamba hawataweza kufanya majumuisho ya kura za udiwani kwa sababu fomu za matokeo ya vituo 23 hazipo. Shahidi alidai baada ya kumuhoji kupata ufafanuzi zaidi alidai fomu hizo ni za urais, ubunge na udiwani na hajui alipoziweka hivyo apewe muda wa kuzitafuta.

Alidai wapiga kura katika kila kituo idadi yao ilikuwa kati ya 450-500, na kwamba aliendelea kumsumbua ofisa mtendaji kila baada ya saa mbili akitaka kujua kama fomu zimepatikana, lakini siku ya pili yake aliwafahamisha kuwa zilipatikana fomu 16 na zingine hazijulikani zilipo.

Alidai kulikuwa na kundi kubwa la watu waliokuwa wakisubiri matokeo ya udiwani ambayo yalitakiwa kutangazwa katika kata na baadaye
aliingia mtu aliyekuwa kavaa tisheti yenye nembo ya tume akiwa kaongozana na askari polisi zaidi ya nane wenye silaha. Mtu huyo alipofika alitoa amri kwamba ametumwa na Mkurugenzi wa NEC kuondoka na msimamizi wa uchaguzi wa kata pamoja na vifaa vya uchaguzi.

Tulihoji bila kuogopa polisi, ataondokaje naye wakati kuna fomu hazijaonekana kwa ajili ya kufanya majumuisho, alijibu ameagizwa hivyo kwa sababu saa 72 za kutangaza matokeo zimeshapita hivyo kila kitu kitafanyika Anartoglo, alidai Barandaje na kuongeza kuwa askari polisi waliwapangua waratibu kutengeneza njia kisha msimamizi wa uchaguzi kata alifuata na kuondoka kuelekea alikohitajika pamoja na vifaa vya uchaguzi.

Alidai kuwa baada ya kuondoka msimamisi wananchi walihamaki wakihoji kwanini waliruhusu aondoke wakati kuna fomu za matokeo hazikupatika na kuwa hasira hizo ziliwafanya wachome ofisi ya Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kiwalani.
Na bado, mtasikia mengi! Hivi ndivyo watawala wetu walivyoshinda, hivi ndivyo polisi wetu wanavyotumiwa, hivi ndivyo tume 'huru' ya uchaguzi hufanya
 
Shahidi wa pili Gervas Barandaje (29), amedaikuwa kura za urais zaidi ya 10,000 za Kata ya Kiwalani, Jimbo la Segerea, hazikujumuishwa katika matokeo yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, 2010. Barandaje ambaye ni shahidi wa upande wa mlalamikaji, alikuwa mratibu wa mawakala wote wa Kata ya Kiwalani wa Chadema alitoa ushahidi huo katika kesi ya kupinga ushindi wa Mbunge wa Jimbo la Segerea, Makongoro Mahanga (CCM).

Hizi kura za nafasi ya Urais kutoka kata moja tu kura 10,000 zilienguliwa, je kwa nchi nzima haki ingetendeka nani angekuwa rais wa nchi leo hii? Wizi mtupu na laani ya wizi huo ndiyo matatizo yanayowaandama kila kukicha bila kuwa na suluhisho.
 
Hii kesi inafanya watu watembee uchi sasa, na bado yataibuliwa zaidi.
 
Mimi ndiyo maana najisemea kuwa, shida zote zinazowasumbua watanzania ni kutokana na kuongozwa na viongozi wasiowataka. Hawa viongozi akiwemo JK hawakutakiwa wawepo madarakani baada ya uchaguzi 2010, ila kwa kutoogopa, tamaa na kuvunja taratibu za kidemocrasia, basi ndiyo inatugharimu hadi leo. Natamani hii kesi iibue mengi zaidi na haki itendeke.
 
Tabia ya wizi wizi ni mbaya. But its never permanent! Hata paka mwizi wa kuku kuna siku hukamatwa tuu.
 
Mahanga 1(4).jpg

Mbunge wa Jimbo la Segerea, Makongoro Mahanga (CCM).

