Unyonyaji - That forgotten term...

Kama kuna neno ambalo leo tunaliogopa kuligusa ni neno "unyonyaji". Kimsingi neno hili lilitokana na dhana ya jinsi kupe anavyoishi kwa kunyonya "host" wake kama ng'ombe, mbwa n.k Kwa maneno mengine mnyonyaji ni mtu ambaye anatumia kila mbinu kujitajirisha kwa kutumia "migongo" ya wengine.

Mwanzoni mwa jamhuri yetu wanyonyaji tuliwaimba na kuweka misemo kama "usiwe mnyonyaji kama kupe" tukiwahimiza watu wafanya kazi au wale kutokana na jasho lao. Tukasema kuwa watu pekee ambao wanastahili kuishi kwa jasho la watu wengine ni watoto, wagonjwa, na wazee ambao wameshachumia juani. Tukawakatalia watu wengine wote ambao wanataka kuishi "kwa njia za mkato".

Hata hivyo baada ya mabadiliko ya kiuchumi yaliyotokea tabaka la wanyonyaji limeanza kujitokeza kwa kiasi kikubwa ambapo kuna watu ambao pasipo kufanya kazi (biashara au kuchakarika kihalali) wanatumia nafasi zao na vyeo vyao kutengeneza fedha ya haraka haraka.

Ni hapo ndipo tumeanza kuona kundi la watu tuwaitao "mafisadi". Wakati neno fisadi linatumika kuelezea kila aina ya uovu katika utumishi wa umma (rushwa, wizi, ubadhirifu, matumizi mabaya ya cheo, ofisi au jina n.k) neno "mnyonyaji" lilikuwa linatumika kuelezea mtu ambaye kimsingi anavuna asichopanda na anameza asichotafuna.

Mnyonyaji ni mtu ambaye hana wasiwasi wa maisha yake kwa sababu ametegesha mirija yake kwenye mabenki, ofisi, n.k ambapo hata akiwa katika ziara ya Rais au akikaa kwenye kiti chake cha ngozi nyeusi mirija hiyo inaendelea kufyonza kama ina kichaa. Mnyonyaji haitaji kufanya kazi yoyote isipokuwa kuweka mrija huo mdomoni na kama mtu anayefyonza ulanzi au mzee aliyekalia kibuyu cha chimpumu au yule anayepulizia mbege basi anajinoma taratibu huku mashavu yake yakitanuka kama chura apigaye mluzi!

Tunachoona sasa hivi ni kuwa wanyonyaji ambao tuliwakatia mirija mwaka 1967 ili angalau na wengine tuweze kunenepa ndio wamerudi kwa ari na nguvu mpya na sasa hivi wananyonya huku wameinua miguu juu kwani wanajua hawanyonyi peke yao. Wakati umefika wa kuchora katuni ya "wanyonyaji mambo leo" ambao wamemzunguka Mtanzania na mirija yao mdomo wakimfyonza kama vile mbu anavyonya damu kama anatumia drill ya kufyonza mafuta!

Wanyonyaji hawa weusi, leo wanasimama wakijua kuwa wanalindwa na hakuna mwenye ujasiri wa kuifyeka mirija yao na kuwakatisha uhondo wao huo. Cha kuudhi ni kuwa sisi Watanzania ndio tumekaa pembeni na kupiga kelele lakini ni kelele za kushangaa siyo kukasirika na kutaka kuikata mirija hiyo. Ndio maana hadi leo hii tunaendelea kuwalipa dowans, Mkapa ameendelea kushika mrija wa Kiwira, na wengine wameshikilia mirija yao huku baadhi yao wakishikilia mirija kwenye kila kidole huku wakicheka cheka na kucheua mafuta yanukayo!

Kinachoendelea si ubepari jinsi unavyoeleweka Magharibi ambapo unajitahidi kuonesha angalau huruma kwa wanyonywaji; wa kwetu ni unyonyaji unaojifanya ni ubepari! Ni nani atakayethubutu kukata mirija hii na kuwakatisha wanyonyaji hawa uhondo wao! Ni nani ambaye yeye mwenyewe si mnyonyaji atakayeona uchungu wa kile kinachoendelea?

Je, mfanyabiashara na mwekezaji anaweza kufanya biashara yake vizuri na akapata faida bila kuwa mnyonyaji wa kutupwa. Je tunaweza kuwaacha watunyonye ilimradi wanatulisha na tunanenepa kidogo kuliko wakitunyonya tukiwa kimbaumbau!? Tufanye nini ili tuwanyang'anye mirija hiyo au tufanye nini ili tuweke machujio kwenye mirija hiyo ili wanapofyonza basi wasivyonze vyote!?

