Ungependa kusoma nini ukiwa kule kwenu..brainstorming

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,463
39,929
Fikiria unapata kijarida cha kurasa mbili au nne hivi cha Kiswahili ambacho ni cha bure kabisa. Ni kijarida cha habari na maoni kinachojaribu kuunganisha mambo yanayozungumzwa kwenye mitandao mbalimbali na mtu wa mitaani ambaye hana internet lakini anaweza kunufaika na mijadala hiyo. Kijarida ambacho ukianza kusoma huwezi kuweka chini na ukifika mwisho unataka kumpatia mwingine naye asome. Ni kijaridha chenye mvuto wa ajabu, chenye habari za kina, hoja zenye ushawishi na burudani ya kuangalia. Kijarida ambacho ni cha bure kabisa lakini ubora wa kinachopatikana ndani yake unashindana na magazeti makubwa.

Sasa wewe jichukulie ni mtu wa "kawaida" whatever that means, unayejua lugha ya Kiswahili, Kiingereza cha kuyupia maji, na mikononi mwako hauna zaidi ya dakika kumi na tano za kupoteza. Unapewa kijarida mkononi na rafiki yako, unategemea kitu gani kimo ndani ya kijarida hicho ambacho kitakufanya utafute siku nyingine na nyingine na nyingine?

Yaani kijarida ambacho unaweza kumwambia rafiki yako, jamaa au ndugu kuwa lazima akitafute. Na hakihusiani na mambo ya ngono lakini kinavutia kina baba na kina mama, wasomi na wasio wasomi, matajiri na maskini na wote wanaposoma wanajiambia moyoni "hiki ni kijarida chetu".

NINI UNATARAJIA KIWEMO NDANI YA KIJARIDA HICHO? Sasa msilete stori ndeeeefu.. toa wazo na mawazo yote yanapokelewa na hakuna wazo lolote baya, duni, dhaifu, au la kuchekesha au kuudhi!
 
Ningependa kizungumzie jinsi muda unaotumika kulalamika bila kufikia tamati ya kuwa na mkakati thabiti wa kubadili matatizo yanayowakabili wadanganyika unavyoweza kutumika vema na kubadili fikra na maisha yao.
 
Ningependa kiwe na habari za ujumla zinaizunguka jamii,kama siasa,burudani michezo, dini/imani na kadhalika.

Lakini ili kiwe na ushawishi na mvuto, kiwe kinatoa habari ambazo hazipatikani katika media nyingine, kwa maana kitoe behind-the-scene info zinazohusu matukio makubwa katika lugha nyepesi na inayoeleweka.

Kijarida hicho kinaweza kuwa na mjumuisho pia wa matukio mengine makubwa ulimwenguni lakini yenye "positive relevance" kwa Tanzania.

Kijarida hicho,kikiweza kuwa na vikaragosi,hata kwa uchache tu,pia itasaidia kutoa mvuto na kufikisha ujumbe kwa jamii. Hapa nachukulia mfano wa magazeti yaliwahi kuwa na mvuto sana kama Sanifu.
 
Ningependa kiwe na habari za ujumla zinaizunguka jamii,kama siasa,burudani michezo, dini/imani na kadhalika.

Lakini ili kiwe na ushawishi na mvuto,

kiwe kinatoa habari ambazo hazipatikani katika media nyingine kwa maana kitoe behind-the-scene info zinazohusu matukio makubwa katika lugha nyepesi na inayoeleweka.

b. Kiwe na mjumuisho pia wa matukio mengine makubwa ulimwenguni lakini yenye "positive relevance" kwa Tanzania.

c. Kijarida hicho,kikiweza kuwa na vikaragosi,hata kwa uchache tu,pia itasaidia kutoa mvuto na kufikisha ujumbe kwa jamii.

Asante sana;
 
Ningependa kizungumzie jinsi muda unaotumika kulalamika bila kufikia tamati ya kuwa na mkakati thabiti wa kubadili matatizo yanayowakabili wadanganyika unavyoweza kutumika vema na kubadili fikra na maisha yao.

unafikiri hili linaendana na dhana nzima ya kijarida hicho kama nilivyoeleza hapo juu?
 
