kazabutivutasox
Member
- Sep 13, 2011
- 8
- 0
Nimekuwa adicted to coffee,nina mwezi mmoja tangu nianze kunywa kahawa seriously sijaona tatizo lolote,je inaweza kuniletea madhara yoyote hapo baadae?
Nimekuwa adicted to coffee,nina mwezi mmoja tangu nianze kunywa kahawa seriously sijaona tatizo lolote,je inaweza kuniletea madhara yoyote hapo baadae?
kazabutivutasox title yako inasema unyaji wa kahawa.... hoja yako ni kahawa unayoinya baada ya kunywa kahawa au vipi?? sijawahi sikia mtu anakunya kahawa, bali hunya kinyesi
kama kweli unakunya kahawa, then lazima umuone daktari maana inawezekana una issue na digestion system aisee
Mimi nina tatizo jingine kuhusiana na kahawa! Wengi (tangu niko shule-boarding) ninawasikia wakisema......wakinywa (siyo WAKINYA) kahawa, huwapotezea usingizi, kwangu mimi hunitokea kinyume. Yaani nikinywa kahawa huwezi kuamini, huwa nalala fofofo!! Je, kuna sababu yoyote hapo? Au ambao hawapati usingizi ndiyo wenye matatizo??
Toa ushahidi wako Kuhusu sumu ya kahawa usiseme tu sumu wacheni kuinywa?Sumu tu hiyo kahawa wacheni kuinywa
Mimi nakunywa kahawa kwa zaidi ya miaka 30 sasa na ni heavy drinker (kwa standard yetu) nakuambia kwa standard yetu kwa kuwa nimetembea nchi za magharibi na huko siwafikii unywaji wao wa kahawa hata nusu.
Nimekuwa adicted to coffee,nina mwezi mmoja tangu nianze kunywa kahawa seriously sijaona tatizo lolote,je inaweza kuniletea madhara yoyote hapo baadae?
Ijulikane wazi kwanza kwamba kahawa ni dawa ya kulevya!
miaka michache tu iliyopita hii ya 2000 na kitu wakati nasoma kidato cha tatu katika somo la biolojia katika mada ya 'drug and drug abuse', mwalimu wangu wa biolojia alinifundisha kuwa kafeina (kitu kinachopatikana katika kahawa) ni madawa ya kulevya kundi la 'stimulants'. kahawa ni madawa ya kulevya. sijui kama wamebadili mtaala kwamba kidato cha tatu wa siku hizi hawafundishwi mada hii.
kahawa ina sifa nyingine ya kuwa ni kikojoshi (diuretic properties), yaani kahawa huulazimisha mwili kutengeneza mkojo, hilo siyo tatizo, tatizo ni kuwa yenyewe hufanya mara 2 zaidi, yaani kama umekunywa kikombe 1 cha kahawa, basi muda si mrefu utaenda kukojoa vikombe 2, kimoja ulichokunywa na kingine kimelazimishwa toka mwilini mwako!, kwahiyo kahawa hulazimisha matumizi yasiyo halali ya maji ya mwili, KUMBUKA MAJI NI UHAI.
Ili kujikinga na kansa nyingi, tunashauriwa kula na kunywa vinywaji vyenye alkalini zaidi na asidi kidogo ili kuufanya mwili ubaki katika 7.4 katika kipimo cha PH (pontential hydrogen), bali kahawa yenyewe ni asidi tupu hivyo unywaji wa kahawa wa mara nyingi hukuandalia daraja la kupata kansa fulani hapo baadaye.
kwa sababu kahawa ni dawa ya kulevya, basi hufanya kazi pia katika ubongo, inasemwa kuwa ni mojawapo ya visababishi vya ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu, kahawa si kinywaji ambacho watoto au wanafunzi wanashauriwa kukitumia.
unaona jinsi kahawa ilivyo nyeusi kama ilivyo cocacola, pepsi, azam cola, sayona cola twist?.
kahawa husababisha kansa ya kibofu cha mkojo, kushuka damu, mauzauza, shinikizo la damu na orodha inaendelea. kama unaona unaweza kunywa kikombe 1 tu, basi kunywa lakini ujuwe hayo ni madawa ya kulevya, watumiaji wa madawa ya kulevya wanasema ukianza 1 basi itafuatia 2, baadaye 3 na mwisho unakuwa TEJA. Tafadhari kunywa kistaarabu.
kafeina hupatikana katika kahawa, chai ya rangi, na katika soda nyingi za viwandani.
Utangulizi | maajabu ya maji
Nimekuwa adicted to coffee,nina mwezi mmoja tangu nianze kunywa kahawa seriously sijaona tatizo lolote,je inaweza kuniletea madhara yoyote hapo baadae?
HII NDIO FAIDA YA KUNYWA KAHAWA KWA AFYA YAKO...SOMA HAPA
Utafiti unaonyesha wanaume wanaokunywa kahawa kwa wingi wana nafasi nzuri ya kuepuka kensa ya tezi la kibofu cha mkojo Kahawa ni kinywaji kikubwa katika nchi za Afrika Mashariki kama Tanzania, Kenya...
Utafiti mpya uliofanywa kwa kushirikisha wanaume elfu 50 unasema kuwa watu wanaokunywa kahawa kwa wingi wana nafasi nzuri ya kuepukana na saratani au kensa ya tezi la kibofu cha mkojo.
Kwa muda wa zaidi ya miaka 20 kumekuwa na imani kuwa unywaji kahawa unasaidia katika kuepusha kensa hiyo, lakini katika tafiti huu mpya wanasayansi wanasema wamegundua tofauti kubwa katika kuepusha saratani kali.
Mwanasayansi Kathryn Wilson wa Idara ya afya ya umma ya chuo kikuu cha Havard nchini Marekani anasema "wanaume wanaokunywa vikombe sita au zaidi vya kahawa kwa siku wanapunguza uwezekano wa kupata kensa hiyo kwa asilimia 60 ukilinganisha na wanaume wasiokunywa kabisa kahawa."
Kahawa ina kemikali mbali mbali, ikiwa na viambatisho vinavyopambana na magonjwa na hiyo huenda ni pamoja na kemikali zinazozuia kensa ya tezi la kibofu cha mkojo.
Kensa hiyo ni ya pili kwa kuuwa wanaume duniani, ikiwa inasababisha vifo vya watu wapatao robo millioni kwa mwaka.
"wanaume wanaokunywa vikombe sita au zaidi vya kahawa kwa siku wanapunguza uwezekano wa kupata kensa hiyo kwa asilimia 60 ukilinganisha na wanaume wasiokunywa kabisa kahawa.
faida zake ni chache sana kuliko hasara. .
ushauri: TUACHE KUNYWA KAHAWA.