Unazi na Ushabiki wa CCM: chimbuko na siri yake nini?

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Kwa nini watu wamelewa mvinyo wa CCM? Je ni kwa ajili ya imani ya siasa za ujamaa na kujitegemea? au ni kwa kuwa CCM ni mtoto wa TANU na ASP waliotupatia Uhuru?

Nikijiuliza falsafa na mrengo wa siasa za Tanzania na hasa CCM, sipati jibu! Najiuliza tena ni vipi CCM iwe na washabiki wengi kiasi hicho ambao ni vipofu wa kutupa?

Sikatai miye ni CCM mfu, lakini siwezi kuendelea kuipepea CCM kuwa ni chama thabiti and ndio chama pekee, huku kutoka kushoto mpaka kulia ni vurugu tupu.

Nilipata kumuuliza Mzee wangu moja (jina siri) kuhusu vyama vya siasa na CCM, akanijibu CCM ndio jibu na chama pekee. nilipomuuliza sababu, nikaanza kuimbiwa historia.

Najiuliza hivi ikiwa tunajianda na chaguzi mbili kubwa, ya kwanza ni ya Serikali za mitaa mwaka huu 2009 na uchaguzi mkuu mwakani wa Wabunge na Urais, je wananchi wataichagua CCM kwa kutumia vigezo gani? Je ni mazoea au?

Nikijikumbusha Unazi wa vyama vya siasa Marekani, kati ya Republicans na Democrats, walau unaweza kujua kuna mambo makuu ambayo wanapingana.

Republicans ni mabepari, wanapenda mfumo huria, Serikali ndogo, kodi nafuu, uhuru wa Bunduki, Udini wa Yesu kwa amri za kupinga Uchoko na U S E N G E, kutoa mimba na hili la Usungusungu tangu 9/11.

Democrats pamoja na Ubepari wao wa kijamaa, ndoa za mashoga ni poa, serikali kubwa ni swadakta, kodi kubwa kwa matajiri na dezo dezo kwa wengine ni kama kawaida, kutoa mimba wanadai ni mwanamke na mwili wake na siku hizi suala la mazingira.

Nikirudi Tanzania yetu najiuliza ushabiki ule wa CCM ni kutokana na nini? Walau hata ule wa CUF na CHADEMA japo tunadai ni spesheli kwa mambo ya Udini au Ukabila, unawafuasi kdhaa ambo tunaweza kuwaona kwa tafsiri hizo za mcaho yetu ambazo si lazime kuwa sahihi za Udini na Ukabila, lakini sielewi ni vipi watu tumelewa mvinyo wa CCM!

Je ni mapenzi yetu kwa Nyerere, Azimio la Arusha, Ujamaa au ni vipi? Mbona Azimio na Ujamaa tunaona ni mchungu sasa hivi na umasikini tulionyo, lakini tumefia kidonda hata tukiambiwa CCM itatuzika hai hatusituki?

Wananchi na wale wanachama wa kawaida, niko tayari kukiri wamepotoka na kulewa mvinyo wa Ujamaa na Kujitegemea na Azimio la Arusha (kama mimi ninavyoendelea kucheua chicha la Azimio na Ujamaa) lakini ukienda kwa Viongozi na Watendaji, hawaendani kabisa na imani za Wananchi na Wanachama wa kawaida.

Viongozi wa CCM wanaimba "wananchi inabidi tule mchunga" lakini ukienda nyumbani kwao, wao wanakula kabichi! Viongozi wa CCM wanalia tunywe togwa, rubisi na chimpumu, wao wanashindilia Joni Woka, Brandy na Mvinyo wa ulaya ulaya!

Sasa najiuliza tena ikiwa tunajua hawa jamaa ni walaghai, kwa nini tunaendela kuwaamini na kukienzi chama na tusikimbilie kwa kina UDP, TLP japo wao hawana lolote na ni alosto kama sisi?

Unazi wetu wa kudai CCM ina wenyewe huku sisi tukiwa wajakazi, taarishi, manamba na makuli tunaupata wapi? ni imani gani kubwa hiyo tuliyonayo kwa CCM kumzidi Tanzania, Yesu na Muhamed?