Shahidi wa pili Gervas Barandaje (29),
amedaikuwa kura za urais zaidi ya 10,000 za Kata ya Kiwalani, Jimbo la Segerea, hazikujumuishwa katika matokeo yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, 2010. Barandaje ambaye ni shahidi wa upande wa mlalamikaji, alikuwa mratibu wa mawakala wote wa Kata ya Kiwalani wa Chadema alitoa ushahidi huo katika kesi ya kupinga ushindi wa Mbunge wa Jimbo la Segerea, Makongoro Mahanga (CCM).

Alitoa ushahidi huo mbele ya Jaji, Profesa Ibrahimu Juma wakati akiongozwa na wakili wa mlalamikaji, Fred Mpendazoe (Chadema), Peter Kibatara, katika Mahakama Kuu Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam. Alidai kuwa akiwa katika ofisi ya Ofisa Mtendaji kwa ajili kufanya majumuisho kwa Kata ya Kiwalani, wasimamizi wasaidizi walianzisha vurugu za kudai posho kwa ofisa mtendaji wa kata hiyo.

Alidai wasimamizi waligoma kukabidhi fomu za matokeo ya wagombea wa urais, ubunge na udiwani wakidai kulipwa posho zao kwanza kama walivyokubaliana. Alidai baada ya mtendaji kukabidhiwa fomu hizo aliwafahamisha waratibu kwamba hawataweza kufanya majumuisho ya kura za udiwani kwa sababu fomu za matokeo ya vituo 23 hazipo. Shahidi alidai baada ya kumuhoji kupata ufafanuzi zaidi alidai fomu hizo ni za urais, ubunge na udiwani na hajui alipoziweka hivyo apewe muda wa kuzitafuta.

Alidai wapiga kura katika kila kituo idadi yao ilikuwa kati ya 450-500, na kwamba aliendelea kumsumbua ofisa mtendaji kila baada ya saa mbili akitaka kujua kama fomu zimepatikana, lakini siku ya pili yake aliwafahamisha kuwa zilipatikana fomu 16 na zingine hazijulikani zilipo.

Alidai kulikuwa na kundi kubwa la watu waliokuwa wakisubiri matokeo ya udiwani ambayo yalitakiwa kutangazwa katika kata na baadaye
aliingia mtu aliyekuwa kavaa tisheti yenye nembo ya tume akiwa kaongozana na askari polisi zaidi ya nane wenye silaha. Mtu huyo alipofika alitoa amri kwamba ametumwa na Mkurugenzi wa NEC kuondoka na msimamizi wa uchaguzi wa kata pamoja na vifaa vya uchaguzi.

“Tulihoji bila kuogopa polisi, ataondokaje naye wakati kuna fomu hazijaonekana kwa ajili ya kufanya majumuisho, alijibu ameagizwa hivyo kwa sababu saa 72 za kutangaza matokeo zimeshapita hivyo kila kitu kitafanyika Anartoglo,” alidai Barandaje na kuongeza kuwa askari polisi waliwapangua waratibu kutengeneza njia kisha msimamizi wa uchaguzi kata alifuata na kuondoka kuelekea alikohitajika pamoja na vifaa vya uchaguzi.

Alidai kuwa baada ya kuondoka msimamisi wananchi walihamaki wakihoji kwanini waliruhusu aondoke wakati kuna fomu za matokeo hazikupatika na kuwa hasira hizo ziliwafanya wachome ofisi ya Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kiwalani.

Ushaidi huu una tofauti sana na ule wa Arusha mjini,maana ushaidi unaotolewa Arusha mjini ni vichekesho tu!ila huu wa Ukonga naona unawaweka uchi tume ya uchaguzi na watawala (si viongozi) walioingia kwa hila!!hv hakuna sheria itakayoweza kuwahukumu hawa watu waliofanya mchezo huu mchafu hata kama ni 2020?
 
Lakini mwisho utaona ........maamuzi ya majaji wetu eti ushahidi wa wadai haujitoshelezi! Mahanga ataendelea kupeta!
Hivi unajisikiaje kuwaongoza watu ambao hawakukuchagua!?
 
Back
Top Bottom