Natamani sana turudi enzi zile mambo yalikuwa shwari sana,ukamera man ulikuwa dili sana na madem walikuwa bomba sana tofauti na wa siku hizi wamechakachuliwa sana,mpaka wamepoteza radha alafu hawajui hata majambozi,HIZO NDIO ENZI ZA NGAZI TATU BWANA,danga chee dukinaa salam za mablazaman enzi hizo.
Duuu hao walikuwa wanaitwa, magangwe au check bob.Safi sana.
Picha ya juu jamaa wapo beach,naona kuna gangwe mmjo amevaa chupi ya james bond 007 ilikuwa na kamfuko kamoja mbele.
Looh! Wakati umekwenda wapi jamani....!? Asante mdau kwa picha hizi chache bali zenye ujumbe na nguvu ya fikira isiyoweza kupimika wala kuonekana kwa macho. Asante tena na hongera Mkuu!
Aaah umenikumbusha mbali sana, enzi hizo wasiwasi wa maisha ulikuwa haupo, mtu anatembea mpaka kijiji cha tatu usiku wa manane kufuatilia demu. Tofauti na siku hizi gari ikifunga breki wanabanana madirishani kukuonyesha bidhaa zao!
Jamani hakika imenikuna sana kwa picha hizo. Zimenikumbusha mambo mengi. Nakumbuka enzi hizo ukienda kumtembelea ndugu yako utakuta sebure imejaa picha ukutani za staili mbalimbali.
Inaelekea zamani kulikuwa hakuna wanene. Picha za siku hizi vijana wanaonekana matipwatipwa. Zamani walikuwa wamekaukiana. sijui ni sababu ya shida au vipi. hebu tuelezeni.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.