Nasubiri jibu lenu!
 
Imani ya watanzania kwa CCM ni mazoea tu. Zamani enzi za mwalimu tulikuwa tukiimba ile sloglan, tena kabla ya kipindi cha somo la siasa hakijaanza. Mwalimu akiingia darasani, kiranja wa darasa anapiga kofi paa, wote twasimama na kusema!

Ili tuendelee tunahitaji vitu vinne
> watu
> ardhi
> siasa safi
> uongozi bora

Nadhani kadri siku zinavyozidi kwenda, tunazidi kupungukiwa na hivyo vigezo vinne vya maendeleo. nachelea kusema kimebaki kigezo kimoja tu "WATU".

Kama kuna mapenzi ya kweli na CCM, basi ni mazoea tu!!
 
Mkuu rev. mimi nadhani ni mazoea na majority kutokuelewa the gigantic influence ya siasa katika maisha yetu.
 
Pamoja na maneno ya dhihaka CCM kinabaki kuwa chama pekee ambacho kina sifa zote za kuitwa chama. Umezungumzia mazoea kuwa pengine ndio yamesababisha kwa watu kuwa na mvuto na imani kwa CCM. Hiyo inaweza kuwa moja ya sababu kubwa lakini sio sababu teule ya kuwazuia watu wasipende vyama vingine.

Wakati wa kurudi kwa mfumo wa vyama vingi nchini, kulikuwa na kila aina ya vioja toka katika chama tawala hadi vya upinzani, wakati ule ndio ulikuwa wakati mzuri wa kuweza kupima vyama na wananchi wenyewe aidha kuona vipi viongozi wakijibadilisha na kuweza kukabiliana na mfumo huo.

Mfano wakati A. Mrema akiwa bado yupo CCM na akitamba na kauli zake za siku saba na ulinzi wa sungusungu, aliwahi kualikwa kwenye ufunguzi wa polisi posti kule Zenj, kibanda kilichojengwa na mfanya biashara maarufu kipindi kile Moh'd Raza. Akihutubia mamia ya wakaazi wa eneo la polisi posti hiyo mpya, Mrema alivibonda vyama pinzani na kuwaonya wakaazi wale kuwa iwapo watathubutu kuchagua upinzani basi huo ndio utakuwa mwanzo wa vita vya ndani nchini na wakatao umia ni wananchi wenyewe kwani yeye na Raza watapanda helikopta na kwenda kuishi nje ya nchi.
Mrema alithubutu kutoa kauli hii kwa kuwa alikuwa ni CCM na ana dhamana kubwa serikalini. Kilichotokea baada ya kuondolewa kwa wadhifa wake kinajulikana.

Ukiangalia kwa kina wengi walioanzisha vyama vya upinzani ni wale waliofeli katika CCM. Chama cha CUF wanajinadi kwa haki sawa kwa wote, ukipitia sera za chama hicho kwa makini na nini watafanya watakapo kuwepo madarakani si kingine bali ni kuondoa haki toka kwa mtu mmoja na kupeleka kwa mtu mwingine. Hapo dhana nzima ya haki sawa kwa wote inakosekana na walio wengi wanaona chama hicho hakina la ziada zaidi ya kuwa chama cha kulipiza visasi kwa kufeli kwao ndani ya CCM.

UDP waliweza kutamba na sera ya kujaza mapesa mifukoni, kauli ambayo ilivuma sana kutokana na ulofa wa walio wengi nchini. Lakini ukiangalia vizuri wale ambao wanategemewa kujazwa mapesa mifukoni mwao wanapatikana katika sehemu fulani ya nchi. Je sehemu zilizobaki watajazwa vipi hayo mapesa mfukoni? Chama hicho hadi leo hakina jibu.

Hawa ambao sasa wamekuwa gumzo na kuonekana kuwa pengine wataweza kutoa upinzani wa dhati hawana lolote jipya. Wao wanachonadi ni mabadiliko ya kweli na Chama kilipoanzishwa kilikuwa kinajinadi kwa kuleta maendeleo kwa wote. Sasa wanasema wanataka mabadiliko ya kweli inawezekana mabadiliko hayo yakawa kwa CCM, kwa wananchi au kwao wenyewe Chadema. Hivyo kwa namna moja ama nyingine unaweza kupata picha kuwa hata hawa bado hawajui ni nini wanachohitaji na nini watatoa kwa wananchi pale watakapo kabidhiwa nchi.
 
