VISIONEER
Senior Member
- Apr 29, 2011
- 141
- 20
Habari ya kwenu wana jf.
Mimi nina rafiki ambaye ni jinsia ya kike alikuja kuniomba ushauri afanyeje anasema kuwa ametokea kumpenda kijana ambaye ni wa mtaani kwao,anasema anampenda kwa dhati na ana malengo ya ndoa pia ikiwa wataelewana, lakini utata upo hapa yeye ni mtoto wa kike na kwa taratibu zetu au sijui mila za mtanzania mwanaume mpaka amtokee mwanamke kwanza,sasa yeye anasema anaogopa kumwambia kwasababu hizo na asije onekana labda malaya.
Mwanamke ana miaka 31,anaishi maisha ya wastani, anafanya kazi na ana kipato cha wastani kilichomwezesha kujenga nyumba moja na ana gari ya kutembelea moja.
Lakini yeye anasema anabahati mbaya kuwa kila mwanamme anayemtaka kumuoa hampendi, ila anaowapenda hawampendi. Na akiangalia umri unazidi kwenda mbele sasa afanyeje amwambie huyo kijana na je ni hali ya kawaida kwa watanzania au ataonekana malaya?
Tunaomba msaada kwa hili wanaume wa tanzania mnalichukuliaje? Kama ndio wewe mwanamke anakutokea kwa malengo mazuri utamchukuliaje.
Msaada plse!
Mimi nina rafiki ambaye ni jinsia ya kike alikuja kuniomba ushauri afanyeje anasema kuwa ametokea kumpenda kijana ambaye ni wa mtaani kwao,anasema anampenda kwa dhati na ana malengo ya ndoa pia ikiwa wataelewana, lakini utata upo hapa yeye ni mtoto wa kike na kwa taratibu zetu au sijui mila za mtanzania mwanaume mpaka amtokee mwanamke kwanza,sasa yeye anasema anaogopa kumwambia kwasababu hizo na asije onekana labda malaya.
Mwanamke ana miaka 31,anaishi maisha ya wastani, anafanya kazi na ana kipato cha wastani kilichomwezesha kujenga nyumba moja na ana gari ya kutembelea moja.
Lakini yeye anasema anabahati mbaya kuwa kila mwanamme anayemtaka kumuoa hampendi, ila anaowapenda hawampendi. Na akiangalia umri unazidi kwenda mbele sasa afanyeje amwambie huyo kijana na je ni hali ya kawaida kwa watanzania au ataonekana malaya?
Tunaomba msaada kwa hili wanaume wa tanzania mnalichukuliaje? Kama ndio wewe mwanamke anakutokea kwa malengo mazuri utamchukuliaje.
Msaada plse!