Ungekuwa wewe ungefanyaje?

yus4tanzania

New Member
Sep 12, 2008
1
0
Jamaa mmoja alikuwa akitokea shamba pamoja na mkewe. Wakiwa njiani
waliona uyoga, wakaung'oa na kwenda nao nyumbani kwa lengo la kwenda
kupika na kuula. Lakini kabla ya kufika nyumbani, wakahofu kwenda kula ule
uyoga wakihisi unaweza kuwa si uyoga wa kula.
Basi wakaamua wapike uyoga kidogo,na kiasi waubakishe, halafu ule
waliopika wampe mbwa wao, asipokufa mbwa basi ule waliobakisha nao wale.

Mbwa akala uyoga ule. Wakakaa siku ya kwanza,ya pili, mbwa hajafa
wakaamua wapike ule uyoga uliobakia nao wakala.

Walipomaliza kula tu, mara mtoto wao wa kiume akaingia ndani akitokea shule, na kuwaeleza wazazi kuwa amemuona mbwa wao amekufa.

Wazazi wakapigwa na butwaa wakijua basi nao mwisho wa maisha yao
umefika, na muda wowote watakufa tu kwa kuwa nao wamekula uyoga kama mbwa
alivyokula.

Basi yule baba akaamua kumwambia mkewe anaomba atubu mbele yake kwa
kuwa kifo kinamjia wakati wowote. Jamaa akaanza kumwambia mkewe amsamehe
kwani ni maovu mengi alifanya. Kwanza msichana wa kazi waliomfukuza
akiwa na ujauzito, ule ni ujauzito wake. Mdogo wake na mkewe wa kike
anayeishi naye pale ni mpenzi wake wa siku nyingi. Pia ana watoto wengine
watatu nje ya ndoa, na kila mtoto ana mama yake.

Mama akasema nashukuru kwa hayo yote, Basi naomba nani nitubu Kwako.
Huyu mtoto wa kiume mdogo si wakon nilizaa na Shamba boy wetu na huu
ujauzito nilionao sasa ni wa mpangaji wetu humu ndani.

Jamaa kusikia hayo akapandwa na jazba ukawa ugomvi mkubwa mule ndani.

Wakati wakigombana, mara mtoto wao wa kwanza wa kike akaingia ndani
na kukuta wakigombana. Akawauliza ,Baba na mama mnagombania nini humu
ndani,badala ya kwenda kuona mbwa wetu amekufa kwa kugongwa na gari kule
nnje?
Wazazi waliposikia kuwa mbwa amekufa kwa kugongwa na gari walibaki
wanatazamana na kupigwa na bumbu wazi.

Fikiria ni wewe ITAKUWAJE?
 
Jamaa mmoja alikuwa akitokea shamba pamoja na mkewe. Wakiwa njiani
waliona uyoga, wakaung'oa na kwenda nao nyumbani kwa lengo la kwenda
kupika na kuula. Lakini kabla ya kufika nyumbani, wakahofu kwenda kula ule
uyoga wakihisi unaweza kuwa si uyoga wa kula.
Basi wakaamua wapike uyoga kidogo,na kiasi waubakishe, halafu ule
waliopika wampe mbwa wao, asipokufa mbwa basi ule waliobakisha nao wale.

Mbwa akala uyoga ule. Wakakaa siku ya kwanza,ya pili, mbwa hajafa
wakaamua wapike ule uyoga uliobakia nao wakala.

Walipomaliza kula tu, mara mtoto wao wa kiume akaingia ndani akitokea shule, na kuwaeleza wazazi kuwa amemuona mbwa wao amekufa.

Wazazi wakapigwa na butwaa wakijua basi nao mwisho wa maisha yao
umefika, na muda wowote watakufa tu kwa kuwa nao wamekula uyoga kama mbwa
alivyokula.

Basi yule baba akaamua kumwambia mkewe anaomba atubu mbele yake kwa
kuwa kifo kinamjia wakati wowote. Jamaa akaanza kumwambia mkewe amsamehe
kwani ni maovu mengi alifanya. Kwanza msichana wa kazi waliomfukuza
akiwa na ujauzito, ule ni ujauzito wake. Mdogo wake na mkewe wa kike
anayeishi naye pale ni mpenzi wake wa siku nyingi. Pia ana watoto wengine
watatu nje ya ndoa, na kila mtoto ana mama yake.

Mama akasema nashukuru kwa hayo yote, Basi naomba nani nitubu Kwako.
Huyu mtoto wa kiume mdogo si wakon nilizaa na Shamba boy wetu na huu
ujauzito nilionao sasa ni wa mpangaji wetu humu ndani.

Jamaa kusikia hayo akapandwa na jazba ukawa ugomvi mkubwa mule ndani.

Wakati wakigombana, mara mtoto wao wa kwanza wa kike akaingia ndani
na kukuta wakigombana. Akawauliza ,Baba na mama mnagombania nini humu
ndani,badala ya kwenda kuona mbwa wetu amekufa kwa kugongwa na gari kule
nnje?
Wazazi waliposikia kuwa mbwa amekufa kwa kugongwa na gari walibaki
wanatazamana na kupigwa na bumbu wazi.

Fikiria ni wewe ITAKUWAJE?
.....Tumeshasameana kila mtu ameanika uovu wake umejulikana maisha yanaendelea.....Ngoma draw!!!!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom