Upande wa pili wa maswali kwa Dr. Ulimboka

PAMOKONUNDA

Member
Jul 3, 2012
66
10
Ivi kwa haraka haraka najiuliza dr ULimboka alipigiwa cmu na Abeid (as per dr Deo statement) wakutane stereo na wao Wanasema Kwamba huyo jamaa wanamjua walikuwa wakifanya nae mawasiliano juu ya mgogoro wao baada ya hapo wakachange venue to kibona. Regarding to the situation the following are the question to be answered;
(I) kwanini wakutane sehemu Kama izo na dr akiwa na mtu ambae sio kiongozi wa Madr?
(ii) kwani jumuiya ya madactari Hawana ofisi hadi wakutane bar?
(iii) kwanini Dr ULimboka alikuwa anachukua yeye binafsi jukumu la kuongea na upande wa pili bila kushilikisha viongozi wenzake wa jumuiya nini kilikuwa kinaendelea hapa au ndo zana nzima ya "You have to make me quite first so asto solve the problem"
 
mtoa maada unajaribu kkubrain wash watuu

Maswali kwako
  1. Hivi kwa mtaamo wako unafikiri tangu mgomo uanze serikali haijajaribu kuuzima kwa kuwaweka vizuri viongozi wa mgomo?
  2. Na kama ilijaribu vipi walifanikiwa au walishindwa?
  3. then hatua ya kumteka mtu na kumuua kujaribu kumzika akiwa hai etc maana yake nini kwa wewe mwenye uelewa thabiti?

Kwa uelewa wangu mfupi ni kuwa jamaa wamejaribu njia zote chafu na za kisheria baada ya kushindwa ndio assissination ikawa the only option and just because they are thinking is so small assuming that if u will eliminate the ring leader then watakuwa wamesolve sasa yamewatokea puani na walilohusika cha moto watakiona lazima wakione cha mtema kuni kuanzi na KUBWA LA MAJAMBAZI aka DHAIFU
 
Comrade Hapana shaka Serikali ipo nyuma ya hili tukio jiulize swali hili hivi ni mtekaji gani wa kawaida amteke mtu kisha amtoe kucha na meno mambo haya hufanywa na usalama wa taifa na polisi kumfanya mtu afichue siri hawawezi kukwepa hapa

Afichue siri gani? Si inajulikana kuwa jamaa ni kiongozi wa mgomo?
 
mtoa maada unajaribu kkubrain wash watuu

Maswali kwako
  1. Hivi kwa mtaamo wako unafikiri tangu mgomo uanze serikali haijajaribu kuuzima kwa kuwaweka vizuri viongozi wa mgomo?
  2. Na kama ilijaribu vipi walifanikiwa au walishindwa?
  3. then hatua ya kumteka mtu na kumuua kujaribu kumzika akiwa hai etc maana yake nini kwa wewe mwenye uelewa thabiti?

Kwa uelewa wangu mfupi ni kuwa jamaa wamejaribu njia zote chafu na za kisheria baada ya kushindwa ndio assissination ikawa the only option and just because they are thinking is so small assuming that if u will eliminate the ring leader then watakuwa wamesolve sasa yamewatokea puani na walilohusika cha moto watakiona lazima wakione cha mtema kuni kuanzi na KUBWA LA MAJAMBAZI aka DHAIFU

Mkuu umeuliza kabla ya kujibu. Kwa ni ishu kama hiyo ilipangwa kuzungumza baa? Je hao madaktari walikuwa wanajua wanaongea na mtu mwenye wadhifa gani katika serikali? Waliwahi kumuuliza yeye alikuwa amamuwakilisha nani? Kwa nini serikali umtume mjumbe mmoja tu kwa ishu muhimu kama hiyo?
 
Well,,nimehuzunishwa na yaliyomkuta lkn kweli tunatakiwa kujiuliza ilikuwaje jamaaa (Dr) kulichukulia tatizo kama lake binafsi? kama vile kukutana na mtu mida late haf mtaani tu? why nat ofcn na mida mwafaka?
 
Bado haueleweki mtoa hoga inaonekana haujelewa na wala hauna history kuhusiana ma mgomo wa madaktari.
 
Huna hoja na inaonyesha huna ufahamu wa kutosha juu ya hoja uliyoileta.
 
Well,,nimehuzunishwa na yaliyomkuta lkn kweli tunatakiwa kujiuliza ilikuwaje jamaaa (Dr) kulichukulia tatizo kama lake binafsi? kama vile kukutana na mtu mida late haf mtaani tu? why nat ofcn na mida mwafaka?

hilo hata mi nimejiuliza na kingine huyu jamaa alikua sio mtumishi wa serikali, je kwanini yeye ndio alipewa shuhuli ya kutetea maslahi ya madaktari waliojariwa na serikali? ina maana hakuna daktari anayefanya kazi serikalini ambae ana uwezo wa kutetea haki zao?
 
Well,,nimehuzunishwa na yaliyomkuta lkn kweli tunatakiwa kujiuliza ilikuwaje jamaaa (Dr) kulichukulia tatizo kama lake binafsi? kama vile kukutana na mtu mida late haf mtaani tu? why nat ofcn na mida mwafaka?

Kaka,issue ya Dr Uli ni very conflicting. Mimi nilianzisha Thread hapa niliyoiita Ukweli Mchungu na Dr katolewa kafara. Kule maswali yoote haya niliyauliza.

Kiufupi tuombe Dr.apone atasaidia sanakujibu haya maswali. Huyu Dr Deo naye pia anamsaada mkubwa kwenye uchunguzi huu.

Issue sensitive hizi mara wende Stereo mara Leaders. Ukisoma between the lines utaona kama hawa madaktari ndio walikuwa desparate zaidi. Kukutana na huyo jamaa. Nimesema hivi kwa kuzingatia attempts zilizofanywa na ma Dr wetu hawa kukutana na huyo jamaa bila kutumia common sense (mnisamehe nimekosa neno zuri zaidi) kwa sababu kuu muhimu.
1. Time of the meeting. Usiku!
2. Location of the meeting. Kilabuni
3. Audience.
Tunaamini kama madkatari zetu ni watu vipanga darasani, basi tusaidieni kudadavua hizi hoja za mshangao.
 
Kaka,issue ya Dr Uli ni very conflicting. Mimi nilianzisha Thread hapa niliyoiita Ukweli Mchungu na Dr katolewa kafara. Kule maswali yoote haya niliyauliza.

Kiufupi tuombe Dr.apone atasaidia sanakujibu haya maswali. Huyu Dr Deo naye pia anamsaada mkubwa kwenye uchunguzi huu.

Issue sensitive hizi mara wende Stereo mara Leaders. Ukisoma between the lines utaona kama hawa madaktari ndio walikuwa desparate zaidi. Kukutana na huyo jamaa. Nimesema hivi kwa kuzingatia attempts zilizofanywa na ma Dr wetu hawa kukutana na huyo jamaa bila kutumia common sense (mnisamehe nimekosa neno zuri zaidi) kwa sababu kuu muhimu.
1. Time of the meeting. Usiku!
2. Location of the meeting. Kilabuni
3. Audience.
Tunaamini kama madkatari zetu ni watu vipanga darasani, basi tusaidieni kudadavua hizi hoja za mshangao.

1. kilabuni kwasababu ni open space
2. usiku kwa sababu ndo muda waliokuwa free mchana walikuwa msibani
3. yule mtu walikuwa wanamjua alikuwa ndo kiungo cha wao na serikali na pia hata kwenye mgomo wa kwanza walishirikiana nae
 
Afichue siri gani? Si inajulikana kuwa jamaa ni kiongozi wa mgomo?

wakati anateswa alitakiwa kusema nani yupo nyuma ya mgomo?? yaana ametumwa na nani kuhamasisha mgomo??
Tafakari chukua hatua... swala hili halihitaji elimu ya darasani mkuu
 
Sasa hapo kwenye watu wengi namna hiyo mtu anaweza kuwa "kidnapped" bila mashahidi wengine kuwepo ambao walishuhudia tukio? Maana hapa stori ya kutekwa inasemwa na Ulimboka na kuwa substantiated na daktari mwenzake/wenzake pasi na kuwepo independent party aliyeona mchezo mzima.

Mimi narudia tena na tena ulimboka hakutekwa aliondoka na watu anaowafahamu vizuri akapanda nao kwenye gari sasa tuombe apone atuambie alikuwa na kina nani?
 
1. kilabuni kwasababu ni open space
2. usiku kwa sababu ndo muda waliokuwa free mchana walikuwa msibani
3. yule mtu walikuwa wanamjua alikuwa ndo kiungo cha wao na serikali na pia hata kwenye mgomo wa kwanza walishirikiana nae

Hao madaktari wachache walikuwa wabinafsi walitaka kutumia huo mgomo kwa maslahi yao wenyewe ndio maana hawawezi kuja mbele ya watu wakaelezea mambo yalivyokuwa na kilichotokea wanasubiri ulimboka apone wajipange nini cha kuongea ili stori zao zisipishane. Kwanini huyo Dr Deo haji mbele ya vyombo vya habari atuambie hasa nini kilitokea maana naona anakimbilia kwenda kusema kwa wanaharakati badala ya kwenda kwenye vyombo husika.
 
