Alfred Daud Pigangoma
JF-Expert Member
- Mar 30, 2009
- 1,826
- 966
Chadema inaonekana kuwa makini sana pale bungeni na hata kwenye mahojiano na vyombo vya habari na wamekuwa hawasikii ,wakiambiwa wakielekezwa wanakuwa na misimamo isiyoambilika.Wanajiona wao ni wao hizi ni kasumba za Mwalimu Nyerere kiasi kufika kuitwa baba haambiliki ,jina ambalo alilichukia sana.
Safu hii ya Chadema iwapo watafanikiwa kuongoza dola hii,(Inshaallah wafanikiwe) tumeichoka CCM,kuna uwezekano kuiendesha au kuiongoza Tanzania kama itakuwepo kwa kutumia utawala wa kidikteta ni kushinda CCM ,bila ya shaka kutaiweka nchi katika woga na uhuru wa mwananchi utakuwa finyu.
Sioni busara yeyote ile wanayoitumia pale bungeni ,sioni hekima yeyote ile wanayoitumia katika lugha dhidi ya vyombo vya dola ,hivi wanataka kutuambia watakapo ingia katika duru ya kuiongoza Tz watavunja vyombo hivi wanavyovidharau na kuona haviwatendei haki.
Unyanyapaa huu wa kuvikomalia vyombo vya dola na kuvibeza ni jambo linalotia hofu sana.
Unayejiita MWIBA! Salam ama baada ya salam sisi huku hatujambo hofu na mashaka ni kwako wewe uliye mbali na upeo wa mach yetu.
Nimepitia comment za watu wengi ambao unataka wa comment kama unavyotaka na baada ya wewe pia kuzipitia comment hizo umediliki kusema kuwa "KAMA UNGEKUWA MOD UNGEWAKATA VIDOLE NA KUWATOBOA MACHO" wachangiaji wote.
MY TAKE: Wewe ni mmojawapo wa waliomteka Dr. Ulimboka na kumfanyia kama unavyotuthibitishia humu JF. Na ole wako tusikie katekwa mwingine tunaanza na wewe.