Uongozi Wa JF: Onyesheni Uzalendo Kipindi Hiki

Superman

JF-Expert Member
Mar 31, 2007
5,695
1,696
Maxence na Mods Wote Wa JF;

Kipindi hiki cha Uchaguzi ongezeko la wanaotembelea na kujiandikisha kuwa members JF bila ya shaka limekuwa kubwa. Hii inashabihiana na ukweli kuwa JF imekuwa mstari wa mbele na kuchangia kwa kiasi kikubwa kupiga vita maovu na hata kuchangia katika siasa za Tanzania.

Waliomsikia JK bila ya shaka wanafahamu kuwa Rais pia anapata taarifa ya nini kinaendelea katika mitandao. Ni wazi pia Dr. Slaa, Zitto na wanasiasa wengine wengi ni Wanachama wa JF ama wanatembelea JF kupata habari. Ni katika maantiki hii nashauri ni vema JF Uongozi na Mods wakaonyesha uzalendo wa hali ya juu kuliko wakati wowote kwa kuwa stricts kwa kuwa heavy weights wote wa vyama mbalimbali katika kipindi hiki cha Uchaguzi wanapitia posts nyingi. Tusipokuwa makini, JF inaweza kwa namna fulani fulani kuwa source ya mema au mabaya. (NB: Wote mnakumbuka Zeutamu ilivyoleta sokomoko). Sasa hivi JF ina wanachama 10,000 (+ or -).

Ushauri wangu ni kama ifuatavyo:

- Thread na Posts Zozote zisizo na muelekeo wa ukweli zaidi ya Ushabiki, na Uzandiki zisiruhusiwe ama zifutwe mara tu zikijulikana.

- Wale wanaobadili ID mara nyingi na kuendeleza pumba na ligi zisizo na msingi wala tija, wapewe "pumziko la amani".

- Wanaochichea debate za chuki za namna yoyote wapewe ban haraka sana na IP zao ziwe monitored.

- Wana JF washindane kwa hoja na facts bila kukebehiana na katika yote haya Uzalendo wa Nchi na Maslahi ya Taifa yapewe kipau mbele.

Katika hili, niko tayari kutoa mchango wangu wa ziada na Maxe, bila ya shaka nitakuona.

JF inayo nafasi katika siasa za Tanzania, ni wakati sasa iwe na msimamo na kutake advantage ya kuweka vipaumbele vyake.

Wasalaam

Superman!
 
Ni matumaini yangu kuwa tukiwa makini tunao uwezo wa kutoa muelekeo wa Siasa za Tanzania kuzingatia Uzalendo na Maslahi ya Taifa.
 
Wewe ndio unaonekana hufuati utaratibu kuna sehemu ya kupeleka vitu kama hivi ushauri na malalamiko. Afterall ukiangalia Sticky thread ya forum hii kuna thread imeanzishwa na Invisible na bado ipo sijui kama umetoa ushauri huko. Ni mawazo mazuri lakini jaribu na wewe kufuata utaratibu.
 
Wewe ndio unaonekana hufuati utaratibu kuna sehemu ya kupeleka vitu kama hivi ushauri na malalamiko. Afterall ukiangalia Sticky thread ya forum hii kuna thread imeanzishwa na Invisible na bado ipo sijui kama umetoa ushauri huko. Ni mawazo mazuri lakini jaribu na wewe kufuata utaratibu.

Kamanda nafahamu sana. Na bila ya shaka ninafanya mawasiliano zaidi ya kuandika hapa JF. Kusudio la post hii si malalamiko bali ni kwa wote: Members, Guests nk waweze kuona umuhimu wa namna gari bora cha kuendesha mijadala hasa ya uchaguzi katika kipindi hiki. Kwa jinsi mambo yanavyokwenda ni budi kukumbushana kwa hili kwa njia ya pekee.
 
Kamanda nafahamu sana. Na bila ya shaka ninafanya mawasiliano zaidi ya kuandika hapa JF. Kusudio la post hii si malalamiko bali ni kwa wote: Members, Guests nk waweze kuona umuhimu wa namna gari bora cha kuendesha mijadala hasa ya uchaguzi katika kipindi hiki. Kwa jinsi mambo yanavyokwenda ni budi kukumbushana kwa hili kwa njia ya pekee.
Sawa, elewa kwamba hata kama mtu ni guest kuna sheria lazima azisome kama hazisomi anafanya makosa atakutana na msumeno. Mbali ya sheria hizo Invisible amejaribu kuzifafanua zaidi na sisi tulichangia mawazo yetu huko. Kama kila mtu akiona mambo hayaendi vizuri anaanzisha thread nafikiri itakuwa vurugu. Mfano mimi nianzishe thread ya kumwaambia MODS watu wenye tabia kama hii (samahani) yakutofuata utaratibu wapewe ban, nafikiri itakuwa vurugu mechi.
 
Sawa, elewa kwamba hata kama mtu ni guest kuna sheria lazima azisome kama hazisomi anafanya makosa atakutana na msumeno. Mbali ya sheria hizo Invisible amejaribu kuzifafanua zaidi na sisi tulichangia mawazo yetu huko. Kama kila mtu akiona mambo hayaendi vizuri anaanzisha thread nafikiri itakuwa vurugu. Mfano mimi nianzishe thread ya kumwaambia MODS watu wenye tabia kama hii (samahani) yakutofuata utaratibu wapewe ban, nafikiri itakuwa vurugu mechi.

Sawa kamanda, tusianzishe ligi. Si kila mtu anasoma sheria za JF kwa uhakika. pamoja na ukongwe wangu toka 2007, zizifahamu zote kama vile Watanzania wasivyofahamu sheria zote.

Ukiichukulia post hii in a positive way, utaona mantiki yake.

It is your choice kuona kama kama "the glass is full empy or is half full"
 
nimeamini zito si mzalendo kama tuzaniavyo, arudi ccm watampokea angalau awe mwanachama tu bila madaraka ila kurudi chadema ni aibu upu, kuongea kwa wananchi aibu, sasa aende wapi. big up chadema mnaweza hata 2015 mkishika nchi mnaweza kutimua mafisadi wote. ccm wafuate nyayo zenu ili wafumue mafisadi na wanafiki wa chama na kuwafukuza.
 
Back
Top Bottom