Last edited:
Mimi kwa mtazamo wangu ukiona mtu anashabikia CCM katika nyakati hizi basi kuna mambo kadhaa ambayo mtu huyo

anakuwa ameyalenga.

Mosi wanaingia ndani ya chama hiki wapate kinga kutoka kwa watawala na watumie mwanya huo kujipatia na kujiongezea manufaa fulani ya mali au fedha tumeona na tunazidi kushuhudia

[hatuna haja ya kutaja majina you know yourselves] si jambo la kushangaza nikisema CCM ni jalala ambalo vichaa hukimbilia kupata chochote, Ingawa sina takwimu rasmi lakini

matendo ya watu hao mnayafahamu

Pilli kuna watu wanaingia kwenye chama hiki kwa ahadi fulanifulani za kupata madaraka yatakayowapelekea kupata mali au fedha [ Hakuna misingi ya AZIMIO la Arusha, la MUSOMA wala ZANZIBAR hapa ni wizi mtupu]

na mwisho kuna kundi la watu mimi nawaita Fools kwa sababu wao ni bendera fuata upepo na hawafikirii, Hawa ni wengi sana na wanahitaji kuelimishwa sana, Wao wamekuwa wakidangaywa

kila siku kwa ahadi Feki, wanadhani maendeleo yanaletwa kwa maneno, ndio maana baadhi ya wanasiasa wa CCM huwadanganya kwa vitu vidogovidogo kama khanga, Tsh.10,000/, T-shirts za kijani feki, nk

nyakati za chaguzi mbalimbali.

CCM kama CCM sio tatizo, kwani ina sera nzuri tatizo ni watu, Nyerere ataendelea kubaki kwenye chart kwa muda mrefu sana kwa mienendo ya siasa zetu.

CCM ni chama ambacho kiongozi akionyesha uwezo na uzalendo dhabiti wa kuwatumikia wananchi wake anatafutiwa zengwe, njama na kuhujumiwa aonekane hafai,

Baadhi ya viongozi wa CCM hawako tayari kwa changamoto, ndo maana baadhi ya voingozi wake wako radhi damu imwagike kuliko kuachia ngazi kwa wengine

Baadhi ya wana CCM wanatumia vibaya jina la Mwalimu Nyerere kujipatia umaarufu feki na kudanganya wananchi.

Sioni sababu ya kuendelea kukumbatia chama chenye viongozi wenye hoja chakavu.
 
Sikatai miye ni CCM mfu, lakini siwezi kuendelea kuipepea CCM kuwa ni chama thabiti and ndio chama pekee, huku kutoka kushoto mpaka kulia ni vurugu tupu.

Mkuu Kishoka, hilo linalokufanya uwe CCM mfu, ndio nawengine linawafanya wawe CCM. Ila hakuna lolote kuwa CCM kina wafuasi wengi ndio maana kinashinda chaguzi. Kama CCM wangekubali tuwe na tume huru za uchaguzi, sasa hivi tungekuwa tunazungumza mengine, hata kama Rais ingekuwa hajapatikana toka upinzani, lakini idadi ya Wabunge na Madiwani ingeongezeka sana
 
Mimi nadhani:

1. Bado Watanzania wengi, hasa vijijini wamejifunika blanketi zito.
2. Umasikini wao unawafanya wanunuliwe na CCM kiurahisi, hasa wakati za chaguzi -- kwani akishapewa Tshirt (bila nguo ya chini) basi kaona kapata. Na wananuliwa kwa mahela yao wenyewe wanayoyaiba kutoka kwao.
3. Bado hakuna upinzani wa dhati, viongozi wa upinzabni ni masikini na wamekuwa matapeli. Kwa mfano agenda ya ufisadi (EPA etc) ingewezesha kuisambaratisha CCM, lakini wapi, pesa walizoiba CCM bado zina nguvu kuwasambaratisha wao.
4. Kwa wasomi kama Rev Kishoka, labda ni kwa sababu ya kutaka masilahi fulani, kwani si tuliambiwa kwamba "ukitaka biashara zako zikunyookee ingia CCM?"
5. Nakubaliana na Zakumba kwamba "Tulipata uhuru mapema kabla hatujabarehe."
6. CCM ndiyo inadhibiti dola, vyombo vyake na hazina -- cha mwisho ni nyenzo muhimu kutawala milele na milele.
LAKINI:
Pamoja na haya yote bado kuna kila dalili kwamba kuna kitu kikubwa kinachoweza kutokea hata nchini katika medani ya kisiasa bila kutarajiwa. Hii ni inkling ambayo ninayo, na kinaweza kuwa kibaya sana, kwani naamini usemi kwamba "sikio la ajali halisikii"

Na mwisho kabisa tusisahau kwamba mwaka 1995 CCM ilitikisika sana na NCCR-Mageuzi (kabla ya viongozi wa upinzani nao kuanza kuwa kama wale wa CCM) hadi kukawa na wasiwasi miongoni mwao kupoteza kura ya urais, hivyo kuvuruga uchaguzi wa mkoa wa Dar.
 
Originally Posted by Rev. Kishoka
Sikatai miye ni CCM mfu, lakini siwezi kuendelea kuipepea CCM kuwa ni chama thabiti and ndio chama pekee, huku kutoka kushoto mpaka kulia ni vurugu tupu.

**************

Pengine Rev Kishoka kawa CCM mfu kutokana na imani yake ya kiroho.
 
Ni mambo ya zamani za kale ,uhakika hivi sasa hakuna anaemjali SUltani CCM ,wanakiita chama cha majizi au mafisadi, sio kuwa naandika kwa kupenda wandugu nimetembelea vigenge kibao na kupita kwenye masoko ya kila aina hata ya samaki ,na kwa kweli wananchi waleo hawatoi lugha safi juu ya Mtawala huyu CCM ,ni kuponda juu ya kuponda tu ,hakuna la kheri hata moja utakalolisikia kutoka kwao ,halafu wanaongezea na mijineno ya aibu yake ,ni balaa tu ,tena usije ukajaribu kuitetea CCM kwenye vigenge au sokoni watakuumbua na pengine wakunadie mwizi.

Ikiwa utabahatika kukuta watu wanaoisifia Chama hiki Cha kisultani au tuseme chenye imani ya Kisultani kutawala maisha basi watu hao watakuwa wafagiaji kwenye ofisi zao za Chama au wafanyakazi wa humo ambao hupata kutumia internate bure ,kama tuwaonavyo hapa wengine kumbe ni wana balozi alimradi utawajua wengine wako katika ofisi za Bunge na wengine makazi ya serikali hao kidogo huwa wagumu kukwambia ukweli kwa sababu wanafaidika kiaina.

Ila kama nilivyosema kama ni mwoga basi kwenye mazungumzo ya mitaani unaweza usivumilie ,utaona mtakamatwa sasa hivi ,si unafahamu Sultani CCM amejenga hofu kwa wananchi ili azidi kuwatawala.

Matokeo ambayo kama Sultani CCM anajiamini kushinda uchaguzi na kupata wabunge kura uraisi na kuendelea kuwa Sultani wa Nchi hii basi akubali kuibadilisha tume ili iwe huru halikadhalika na Katiba yake ili iendane na mfumo wa vyama vingi ,hapo ndipo utakapojua kama Sultani ni maguvu tu lakini hakuna wananchi wanaompenda. Tena nini ? Huo ndio ukweli na ukweli unaauma na lazima usemwe.
 
Mwiba

Bado kabisa ujajibu swali, kinachuzungumziwa hapa ni ushabiki wa mamilioni ya watz(hii ni pamoja na kule Pemba) kwa CCM, kwa nini inakuwa hivyo ilhali kuna zaidi ya vyama 10 vya siasa. Au kwa maneno mengine kwa nini mamilioni ya watz(Pemba miongoni) wanaendelea kuifagilia CCM na sio CUF wala Chadema?
 
Mwiba

Bado kabisa ujajibu swali, kinachuzungumziwa hapa ni ushabiki wa mamilioni ya watz(hii ni pamoja na kule Pemba) kwa CCM, kwa nini inakuwa hivyo ilhali kuna zaidi ya vyama 10 vya siasa. Au kwa maneno mengine kwa nini mamilioni ya watz(Pemba miongoni) wanaendelea kuifagilia CCM na sio CUF wala Chadema?

Achana naye huyo,maana yeye kila wakati n sultani CCM tuuu,nadhani kila siku akilala anaiota CCM.Kwa kweli CCM inamnyimaa usingizi huyu Sultani Orijino Mwiba
 
Mwiba

Bado kabisa ujajibu swali, kinachuzungumziwa hapa ni ushabiki wa mamilioni ya watz(hii ni pamoja na kule Pemba) kwa CCM, kwa nini inakuwa hivyo ilhali kuna zaidi ya vyama 10 vya siasa. Au kwa maneno mengine kwa nini mamilioni ya watz(Pemba miongoni) wanaendelea kuifagilia CCM na sio CUF wala Chadema?

Wacheni kujivisha kilemba cha ukoka ,ni lini uchaguzi hapa Tanzania ulifanyika bila ya valange valange ,sio mnakuja na utashi wa kisiasa ili kutaka kujijengea hoja na mapema.
Wekeni uchaguzi wa haki halafu ndio mje na mahesabu ,hayo mahesabu mtabaki nayo wenyewe tu ili kujikoimba kwa Sultani CCM aone vijana wake wanalinda nguvu za wizi kwa maneno ya poropaganda.

Huo ushabiki ndio haupo kama ulikuwepo ni zamani za kale lakini sasa hayo mamilioni yanataka mageuzi ya Chama Tawala ,hawataki tena kuburuzwa na Utawala wa Sultani CCM na vikaragosi vyake ,inafika time watu wanasema imetosha kila mfuasi ameshachukua chake mapema hivyo asie chukua ndio amepoteza nafasi ,kwani ikiwa utakwiba wakati Sultani anaongoza na wewe ni mfuasi wake basi unakuwa huna kosa umefuata sera yao ya kuchukua mapema.

Tunasema badilisha Tume badilisha mfumo wa Katiba ,weka nguvu za Dola kando ,halafu ndio unakuja na mahesabu ya mamilioni ,ikiwa wakati wa Nyerere watu waliweza kupinga na kumpinga itakuja kuwa leo shida kila kona.
 
Wacheni kujivisha kilemba cha ukoka ,ni lini uchaguzi hapa Tanzania ulifanyika bila ya valange valange ,sio mnakuja na utashi wa kisiasa ili kutaka kujijengea hoja na mapema.
Wekeni uchaguzi wa haki halafu ndio mje na mahesabu ,hayo mahesabu mtabaki nayo wenyewe tu ili kujikoimba kwa Sultani CCM aone vijana wake wanalinda nguvu za wizi kwa maneno ya poropaganda.

Huo ushabiki ndio haupo kama ulikuwepo ni zamani za kale lakini sasa hayo mamilioni yanataka mageuzi ya Chama Tawala ,hawataki tena kuburuzwa na Utawala wa Sultani CCM na vikaragosi vyake ,inafika time watu wanasema imetosha kila mfuasi ameshachukua chake mapema hivyo asie chukua ndio amepoteza nafasi ,kwani ikiwa utakwiba wakati Sultani anaongoza na wewe ni mfuasi wake basi unakuwa huna kosa umefuata sera yao ya kuchukua mapema.

Tunasema badilisha Tume badilisha mfumo wa Katiba ,weka nguvu za Dola kando ,halafu ndio unakuja na mahesabu ya mamilioni ,ikiwa wakati wa Nyerere watu waliweza kupinga na kumpinga itakuja kuwa leo shida kila kona.

