Underground vs Wakongwe wa JF

Bitoz

JF-Expert Member
Aug 27, 2015
30,823
126,536
Mambo vipi wanangu?

Sio siri hapa JF kuna battle ya chini kwa chini kati ya wakongwe(member wa muda mrefu) dhidi ya Underground(member wasio na muda mrefu hapa jukwaani),
Wakongwe wanataka kubaki juu, huku underground wakitaka kutoka na kuwafunika wakongwe!
Ni full raha....

1/Jukwaa la "Polifix"
Hili linajumuisha General forum na majukwaa yake kama vile Jukwaa la siasa,jamii intelligence,habari na hoja mchanganyiko n.k..
Huku wakongwe wanaendelea kutamba na kila underground anayejaribu kuliteka Jukwaa anakula za uso kamavile kukosolewa lugha anayotumia au kutimuliwa kwa kutafutiwa BAN!!! Kimsingi hili Jukwaa wakongwe ni kama wamelininafsisha tu...

2/Social Forums
Huku kunajumuisha majukwaa kama vile Chit Chat , celebrities forum(Jukwaa la umbea),Jamii photos,Sports and entertainment n.k
Huku vita unaonekana kuwa kali kinoma ina sura mbili : mosi, Underground wanaonekana kuteka jukwaa kwa kuja na vitu vyenye ubunifu huku wakongwe wakibaki solemba !
Pili baada ya wakongwe kugundua wameanza kufunikwa wameanza mbinu ya kutumia ID zaidi ya 1 ili kujipaisha kwa kuanzisha thread na kujitajataja mfano "Nampenda fulani".Hata uje na ID 1k hutuwezi underground!
Tatu, baada ya kuona maji yamezidi unga uamua " kufukua makaburi" kwa kuzirudisha thread zao za zamani zilizowahi kubamba ili kuwapunguza nguvu underground lakini bado wamebugi !!


Kwa ujumla wakongwe wapo hoi nawashauri ili kuepuka kugaragazwa zaidi na madogo leteni vitu vyenye ubunifu shtukeni kabla hamjapata aibu ya kifo cha mende!!
Underground wote salute kwenu
f3834afcbdc8d41262e4ef60dafbcf18.jpg


***Ukinuna...ww ni mchawi !**

Sharo wa Uswaz
The Bitoz
 
Hivi nikitaka kwenda mbagala kutokea masaki napita njia gani vile ????!!
 
Back
Top Bottom