Ninaishi U.S.A. Mara nyingi napenda kuwasiliana kwa simu na jamaa zangu huko nyumbani Tanzania na marafiki wengine walioko Uganda. Kinachonishangaza ni hiki: Iwapo unaweka $ 2 kwenye simu na unampigia mtu wa Tanzania unatumia dakika 11 za Maongezi. Lakini ukiweka $ 2 na kumpigia simu mtu aliye Uganda unatumia dakika 30 za maongezi.
Sasa najiuliza hivi Tanzania tunakwenda wapi? Mbona kila kitu kinakuwa kigumu? Tutafika kweli? Ndio kusema maisha ya watanzania ni magumu mno zaidi ya mara mbili kuliko Uganda? Au hayo ndiyo malupulupu ya ufisadi? Tanzania inasikitisha! Jamani watanzania tumuombe Mungu ainusuru nchi yetu kutoka mikononi mwa vibaka!
Sasa najiuliza hivi Tanzania tunakwenda wapi? Mbona kila kitu kinakuwa kigumu? Tutafika kweli? Ndio kusema maisha ya watanzania ni magumu mno zaidi ya mara mbili kuliko Uganda? Au hayo ndiyo malupulupu ya ufisadi? Tanzania inasikitisha! Jamani watanzania tumuombe Mungu ainusuru nchi yetu kutoka mikononi mwa vibaka!