CUF daima ndo mnaanzisha valange wewe.Kukweli CUF mmnachangia sana kuudhoofisha upinzani wa Tanzania(angalia kama mlivyofanya katika uchaguzi mdogo wa Mbeya vijijini),cha msingi kaeni chini na mjipange la sivyo mtaendelea kusoma namba za CCM Express
 
CUF daima ndo mnaanzisha valange wewe.Kukweli CUF mmnachangia sana kuudhoofisha upinzani wa Tanzania(angalia kama mlivyofanya katika uchaguzi mdogo wa Mbeya vijijini),cha msingi kaeni chini na mjipange la sivyo mtaendelea kusoma namba za CCM Express


Tanzania hakuna uchaguzi kuna uchafuzi hivyo kilichotokea Mbeya au kwengineko huwezi kusema kumefanywa Uchaguzi zaidi ya Uchafuzi.
Naona umekubali kuwa hakuna mamilioni na ndio umelukia Mbeya ,inaonekana una jazba ya kushabikia Usultani wa CCM ,hiyo ni hasara kwa Mtanzania ambae Taifa lake linaangamizwa na wajanja wachache na yeye anaingia kati kupiga makelele hajui kama anampigia kelele na kumshangilia mwendawazimu.

Kikwete amejitahidi kuweka sawa amebadilisha Mawaziri mbali ya walio achia ngazi ,amepanga mikakati ya kikazi kwa vyombo mbali mbali vya kiraia na kipolisi na usalama ,wamekutana Ngurdoto na kutoa miongozi ,ndugu nani amemsikiliza Raisi wa Tanzania aliyepatikana kwa tiketi ya Sultani CCM, nani amemsikiliza ? Pima vizuri usikurupuke tu .

Amepangua Jeshi la polisi mpka ameona bora kura kuliko jeshi la polisi ,huko ni kushindwa kiutawala kwa maana Chama kimeshindwa kutumia vyombo vilivyopo ambavyo vipo kwa ajili ya kupambana na hali hiyo.

Kikwete amesahau kuwa ndani ya vyombo hivyo wapo waliopo chini ambao wanaweza kuifanya kazi kiufasaha kabisa kwa moyo mmoja ,wapo ambao wanatamani wangekuwa wao ni MaRPC ,wapo wengi tu ambao ni wasomi na wana uchungu wa Nchi ,Moja ya ushauri aliopewa ni kuwashusha au kuwastopisha kazi MaRPC wote na kuteua vijana wepya wenye ari mpya ,Kikwete anaenda ana pangua wa huku amepeleka huku wa kule amleta hapa ,hivi anacheza draft hapa au vipi ?

Usione namponda lakini wafuasi wa Sultani CCM wamemzidi kete wanamshauri vibaya na yeye anafuata ,ameishiwa masikini kijana wa Kikwere hajui akamate wapi ,kila anapojaribu kuna haribika baadae matokeo ni sifuri ,sijui nani kamshauri juu ya kupiga kura labda Karume ? Raisi mtarajiwa wa Tanzania :D

Sasa uchaguzi chini ya Utawala wa Sultani CCM unaendeshwa kiubabe hadi hii leo kwa taarifa yako hakujabadilika kitu tokea mfumo wa vyama vingi ni ule ule mkakati wa Baba yenu wa Taifa Mareemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ...kataa basi ?

Wakati wa Nyerere alikuwa ni yeye peke yake labda mwaka 1962 nafikiri alikuwa na mgombea akiitwa Mtemvu kama sikosei kutoka TAA au hiyo hiyo Tanu, whatever ! Na hapa tulipo ndio tupo pale pale ila kilichobadilika ni aina ya Sultani ,tukitaka tusiotake ni Sultani CCM kwa maana mfuasi wa Sultani lazima ashinde vyovyote vile piga ua galagaza lazima Mfuasi wa Sultani CCM aibuke kidedea na ndivyo matokeo ya uchagzui yanavyopangwa na Tume hii tunayotaka na kudai ifanyiwe mabadiliko makubwa na ya kisasa.

Usiniletee habari za Pemba ,Pemba wameamua kufa na kupona ,kupigana kiume na lolote lile ambalo litatokea wapo tayari jambo ambalo bado wenzetu wa Tanganyika na Unguja hamjalifikia au stage yao bado hamjaifikia ,wao hivi sasa wapo mbali sana sana ,maana kufika kusema na kupeleka maombi UN si stage ndogo.

Hivyo Sultani CCM akubali kubadilisha tume ya uchaguzi na Katiba ili tuitite uchaguzi safi na sio uchafuzi la si hivyo yaliyotokea Pemba mkae mkijua yanabisha hodi Tanganyika muda si mrefu ,WaPemba wameonyesha njia na lile ni pigo kwa Utawala wa Sultani CCM. Tena wala msijipe imani kuwa huku hayawezi kufika au kutokea ,Kenya ilivyotingishika ,viongozi wa Sultani CCM kidogo walisika na kauli za kuonyesha kuwa wamepata msituko ambao wasipo uangalia hali iliyotokea Kenya inaweza kutokea na hapa Tanzania ,sasa muda mrefu umepita kwa wanavyohisi wao na wamejifanya wamesahau na kuanza kujipa tamaa ,waswahili tuna msemo tamaa mbele mauti nyuma.
 
Tanzania hakuna uchaguzi kuna uchafuzi hivyo kilichotokea Mbeya au kwengineko huwezi kusema kumefanywa Uchaguzi zaidi ya Uchafuzi.
Naona umekubali kuwa hakuna mamilioni na ndio umelukia Mbeya ,inaonekana una jazba ya kushabikia Usultani wa CCM ,hiyo ni hasara kwa Mtanzania ambae Taifa lake linaangamizwa na wajanja wachache na yeye anaingia kati kupiga makelele hajui kama anampigia kelele na kumshangilia mwendawazimu.

Kikwete amejitahidi kuweka sawa amebadilisha Mawaziri mbali ya walio achia ngazi ,amepanga mikakati ya kikazi kwa vyombo mbali mbali vya kiraia na kipolisi na usalama ,wamekutana Ngurdoto na kutoa miongozi ,ndugu nani amemsikiliza Raisi wa Tanzania aliyepatikana kwa tiketi ya Sultani CCM, nani amemsikiliza ? Pima vizuri usikurupuke tu .

Amepangua Jeshi la polisi mpka ameona bora kura kuliko jeshi la polisi ,huko ni kushindwa kiutawala kwa maana Chama kimeshindwa kutumia vyombo vilivyopo ambavyo vipo kwa ajili ya kupambana na hali hiyo.

Kikwete amesahau kuwa ndani ya vyombo hivyo wapo waliopo chini ambao wanaweza kuifanya kazi kiufasaha kabisa kwa moyo mmoja ,wapo ambao wanatamani wangekuwa wao ni MaRPC ,wapo wengi tu ambao ni wasomi na wana uchungu wa Nchi ,Moja ya ushauri aliopewa ni kuwashusha au kuwastopisha kazi MaRPC wote na kuteua vijana wepya wenye ari mpya ,Kikwete anaenda ana pangua wa huku amepeleka huku wa kule amleta hapa ,hivi anacheza draft hapa au vipi ?

Usione namponda lakini wafuasi wa Sultani CCM wamemzidi kete wanamshauri vibaya na yeye anafuata ,ameishiwa masikini kijana wa Kikwere hajui akamate wapi ,kila anapojaribu kuna haribika baadae matokeo ni sifuri ,sijui nani kamshauri juu ya kupiga kura labda Karume ? Raisi mtarajiwa wa Tanzania :D

Sasa uchaguzi chini ya Utawala wa Sultani CCM unaendeshwa kiubabe hadi hii leo kwa taarifa yako hakujabadilika kitu tokea mfumo wa vyama vingi ni ule ule mkakati wa Baba yenu wa Taifa Mareemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ...kataa basi ?

Wakati wa Nyerere alikuwa ni yeye peke yake labda mwaka 1962 nafikiri alikuwa na mgombea akiitwa Mtemvu kama sikosei kutoka TAA au hiyo hiyo Tanu, whatever ! Na hapa tulipo ndio tupo pale pale ila kilichobadilika ni aina ya Sultani ,tukitaka tusiotake ni Sultani CCM kwa maana mfuasi wa Sultani lazima ashinde vyovyote vile piga ua galagaza lazima Mfuasi wa Sultani CCM aibuke kidedea na ndivyo matokeo ya uchagzui yanavyopangwa na Tume hii tunayotaka na kudai ifanyiwe mabadiliko makubwa na ya kisasa.

Usiniletee habari za Pemba ,Pemba wameamua kufa na kupona ,kupigana kiume na lolote lile ambalo litatokea wapo tayari jambo ambalo bado wenzetu wa Tanganyika na Unguja hamjalifikia au stage yao bado hamjaifikia ,wao hivi sasa wapo mbali sana sana ,maana kufika kusema na kupeleka maombi UN si stage ndogo.

Hivyo Sultani CCM akubali kubadilisha tume ya uchaguzi na Katiba ili tuitite uchaguzi safi na sio uchafuzi la si hivyo yaliyotokea Pemba mkae mkijua yanabisha hodi Tanganyika muda si mrefu ,WaPemba wameonyesha njia na lile ni pigo kwa Utawala wa Sultani CCM. Tena wala msijipe imani kuwa huku hayawezi kufika au kutokea ,Kenya ilivyotingishika ,viongozi wa Sultani CCM kidogo walisika na kauli za kuonyesha kuwa wamepata msituko ambao wasipo uangalia hali iliyotokea Kenya inaweza kutokea na hapa Tanzania ,sasa muda mrefu umepita kwa wanavyohisi wao na wamejifanya wamesahau na kuanza kujipa tamaa ,waswahili tuna msemo tamaa mbele mauti nyuma.

Hizi ni kauli za Mfa maji,ambaye daima haishi kutapatapa..Lol
 
Mkuu Kishoka, hilo linalokufanya uwe CCM mfu, ndio nawengine linawafanya wawe CCM. Ila hakuna lolote kuwa CCM kina wafuasi wengi ndio maana kinashinda chaguzi. Kama CCM wangekubali tuwe na tume huru za uchaguzi, sasa hivi tungekuwa tunazungumza mengine, hata kama Rais ingekuwa hajapatikana toka upinzani, lakini idadi ya Wabunge na Madiwani ingeongezeka sana
Hizo ni propaganda za CUF ambao wamezoea kushindwa hata uweke tume ya uchaguzi ya malaika wote CCM itashinda.Bwana Hivi vyama vya upinzani bado viko mijini mbona hamtaki kukubali ukweli?.CCM inayo matawi katika vijiji vyote tanzania ambavyo zaidi ya vijiji kumi elf
 
Mimi nadhani:


4. Kwa wasomi kama Rev Kishoka, labda ni kwa sababu ya kutaka masilahi fulani, kwani si tuliambiwa kwamba "ukitaka biashara zako zikunyookee ingia CCM?"

Hapa ndio kuna tatizo kubwa. Wengi wa wasomi ni wabinafsi na wanafiki ambao wapo tayari kuuza uhuru wao kwa ajili ya maslahi na njaa za kutafuta shilingi. Kwa mtazamo wangu msomi ni independent thinker, ni mtu mwenye upeo wa kupembua mambo. Kama wasomi wote nchi hii wangekuwa wanatimiza wajibu wao, tusingekuwa hapa tulipo. Siku moja niliwahi kusoma kuhusu challenge ya mzee mmoja wa kijijini aliyewachambua wasomi wa nchi hii, kuwa ni wasomi njaa, wenye kufanya mambo ya ajabu, nadhani hakukosea. Wasomi ndio waliotakiwa kuongoza njia, lakini tuko tayari kutetea uovu ili msosi upatikane. Itatuchukua muda mrefu sana kufika mahali kama elimu yetu haitusaidii kupambanua mambo. Si jambo la ajabu kuona kuwa maprofesa na wasomi wa kuheshimika nchi hii wanakimbilia ujumbe wa CCM kwa sababu wanajua wanajiweka katika tabaka la kitawala wakisahau wajibu muhimu wa kupigania umma.
Tukizungumzia kudorora kwa siasa za nchi hii utasikia watu wakisema ujinga wa watz, mara nyingine nakataa kwa sababu hata wasomi wetu hawajajua namna ya kuondokana na matatizo haya, nadhani kuna tatizo na namna ya mfumo wetu wa elimu ulivyo, ni wa kukariri mambo bila ya kuyapambanua.
 
Back
Top Bottom