wakati anateswa alitakiwa kusema nani yupo nyuma ya mgomo?? yaana ametumwa na nani kuhamasisha mgomo??
Tafakari chukua hatua... swala hili halihitaji elimu ya darasani mkuu

kwani hujui NANI YUKO NYUMA YA MGOMO?
 
wakati anateswa alitakiwa kusema nani yupo nyuma ya mgomo?? yaana ametumwa na nani kuhamasisha mgomo??
Tafakari chukua hatua... swala hili halihitaji elimu ya darasani mkuu

Yote ilikuwa ku divert attention jamaa wana motive nyengine tofauti kabisa.
 
PAMOKONUNDA Naomba nikiri awali ya yote kwamba mimi si msemaji wa DR Ulimboka. Naamini maswali yako yameelekezwa kwa Dr Ulimboka ambaye kwasasa anapigania uhai wake baada ya ufedhuli aliofanyiwa ambao kwa MASWALI YAKO naona unajenga hoja kwamba ni kosa lake yalioyomkuta/yaliyompata. Nakupa majibu kwa uelewa nilionao kama ifuatavyo:

I) "kwanini wakutane sehemu Kama izo na dr akiwa na mtu ambae sio kiongozi wa Madr?"
JIBU: Ni kawaida ya watu kukutana sehemu zenye huduma mbalimbali kwa maongezi. Vikao kuanzia vya kazi hadi vya kijamii hufanyika na kuwakutanisha watu sehemu kama "izo". Sehemu za bustani kama ilivyokua zamani zilee pale clock tower, Opposite karimjee(garden),mnazimmoja n.k ambazo watu walikua wakikutana na kuongea kwasasa hazipo tena. Kuhusu kuandamana na daktari mwenzie ni hali ya kawaida sana. Wewe utakua tofauti na walio wengi kwa kutembea peke yako au na watu wa kada yako Mfano kama wewe kiongozi viongozi wenzio.

2. "kwani jumuiya ya madactari Hawana ofisi hadi wakutane bar?"
JIBU: Ni vyema ni nikakusaidia kukutafsiria maana ya Jumuia ya Madaktari. "JUMUIA WA MADAKTARI NI MKUSANYIKO AU JUMUIKO LA WATU WENYE KADA YA UDAKTARI KWA KIPINDI FULANI LIKIWA NA AJENDA YA PAMOJA" Mkusanyiko huu unaweza kutokea wakati wowote kikundi hiki kinapokutana na sio chama ambacho kinaongozwa na katiba.

Kwa maana hiyo siyo lazima Mkusanyiko wa namna hii kuwa na ofisi. Mahali popote hata chini ya mti panaweza kuwa mahala muafaka kwa kiongozi wa jumuia kukutana na watu mbalimbali. Ikumbukwe kiongozi wa jumuia kama hii ni kwa kipindi cha ajenda husika tu na sio kazi au jukumu la kudumu.

3. Kwanini Dr ULimboka alikuwa anachukua yeye binafsi jukumu la kuongea na upande wa pili bila kushilikisha viongozi wenzake wa jumuiya nini kilikuwa kinaendelea hapa au ndo zana nzima ya "You have to make me quite first so asto solve the problem"

JIBU:Kwasababu hakuna namna ya kuvua uongozi wakati unapokuwa kwenye shuguli binafsi, yaani unaendelea kuwa kiongozi hata pale unapokutana na marafiki na watu mbalimbali ni kosa kufikiria kwamba kwa kila atakayekutana naye ni lazima awe ameambatana na viongozi wengine au hatakufikiria ni lazima afanye maongezi au maamuzi kama kiongozo na sio Ulimboka the doctor. As for your last statement in English I belive it reflects your thoughts rather than the situation that had envolved Dr Ulimboka with very sad consequences.
 
Last edited by a moderator:
Well,,nimehuzunishwa na yaliyomkuta lkn kweli tunatakiwa kujiuliza ilikuwaje jamaaa (Dr) kulichukulia tatizo kama lake binafsi? kama vile kukutana na mtu mida late haf mtaani tu? why nat ofcn na mida mwafaka?

Yaani mwenyewe nakuna kuchwa kuhusu hilo nashindwa kuelewa. Hivi hawa ma Dr walimchukulia mtu huyo kama nani hasa? Kwa ni muwakilishi wa serikali awasiliane nao peke yake nao wakamuamini? Huyo mtu ana cheo gani serikalini mpaka akutane na hawa jamaa usiku, tena kilabuni?
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom