Yaani saluni za wanawake zina vibweka, majungu, umbea, magigambo na uwongo wa kila namna.
Leo nikiwa saluni kujiweka safi, mara akaingia dada mmoja na mizigo yake, anaonekana ametoka shopping.
Kaja, hata bila kuulizwa kaanza kusimulia jinsi ndege za vita zilivyopita chinichini akiwa Karikoo. Eti rubani mmoja akamuona msichana wake, akaigandisha ndege hewani na wakaanza kupiga soga, baada ya muda kidogo akaipaisha tena.
Yaani saluni ndio makao makuu ya uwongo.
Naomba na nyie muongeze na nyie uwongo mliousikia huko.
Tangu lini umbea ukawa umejaa ukweli?
Siku zote umbea lazima uwe umeongezwa chumvi ama sukari, zaidi ya hapa yanakua maongezi na sio umbea.
Mhhhhh!!! mkuu we c wakiume? hahahahaaa....
raha ya saluni umbea babu we!
Ndo nini kutengenezana kimya kimya?
Hivi watu hua mnaenda saluni kupiga na kutafuta umbea au kujitengeneza?
Ukifika weka mziki wako uwe unatoa pale unapohitaji kutoa maagizo tu. . . maana hata kusikiliza na kwenda kuhadhithia kwingine ni umbea tosha.
Ukitaka ku-enjoy umbea wa salun, nenda zile za wadada walio-high class utacheka hadi uzimie.
Kila mmoja anataka kuonekana Beyonce, Oprah au michele Obama, yani huwa full burudani kama uko kwenye movie vile.
yaani saluni za wanawake zina vibweka, majungu, umbea, magigambo na uwongo wa kila namna.
Leo nikiwa saluni kujiweka safi, mara akaingia dada mmoja na mizigo yake, anaonekana ametoka shopping.
Kaja, hata bila kuulizwa kaanza kusimulia jinsi ndege za vita zilivyopita chinichini akiwa karikoo. Eti rubani mmoja akamuona msichana wake, akaigandisha ndege hewani na wakaanza kupiga soga, baada ya muda kidogo akaipaisha tena.
Yaani saluni ndio makao makuu ya uwongo.
Naomba na nyie muongeze na nyie uwongo mliousikia huko.
Utasikia wanasema "Ile range rover juzi nilimpelekea fundi aniweke subwoofer nyuma mwee hela aliyochaji ni ndogo sana maana nilitegemea anichaji laki 8 hivi"
Au mwingine ataongezea " Mwanangu hahahaaaa juzi kanichekesha, eti alimwona babu yake huko Uk akimpungia wakati ndege inajaribu kutua kwenye runway!"
Funga kazi ni hii, "Unajua msusi, sipendi nywele za uswazi nataka hii ya 70,000 unisuke sawa?"
Na zile nyumba mnazoendas kufanya massage nazo pia hazijambo kwa kuuza maneno.usiniambie ulikuwa Lisa Magic Hands?
Saluni(za kike na za kiume) umbea ndo mahala pake. Ukitaka kujua nani kaachika, nani muathïrika, yupi amefumaniwa juzi, nani anatembea na nani, vyote utavipata huko.
Watu huwa wanashambulia za kike peke yake, lakini hata za kiume nazo ni b'laa, hasa zile zenye vinyozi wakazi!