Au tukubali tu kuwa wanyonyaji wana haki ya kutunyonya kwa sababu tumeweka wenyewe migongo yetu wazi ili watunyonye huku tumeipakaa mafuta ili kuitamanisha? Je tuwaache watunyonye kwa sababu wanaweza na jaribio lolote la kutishia kukata mirija hiyo litakutana na upinzani kuwa tunataka kurudia "utaifishaji" na tunataka kutishia wawekezaji?

M'kijiji,

Vitu hivi tusivisahau...

- Kabla ya Azimio la Arusha kulikuwa na baadhi ya watu na tabaka fulani za watu zilizokuwa zimefaidika tokea enzi za ukoloni na kujijengea economic base nzuri ya kujenga utajiri. Utajiri wao uliongezeka kwa kasi na gap kati ya maskini na matajiri ikawa kubwa sana.

- Come 1967, Nyerere and TANU had no option but to Nationalize utajiri huu kuondoa hatari ya tabaka lisilo na mali ambalo lilikuwa majority kulipiga tabaka la matajiri ambalo lilikuwa minority. Though Azimio lile liliumiza matajiri but in another way liliwaokoa na kilichokuwa kinakuja mbele.

- 1977 Sokoine akachukua uPM. Operation ya Azimio la Arusha iliingiliwa na vita. Vita viliathiri uchumi na ile system iliyokuwa imeanza kujengeka ikabomoka. Likazuka tena tabaka la WABADHIRIFU wakishirikiana na WAHUJUMU wa uchumi. Sokoine akaanza kamata kamata tena na kutaifisha mali zao. Haikusaidia tukazidi kudidimia na hayo mashirika, WABADHIRIFU wakawa wengi.

- 1984 Sokoine akafariki. Nyerere akatambua wazi kwamba hana kingine cha kutaifisha na mpira ulikuwa kwake, amlaumu nani? Cha kufanya...akaamua amwage manyanga 1985.

- Mwinyi alichofanya na kuachia tena watu wajenge vitakavyokuja kutaifishwa baadaye? Au aliamini tuko level moja na tunaweza wote compete sawa? Pamoja na kuonekana kuwa mzee wa ruksa. Mabadiliko mengi yalifanyika enzi zake.

- Mkapa alikamata kijiti wakati watu waliheshimu biashara kuliko kufanya kazi serikalini. Mkapa akajenga tena lile tabaka la civil servants ambao hutumia ofisi zao kama biashara zao. Hawa ndio waliokufuru katika kujilimbikizia mali.

Hawa ni wanyonyaji kwani:-

(1) RADAR - Wametubebesha mzigo mkubwa katika bei kuliko ilivyokuwa.
(2) IPTL - Wametubebesha mzigo mkubwa katika bei ya umeme.
(3) EPA - Tumeamini deni letu la nje limepungua kumbe hela wamechukua wao.
(4) TANGOLD/MEREMETA - Kiini macho cha kuchukua hela zaidi.
(5) Import Support - Wamegawana wao na kutengeneza makampuni yao.

The list goes on...

Sasa swali? Tutaifishe kila kitu tena? Au tutumie selective Nationalization?

NB: Usisahau na Ukabaila ;-)
 
Insurgent.. hivi mara ya mwisho CCM kusema wanapinga "Unyonyaji" ilikuwa lini... point zako ni nzito mno..!
 
unataka EXACTLY QUOTE na neno unyonyaji ndani au statement yoyote inayoashiria kupinga unyonyaji ?

Najua utakuwa unataka exactly quote vile unavyotaka wewe(neno unyonyaji likiwemo ndani), bahati mbaya haipo lakini walishawahi na wanasema almost kila mwezi kuashiria !! good luck !
 
Tatizo watanzania ni wapokeaji wa kila kitu, kiwen kibaya au kizuri, kikiwa kibaya tutakizungumzia kijiweni halafu aliyekifanya akipita na Vogue tunamsifia. hao ndiyo wa TZ bwana.Ila sasa naona wameanza kuamka ,watu sasa hawaogpi kutoa maoni ya mbele ya kadamnasi nadhani tusikate tamaa tunaelekea kuzuri na viongozi wetu walitambue hilo. iko siku kiongozi akichemsha atachapwa viboko na aliyemchapa asifanywe kitu.
 
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu Unyonyaji sasa hivi ni RUKSA!.. kwa tafisri fupi Unyonyaji lazima uwe na mirija ya kufyonzea uchumi wa nchi kama vile kunguni ama imani ya Mumiani (vimpare) wanavyonyoinya damu za watu pale unapoamua kufumba macho..
Kulingana na mfumo mzima wa Ubepari mirija ni lazima iwepo na process nzima haitegemei pakacha kujazwa isipokuwa kuwepo kwa njia mbili za kuingiza na kutoa..Hivyo balance ya malipo yake inategemea zaidi bomba kubwa linalojaza.
Mkuu, kama hutaki kunyonywa basi usilale wala kutembea kizani maanake vitanda vyote vimejaa kunguni hata Benki zetu zinaendeshwa kwa na damu yako, isikuzuie kulala hata kidogo utakuja zoea.

Ufisadi on the other hand ni Uharibifu kama vile nguchiro na nzige wanavyoweza haribu mazao, hawa wanafuata the base ya uzalishaji na kuharibu taratibu zote za kupata mazao bora ama kuharibu pato la mavuno. Hawa pia inaonyesha wanaanza kuhalalishwa kwa sababu huyo nguchiro ni pet wetu wenyewe ndani ya nyumba...
 
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu Unyonyaji sasa hivi ni RUKSA!.. kwa tafisri fupi Unyonyaji lazima uwe na mirija ya kufyonzea uchumi wa nchi kama vile kunguni ama imani ya Mumiani (vimpare) wanavyonyoinya damu za watu pale unapoamua kufumba macho..
Kulingana na mfumo mzima wa Ubepari mirija ni lazima iwepo na process nzima haitegemei pakacha kujazwa isipokuwa kuwepo kwa njia mbili za kuingiza na kutoa..Hivyo balance ya malipo yake inategemea zaidi bomba kubwa linalojaza.
Mkuu, kama hutaki kunyonywa basi usilale wala kutembea kizani maanake vitanda vyote vimejaa kunguni hata Benki zetu zinaendeshwa kwa na damu yako, isikuzuie kulala hata kidogo utakuja zoea.

Ufisadi on the other hand ni Uharibifu kama vile nguchiro na nzige wanavyoweza haribu mazao, hawa wanafuata the base ya uzalishaji na kuharibu taratibu zote za kupata mazao bora ama kuharibu pato la mavuno. Hawa pia inaonyesha wanaanza kuhalalishwa kwa sababu huyo nguchiro ni pet wetu wenyewe ndani ya nyumba...

Kwa maelezo yako kuhusu unyonyaji, ujamaa nao unaangukia katika kundi katika kundi la unyonyaji. Matumizi katika Ujamaa ni mirija tosha ya kunyonya uchumi.
 
Bin Maryam,

Mkuu hakuna anayesema itikadi haiwezi kutokuwa na matokeo tofauti ya mfumo mzima...Of cause hata ktk mfumo wowote ule kuna tobo ambazo zinaweza kuharibu ufanisi, nikiwa na maana Ujamaa ulikuwa kama fence around shamba letu lakini tatizo likawa hakuna mwananchi anayeweza kuingia shambani bila yule mwenye funguo. Na waliokabidhiwa funguo walipolala, kazi yote ilisimama na bahati mbaya fence hilo halikuweza kuzuia manyani..
Kwa hiyo hata China na Urusi under communism walikuwepo mirija wenye funguo na hawa ndio waliharibu zaidi mfumo mzima wa Kiuchumi kwa sababu walishika madaraka na funguo zote lakini uwezo wao kama wakulima ulikuwa zero..
Hivyo basi hata Kenya na Zambia waliokuwa mabepari walishindwa kwenda mbele kwa sababu sisi sote ni njaa na tulitawaliwa then na bado tunatawaliwa... viongozi wote waliokabidhiwa madaraka wanachokitaka ni kuwa wakoloni weusi... period tofauti na Mwalimu aliyetaka kuongoza. Matokeo mengine ni baada ya sisi wenyewe kutofahamu kujitawala...
Kumbuka tu hizi itikadi zote zinahitaji ufuatiliaji kama vile tunaposema Mkapa na UWAZI... ama neno good governance haiwezi kuwepo ktk maandishi tu ila inatakiwa kuwa mwongozo ambao watu wote mnatakiwa kuufuata.
Ujamaa ulikataza Unyonyaji lakini ndani yake kulitokea tatizo la bomba kuu la ujazo!..
Yaani kimsingi ukifunga mirija wakati maji yanazidi kujaa ndani ya gudulia na wananchi hawapati kuchota isipokuwa kwa utaratibu wa msitari, basi kuna uwezekano mkubwa wa msitari huo kuvunjika hasa subira inapokuwa haiwezi kuvumilika tena..
Nyerere pamoja na makosa yake Ujamaa ulikuwa na mazuri yake kinadharia isipokuwa njaa yetu ndio ilitushinda kuvumilia.
Mkuu pamoja na record high ya mafuta leo hii lakini bado tunashindwa kuelewa kwamba mbei ya mafuta ya mwaka 1982 ilikuwa na impact kubwa zaidi ya hii leo kwani shilingi 100 ya mwaka huo haiwezi kuwa sawa na hii ya leo.
Pipa moja la mafuta wakati ule liliweza kununua magunia 100 ya mazao ya mkulima tofauti na leo hii ambapo litanunua gunia 10 kisha kulingana na hali ya uchumi huu mazao pia yanapanda bei kupunguza gharama ya mkulima tofauti na wakati ule.
Mkuu, msifanye mchezo enzi za vita baridi, adui wa Ubepari alikuwa ni sawa na Terrorist na alipighwa vita kushoto kulia..
 
Mwanakijiji,

Unyonyaji si Ubepari. Ila Watanzania tulioanisha Ubepari (umiliki wa mali nyingi/utajiri) na Unyonyaji (kujipatia mali kwa ziada kwa migongo ya watu, bila malipo bora) kutokana na msukumo uliokuja wa kuleta mfumo sawa wa uzalishaji mali hasa baada ya Azimio la Arusha.

Tulimwita Mkoloni na nchi za Kibepari, Wanyonyaji kwa kuwa walitumia mbinu za kujipatia ziada kutokana na jasho letu na kutupa ujira haba au batili ambao hauendani na gharama zetu za uzalishaji mali.

Nina uhakika hata kama mfumo wa Kibepari ambao huelemea kwa mwenye pesa kuwa na uamuzi wa mwisho na si mwenye mali ungekuwa na nia njema ya kuleta usawa na malipo yenye uwiano na uzalishaji mali, bado tungeshindwa kuona ubora wa ubepari.

Ubepari (capitalism) si Unyonyaji (exploitation). Ila katika ubepari kuna vigezo vingi ambavyo huonekana na hufanyika kwa njia ya unyonyaji na ndio maana hasira za Mtanzania dhidi ya mfumo wa ubepari zilihitimisha Mtanzania kuuona mfumo wa Ubepari kama mfumo wa Unyonyaji.

Nakubaliana na Bin Maryam na Mkandara kuwa hata mfumo tuliochukua wa Ujamaa na Kujitegemea, uliingia maksoa kutokana na mianya ya kinyonyaji iliyotokea. Mfano mkubwa ni Tabaka la viongozi kuendelea kurutubika na kunyonya kwa kutumia madaraka yao na si kurutubika kwa matunda ya kazi na jasho lao.

Yanayotokea sasa hivi si uharamia, uhujumu na ufisadi pekee, bali ni mfumo mpya wa Unyonyaji katika jamii yetu ambapo njia fupi zilizojaa harufu za rushwa zinatumika kuhalalisha Uhujumu na ufujaji mali ya umma.

Kufuja mali, kulalia watu, uhujumu, kudhulumu watu vyote hivi ndivyo vigezo vya Unyonyaji na si mifumo ya Ubepari au Ujamaa.
 
Rev. Kishoka,
Sina la kuongeza mkuu umemaliza darasa!duh ukiamua wewe mchafu sana ktk maswala haya..
 
Rev. Kishoka,
Sina la kuongeza mkuu umemaliza darasa!duh ukiamua wewe mchafu sana ktk maswala haya..
Mkuu Bob,

Watanzania tulikimbilia kuimba wimbo wa kupiga vita Unyonyaji na hivyo kuua kabisa matumaini ya kuwepo mfumo wa Kibepari maana tuliambiwa ubepari ni Unyama.

Yes ubepari una unyama, na hata Ujamaa, lakini hukumu ya kuwa Ubepari ni Unyonyaji ilikuwa ni upotofu.

Hawa kina Chenge na Mafisadi wao si Mabepari! Wao ni Wahujumu Wanyonyaji, Mijizi!
 
Mkuu Bob,

Watanzania tulikimbilia kuimba wimbo wa kupiga vita Unyonyaji na hivyo kuua kabisa matumaini ya kuwepo mfumo wa Kibepari maana tuliambiwa ubepari ni Unyama.

Yes ubepari una unyama, na hata Ujamaa, lakini hukumu ya kuwa Ubepari ni Unyonyaji ilikuwa ni upotofu.

Hawa kina Chenge na Mafisadi wao si Mabepari! Wao ni Wahujumu Wanyonyaji, Mijizi!

Nimeipenda hiyo ya "mijizi"....there you kinda sound like me....kwikwikwiii
 
Back
Top Bottom