Ningependa liwe na sehemu ambayo kutakuwa na mazungumzo ya watu wa pande mbili,ya kwanza ni ile ya serikali ikieleza namna ilivyojipanga kumkomboa Mtanzania(hasa mwenye kipato cha chini)pia maelezo ya progress ya implementation ya hzo strategy.Kwa upande wa pili,Mtanzania wa chini apewe nafasi ya kueleza ni yapi anayaona kama mdau mlengwa wa strategy za serikali.Challenges,failures and areas of success from their point of view.Kwa hitimisho la hayo,awepo mtu huru&mtaalamu ambaye ataanalyze maoni ya pande zote mbili bila kuwa biased na ushauri wake kama itabidi.
 
Pamoja na yaliyosemwa na waliotangulia ku post.. pia ningependa kiwe na " summary" ya mambo muhimu yanayoandikwa na magazeti ya kiingereza kama East Africa etc ili nami nisiyejua kiingereza nisipitwe; ningependa kiwe na matangazo ya fursa mbalimbali - kazi, biashara, n.k lakini siyo matangazo ya waganga wa kienyeji na dawa zao za mapenzi etc; aidha font zake zisiwe ndogo sana; kiwe cha rangi pia itanivutia zaidi.
 
Ningependa kiwe 'website based' kihabarishe kwa ufupi habari zilizojiri kutoka mitandao ya tanzania na ya watanzania walio nje, kwa nia ya kuhabarisha na sio ngono au udaku kwa vile vijarida vya udaku viko kila kona Tanzania, vilevile kuwe na kurasa mbili tatu maalumu kwa comments za wadau ambazo zitolewe direct toka kwenye forums kama hii ya JF nk, kwani mara nyingi comments zina michango mikubwa kwa vile ni mawazo ya watu tofauti,ila zisiwe 'filtered' au 'edited' hilo wazo la kijarida ni la busara sana kwani nilikuwa nyumbani mwezi Juni na ingawa nilikua napata habari magazetini, luninga nk, bado nilihisi kwa habari zenye kukidhi kiu inabidi niingie mitandandaoni, ukizingatia connection speed na time factor nilikuwa siwezi kwenda internet cafe kila siku. Kulingana na hali ya wa-Tanzania walio wengi hawafaidiki na habari tunazopata humu mitandaoni, kwani hawana uwezo ama wakati wa kutembelea mitandao kila siku, hicho kijarida kitasaidia sana. Ni hayo tu.
 
Ningependa kiwe na habari za ujumla zinaizunguka jamii,kama siasa,burudani michezo, dini/imani na kadhalika.

Lakini ili kiwe na ushawishi na mvuto, kiwe kinatoa habari ambazo hazipatikani katika media nyingine, kwa maana kitoe behind-the-scene info zinazohusu matukio makubwa katika lugha nyepesi na inayoeleweka.

Kijarida hicho kinaweza kuwa na mjumuisho pia wa matukio mengine makubwa ulimwenguni lakini yenye "positive relevance" kwa Tanzania.


Pamoja na yaliyosemwa na waliotangulia ku post.. pia ningependa kiwe na " summary" ya mambo muhimu yanayoandikwa na magazeti ya kiingereza kama East Africa etc ili nami nisiyejua kiingereza nisipitwe;


Ningependa kiwe 'website based' kihabarishe kwa ufupi habari zilizojiri kutoka mitandao ya tanzania na ya watanzania walio nje, kwa nia ya kuhabarisha na sio ngono au udaku kwa vile vijarida vya udaku viko kila kona Tanzania, vilevile kuwe na kurasa mbili tatu maalumu kwa comments za wadau ambazo zitolewe direct toka kwenye forums kama hii ya JF nk,





I like this thread!
Kweli, umewahi kutembelea website ya LHRC au kusoma vitabu vyao?
Kila mwaka hutoa kitabu kinaitwa "Tanzania Human Rights Report" (Available online).
Ukianza kusoma huwezi kuweka chini na ukifika mwisho unataka kumpatia mwingine naye asome.

Sasa hivi niko kwenye Publication >> Books. Nime-download pdf moja ya Bad Laws (Sheria mbaya Arobaini).




Some of my favorite:
www.humanrights.or.tz
www.hakielimu.org





.
 
Pamoja na yaliyosemwa na waliotangulia ku post.. pia ningependa kiwe na

1. " summary" ya mambo muhimu yanayoandikwa na magazeti ya kiingereza kama East Africa. (hiyo summary iwe kwa Kiingereza au Kiswahili?)

2. kiwe na matangazo ya fursa mbalimbali - kazi, biashara, n.k lakini siyo matangazo ya waganga wa kienyeji na dawa zao za mapenzi etc;

3. aidha font zake zisiwe ndogo sana; kiwe cha rangi pia itanivutia zaidi.

Asante sana...
 
Ningependa liwe na sehemu ambayo kutakuwa na mazungumzo ya watu wa pande mbili,ya kwanza ni ile ya serikali ikieleza namna ilivyojipanga kumkomboa Mtanzania(hasa mwenye kipato cha chini)pia maelezo ya progress ya implementation ya hzo strategy.Kwa upande wa pili,Mtanzania wa chini apewe nafasi ya kueleza ni yapi anayaona kama mdau mlengwa wa strategy za serikali.Challenges,failures and areas of success from their point of view.Kwa hitimisho la hayo,awepo mtu huru&mtaalamu ambaye ataanalyze maoni ya pande zote mbili bila kuwa biased na ushauri wake kama itabidi.


Nimekupata vilivyo...
 

1. Ningependa kiwe 'website based' kihabarishe kwa ufupi habari zilizojiri kutoka mitandao ya tanzania na ya watanzania walio nje,

2. Kuwe na kurasa mbili tatu maalumu kwa comments za wadau ambazo zitolewe direct toka kwenye forums kama hii ya JF nk,

Hewala, mawazo yamepokelewa.
 
Ningependa kizungumzie hali ya umaskini tuliyonayo tangu tumepata uhuru na kitoe mapungufu yanayosababisha nchi isipige hatua kiuchumi pamoja na raslimali nyingi tulizonazo na amani pia;na hii iwe kwa kuchambua marais walioiongoza nchi hii na waliahidi nini katika masuala ya uchumi na walifanikisha yapi katika kuboresha uchumi na kwanini walishindwa kuwajibika kwa yaliowashinda kuwa timizia watanzania na kuna aliomba radhi kwa wananchi katika hilo.
 
Serious stuff. Huko nyuma nilimuomba Rev. Kishoka kama angefanya hivyo kwa ule waraka wake.

Rev. Kishoka,

Huwezi kufanya mpango na kuchapisha vijarida vidogo vya kusambaza nchi nzima BURE, ili uwafikie walio wengi? Manake nadhani watu wengi vijijini huku hawanunui magazeti. Asante.

Kwa hicho kijarida chako Mzee Mwanakijiji. Unaweza kuzungumzia/kufuatilia utendaji wa vyombo vya serikali manake uzembe ni mwingi sana. Kila toleo unawa-interview watu wa kawaida kabisa kona zote Tanzania nawatakueleza maoni yao. Ambayo unaweza kutumia kama msingi wa matoleo. Kasi na uhakika wa habari.
 
Kwa hicho kijarida chako Mzee Mwanakijiji. Unaweza kuzungumzia/kufuatilia utendaji wa vyombo vya serikali manake uzembe ni mwingi sana.

Kila toleo unawa-interview watu wa kawaida kabisa kona zote Tanzania nawatakueleza maoni yao. Ambayo unaweza kutumia kama msingi wa matoleo. Kasi na uhakika wa habari.

Kwa hiyo liwe na interview ya watu wa kawaida pia. Point nzuri sana.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom