Uongo wa gazeti la Tanzania Daima

yes.home of great thinkers.......chadema damu......
Tanzania daima+jamii forums /mwananchi = chadema/mtei/mbowe/slaa+wengineo vidagaa e.g mnyika/kafulila/halima mdee/zito kabwe etc:behindsofa:
sioni tofauti na hesabu za hapo juu za makamba/ccm
ccm nambari :A S-rap:
 
Hatari ni Nec walioiba kura zetu. Ni makamba, RA,EL na Riz1. Ujasoma Mwananchi ya Leo? Eti kichwa chake kikubwa imeandikwaje vile? Wewe umetumwa!
 
Uongo na uzushi wa Jambo Leo
Vichwa hivi vya habari vinaweza kuandikwa na gazeti la namna gani ?
(Slaa ana Wazimu)


Tarehe 20.01.2011 gazeti la Jambo Leo lilinadi habari yake muhimu kama ifuatavyo: 'Slaa ana wazimu: Adaiwa Sasa anebakiza Kuvua Nguo.'
Kwa heshima na taadhima zote, Dk. Wilbroad Slaa (dokta kwa kusoma na sio kupewa) ni kiongozi wa nchi sawasawa na Mheshimiwa Mrisho Jakaya Kikwete. Kumuandika kwa namna ambayo Jambo leo imemuandika kunazua maswali mengi na hususan, nani hasa ni waandishi na wahariri wa gazeti hilo na wamiliki wake ni kina nani na wana ajenda gani dhidi ya Slaa na CHADEMA.

Ingawa gazeti hilo lina waandishi na wahariri wachache wanaostahili kuitwa waandishi kutokana na rekodi zao za huko nyuma, kazi kubwa inafanywa na watu walisohdindwa maisha na kazi nyingine na kuokolewa na watu waliojikuta wanapata fedha kirahisi sana katika nchi hii kiujanja ujanja na kwa kuwa watwana na vijakazi wa ofisi moja kubwa nchini.

Wanaomiliki gazeti hilo ni watu ambao hawana hata elimu ya sekondari na walikuwa makanjanja kwenye vyombo vya habari wakati wa enzi ya mheshimiwa Mkapa.

Mmojawao ni mpiga picha ambaye amewahi kulifanyia kazi gazeti la majira bila kuwa na elimu na ujuzi wowote unaoendana na photographer katika dunia hii ya leo, ikiwemo ugwiji katika matumizi ya digital camera.

Yeye ni kama kaokolewa na mmiliki wa kwanza, kwa kumfanyia kazi zake mbalimbali za nyumbani, ikiwemo pia kumtafutia wanawake wazuri wa jijini Dar es salaam na kokote mwenzake huyo anakokwenda duniani isipokuwa tu Uingereza (tutaeleza baadaye kwanini haendi uk.)
Kuwadi huyo pia anasimamia biashara nyingine mbalimbali na ujenzi wa nyumba za Kifahari ufukweni mwa bahari ya Hindi katika maeneo mbalimbali hapa jijini ikiwemo Masaki na Kigamboni. Pamoja na kukodi magari ya kifahari kwa sherehe za harusi na kadhalika.
Tajiri mwenyewe wa jambo leo ni bwana mmoja mfupi, mnene (kibushuti) ambaye aliishia darasa la sita huko Morogoro mji kasoro bahari nchi hizo.

Bwana huyo amepigwa marufuku uingereza kutokana na kughushi vyeti mbalimbali, kutumia majina ya uongo, wizi katika supamaketi na ulaghai wa aina mbalimbali. Lakini bwana huyu ndiye aliyesaidia sana jamaa wa wakubwa wa nchi hii walipokuwa na matatizo huko Ulaya. Hvi leo aruhusiwi kutia mguu wake ulaya ingawa inadaiwa bado mke wake wa pili au wa tatu anaishi huko Uingereza.
Neema ilimwangukia pale rais alipotembelea Uingereza na kuagiza wasaidizi wake wampe kitita cha fedha na baadaye kontrakti mbalimbali ambazo hakustahili kuzipata kwa sababu hana elimu wala ujuzi wa kuvipata. Lakini amri ya wakubwa nchi hii na waoto zao ndio inayofanya kazi na sio vinginevyo.

Jamaa hawa ni watu wanaokula vizuri sana kwa kutumia uhusiano wao na ofisi kuu nchini-ambayo si zamani sana baba taifa alitahadharisha isije iakgeuzwa makao ya makahaba. Lakini kwa bahati mbaya wameingia humo aina mpya ya makahaba wa kisiasa na wahuni wa ukweli, haki na ufuataji sheria. Wakiongoza na mmojawapo wa wamiliki wa zamani wa magazeti ya Mtanzania na nduguze.
Kihistoria, watu hawa ni kombamwiko kwa maana watu wanaopenda kulamba wakubwa, wanapenda sana wanawake wadogo na wanaendesha hata mashindano ya urembo nchini na ni watu wanaotumia fedha kwa fujo na wanaoishi kifahari mno ukilinganisha na umasikini unaowazunguka.

Pamoja na kupewa tenda mbalimbali hapa nchini kaitka biashara mbalimbali, si watu wanaoweza kutengeneza chochote cha kudumu maana hawana uwezo wala akili ya kufanza kitu kama hicho.

Wote wanaowafanyia kazi wanawafanyia tu basi kwa kuwa hawajapata ajira nyingne iliyo bora. Lakini si watu kabisa wa kuwaamini kwa lolote lile. Wapo tu kwa ajili ya matumbo yao na jamaa zao na warembo wao wanaowabadilisha kama nguo kila siku. Au sawasawa na utitiri wa magari ya kifahari wanayoyamiliki bila tija yoyote ya maana duniani.

Utajiri walionao katu usingelikuja kama isingelikuwa koneksheni yao na Ikulu na wakazi wake wa leo. Utaona kifadhila, wana deni kubwa sana kwa ikulu na ndio maana wanaweza wakachukua uharo na matapishi toka ikulu na kuyabandika bila aibu wala haya kwenye magazeti yao na yale ya watwana na wajakazi wao yakiwemo Habari Leo, Mtanzania, Daily News na vijarida visivyona sura wala jina vya kusafisha uoza uliopo leo hapa nchini.

Msomaji ukisoma vichwa kama hicho cha Jambo Leo hapo juu, na ukabahatika kujua kwa ufupi historia ya wamiliki na waendeshaji wake inakuwa ni rahisi kujua hilo ni gazeti la namna gani, liko kwa ajili ya nani, linalipwa na nani hata kama linaendeshwa kihasara na vilevile kiwango chake cha ukweli na kuaminika ambacho ni chini ya sifuri kwa hivi sasa.
Huwezi kamwe kwa akili yangu ndogo, ukaisafisha nguo chafu kwa kuchafua nguo safi.

Sihitaji kumwambia Slaa na chama chake kwamba uandikaji wa kichwa kama hicho una dhamira na umekusudia kufanya yeye aonekane si mkweli na mwenda wazimu na hilo gazeti na hao linaowafanyia kazi eti ndio wenye akili timamu na wanaosema ukweli. Bado waandishi, wahariri na wamiliki wa gazeti hilo wanaishi katika enzi ambazo Watanzania walikuwa wajinga na wasioweza kupambanua kati ya nafaka safi na pumba, kati ya uongo na kweli, kati ya kilicho safi na bora na kilichooza na kimeshaanza kunuka kwa hivi sasa!!!!
 
Nadhani Kibanda ndiye anayeliharibu gazeti la Tanzania Daima kutokana na uswahiba wake na mafisadi wakuu RA na EL. Kama wamiliki wa gazeti hili wanataka kurejesha credibility ni lazima wamng'oe Kibanda ili akawatumike vizuri zaidi mabwana zake waliomnunulia na gari.
 
Barza la mawaziri linakuwa chaired na rais
hako ni kakikao tu cha kukumbushana majukumu

pi.jpg

waziri mkuu mizengo pinda jana amefanya mkutano na baraza la mawaziri la kazi linalojumuisha mawaziri na manaibu waziri ofisini kwake mtaa wa magogoni jijini dar es salaam juzi.
 
hizi zimeandikwa na magazeti yote ya leo kasoro TZ Daima.

Wadau: Katika tasnia ya habari, Je, hamuoni kama gazeti hili ni hatari kwa usalama wa nchi yetu?.

Una usalama gani wewe. Ni kawaida kwa serikali kukanusha vitu vya ukweli kwa visingizio mbali mbali. Ebu tuambie wewe baraza la mawaziri lilifanya kikao halikufanya?
 
Wewe hujui gazeti hatari ktk nchi yetu?..............ni mtanzania , al nuur, na vijarida vingine vya kiislamu vyenye kufagilia na kuchochea udini
jamani mi nadhani tuache kdhani kuwa kila jambo lianzishwalo na waislamu ni hatari,mi sioni msingi wake ama kwa kuwa ni la waislamu
tuache fikra zenye KUTU na mchanga Kichwani kwetu

mapinduziii daimaaaaaa:plane:
 
Wandugu, hapa tunategemewa kujibu au kuchangia kwa hoja.

Suala ni kwamba Sitta na Mwakyembe wamekanusha. Hii imetokea kwa sababu tumekubali tabia ya magazeti ya 'chanzo chetu cha habari'. Tabia hii imeota mizizi na sisi wasomaji tumeikubali nakuona sawa.

Sasa mtu akikanusha anajua kabisa hakuna jinsi gazeti litathibitisha habari hiyo. Huo ndio uhuru wa vyombo vya habari.

Habari muhimu zote zitatufikia kama 'umbea'. Hatuthubutu kusema zimetoka wapi! Huo ndio uandishi wetu.

Nitasema na nitasema kweli daima, hakuna gazeti ambalo haliandiki habari kwa kuangalia maslahi fulani. Aidha, kwa ajili ya kuuza, kutetea wizi fulani au kumfurahisha fulani. Huo ndio uandishi wetu wa siku hizi.

Kama Tanzania Daima wana uhakika na habari waliyotoa wathibitishe na tutawaamini zaidi. Kama watakaa kimya kama walivyofanya kwa Membe tutaanza
Kuamini kwamba wanapika habari na wao wenyewe ndio chanzo cha habari ili wauze.

Ni mara ngapi humu ndani zinawekwa post za aina fulani ili mradi tu watu wachangie kwa wingi? Ni msukumo huo huo upo kwa waandishi wetu. Saa nyingine wanaover do!
 
magazeti huandika kupata wanunuzi wengi...na si kutoa habari........RAIS MKAPA aliwahi kuwabeza hadharani........huandika vitu vya kufikirika na si uhalisia
SHAME ON PIPOZ PAWA NYUZPEPA
 
Wandugu, hapa tunategemewa kujibu au kuchangia kwa hoja.

Suala ni kwamba Sitta na Mwakyembe wamekanusha. Hii imetokea kwa sababu tumekubali tabia ya magazeti ya 'chanzo chetu cha habari'. Tabia hii imeota mizizi na sisi wasomaji tumeikubali nakuona sawa.

Sasa mtu akikanusha anajua kabisa hakuna jinsi gazeti litathibitisha habari hiyo. Huo ndio uhuru wa vyombo vya habari.

Habari muhimu zote zitatufikia kama 'umbea'. Hatuthubutu kusema zimetoka wapi! Huo ndio uandishi wetu.

Nitasema na nitasema kweli daima, hakuna gazeti ambalo haliandiki habari kwa kuangalia maslahi fulani. Aidha, kwa ajili ya kuuza, kutetea wizi fulani au kumfurahisha fulani. Huo ndio uandishi wetu wa siku hizi.

Kama Tanzania Daima wana uhakika na habari waliyotoa wathibitishe na tutawaamini zaidi. Kama watakaa kimya kama walivyofanya kwa Membe tutaanza
Kuamini kwamba wanapika habari na wao wenyewe ndio chanzo cha habari ili wauze.

Ni mara ngapi humu ndani zinawekwa post za aina fulani ili mradi tu watu wachangie kwa wingi? Ni msukumo huo huo upo kwa waandishi wetu. Saa nyingine wanaover do!


BABA UMENENA....nadiriki kusema post yako haitadumu
 
Nilitegemea watakanusha,sasa ukishafungwa mdomo unafikiri inakuwaje??? ukiufungua unakanusha tu.............lol
ni kweli ukishafungwa mdomo na Mkuu wako wa kazi uwezi dhubutu tena, na kwa kukazia wanakwambia kakanushe alfu tukone tenaTehteheee!!!!!
 
Jana kulikuwa na thread iliyokuwa na kichwa cha habari "Sitta na Mwakyembe wafungwa mdomo kuhusu Dowans" Source ya thread hiyo ilikuwa gazeti la "TZ Daima". Watu wengi tulipoteza MUDA mwingi kuchangia thread hiyo. Katika gazeti hilo kulinukuliwa habari zilizotoka katika kikao cha baraza la Mawaziri ambacho JK alikuwa ni mwenyekiti wake. Nukuu mbalimbali zilitolewa kama ushahidi wa kilichosemwa kikaoni.

Habari zilizothibitishwa na Sitta mwenyewe na Pia Katibu mkuu Ndg. Ph. Luhanjo zinasema HAPAKUWA NA KIKAO CHA MAWAZIRI WALA HAKUNA ALIYEWAZIBA MDOMO SITTA NA MWAKYEMBE. habari hizi zimeandikwa na magazeti yote ya leo kasoro TZ Daima.

Wadau: Katika tasnia ya habari, Je, hamuoni kama gazeti hili ni hatari kwa usalama wa nchi yetu?. Je, gazeti kama hili katika utawala unaojali sheria za vyombo vya habari halipaswi kufungiwa kwa muda? Je, si kweli kwamba waandishi wa gazeti hili ni MAKANJANJA?. naomba tuwe wazalendo katika kujadili hili. Tanzania ni yetu na ni sisi wenye damu mpya tunaoweza kuifikisha nchi tunapopataka kwa AMANI.


Kama ukiangalia vizuri sheria nyingi za nchi yetu zimekaa tofauti kabisa na za wenzetu walioendelea. Badala ya kupendekeza kuwafungia wenye gazeti, sheria zingewekwa zilenge kwenye kuwafilisi wale wanaoandika uongo kama wanavyofanya wenzetu walioendelea. Kufungia gazeti ni kuipa serikali dictatorial power na kuturudisha kule tulikotoka. Kukiwa kuna penalty ya $50,000 kama gazeti likithibitishwa kuwa limeandika uongo, nakuhakikishia kuwa kama mhariri atapitisha story yeyote isiyokuwa na vielelezo toka kwa mwandishi it will be only once, kwa sababu hiyo penalty atakayopewa mwenye gazeti itabidi amfukuze kazi mhariri wake na mwandishi wa hiyo story. Pamoja na penalty mind you, sheria pia inatakiwa iwe clear na itoe support kwa wale wanaoonewa kwenye habari na kesi ziamuliwe haraka. A good example, juzi juzi Waziri Membe alidai kusingiziwa na aka-sue lakini ujue kuwa hiyo kesi yake (kama anayo) itakaa mahakamani kwa muda mrefu na baadae itayeyuka. Sheria zetu zilenge kuwaadhibu watu pale ambapo ina-matter – in the pocket. Mtu anagonga na kuua binadamu wawili na gari isiyokuwa na insurance na anapigwa fine ya laki saba (measly $400). It would be laughable if it wasn't so sad. Hii nchi yetu haitafika popote kama hakuna mabadiliko ya serikali (wholesale change), kwa sababu hawa walioko sasa hivi, hata wale wasomi, wengi wao ulafi unawalazimisha kuyafumbia macho mambo mabaya ya wazi. Wengine wanashindwa kuwachukulia wabaya hatua kwa sababu ya complicity yao kwenye corruption. Wengi wamekaa kwenye uongozi kwa muda mrefu kiasi ambacho wanajua somehow at some point wakiwa njiani kufika hapo walipo, waliwahi kuhusika na maovu kwa hiyo wakianza kuwafunga watu na wao wanaweza kutajwa. Quite honestly, wale ambao wanataka kufanya mabadiliko genuine ni wachache kiasi kwamba hata wanapofanya mabadiliko wanayotaka yanamezwa na maovu ya wengine. Viongozi wanaoonekana kuwa wanawafanya wengine waonekane wabaya, wanaitwa kikao na wenzao walio wengi na wanaonywa na baada ya hapo wanaita news conference na kusema haya yalikuwa maoni yangu binafsi mambo yanaisha. Imetokea tu kwamba Sitta na Mwakyembe in this case ni watu wenye smarts na ndio maana hawajatoa hizo official CCM remarks ("mawazo yangu binafsi") lakini baada ya kukalishwa chini nilitegemea watakanusha. Look, njia pekee itakayowaondoa maskini wa TZ kwenye shida ni kuleta serikali mpya na hiyo itatokea kama katiba itabadilika kabla ya 2015. Wananchi tukazane kuwasambaratisha viongozi wezi na corrupt hadi katiba ibadilike.
 
magazeti hatari ni al huda na al nuru,sauti huru,tazama,mtanzania,rai,habari leo

Ongezea na Uhuru hapo. Hata sijui kina nani huwa wanalisoma ukiachilia mbali ofisi za serikali ambazo zimelazimishwa kulinunua.
 
Uongo na uzushi wa Jambo Leo
Vichwa hivi vya habari vinaweza kuandikwa na gazeti la namna gani ?
(Slaa ana Wazimu)

Tarehe 20.01.2011 gazeti la Jambo Leo lilinadi habari yake muhimu kama ifuatavyo: 'Slaa ana wazimu: Adaiwa Sasa anebakiza Kuvua Nguo.'
Kwa heshima na taadhima zote, Dk. Wilbroad Slaa (dokta kwa kusoma na sio kupewa) ni kiongozi wa nchi sawasawa na Mheshimiwa Mrisho Jakaya Kikwete. Kumuandika kwa namna ambayo Jambo leo imemuandika kunazua maswali mengi na hususan, nani hasa ni waandishi na wahariri wa gazeti hilo na wamiliki wake ni kina nani na wana ajenda gani dhidi ya Slaa na CHADEMA.

Ingawa gazeti hilo lina waandishi na wahariri wachache wanaostahili kuitwa waandishi kutokana na rekodi zao za huko nyuma, kazi kubwa inafanywa na watu walisohdindwa maisha na kazi nyingine na kuokolewa na watu waliojikuta wanapata fedha kirahisi sana katika nchi hii kiujanja ujanja na kwa kuwa watwana na vijakazi wa ofisi moja kubwa nchini.

Wanaomiliki gazeti hilo ni watu ambao hawana hata elimu ya sekondari na walikuwa makanjanja kwenye vyombo vya habari wakati wa enzi ya mheshimiwa Mkapa.

Mmojawao ni mpiga picha ambaye amewahi kulifanyia kazi gazeti la majira bila kuwa na elimu na ujuzi wowote unaoendana na photographer katika dunia hii ya leo, ikiwemo ugwiji katika matumizi ya digital camera.

Yeye ni kama kaokolewa na mmiliki wa kwanza, kwa kumfanyia kazi zake mbalimbali za nyumbani, ikiwemo pia kumtafutia wanawake wazuri wa jijini Dar es salaam na kokote mwenzake huyo anakokwenda duniani isipokuwa tu Uingereza (tutaeleza baadaye kwanini haendi uk.)
Kuwadi huyo pia anasimamia biashara nyingine mbalimbali na ujenzi wa nyumba za Kifahari ufukweni mwa bahari ya Hindi katika maeneo mbalimbali hapa jijini ikiwemo Masaki na Kigamboni. Pamoja na kukodi magari ya kifahari kwa sherehe za harusi na kadhalika.
Tajiri mwenyewe wa jambo leo ni bwana mmoja mfupi, mnene (kibushuti) ambaye aliishia darasa la sita huko Morogoro mji kasoro bahari nchi hizo.

Bwana huyo amepigwa marufuku uingereza kutokana na kughushi vyeti mbalimbali, kutumia majina ya uongo, wizi katika supamaketi na ulaghai wa aina mbalimbali. Lakini bwana huyu ndiye aliyesaidia sana jamaa wa wakubwa wa nchi hii walipokuwa na matatizo huko Ulaya. Hvi leo aruhusiwi kutia mguu wake ulaya ingawa inadaiwa bado mke wake wa pili au wa tatu anaishi huko Uingereza.
Neema ilimwangukia pale rais alipotembelea Uingereza na kuagiza wasaidizi wake wampe kitita cha fedha na baadaye kontrakti mbalimbali ambazo hakustahili kuzipata kwa sababu hana elimu wala ujuzi wa kuvipata. Lakini amri ya wakubwa nchi hii na waoto zao ndio inayofanya kazi na sio vinginevyo.

Jamaa hawa ni watu wanaokula vizuri sana kwa kutumia uhusiano wao na ofisi kuu nchini-ambayo si zamani sana baba taifa alitahadharisha isije iakgeuzwa makao ya makahaba. Lakini kwa bahati mbaya wameingia humo aina mpya ya makahaba wa kisiasa na wahuni wa ukweli, haki na ufuataji sheria. Wakiongoza na mmojawapo wa wamiliki wa zamani wa magazeti ya Mtanzania na nduguze.
Kihistoria, watu hawa ni kombamwiko kwa maana watu wanaopenda kulamba wakubwa, wanapenda sana wanawake wadogo na wanaendesha hata mashindano ya urembo nchini na ni watu wanaotumia fedha kwa fujo na wanaoishi kifahari mno ukilinganisha na umasikini unaowazunguka.

Pamoja na kupewa tenda mbalimbali hapa nchini kaitka biashara mbalimbali, si watu wanaoweza kutengeneza chochote cha kudumu maana hawana uwezo wala akili ya kufanza kitu kama hicho.

Wote wanaowafanyia kazi wanawafanyia tu basi kwa kuwa hawajapata ajira nyingne iliyo bora. Lakini si watu kabisa wa kuwaamini kwa lolote lile. Wapo tu kwa ajili ya matumbo yao na jamaa zao na warembo wao wanaowabadilisha kama nguo kila siku. Au sawasawa na utitiri wa magari ya kifahari wanayoyamiliki bila tija yoyote ya maana duniani.

Utajiri walionao katu usingelikuja kama isingelikuwa koneksheni yao na Ikulu na wakazi wake wa leo. Utaona kifadhila, wana deni kubwa sana kwa ikulu na ndio maana wanaweza wakachukua uharo na matapishi toka ikulu na kuyabandika bila aibu wala haya kwenye magazeti yao na yale ya watwana na wajakazi wao yakiwemo Habari Leo, Mtanzania, Daily News na vijarida visivyona sura wala jina vya kusafisha uoza uliopo leo hapa nchini.

Msomaji ukisoma vichwa kama hicho cha Jambo Leo hapo juu, na ukabahatika kujua kwa ufupi historia ya wamiliki na waendeshaji wake inakuwa ni rahisi kujua hilo ni gazeti la namna gani, liko kwa ajili ya nani, linalipwa na nani hata kama linaendeshwa kihasara na vilevile kiwango chake cha ukweli na kuaminika ambacho ni chini ya sifuri kwa hivi sasa.
Huwezi kamwe kwa akili yangu ndogo, ukaisafisha nguo chafu kwa kuchafua nguo safi.

Sihitaji kumwambia Slaa na chama chake kwamba uandikaji wa kichwa kama hicho una dhamira na umekusudia kufanya yeye aonekane si mkweli na mwenda wazimu na hilo gazeti na hao linaowafanyia kazi eti ndio wenye akili timamu na wanaosema ukweli. Bado waandishi, wahariri na wamiliki wa gazeti hilo wanaishi katika enzi ambazo Watanzania walikuwa wajinga na wasioweza kupambanua kati ya nafaka safi na pumba, kati ya uongo na kweli, kati ya kilicho safi na bora na kilichooza na kimeshaanza kunuka kwa hivi sasa!!!!

Sheikh,
Maelezo yako yananifanya kuamini jamaa unayemzungumza hapa ni JUMA PINTO.

Unajua unapotoa maelezo yote hayo ni vigumu kuifanya JF kutofahamu ni nani unamuongelea, bora ungetaja jina ili sije JF ikaonekana kama ni jamvi la UDAKU. Kwa njia hii watatokea watu watakao mtetea au kumkandamiza au hata yeye Juma Pinto kuja kukanusha thread yako.
 
Back
Top Bottom