Jeni
JF-Expert Member
- Apr 23, 2008
- 200
- 12
Unyama wodini!
2008-10-23 19:35:11
Na Emmanuel Lengwa, Mwananyamala.
Hassan Salum, mume wa mwanamke aliyeripotiwa juzi kupoteza maisha kutokana na kuchelewa kupewa huduma katika hospitali ya Mwananyamala Jijini, ametoa madai mazito dhidi ya wauguzi hospitalini hapo akidai kuwa, mkewe alichelewa kuhudumiwa baada ya kukosa shilingi alfu kumi ya kuwahonga.
Bw. Hassan alitoa madai hayo mazito wakati akizungumza na Alasiri hospitalini hapo, ambako yeye na ndugu zake walikwenda kufuata mwili wa marehemu mkewe na wa kichanga.
Bw. Hassan amedai kuwa alipokwenda hospitalini hapo kumsalimia mkewe Salma Salum, alimvuta pembeni na kumuambia kwamba, manesi wa wodi ya wazazi alimokuwa amelazwa kwa siku kadhaa, walimuomba fedha ili waweze kumpeleka kwa madktari wamhudumie fasta fasta.
``Mke wangu alikuwa na shilingi 3,000 tu...alisema alipowapa hizo lakini wakagoma kuzichukua huku wakimuambia, bila wekundu hapa, hakieleweki kitu,`` akadai Bw. Hassan.
Amedai kuwa mkewe alimwambia kwamba licha ya kuwabembeleza huku akilia machozi kutokana na maumivu aliyokuwa nayo, walimkatalia kata kata wakisema hawapokei pesa pungufu ya alfu kumi.
Sakata hilo tangu mwanamke huyo alipofikishwa hospitalini hapo hadi Mungu anamtwaa liko hivi:
Jumanne Oktoba 14, mama huyo mjamzito alihisi uchungu wa kujifungua na akapelekwa haraka haraka hospitalini hapo kwa ajili ya huduma za uzazi.
Alipofikishwa hospitalini hapo, akapelekwa chumba kujifungulia almaarufu kama `leba` lakini akarejeshwa tena wodini kwa maelezo kuwa njia ya uzazi ilikuwa haijafunguka.
Jumapili Oktoba 19, hali ikawa mbaya na ikagundulika kuwa hata kiumbe kilicho tumboni kilikuwa hakichezi tena kama ilivyo kawaida.
Usiku wa Jumapili hiyo akapelekwa kwa daktari ambaye baada ya kumuona aliona hakuna namna nyingine zaidi ya kumfanyia upasuaji ili kutoa mtoto aliye tumboni.
Hata hivyo wakati akifanyiwa upasuaji, mwili wa mama huyo ukaanza kubadilika na kuwa wa bluu na hatimaye akafariki wakati akiwa huko huko ndani ya chumba cha upasuaji.
Akizungumzia madai hayo, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mwananyamala, Suleiman Muttani amesema hana taarifa kwamba wauguzi wake walimuomba fedha mama huyo ambaye hivi sasa ni marehemu.
Akasema tangu juzi amekuwa pamoja na ndugu wa marehemu huyo hospitalini hapo wakishughulikia suala la kuchukua miili lakini hawakumweleza madai hayo ya kuombwa fedha na wauguzi.
Alasiri ilipomuuliza chanzo cha kifo hicho, Dk. Muttani alisema hawezi kujua kwa vile ndugu wa marehemu jana walikataa mwili wa mpendwa wao kufanyiwa uchunguzi.
``Tulipowaambia tufanye uchunguzi, walikataa na kukuuchukua kwenda kuzika,`` akadai Dk. Mutani.
Alasiri ilipomtaka Dk. Mutani kueleza sababu za mama huyo kukaa hospitalini hapo kwa siku sita bila kupewa huduma, alisema hawezi kujibu swali hilo.
``Hilo siwezi kulijibu,`` akasema Dk. Mutani na kisha akakata simu.
Mwili wa mama huyo ulichukuliwa hospitalini hapo na ndugu zake jana mishale ya saa 9:00 alasiri na kuzikwa jana hiyo hiyo katika makaburi ya Tandale uzuri, Jijini.
Hii ni mara ya pili kwa hospitali ya Mwanayamala kukumbwa na kashfa ya kusababisha kifo cha mama mjamzito katika kipindi cha mwaka mmoja.
SOURCE: Alasiri
Hivi jamani haya matatizo yataisha lini??
2008-10-23 19:35:11
Na Emmanuel Lengwa, Mwananyamala.
Hassan Salum, mume wa mwanamke aliyeripotiwa juzi kupoteza maisha kutokana na kuchelewa kupewa huduma katika hospitali ya Mwananyamala Jijini, ametoa madai mazito dhidi ya wauguzi hospitalini hapo akidai kuwa, mkewe alichelewa kuhudumiwa baada ya kukosa shilingi alfu kumi ya kuwahonga.
Bw. Hassan alitoa madai hayo mazito wakati akizungumza na Alasiri hospitalini hapo, ambako yeye na ndugu zake walikwenda kufuata mwili wa marehemu mkewe na wa kichanga.
Bw. Hassan amedai kuwa alipokwenda hospitalini hapo kumsalimia mkewe Salma Salum, alimvuta pembeni na kumuambia kwamba, manesi wa wodi ya wazazi alimokuwa amelazwa kwa siku kadhaa, walimuomba fedha ili waweze kumpeleka kwa madktari wamhudumie fasta fasta.
``Mke wangu alikuwa na shilingi 3,000 tu...alisema alipowapa hizo lakini wakagoma kuzichukua huku wakimuambia, bila wekundu hapa, hakieleweki kitu,`` akadai Bw. Hassan.
Amedai kuwa mkewe alimwambia kwamba licha ya kuwabembeleza huku akilia machozi kutokana na maumivu aliyokuwa nayo, walimkatalia kata kata wakisema hawapokei pesa pungufu ya alfu kumi.
Sakata hilo tangu mwanamke huyo alipofikishwa hospitalini hapo hadi Mungu anamtwaa liko hivi:
Jumanne Oktoba 14, mama huyo mjamzito alihisi uchungu wa kujifungua na akapelekwa haraka haraka hospitalini hapo kwa ajili ya huduma za uzazi.
Alipofikishwa hospitalini hapo, akapelekwa chumba kujifungulia almaarufu kama `leba` lakini akarejeshwa tena wodini kwa maelezo kuwa njia ya uzazi ilikuwa haijafunguka.
Jumapili Oktoba 19, hali ikawa mbaya na ikagundulika kuwa hata kiumbe kilicho tumboni kilikuwa hakichezi tena kama ilivyo kawaida.
Usiku wa Jumapili hiyo akapelekwa kwa daktari ambaye baada ya kumuona aliona hakuna namna nyingine zaidi ya kumfanyia upasuaji ili kutoa mtoto aliye tumboni.
Hata hivyo wakati akifanyiwa upasuaji, mwili wa mama huyo ukaanza kubadilika na kuwa wa bluu na hatimaye akafariki wakati akiwa huko huko ndani ya chumba cha upasuaji.
Akizungumzia madai hayo, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mwananyamala, Suleiman Muttani amesema hana taarifa kwamba wauguzi wake walimuomba fedha mama huyo ambaye hivi sasa ni marehemu.
Akasema tangu juzi amekuwa pamoja na ndugu wa marehemu huyo hospitalini hapo wakishughulikia suala la kuchukua miili lakini hawakumweleza madai hayo ya kuombwa fedha na wauguzi.
Alasiri ilipomuuliza chanzo cha kifo hicho, Dk. Muttani alisema hawezi kujua kwa vile ndugu wa marehemu jana walikataa mwili wa mpendwa wao kufanyiwa uchunguzi.
``Tulipowaambia tufanye uchunguzi, walikataa na kukuuchukua kwenda kuzika,`` akadai Dk. Mutani.
Alasiri ilipomtaka Dk. Mutani kueleza sababu za mama huyo kukaa hospitalini hapo kwa siku sita bila kupewa huduma, alisema hawezi kujibu swali hilo.
``Hilo siwezi kulijibu,`` akasema Dk. Mutani na kisha akakata simu.
Mwili wa mama huyo ulichukuliwa hospitalini hapo na ndugu zake jana mishale ya saa 9:00 alasiri na kuzikwa jana hiyo hiyo katika makaburi ya Tandale uzuri, Jijini.
Hii ni mara ya pili kwa hospitali ya Mwanayamala kukumbwa na kashfa ya kusababisha kifo cha mama mjamzito katika kipindi cha mwaka mmoja.
SOURCE: Alasiri
Hivi jamani haya matatizo yataisha lini??